Kwanini bond ya mama na mtoto wa kiume ni kali sana tofauti na kwa baba?

Kwanini bond ya mama na mtoto wa kiume ni kali sana tofauti na kwa baba?

Inasemekana pia kina mama wanawapenda zaidi watoto wao wa kiume kuliko wa kike ingawa nadhani kwenye kuzaa ni kama vile wanapenda wajifungue watoto wa kike
 
Inatokea kwa jamii nyingi kuwa mtoto wa kiume kawaida au mara nyingi kwenye familia huwa na upendo mkubwa sana kwa mama yake kuliko kwa baba yake.

Yuko tayari kuomba ushauri au kumshirikisha mambo yake ya ndani sana mama yake kuliko kumshirikisha baba.
Mkuu haya mambo sio kwwmba ni nature ilivyo hapanaaa hapanaaa,bali ni ATHARI ZA MALEZI YA TOKEA UTOTONI.

Katika umri ambao unatakiwa kumjengea mtoto ukaribu ni ule umri tokea anaanza kujifunza mambo yanayomhusu yaani kutembea,kuongea n.k

Sasa shida inakuja wakati wa umri huu kwa mtoto mara nyingi sana mama ndio huwa karibu na mtoto mchana wote baba akirudi usiku kachoka analala na maisha yanaendelea.

Hivyo katika masaa 24 mazima utakuta baba anaonana na mtoto masaa 3 mpaka 4.

Yaani kwa mwezi baba hukaa na mtoto masaa kama 120 tu sawa na siku 5 tu.

Na mama hukaa na mtoto masaa 600 sawa kama na siku 25 hivi.

Utaona kwamba mama hukaa na mtoto muda mwingi kuliko baba kwa familia nyingi za kwetu afrika.

Hii inapelekea mtoto kumzowea saaana mama yake kwa sababu ndie ambae anakuwa naye karibu muda mwingi,mambo yote ya kimwili anahudumiwa na mama yake.

Mpaka inafikia hatua mtoto huyu akifanya soo hapo ndo utasikia subiri baba yako arudi uone,yaani baba ni mtu wa kuhukumu tu,hii inapelekea mtoto kumuogopa bbaba yake kwa sababu baba anaplay part pale anapokuwa amekosea huyu mtoto

Kwa maana hiyo mtoto anazidi kukua katika hali hiyo ya kumzowea mama kuliko baba yake,hata akifikia kubaleghe anakuwa yuko katika hali hiyo hiyo.

Ila sasa watoto wengi wakishakuwa wakubwa hujiona kama hawastahiki saaana kukaa karibu na mama zao,ndipo watoto hao huanza kujisogeza kwa baba zao taratiiiibu.
 
Inatokea kwa jamii nyingi kuwa mtoto wa kiume kawaida au mara nyingi kwenye familia huwa na upendo mkubwa sana kwa mama yake kuliko kwa baba yake.

Yuko tayari kuomba ushauri au kumshirikisha mambo yake ya ndani sana mama yake kuliko kumshirikisha baba.
Kwa maisha yetu haya ya Africa baba ndo mtafuta riziki! Hii inatuweka muda mwingi mbali na familia zetu , ni katika kiipndi hiki ambapo baba tupo mbali na familia , mama naye hupata fursa ya kujenga jeshi lake hapo nyumbani, na lazima afanikiwe maana muda wote anakuwa na watoto wake,
Kibaya ni kuwa wakati baba anataabika kutafuta rizik, panapotikea mgongano baina ya mama na baba , mama ana nafasi nzuri sana ya kujitetea mbele za watoto wake maana ana muda wa kutosha na ku edit story za tukio. na atapata huruma ya watoto kuwa baba anamuonea mama.
Ndio sababu tunasomesha watoto wetu kwa upendo , ila ikitokea tukifika uzeee watoto wanamchukua mama yao na kwenda kumjengea nyumba mjini, Baba mtu ambaye alitaabika anabaki kijijini akijifia taratibu .
 
Ni kweli mama zetu wanatupenda sn.
Na ndy wanaotuharibia watoto.

Mfano ,,
Baba anaweza kuchimba biti mtoto asitoke usiku kwenda club
Huku mama ndy anayewafungulia milango wakirudi.
Sasa mama kwann asipendwe?na watoto?
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti, mapenzi ya dhati kuna muda huwa yanapofusha kushindwa kuona uhalisia, hapo unakuta mtu hana kipaji wala bidii, hana connections, n.k

Baba ni kichwa, mlinzi na mtafutaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona mbali maana ukiwatoa kina Diamond, Kiba, Harmonize na wasanii wengine wachache waliofanikiwa, kuna lundo kubwa sana la wasanii miaka nenda rudi wamesota (kwa ambao tumekaa na wasanii tunajua msoto wake), atakupa makavu na hatakusapoti, atakwambia ni bora akutafutie jembe ukalime uwe na uhakika hata wa kula na kuja kilisha familia yako.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaona baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto wa kiume akiacha kuwa tegemezi na kuanza kujitegemea, kuhama, kujitaftia ridhiki, kuwa na familia, n.k basi hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana wanaanza kufanana, mtoto na baba wote wanajitaftia ridhiki, mtoto na baba wote wameoa, mtoto na baba wote walihama kwao kujitegemea, n.k.

yote kwa yote wote wana umuhimu, ukipatwa na tatizo mama atakuwa karibu na wewe sana huku mzee akihangaika huko nje kukunasua kwenye tatizo kadri ya uwezo wake wote, hapo ndipo wengi wanakosea wanadhani mama ndie mwenye umuhimu zaidi lakini wanasahau baba yupo nje anapambana ili kuwanasua kwenye matatizo ya ujinga kwa kuwapa mahitaji ya elimu, kuwaondolea njaa kwa kuwalisha, kuwasitiri kwa kuwavisha, kuhakikisha hamlali nje kwa kulipia kodi ya nyumba au kujenga, kuwatoa uvivu kwa kuwapa kazi za kufanya nyumbani, kuwanusuru katika maamuzi mabaya yanayoweza kuwapeleka jela kwa kuwatia adabu tangu mkiwa wadogo, n.k. mchango wa baba ukitaka kuujua kama wewe ni mtoto wa kiume anza kujitegemea na kisha uwe na familia yako, ila kama bado unaishi kwenu bado hujawa mwanaume wa kuondoka kwenye kiota ukajitegemee hapo itakua kazi kuona mapenzi ya baba.
Asante, haya ndio maelezo yaliyoshiba na ukweli mtupu
 
Ni kweli mama zetu wanatupenda sn.
Na ndy wanaotuharibia watoto.

Mfano ,,
Baba anaweza kuchimba biti mtoto asitoke usiku kwenda club
Huku mama ndy anayewafungulia milango wakirudi.
Sasa mama kwann asipendwe?na watoto?
Mtoto akifanya ujinga nyumbani, mama anamuambia mtoto, "akina baba yako atakuchapa" [emoji23][emoji23]

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mama ni moyo ana mapenzi ya dhati yaliyovuka mipaka kwa mwanae, leo hii hata mama yako ukimwambia unataka kuwa msanii atakupa sapoti, mapenzi ya dhati kuna muda huwa yanapofusha kushindwa kuona uhalisia, hapo unakuta mtu hana kipaji wala bidii, hana connections, n.k

Baba ni kichwa, mlinzi na mtafutaji, leo hji ukimwambia unataka kuwa msanii atatafakari na kuona mbali maana ukiwatoa kina Diamond, Kiba, Harmonize na wasanii wengine wachache waliofanikiwa, kuna lundo kubwa sana la wasanii miaka nenda rudi wamesota (kwa ambao tumekaa na wasanii tunajua msoto wake), atakupa makavu na hatakusapoti, atakwambia ni bora akutafutie jembe ukalime uwe na uhakika hata wa kula na kuja kilisha familia yako.

Hapo ukitumia hisia utaona mama anakupenda ila ukitumia akili unaona baba anakujali.

ila kadri umri unavyoenda mtoto wa kiume akiacha kuwa tegemezi na kuanza kujitegemea, kuhama, kujitaftia ridhiki, kuwa na familia, n.k basi hapo ukaribu kwa baba unaongezeka maana wanaanza kufanana, mtoto na baba wote wanajitaftia ridhiki, mtoto na baba wote wameoa, mtoto na baba wote walihama kwao kujitegemea, n.k.

yote kwa yote wote wana umuhimu, ukipatwa na tatizo mama atakuwa karibu na wewe sana huku mzee akihangaika huko nje kukunasua kwenye tatizo kadri ya uwezo wake wote, hapo ndipo wengi wanakosea wanadhani mama ndie mwenye umuhimu zaidi lakini wanasahau baba yupo nje anapambana ili kuwanasua kwenye matatizo ya ujinga kwa kuwapa mahitaji ya elimu, kuwaondolea njaa kwa kuwalisha, kuwasitiri kwa kuwavisha, kuhakikisha hamlali nje kwa kulipia kodi ya nyumba au kujenga, kuwatoa uvivu kwa kuwapa kazi za kufanya nyumbani, kuwanusuru katika maamuzi mabaya yanayoweza kuwapeleka jela kwa kuwatia adabu tangu mkiwa wadogo, n.k. mchango wa baba ukitaka kuujua kama wewe ni mtoto wa kiume anza kujitegemea na kisha uwe na familia yako, ila kama bado unaishi kwenu bado hujawa mwanaume wa kuondoka kwenye kiota ukajitegemee hapo itakua kazi kuona mapenzi ya baba.
Big up mkuu, big up tena na tena
 
Dr. Chris Mauki aliwahi kusema kuwa "Mother is son's first true love" :pepeRun:
 
Back
Top Bottom