Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

Mkuu lawama na laani ni vitu tofauti sana. Waziri hawezi kuua mtu huko Iringa then Magufuli ndo akamatwe Mmmh!! hapana.

Haya maandiko ya Bible me yananivuruga sana Ukisoma Mwanzo 3:17 Mungu anailaani ardhi sababu ya Adamu sasa ardhi ilifanya kosa gani pale Eden?

Yoshua 7:24+ Akani alifanya dhambi ya kuiba aliteketezwa yeye na uko wake mzima hadi ng'ombe, punda, na vitu vyake vyote. sasa wao viumbe wengine walikosa nini wahusike kwenye adhabu ya Akani?

Sikumbuki ni kitabu gani but utanisaidia kama unakijua. kuna mtumishi mmoja wa Elisha Nabii alifanya kosa kumuomba zawani Naamani alieponya ukoma na Elisha. Huyo mtumishi aliotwa na ukoma yeye na ukoo mzima. sasa wao ndugu zake wengine walifanya kosa gani mpk wahusiswe kwenye adhabu ya huyo mtumishi?

Najiuliza Mungu yukoje? na anatumia kanuni, sheria, utaratibu gani kuadhibu watu vitu ambavyo hata havijahusika kuadhibiwa pasipo kosa?
Mkuu hapo ndio kwenye swali langu sasa mpaka wanyama wanalaaniwa kwa kosa la binadamu hii ni hatari embu wenye kufahamu waje
 
Msingi wa mada nimeuelewa sana ila kuna kitu hapo kuhusu laana ya vizazi kwa vizazi mlijaribu kuzungumzia kama sehemu ya utetezi sasa ndio nataka maoni yako kuhusu hili jambo kutoa laana kwa vizazi ambavyo avijashiriki kwenye uovu uoni sio jambo jema maana mnawanyima fursa ya kutubu ni ilo mkuu
Ok sawa iko hivi laana ya vizazi haiwezi kuwa vizazi viwili tofauti I mean toka kwenye koo mbili tofauti.... Ni ukoo ama kizazi kimoja kwenye chain ya muunganiko wa vinasaba
 
Tukifuata maandiko tujifanyanye kuwa kweli kuna mtu aliwahi kuwepo akiitwa caanan,

sababu ni kuwa,ile nchi waebrania walikuja kutoka Sumeria ya Ur,
iliitwa caanan,
sasa ili wale wenyeji wa pale waonekane hawafai,waebrania wakaja na hii habari kwamba kuliwahi kuwa na mtu aitwae caanan na alilaaniwa na nchi ya caanan ililaaniwa,

lakini tena baada ya waebrania kusimika makazi yake caanan,hiyo nchi ikageuka kuwa tena nchi takatifu,
lakini hii habari ya caanan kulaaniwa ilikuja miaka mingi sana mbele wakati scriber wa kiyahudi wakikaa na kuandika maandiko yenye kukidhi interest zao,
fuatilia kwa makini sana wana wa caanan,utakuta majina yao ni majina ya jamii fulani au nchi fulani,
sio hivyo tu,mfano wana wa Amon,
unakuta eneo hilo ndo upo mji wa Aaman ,jordan,
na hawana taarifa kuhusu mtu aliewahi kuitwa amon,
 
Hii inahitimisha

5 mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Kutoka 20 :5
Yani hapo ndo unanivuruga kabisa. Mfano wewe unikosee halafu eti hata mtoto utakaemzaa nimchukie? ya nn sasa itakuwa sina utu ubinadamu

Sasa Mungu ana hekima kutuzidi sisi iweje aendelee kukomalia maovu waliotenda adamu na Hawa adhabu tupate sisi? Serious!! is not fair
 
Asante mkuu kwa Tag!.
Nakuahidi nitarudi nikiwa free!.
Also sorry kwa kushindwa kuwa active coz ya majukumu ya kikazi but Tupo pa1 kaka
Pamoja sana great thinker na pole kwa majukumu ya kujenga taifa
 
Tukifuata maandiko tujifanyanye kuwa kweli kuna mtu aliwahi kuwepo akiitwa caanan,

sababu ni kuwa,ile nchi waebrania walikuja kutoka Sumeria ya Ur,
iliitwa caanan,
sasa ili wale wenyeji wa pale waonekane hawafai,waebrania wakaja na hii habari kwamba kuliwahi kuwa na mtu aitwae caanan na alilaaniwa na nchi ya caanan ililaaniwa,

lakini tena baada ya waebrania kusimika makazi yake caanan,hiyo nchi ikageuka kuwa tena nchi takatifu,
lakini hii habari ya caanan kulaaniwa ilikuja miaka mingi sana mbele wakati scriber wa kiyahudi wakikaa na kuandika maandiko yenye kukidhi interest zao,
fuatilia kwa makini sana wana wa caanan,utakuta majina yao ni majina ya jamii fulani au nchi fulani,
sio hivyo tu,mfano wana wa Amon,
unakuta eneo hilo ndo upo mji wa Aaman ,jordan,
na hawana taarifa kuhusu mtu aliewahi kuitwa amon,
Duh hii hoja nzito sana..... Nimewahi kusikia claims hizi kuwa kuna uwezekano mwandishi wa kitabu cha mwanzo alionyesha laana imekwenda kwa CANAAN na kwamba uzao wake watakuwa watumwa kwa SHEM yote haya kuwaandaa watu kisaikolojia ili hata wakija kuvamia waseme MAANDIKO YALISHATABIRI!!! Sasa wwe umeiongelea ndio umenipa mwanga zaidi kuwa huenda kuna propaganda zilichezwa hapa

Aseee hatari sana kama hii ni kweli
 
Mkuu lawama na laani ni vitu tofauti sana. Waziri hawezi kuua mtu huko Iringa then Magufuli ndo akamatwe Mmmh!! hapana.

Haya maandiko ya Bible me yananivuruga sana Ukisoma Mwanzo 3:17 Mungu anailaani ardhi sababu ya Adamu sasa ardhi ilifanya kosa gani pale Eden?

Yoshua 7:24+ Akani alifanya dhambi ya kuiba aliteketezwa yeye na uko wake mzima hadi ng'ombe, punda, na vitu vyake vyote. sasa wao viumbe wengine walikosa nini wahusike kwenye adhabu ya Akani?

Sikumbuki ni kitabu gani but utanisaidia kama unakijua. kuna mtumishi mmoja wa Elisha Nabii alifanya kosa kumuomba zawani Naamani alieponya ukoma na Elisha. Huyo mtumishi aliotwa na ukoma yeye na ukoo mzima. sasa wao ndugu zake wengine walifanya kosa gani mpk wahusiswe kwenye adhabu ya huyo mtumishi?

Najiuliza Mungu yukoje? na anatumia kanuni, sheria, utaratibu gani kuadhibu watu vitu ambavyo hata havijahusika kuadhibiwa pasipo kosa?
Watalaam wa maandiko tunao humu ngoja waje
mitale na midimu SALA NA KAZI popbwinyo Online Pastor Che mittoga
 
Kwa akili yako wanaolaniwa kwa makosa ya wazazi wao ww unafikir ni sawa?
Ni Sawa maana hii ni kuwa kama baba yako atatenda dhambi mbele ya Mungu na uzao wake utazaliwa katika dhambi lakini wale watakao badirika kuiacha njia ya baba yao watakuwa wameiacha dhambi wata hesabiwa haki.
 
Ka

sasa inakuaje kosa afanye mwingine aadhibiwe mwengine ambaye ata kuzaliwa akuzaliwa
Ndio maana Mungu anasema anawalehemu maelfu elfu wampendao na kuzishika amri zake
Kwa mfano ukizaliwa katika familia inayo abudu sanamu dhambi ya familia itakuwa na wewe lakini ukiamua kuitafata kweli ukaifata kiroho umejitenga na uovu wa familia hiyo kwamaana hiyo utakuwa ni familia ya wana wa Mungu
 
Msingi wa mada nimeuelewa sana ila kuna kitu hapo kuhusu laana ya vizazi kwa vizazi mlijaribu kuzungumzia kama sehemu ya utetezi sasa ndio nataka maoni yako kuhusu hili jambo kutoa laana kwa vizazi ambavyo avijashiriki kwenye uovu uoni sio jambo jema maana mnawanyima fursa ya kutubu ni ilo mkuu
Soma hapa

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Kutoka 20 :5

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Kutoka 20 :6

Hapa natumai utaelewa lakini ukitaka kujitoa katika dhambi itafute kweli uifuate hapo utakuwa umejitenga na uovu wa laana ya kizazi hicho
 
Mkuu zitto junior ili uweze kuelewa ni kwanini Nuhu alimlaani Caanan na siyo Ham aliyetenda kosa, kwanza unatakiwa ulielewa na kuliamini NENO la MUNGU. Ili ulielewe NENO la MUNGU, kwanza lazima uliamini. Binadamu hatuwezi kumwelewa MUNGU, lakini tunaweza kulielewa NENO lake ambalo ametupa ili litusaidie katika maisha ya sasa na yale yajayo.

Tatizo linakuja pale ambapo watu walio wengi hawataki kuielewa Biblia wala kuiamini, wengi wanaona kile kilichoandikwa kwenye Biblia ni kama hadithi tu, ni kama porojo tu ambazo hazina maana. Ukweli ni kwamba, Biblia ni zaidi ya hadithi, ni zaidi ya Historia, na ni zaidi ya Unabii ambao umekuwa ukitimia kila siku. Kwa kulitambua hili, mimi nitakupa majibu ya Kibiblia ni kwanini Nuhu alimlaani Caanani badala ya Ham. Majibu yote yapo ndani ya Biblia na nje ya Biblia huwezi kupata majibu.

Iko hivi; zamani zile Wazazi hasa baba walikuwa wanatoa baraka au laana kwa kizazi cha watoto wao na siyo kwa mtu mmoja peke yake. Kama ni baraka, baba alikuwa anatoa baraka hizi kwa watoto wake wa kiume na vizazi vyao vyote vinavyofuata kwa sababu walikuwa wanaamini kuwa kizazi hakiishii kwa watoto, bali kinaendelea na kuendelea. Pia huu ndiyo ulikuwa utaratibu waliojifunza kutoka kwa BWANA MUNGU, pale alipotoa laana ya kwanza kwa mwanadamu na nyoka;

"nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino". MWANZO 3:15

Hapo juu utaona hiyo laana siyo kwa Eva na nyoka peke yao, bali ni kwa uzao wao wote utakaotokea duniani. Hii inaonekana kuwa wazee wale wa kale walijifunza pia kutoa laana au baraka kwa kizazi na kizazi. Hebu tuone baraka ya Isaka kwa Yakobo.

"Mataifa na wakutumikie, na makabila wakusujudie. Uwe bwana wa ndugu zako, na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakaye kulaani, alaaniwe na atakayekubariki, abarikiwe". MWANZO 27:29

Hapa pia utaona Yakobo anabarikiwa na baba yake, tena siyo baraka kwa ajili yake tu katika maisha yake yeye kama Yakobo, bali ni kwa ajili yake na uzao wake wote utakaofuatia baada yake. Hivi ndivyo ilivyokuwa, hivi ndivyo wanadamu walijifunza kutoa baraka kwa wana wao au laana. Pia unaweza ukasoma kitabu hicho cha MWANZO sura ya 49, na utaona jinsi ambavyo na yeye Yakobo alivyotoa baraka kwa watoto wake 12.

Tukirudi upande wa BWANA MUNGU, pia tutaona jinsi alivyombariki mzee Ibrahimu, hakumbariki yeye tu kwa wakati ule, bali alimbariki yeye na uzao wake wote utakaofuatia baadaye.

"Nami nitakufanya wewe kuwa Taifa kubwa na kukubariki, na kulikuza jina lako nawe uwe baraka. Nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia zitabarikiwa". MWANZO 12:2-3

Mpaka hapa tutakuwa tumeona jinsi baraka na laana zilivyokuwa zinatolewa na inaonekana wazi kabisa namna ya kutoa baraka au laana, Wanadamu wa kale akiwemo mzee Nuhu walijifunza kutoka kwa MUNGU. Tukumbuke kuwa Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, na aliongea na MUNGU mara nyingi tu katika njozi na maono. Hivyo basi Hamu alipokosea kwa kumwangalia baba yake akiwa uchi na kumcheka, alilaaniwa Caanani ambaye alikuwa ni uzao wa Hamu, yaani kizazi chote cha Hamu kikawa kimelaaniwa.

Huo ndiyo ulikuwa utaratibu wa kutoa laana au baraka, tena ni utaratibu ambao ulikuwa na baraka zote toka kwa MUNGU. Caanan hakumcheka Nuhu, lakini alilaaniwa sababu yeye alikuwa ni uzao wa Hamu, Caanan alikuwa anabeba damu ya Hamu ndani yake na alipaswa kulaaniwa. Pia tukumbuke jinsi MUNGU alivyosema katika zile Amri kumi;

".........nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu". KUTOKA 20:5-6

Nuhu hakukosea kumlaani Caanan, nasema hakukosea sababu Nuhu alifuata utaratibu uliokuwepo. Utaratibu ambao hata BWANA MUNGU aliutumia kwa mara ya kwanza pale Eva alipokula matunda ya mti aliokatazwa asile. Tukihoji kwanini Nuhu Nabii wa MUNGU alimlaani Caanan kwa makosa ya baba yake, itakuwa kama tunataka kuhoji pia ni kwanini sisi leo hii tunabeba laana ya Eva na Adamu wakati siyo sisi tuliokula tunda. Nafikiri hakuna mwanadamu anayeweza kusimama na kumuuliza MUNGU kwanini ulifanya hivyo, kwanini ulitulaani sisi? (Soma ISAYA 45:9 au WARUMI 9:14-21)

MUNGU hakosei na wala MUNGU hamuonei mtu wala kumpendelea mtu. Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, hivyo basi laana ya Nuhu kwa Caanan ilipata baraka zote toka kwa MUNGU. Kama Nuhu angekuwa ametoa laana kwa uonevu bila kufuata utaratibu unaokubalika na MUNGU; basi MUNGU asingekubali Caanan alaanike, angeizuia hiyo laana isitokee.

Nina imani kwa maelezo hayo, utakuwa umeelewa ni kwanini Caanan alibeba laana ya baba yake, tena siyo Caanan tu, bali ni yeye na uzao wake wote uliofuatia. Hata sisi Waafrika tunabeba laana hiyo mpaka leo, lakini tukumbuke kwamba MUNGU aliyetupiga kwa laana, ndiye YEYE huyo huyo aliyetuletea UKOMBOZI kupitia kwa Mwanawe YESU KRISTO.


"Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam Mimi ndiye, wala hapana MUNGU mwingine ila Mimi; naua Mimi, naponya Mimi, nimejeruhi tena nimeponya; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu". KUMBUKUMBU LA TORATI 32:39
Mkuu zitto junior hatuwezi kumwelewa MUNGU hata siku moja, akili zake, wala mawazo yake, hayachunguziki na Mwanadamu wala Malaika. Lakini tunaweza kulielewa NENO lake, kuliamini na kumtii Yeye kama MUUMBA wetu.
 
Mkuu Son of Gamba nashukuru kwa hoja yako iliyoshiba madini nimekuelewa sana tu ingawa ntarudi na swali ila kuna mtoa mada mmoja hapo juu alihoji JE NI HAKI Kosa kufanywa na mtu mmoja alafu laana kwa ukoo mzima?? Akaenda mbali na kusema huo ni uonevu na kadhalika

Hivyo basi kwa hekima yako unafkiri nini chanzo cha Mungu akilaani ni mpaka vizazi na akibariki ni vizazi kwanini haangalii mtu na mtu !!

Barikiwa

Cc Doto Dotto
 
Mkuu lawama na laani ni vitu tofauti sana. Waziri hawezi kuua mtu huko Iringa then Magufuli ndo akamatwe Mmmh!! hapana.

Haya maandiko ya Bible me yananivuruga sana Ukisoma Mwanzo 3:17 Mungu anailaani ardhi sababu ya Adamu sasa ardhi ilifanya kosa gani pale Eden?

Yoshua 7:24+ Akani alifanya dhambi ya kuiba aliteketezwa yeye na uko wake mzima hadi ng'ombe, punda, na vitu vyake vyote. sasa wao viumbe wengine walikosa nini wahusike kwenye adhabu ya Akani?

Sikumbuki ni kitabu gani but utanisaidia kama unakijua. kuna mtumishi mmoja wa Elisha Nabii alifanya kosa kumuomba zawani Naamani alieponywa ukoma na Elisha nabii. Huyo mtumishi alipatwa na ukoma yeye na ukoo mzima. sasa wao ndugu zake wengine walifanya kosa gani mpk wahusishwe kwenye adhabu ya huyo mtumishi?

Najiuliza Mungu yukoje? na anatumia kanuni, sheria, utaratibu gani kuadhibu watu vitu ambavyo hata havijahusika kuadhibiwa pasipo kosa?
Mkuu katika maisha yetu tupo katika mnyororo tunavutana yaani ni hivi watu walio na damu ya baba yako wote na mama yako nyote mu uzao wa damu moja kama baba yenu ambaye ni shina atatenda mabaya nanyi yakawafurahisha nanyi na vizazi vyenu mtahesabiwa katika dhambi ila kama mtajitenga na laana ya kizazi cha damu yenu mtakuwa mtakuwa mmekata cheni inayowazunguka mtahesabiwa haki

Soma hapa ili kujua cheni ya kuambatana inavyowavuta wote wasiotaka kugeuza nia zao na kuangamizwa

10 Eliya akajibu, akamwambia yule akida wa hamsini, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto ukashuka, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Wafalme 1 :10

11 Akatuma tena akida wa hamsini mwingine pamoja na hamsini wake, wamwendee. Akajibu, akamwambia, Ewe mtu wa Mungu, mfalme asema, Shuka upesi.
2 Wafalme 1 :11

12 Eliya akajibu, akamwambia, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Wafalme 1 :12

13 Tena akatuma akida wa hamsini wa tatu, pamoja na hamsini wake. Yule akida wa hamsini wa tatu akapanda, akaenda akapiga magoti mbele ya Eliya, akamsihi sana, akamwambia, Ee mtu wa Mungu, nakusihi, roho yangu, na roho za watumishi wako hawa hamsini, ziwe na thamani machoni pako.
2 Wafalme 1 :13

14 Tazama, moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza wale akida wa hamsini wawili wa kwanza pamoja na hamsini wao; laiti sasa roho yangu na iwe na thamani machoni pako.
2 Wafalme 1 :14



Jiulize kwanini hawa wote waliteketezwa kwa moto ni kwasababu walijifunga katika cheni ya maasi
 
Mkuu ukirudi kwenye maandiko utagundua Si kizazi chore cha Ham kilicholaaniwa, ni Canaan na kizazi chake tu. Wa kwanza ni Cush, Mizraim , Phut na Wa mwisho ni Canaan.
Manaake laana hazikwenda kwa hao wengine Bali kwa Canaan tu na uzao Wa Canaan
 
Mkuu hapo ndio kwenye swali langu sasa mpaka wanyama wanalaaniwa kwa kosa la binadamu hii ni hatari embu wenye kufahamu waje
Soma hiki kisa ili upate kujua kwanini Mungu huangamiza wale wote walipo katika mnyororo wa maasi

10 Eliya akajibu, akamwambia yule akida wa hamsini, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto ukashuka, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Wafalme 1 :10

11 Akatuma tena akida wa hamsini mwingine pamoja na hamsini wake, wamwendee. Akajibu, akamwambia, Ewe mtu wa Mungu, mfalme asema, Shuka upesi.
2 Wafalme 1 :11

12 Eliya akajibu, akamwambia, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Wafalme 1 :12

13 Tena akatuma akida wa hamsini wa tatu, pamoja na hamsini wake. Yule akida wa hamsini wa tatu akapanda, akaenda akapiga magoti mbele ya Eliya, akamsihi sana, akamwambia, Ee mtu wa Mungu, nakusihi, roho yangu, na roho za watumishi wako hawa hamsini, ziwe na thamani machoni pako.
2 Wafalme 1 :13

14 Tazama, moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza wale akida wa hamsini wawili wa kwanza pamoja na hamsini wao; laiti sasa roho yangu na iwe na thamani machoni pako.
2 Wafalme 1 :14

Kinachosababisha ni kuwa kizazi chote kinajiingiza katika mnyororo wa damu ya laana hili ndio tatizo lakini ikitokea mmojawapo amejitoa katika huu mnyororo atakuwa amekata mawasiliano kujiondoa katika laana na kujiweka katika neema hata akida waliotumwa angekuwepo mmoja mwenye haki basis angepona katika moto huu angekuwa amejitenga na laana
 
Mkuu zitto junior ili uweze kuelewa ni kwanini Nuhu alimlaani Caanan na siyo Ham aliyetenda kosa, kwanza unatakiwa ulielewa na kuliamini NENO la MUNGU. Ili ulielewe NENO la MUNGU, kwanza lazima uliamini. Binadamu hatuwezi kumwelewa MUNGU, lakini tunaweza kulielewa NENO lake ambalo ametupa ili litusaidie katika maisha ya sasa na yale yajayo.

Tatizo linakuja pale ambapo watu walio wengi hawataki kuielewa Biblia wala kuiamini, wengi wanaona kile kilichoandikwa kwenye Biblia ni kama hadithi tu, ni kama porojo tu ambazo hazina maana. Ukweli ni kwamba, Biblia ni zaidi ya hadithi, ni zaidi ya Historia, na ni zaidi ya Unabii ambao umekuwa ukitimia kila siku. Kwa kulitambua hili, mimi nitakupa majibu ya Kibiblia ni kwanini Nuhu alimlaani Caanani badala ya Ham. Majibu yote yapo ndani ya Biblia na nje ya Biblia huwezi kupata majibu.

Iko hivi; zamani zile Wazazi hasa baba walikuwa wanatoa baraka au laana kwa kizazi cha watoto wao na siyo kwa mtu mmoja peke yake. Kama ni baraka, baba alikuwa anatoa baraka hizi kwa watoto wake wa kiume na vizazi vyao vyote vinavyofuata kwa sababu walikuwa wanaamini kuwa kizazi hakiishii kwa watoto, bali kinaendelea na kuendelea. Pia huu ndiyo ulikuwa utaratibu waliojifunza kutoka kwa BWANA MUNGU, pale alipotoa laana ya kwanza kwa mwanadamu na nyoka;

"nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino". MWANZO 3:15

Hapo juu utaona hiyo laana siyo kwa Eva na nyoka peke yao, bali ni kwa uzao wao wote utakaotokea duniani. Hii inaonekana kuwa wazee wale wa kale walijifunza pia kutoa laana au baraka kwa kizazi na kizazi. Hebu tuone baraka ya Isaka kwa Yakobo.

"Mataifa na wakutumikie, na makabila wakusujudie. Uwe bwana wa ndugu zako, na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakaye kulaani, alaaniwe na atakayekubariki, abarikiwe". MWANZO 27:29

Hapa pia utaona Yakobo anabarikiwa na baba yake, tena siyo baraka kwa ajili yake tu katika maisha yake yeye kama Yakobo, bali ni kwa ajili yake na uzao wake wote utakaofuatia baada yake. Hivi ndivyo ilivyokuwa, hivi ndivyo wanadamu walijifunza kutoa baraka kwa wana wao au laana. Pia unaweza ukasoma kitabu hicho cha MWANZO sura ya 49, na utaona jinsi ambavyo na yeye Yakobo alivyotoa baraka kwa watoto wake 12.

Tukirudi upande wa BWANA MUNGU, pia tutaona jinsi alivyombariki mzee Ibrahimu, hakumbariki yeye tu kwa wakati ule, bali alimbariki yeye na uzao wake wote utakaofuatia baadaye.

"Nami nitakufanya wewe kuwa Taifa kubwa na kukubariki, na kulikuza jina lako nawe uwe baraka. Nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia zitabarikiwa". MWANZO 12:2-3

Mpaka hapa tutakuwa tumeona jinsi baraka na laana zilivyokuwa zinatolewa na inaonekana wazi kabisa namna ya kutoa baraka au laana, Wanadamu wa kale akiwemo mzee Nuhu walijifunza kutoka kwa MUNGU. Tukumbuke kuwa Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, na aliongea na MUNGU mara nyingi tu katika njozi na maono. Hivyo basi Hamu alipokosea kwa kumwangalia baba yake akiwa uchi na kumcheka, alilaaniwa Caanani ambaye alikuwa ni uzao wa Hamu, yaani kizazi chote cha Hamu kikawa kimelaaniwa.

Huo ndiyo ulikuwa utaratibu wa kutoa laana au baraka, tena ni utaratibu ambao ulikuwa na baraka zote toka kwa MUNGU. Caanan hakumcheka Nuhu, lakini alilaaniwa sababu yeye alikuwa ni uzao wa Hamu, Caanan alikuwa anabeba damu ya Hamu ndani yake na alipaswa kulaaniwa. Pia tukumbuke jinsi MUNGU alivyosema katika zile Amri kumi;

".........nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu". KUTOKA 20:5-6

Nuhu hakukosea kumlaani Caanan, nasema hakukosea sababu Nuhu alifuata utaratibu uliokuwepo. Utaratibu ambao hata BWANA MUNGU aliutumia kwa mara ya kwanza pale Eva alipokula matunda ya mti aliokatazwa asile. Tukihoji kwanini Nuhu Nabii wa MUNGU alimlaani Caanan kwa makosa ya baba yake, itakuwa kama tunataka kuhoji pia ni kwanini sisi leo hii tunabeba laana ya Eva na Adamu wakati siyo sisi tuliokula tunda. Nafikiri hakuna mwanadamu anayeweza kusimama na kumuuliza MUNGU kwanini ulifanya hivyo, kwanini ulitulaani sisi? (Soma ISAYA 45:9 au WARUMI 9:14-21)

MUNGU hakosei na wala MUNGU hamuonei mtu wala kumpendelea mtu. Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, hivyo basi laana ya Nuhu kwa Caanan ilipata baraka zote toka kwa MUNGU. Kama Nuhu angekuwa ametoa laana kwa uonevu bila kufuata utaratibu unaokubalika na MUNGU; basi MUNGU asingekubali Caanan alaanike, angeizuia hiyo laana isitokee.

Nina imani kwa maelezo hayo, utakuwa umeelewa ni kwanini Caanan alibeba laana ya baba yake, tena siyo Caanan tu, bali ni yeye na uzao wake wote uliofuatia. Hata sisi Waafrika tunabeba laana hiyo mpaka leo, lakini tukumbuke kwamba MUNGU aliyetupiga kwa laana, ndiye YEYE huyo huyo aliyetuletea UKOMBOZI kupitia kwa Mwanawe YESU KRISTO.


"Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam Mimi ndiye, wala hapana MUNGU mwingine ila Mimi; naua Mimi, naponya Mimi, nimejeruhi tena nimeponya; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu". KUMBUKUMBU LA TORATI 32:39
Mkuu zitto junior hatuwezi kumwelewa MUNGU hata siku moja, akili zake, wala mawazo yake, hayachunguziki na Mwanadamu wala Malaika. Lakini tunaweza kulielewa NENO lake, kuliamini na kumtii Yeye kama MUUMBA wetu.
Mkuu kunavitu naona wazi unajichanganya au hujavielewa. Mimi kama Mimi sihoji wala sipingi Mungu afanyapo jambo. Bali ili kuweka sawa elimu itokanayo na jambo au funzo la Mungu ndipo tunahitaji mijadala kueleweshana.
Naomba usome tena na uelewe:-
1. Mungu hamkulaani Canaan wala Ham Bali ni Nuhu na kwasababu Nuhu alikua na nguvu ya Agano na Mungu basi ile laana ikafanya kazi (kwa Canaan).
2.Canaan ni mtoto Wa NNE wa Ham na sio kizazi cha NNE cha Ham.
 
Mkuu katika maisha yetu tupo katika mnyororo tunavutana yaani ni hivi watu walio na damu ya baba yako wote na mama yako nyote mu uzao wa damu moja kama baba yenu ambaye ni shina atatenda mabaya nanyi yakawafurahisha nanyi na vizazi vyenu mtahesabiwa katika dhambi ila kama mtajitenga na laana ya kizazi cha damu yenu mtakuwa mtakuwa mmekata cheni inayowazunguka mtahesabiwa haki

Soma hapa ili kujua cheni ya kuambatana inavyowavuta wote wasiotaka kugeuza nia zao na kuangamizwa

10 Eliya akajibu, akamwambia yule akida wa hamsini, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto ukashuka, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Wafalme 1 :10

11 Akatuma tena akida wa hamsini mwingine pamoja na hamsini wake, wamwendee. Akajibu, akamwambia, Ewe mtu wa Mungu, mfalme asema, Shuka upesi.
2 Wafalme 1 :11

12 Eliya akajibu, akamwambia, Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, na ushuke moto kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na hamsini wako. Moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza, yeye na hamsini wake.
2 Wafalme 1 :12

13 Tena akatuma akida wa hamsini wa tatu, pamoja na hamsini wake. Yule akida wa hamsini wa tatu akapanda, akaenda akapiga magoti mbele ya Eliya, akamsihi sana, akamwambia, Ee mtu wa Mungu, nakusihi, roho yangu, na roho za watumishi wako hawa hamsini, ziwe na thamani machoni pako.
2 Wafalme 1 :13

14 Tazama, moto ulishuka kutoka mbinguni, ukawateketeza wale akida wa hamsini wawili wa kwanza pamoja na hamsini wao; laiti sasa roho yangu na iwe na thamani machoni pako.
2 Wafalme 1 :14



Jiulize kwanini hawa wote waliteketezwa kwa moto ni kwasababu walijifunga katika cheni ya maasi
1. Wana wa Israel wote walikuwa wameasi watatumikia miungu wengine

2. Hao waotumwa kwa Eliya inaonekana walikuwa na nia mbaya kwake ndo maana waliangamizwa

So, kiufupi ni kwamba woote walifanya kosa ndo maana wakaangamizwa na si mtu mmoja kafanya kosa wakaangamizwa wengine
 
Yani hapo ndo unanivuruga kabisa. Mfano wewe unikosee halafu eti hata mtoto utakaemzaa nimchukie? ya nn sasa itakuwa sina utu ubinadamu

Sasa Mungu ana hekima kutuzidi sisi iweje aendelee kukomalia maovu waliotenda adamu na Hawa adhabu tupate sisi? Serious!! is not fair
Mkuu hii ipo hivi mnyororo huu hapa chini

Baba-yako-na-kaka-yako-wewe-watoto-wa-kaka-yako-watoto-wa-kwako

Familia hii ina vinasaba vya baba yako kama baba yako ametenda maovu damu ya cheni hii yote inahusika hata vyombo vya ndani vina husika lakini kama ukiamua kujitoa katika hili utakuwa umejiweka huru karibu na Mungu wako
Lakini ukiendelea kuwepo katika hii cheni laana haikuachi
Kwa hiyo fahamu kabisa uovu wako utasababisha laana kwa kizazi chako chote
 
Back
Top Bottom