Kwanini bond ya mama na mtoto wa kiume ni kali sana tofauti na kwa baba?

Kwanini bond ya mama na mtoto wa kiume ni kali sana tofauti na kwa baba?

I am Groot

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
3,929
Reaction score
10,747
Inatokea kwa jamii nyingi kuwa mtoto wa kiume kawaida au mara nyingi kwenye familia huwa na upendo mkubwa sana kwa mama yake kuliko kwa baba yake.

Yuko tayari kuomba ushauri au kumshirikisha mambo yake ya ndani sana mama yake kuliko kumshirikisha baba.
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti, mapenzi ya dhati kuna muda huwa yanapofusha kushindwa kuona uhalisia, hapo unakuta mtu hana kipaji wala bidii, hana connections, n.k

Baba ni kichwa, mlinzi na mtafutaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona mbali maana ukiwatoa kina Diamond, Kiba, Harmonize na wasanii wengine wachache waliofanikiwa, kuna lundo kubwa sana la wasanii miaka nenda rudi wamesota (kwa ambao tumekaa na wasanii tunajua msoto wake), atakupa makavu na hatakusapoti, atakwambia ni bora akutafutie jembe ukalime uwe na uhakika hata wa kula na kuja kilisha familia yako.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaona baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto wa kiume akiacha kuwa tegemezi na kuanza kujitegemea, kuhama, kujitaftia ridhiki, kuwa na familia, n.k basi hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana wanaanza kufanana, mtoto na baba wote wanajitaftia ridhiki, mtoto na baba wote wameoa, mtoto na baba wote walihama kwao kujitegemea, n.k.

yote kwa yote wote wana umuhimu, ukipatwa na tatizo mama atakuwa karibu na wewe sana huku mzee akihangaika huko nje kukunasua kwenye tatizo kadri ya uwezo wake wote, hapo ndipo wengi wanakosea wanadhani mama ndie mwenye umuhimu zaidi lakini wanasahau baba yupo nje anapambana ili kuwanasua kwenye matatizo ya ujinga kwa kuwapa mahitaji ya elimu, kuwaondolea njaa kwa kuwalisha, kuwasitiri kwa kuwavisha, kuhakikisha hamlali nje kwa kulipia kodi ya nyumba au kujenga, kuwatoa uvivu kwa kuwapa kazi za kufanya nyumbani, kuwanusuru katika maamuzi mabaya yanayoweza kuwapeleka jela kwa kuwatia adabu tangu mkiwa wadogo, n.k. mchango wa baba ukitaka kuujua kama wewe ni mtoto wa kiume anza kujitegemea na kisha uwe na familia yako, ila kama bado unaishi kwenu bado hujawa mwanaume wa kuondoka kwenye kiota ukajitegemee hapo itakua kazi kuona mapenzi ya baba.
 
Mkuu hivi unaongelea hawa hawa wakulima wanaolia kila siku kuwa wanapangiwa bei za mazao na serikali au ni wakulima wepi wengine?

Anyway mimi nadhani huyo mtoto angeingia kwenye kilimo asingetoboa kwa sababu gani siyo passion yake hivyo hatafanya kwa ufanisi!

Kina baba wanapofeli ni kulazimisha mtoto afanye kitu kwa sababu tu ya heshima hata kama hakipendi wakati kina mama wao wanaamini tofauti!

Mtoto kitu akikipenda atafanya kwa bidii na kuna uwezekano akatoboa ila asipokipenda hatafanya kwa bidii na hatatoboa sababu siyo passion yake!

You feel me?
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti.

Baba ni kichwa, mlinzi na mtaftaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona usanii kwa asilimia kubwa wengi hawatoboi atakupa makavu na hatakusapoti, atakwambia katafute beba jembe ukalime uwe na uhakika hata wa kula.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaina baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto akianza kujitegemea ,hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana nae anakuwa mtaftaji kama baba yake.
Sidhani kama kuna maelezo mazuri na ya kujitosheleza kama haya. You have nailed it!
 
Inatokea kwa jamii nyingi kuwa mtoto wa kiume kawaida au mara nyingi kwenye familia huwa na upendo mkubwa sana kwa mama yake kuliko kwa baba yake. Yuko tayari kuomba ushauri au kumshirikisha mambo yake ya ndani sana mama yake kuliko kumshirikisha baba.
Unlike charges attract to each other while like charges repel each other. Ni hivyo tu.
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti.

Baba ni kichwa, mlinzi na mtaftaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona usanii kwa asilimia kubwa wengi hawatoboi atakupa makavu na hatakusapoti, atakwambia katafute beba jembe ukalime uwe na uhakika hata wa kula.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaina baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto akianza kujitegemea ,hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana nae anakuwa mtaftaji kama baba yake.
Asante kwa ufafanuzi huu
 
Jibu ni moja tu Wanawake wengine wote watakupenda sababu ya value you deliver to them. Mama yako pekee ndio atakupenda pasi na kigezo chochote sababu you shared blood. Hiyo ni connection ambayo she can't walk away from it.

Bond ya mama na kijana inakua kubwa sababu kijana ana uhakika na upendo wa mama yake 100%.

Kwa ground mwanaume kupendwa hivihivi na mwanamke ni tabu sana ila Mungu alivyo fundi automatically akawafanya wamama wapende vijana wao, na hata huyo mama awe na chuki au awe anapenda wanaume wengine kwa vigezo but the love for her son is there.
 
Teh kwamba hii nchi wakulima wengi ndiyo wanatoboa kuliko wasanii? Basi sawa!
Wakati mwenzako kachukulia kama mfano wewe unaichukulia serious nchi ina safari ndefu sana hii
 
Mkuu hivi unaongelea hawa hawa wakulima wanaolia kila siku kuwa wanapangiwa bei za mazao na serikali au ni wakulima wepi wengine?

Anyway mimi nadhani huyo mtoto angeingia kwenye kilimo asingetoboa kwa sababu gani siyo passion yake hivyo hatafanya kwa ufanisi!

Kina baba wanapofeli ni kulazimisha mtoto afanye kitu kwa sababu tu ya heshima hata kama hakipendi wakati kina mama wao wanaamini tofauti!

Mtoto kitu akikipenda atafanya kwa bidii na kuna uwezekano akatoboa ila asipokipenda hatafanya kwa bidii na hatatoboa sababu siyo passion yake!

You feel me?
Nadhani pia mtoa mada aliongelea baba kumshauri mwanae kilimo ni mfano tu siyo halisi sana kiasi cha kufanya kuwa hoja ya kubishania kilimo na usanii bora nini

Lakini kwa sababu ni mfano unaweza hata kuigeuza kwamba mama ameshauri kilimo na baba ameshauri usanii
Mtoto akaona bora nikalime kwenye usanii sina kipaji siwezi kutoboa ntakuwa vipi kama mondi mzee anazingua


Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Mtoto wa kiume anakuwa na mitazamo yake tangu akiwa na miaka 5, sasa lazima wazinguane mapema na dingi kwani naye ataleta mitazamo yake itakayo kinzana na dogo. Mama yeye ni mjanja anaenda naye sawa na hata kama anataka kumrekebisha atafanya in a very diplomatic way bila mikwara.
 
Inatokea kwa jamii nyingi kuwa mtoto wa kiume kawaida au mara nyingi kwenye familia huwa na upendo mkubwa sana kwa mama yake kuliko kwa baba yake. Yuko tayari kuomba ushauri au kumshirikisha mambo yake ya ndani sana mama yake kuliko kumshirikisha baba.
Mara nyingi wakati wa utoto, mtoto wa kiume atampenda mama sababu ya ujinga,
Mababa huwa hatutaki ujinga,ndio maana mtoto akikosea akiambiwa atashitakiwa kwa baba huogopa sana,
Sisi hupenda kuwafundisha watoto uhalisia wa mambo na si kudekezana,
Eti unakuta toto la miaka kumi linafuliwa na kutandikiwa kitanda na mama yake,
Si ujinga huo,
Ila akikua lazima amkubali baba kwa kumfunza namna ya kukabiliana na mazingira
 
Inatokea kwa jamii nyingi kuwa mtoto wa kiume kawaida au mara nyingi kwenye familia huwa na upendo mkubwa sana kwa mama yake kuliko kwa baba yake. Yuko tayari kuomba ushauri au kumshirikisha mambo yake ya ndani sana mama yake kuliko kumshirikisha baba.
Sababu ni kwamba katika familia nyingi za ki afrika baba hana ukaribu sana na watoto since the beginning. Muda wote yupo kutafta na watoto wanabak nyumban na mama. Pia Wengine ndo kabisaa hawajawahi kuwaona baba zao. Wengine mama zao hawana hekima wanagombanisha baba na watoto zao kwa kuwajaza uongo ili wao waonekane wema na baba zao wabaya.
 
Nadhani pia mtoa mada aliongelea baba kumshauri mwanae kilimo ni mfano tu siyo halisi sana kiasi cha kufanya kuwa hoja ya kubishania kilimo na usanii bora nini

Lakini kwa sababu ni mfano unaweza hata kuigeuza kwamba mama ameshauri kilimo na baba ameshauri usanii
Mtoto akaona bora nikalime kwenye usanii sina kipaji siwezi kutoboa ntakuwa vipi kama mondi mzee anazingua


Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Ndiyo maana kuanzia aya ya pili nilienda kwenye point yangu nikimaanisha kuwa baba anataka mtoto afanye kitu ambacho ni cha heshima bila kujali kama mtoto anakipenda ama la. Ila mama yeye anataka mtoto afanye kile anachopenda yeye sababu mtu akikipenda kitu atakifanya kwa bidii kulikoni akilazimishwa kuna uwezekano mkubwa akaharibu sababu hicho kitu hakipendi.
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti.

Baba ni kichwa, mlinzi na mtaftaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona usanii kwa asilimia kubwa wengi hawatoboi atakupa makavu na hatakusapoti, atakwambia katafute beba jembe ukalime uwe na uhakika hata wa kula.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaina baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto akianza kujitegemea ,hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana nae anakuwa mtaftaji kama baba yake.
hapa umemaliza kila kitu
 
Back
Top Bottom