Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

maneno haya!
 
Mkuu Jo Venture kwanza kabisa unapaswa kuelewa kuwa Nuhu alikuwa kama Nabii wa MUNGU, hivyo basi Nabii wa MUNGU akitoa laana, laana hiyo imetoka kwa MUNGU, na Nabii wa MUNGU akitoa baraka, baraka hizo zimetoka kwa MUNGU, iko hivyo na hiyo haina ubishi.

Sasa ili niweze kujibu hoja yako vizuri, mimi nitaendelea kukujibu kwa kutumia Biblia sababu naamini kila jibu lipo ndani ya kitabu hichi hata kama majibu yamefichika. Labda naomba nikuulize wewe na wengine wote mnaouliza ni kwanini Caanan alilaaniwa na siyo Ham. Hivi ni kwanini Yakobo aliwabariki Efraimu na Manasse moja kwa moja kwa kuwawekea mikono kichwani na hakufanya hivyo kwa wajukuu wake wengine?? Kwanini alifanya hivyo kwa Efraimu na Manasse peke yao, tena kwa kumbariki mdogo ambaye ni Efraimu kwa baraka kubwa zaidi kuliko mkubwa ambaye ni Manasse?? Kwanini alimchagua mdogo??? (soma MWANZO 48:14-20)

Mimi naamini ipo sababu ya kufanya hivyo. Kumbukeni hata Yakobo alikuwa kama Nabii wa MUNGU, hivyo baraka zake au laana zake ni moja kwa moja zinatoka kwa MUNGU. Sasa turudi kwa Nuhu, kwanini alimlaani Caanani moja kwa moja na kuwaacha watoto wengine wa Hamu ambao hawakulaaniwa moja kwa moja kama ilivyokuwa kwa Caanan? Iko hivi; sisi wazazi huwa kuna mtoto tunampenda kuliko wote katika watoto wetu. Mara zote yule mtoto anayependwa zaidi na baba yake huwa kama amebeba roho ya baba yake. Inawezekana kabisa Caanani alikuwa kipenzi cha Hamu kuliko watoto wote aliokuwa nao ambao ni Kushi, Putu, Misri(Mizraim), na Caanan.

Mfano mzuri ni jinsi ambavyo Yakobo alivyokuwa anampenda sana Yusufu kuliko ndugu zake wote na Yusufu alikuwa ni mdogo, ingawa Benyamini alikuwa ndiyo mdogo zaidi. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa roho ya baba huwa inakuwa juu ya mtoto yule anayempenda zaidi kuliko wote. Sasa inapotokea baraka zinamdondokea baba, hizi baraka zitaenda kwa mtoto yule anayependwa zaidi. Na pia kama itatokea laana ikamdondokea baba, laana hii itakwenda kwa yule mtoto anayependwa zaidi. Ndiyo kisa nikawauliza lile swali kwanini watoto wa Yusufu walipokea baraka moja kwa moja kutoka kwa babu yao Yakobo na wajukuu wengine hawakubarikiwa moja kwa moja??

Hivyo hivyo pia, kwa Nuhu kumlaani Caanani moja kwa moja ni lazima alijua kuwa Caanani ndiye kipenzi cha baba yake ambaye ni Ham. Sasa ili kumkomoa Ham ili aumie zaidi ni kumlaani yule anayempenda zaidi ambaye ndiye hasa anabeba roho yake. Siku zote laana ipo kwa ajili ya kukomoa na kuumiza, huwezi kumkomoa mtu na kumuumiza pale pasipo uma zaidi, huwezi kumkomoa mtu kama hutaharibu kile kitu anachokipenda zaidi, ukiharibu kile asichokipenda utakuwa hujamkomoa wala hatadhurika. Lakini ukiharibu kile anachokipenda kuliko vyote, hapo unakua umemkomoa na kumshikisha adabu ipasavyo. Ifahamike kuwa hawa watu wa kale, kitu laana au baraka walikuwa wanazichukulia very seriously. Ni wazi kabisa hizi laana zilimuumiza sana Ham kuliko hata Caanan aliyelaaniwa moja kwa moja.

Mfano mzuri katika hili ni lile lililowakuta Wamisri siku zile za Musa. Wote mnafahamu namna MUNGU alivyoamuru watoto wote wa kiume ambao walikuwa ni wazaliwa wa kwanza wa kila nyumba katika Misri wafe. Usiku ule akapita Malaika na kuwauwa watoto wote ambao ni wazaliwa wa kwanza wa Wamisri. Sasa hapa mtauliza; hivi wale watoto walikuwa na makosa gani mpaka wafe wao wakati siyo wao waliowatesa na kuwanyanyasa wana wa Israeli??? Kwanini waliuwawa watoto wao wasiokuwa na hatia??..... Jibu mnalijua tayari.

Iko hivi; maamuzi ya MUNGU wakati mwingine huwa hayaeleweki kwetu sisi wanadamu, lakini hiyo haina maana kuwa maamuzi yake siyo sahihi. Kwa watu ambao wanamwamini MUNGU na kuzishika Amri zake wanajua kabisa MUNGU huwa hakosei katika maamuzi yake na matendo yake. Kuna watu ambao hawamwamini MUNGU, wala hawazishiki Amri zake, watu hawa wakisoma Biblia, wanakimbilia kusema MUNGU ana makosa, wengine wanasema MUNGU ni muonevu, wanapoteza imani na kuona kama Biblia ni kitabu tu kama vitabu vingine.

Naamini ndugu yangu zitto junior na wengine wote mtakuwa mmenielewa. Swala la roho ya baba kwenda kwa mtoto wengine litakuwa limewachanganya sana, lakini fahamuni kuwa kila baba kuna mtoto wake anabeba roho yake. This is a mystery, it is paradoxical, but it is real. Mfano hata katika jamii zetu mmewahi kusikia watu wakisema; "huyu mtoto yuko kama baba yake kabisa, kuanzia kuongea mpaka kutembea". Mfano ni Adamu jinsi alivyofanana na Sethi;

"Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi". MWANZO 5:3.

Maana yake ni kwamba roho ya Adamu ilihamia kwa Sethi, licha ya kwamba Adamu alikuwa na watoto wengine wengi tu mbali na Sethi.
Cc Doto Dotto
 
pale neno la Mungu mwenye uwezo wote juu ya kila kitu duniani na mbinguni linapo jichanganya lenyewe kwa lenyewe ni hatari sana.Mkuu zitto junior mwisho wa siku hakuna mtu yyte atakaye kuwa na uthibitisho juu ya neno lolote lililo ktk vitabu vya dini kwa hiyo njia rahisi ni kuamini kitakachokupendeza moyoni mwako, sababu hivyo vitabu vinasema uatahukumiwa kutokana na unavyo amini.
nimependa ulivyo malizia hapo kwa wazungu na waaabu,wanavyo tumia maneno ya vitabu vya dini kulaghai na kutenda maovu
 
Mkuu sipingani na wewe.ila umejibu swali kwa mtazamo wako wewe.ungeleta aya ya ushahidi ingekuwa vizuri zaidi...Mjadala huu umetokea kwakuwa aya hazija weka wazi ni kwa nini au kwa sababubu gani? Ndio maana wewe unamtazamo wako na wengine wanamtazamo wao.
 
Kipindi waingereza wakiitawala marekani walihangaika sana kutafuta vibarua katika mashamba yao huko marekani ili kupata malighafi kwajili ya viwanda vyao huko UK!

Baada ya wahindi weusi kushindwa kufanya kazi wakaamua kuwatumia Wazungu wenzao ambao waliokua wemehukumiwa vifungo jela kwa makosa mbali mbali.
Nao pia waliwashindwa kwakua ni wazumgu wenzao na walijua sheri na haki zao za msingi hivyo ilikua ngumu kuwaburuza kwa maslah yao.

Ndipo alipotokea Bishop mmoja akawawapa kisa cha NUHU na watoto wake Hamu, Shame na Yafeth. Kuhusu NUHU alipomlaani huyo mtoto wake Hamu akawa mweusi na kwa laana ile aliapizwa kuwa atakuwa mtumwa wa ndugu zake (Shamu na Yafeth) ambao wao ni weupe.

Hivyo bwana Bishop akawaambia waingereza "Kwanini muhangaike kutafuta vibarua wakati kuna huyu Hamu ambaye ana laana na kwa laana ile atakua mtumishe wetu!? hivyo lazima mumtafute ili aje amitumikie"
Baada ya hapo Wazungu wakaanza kumtafuta Hamu na kizazi chake kwa utambulisho wa rangi yao ambayo ni nyeusi.

Ndipo wapokutana na mtu mmoja (nahisi ni Vasco Dagama ila sina uhakika) akawambia mbona watu weusi wapo wengi sana Africa? Ndio wakaingia Africa kwa mbinu mbali mbali ila lengo lilikua ni kukifuata kizazi cha ndugu yao Hamu ambacho kiasili kimelaaniwa ila wakakitumiishe kama ilivyoagizwa.
Kweli walifanikiwa na wakawachukua Waafrika wengi kwenda USA kwenye mashamba yao na kuwatumikisha, na walikua walikua na nguvu sana, baada ya USA kupata uhuru wakahamia kabisa kwao (kwakina hicho kizazi cha Hamu ambapo ni Africa) kuendelea kuwatumia kwa mbinu mbali mbali kwa maslah yao!
Mwisho.
 
Mkuu ganster siyo kila kitu kilichoandikwa kwenye Biblia kimewekwa wazi wazi, lakini ukiisoma vizuri Biblia na kuielewa basi hata vile vilivyofichika utaelewa maana yake. Mfano mzuri ni hili Swali; kwanini Efraimu na Manasse walibarikiwa moja kwa moja na babu yao Yakobo kwa kuwekewa mikono kichwani na wajukuu wengine hawakubarikiwa moja kwa moja???

Nini cha ziada walichokifanya Efraimu na Manasse kuzidi wenzao, maana wakati wanabarikiwa walikuwa ni watoto wadogo tu??

Ukiweza kujua ni kwanini hawa walibarikiwa wakiwa wadogo, pia utafahamu ni kwanini Caanani alilaaniwa akiwa mdogo.
 
watakwambia mungu ..hapangiwi...yaani trilion 1.5 aibe jiwe halafu hukumu apew jesca like serious "" Mungu huyu Mungu gani aliyejaa visasi kama mzee wa chatle ..na bado watu wana mnyenyekea tu ..lakini mzee wa chatle alipoleta visasi vyake watu wamepga makelele mpaka basi
 
Mkuu Hawa watu na Mungu wao wanayetufundisha tumuamini ni hatari ..mimi sikuhizi sitaki kabisa kuamini hivyo vitabu ...vina mambo mengi ya kushangaza ....waweza kusoma ukasikia Suleiman alikuwa na rundo la wanawake lakini hakuwahi kuitwa mzinzi "" lakini ukifanya hivyo wewe unaonekana mzinzi balaaa....""
 
hapo hapo sasa "" yaani mafundisho mengine wanayotupa kupitia hizi dini na Matendo ya Mungu wanaye tuhubiria ...kama huyu Mungu angelikuwa anaishi duniani ..wallahi angestahiki kuwa jela ..muda huu"" inashangaza kusikia kwamba tunda walikula Eva na adamu...halafu na sisi wengine ambao hatukuwepo tukapewa laana ambayo inatokana na utendaji wa dhambi ambayo hatujawahi kushiriki...huyu Mungu amejaa visasi mnooo aisse...halafu hapo hapo ..anatuasa sisi tuwe tuna samehe 7× 70 wakati yeye mwenyew amediriki kutulaani hata sisi tusio husika na wala hatuwajui hao wahusika...huu siuonevu uliwazi kabisa huu""!!?
 
umeona sasa ..."" basiii kama ndio hivyo ..nashawishika kusema kuwa hivi vitabu ..havipaswi kuaminika aissee....vina ji contradict mnoo""
 
kwahiyo unaona sawa mtoto kulaanika kwa kosa ambalo hajalifanya...yaani na hiyo degree yko uliyonayo unaona kabisa kuwa hilo Lina leta tija "" sindio "" ?? baba fisadi "" basiii na Watoto wake wrote ni mafisadi sindio ??
 
Yani mtu alifanya kosa adhabu yake ni kunyongwa sasa eti unakusanywa ukoo wake wote, mifugo yake yote, vyombo vya ndani vyote, vinachomwa moto hadi nyumba? hii si haki, na si sawa
hahaaa...hatari sana "" tukiambiwa tuna angamia kwakukosa maarifa tunakuwa wakali "" Yaani mtoto asiyejua kitu ahukumiwe kwa ujinga wa mzazi wake ...na bado mnaona sawa ....halafu bado wanajiita wasomi huko shuleni walikwenda kusomea ujinga au ""
 
Yaani doto Mungu ana makusudi yake ndiye anaye fahamu kwanini iwe hivi
uwongo "" Mungu anazushiwa hawezi kuwa katili kiasi hiki....nikuulize swali ..?? kama maamuzi hayo anayoyafnya Mungu " angekuwa nayo kiongozi wa kibinaadamu "" angeonekana ni mtu wanamna gani "" mfano " raisi wa nchi aamue " kumkamata mtu yeyote ambaye ni muhaini " kisha amuhukumu " kifungo kuanzia yeye(muhaini ) mpaka familia yake yote " na mifugo yke " huyo raisi ataeleweka vipi na jamii ??..na kama huyo raisi ataonekana ni muonevu " iweje Mungu aonekane mtakatifu katika maamuzi yake onevu kama hayo "" ?
 
Asee hawa wazungu sio watu kabisa mkuu
 
kwenye biblia unasema "atakae kulaani nitamlaani na atakae kubariki nitambariki" nazani baada ya nuh kujua mungu kashambariki huyo mwanae ilibidi asira amalizie Kwa mjukuu wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…