Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

Hizo nyingine unazo sema zinaitwa taifa la Mungu? BWANA YESU/MUNGU alipokuja dunuani alizaliwa wapi? BETHLEHEM na YERUSALEMU ziko Misri AU MAKKA. Iko ISRAEL? Hekalu la Nabii Selemani? Liko SAUDIA? Mtume Muhamad SAW kwa nini hakushushiwa Quran Makka AU Madina? Akasema alishushiwa hapo JERUSALEM?
Mkuu..

Hebu nisaidie hapo uliposema Mtume Muhammad alisema alishushiwa Quran Jerusalem..

Sijaelewa..
 
Yesu alikuja kwao "wale walio kuwa wake hawakumpokea" (Wayahudi Taifa teule la Mungu), bali waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu wa aminio Jina lake. (Ndio watu wote wa dunia walio mpokea Bwana Yesu wakiwemo wakina Petro-Wayahudi).

Unajua maana ya Taifa Teule la Mungu?

Sio huenda Caanan aliwekwa katika laana ndivyo hivyo ilivyo. Ndio maana kuna taifa teule la Mungu ili kupitia hilo Mungu afanye ukuhani wake hapa duniani. Matendo ya Mungu hayo, ni makuu na ya ajabu.
Nini Maana ya Taifa Teule?..
 
Mtoto wa Gamba.

Kwanza sidhani asomae kama kitabu cha hadithi anaweza fikirisha akili akapata maswali ambayo hana majibu kupelekea kushirikisha wenziwe ili aeleweshwe..

Ukiona msomaji kaleta hoja kama hizi ujue hakusoma kama kitabu cha hadithi..

...
Kutokana na maelezo/hoja hizi ulizoweka hapa, Pia kuna mas
Ni

niajabu mkuu haki yake mwenye haki na uovu wake mwenye uovu kila mtu ahukumiwe kwa matendo yake laana mpaka kizazi cha nne ni hadaa tupu
MUNGU hachunguziki kwani ukisoma kitabu cha mwanzo 15;8-16 kipindi ambacho MUNGU anamwambia Abraham amtolee sadaka katika kuitoa ile sadaka Abraham anasinzia ikawa kama sababu angalau biblia haitaji kama kosa ambalo linapelekea kizazi chake cha 4 kitaenda utumwani miaka mia 4 kwaio hoja ya msingi kwamba BWANA MUNGU hachunguziki na anaweza kutumia ukamilifu wake kwenye namba ndomana ukisoma maandiko namba 7 inaonyesha ukamilifu wa jambo 4 inaonyesha ukamilifu wa vizazi 40 inaonyesha ukamilifu wa toba
 
Hakuna mwanadamu anayeweza kuwalaani wana wa Israeli na laana hiyo ikatokea au ikafanyakazi, hakuna... Lakini, MUNGU peke yake anaweza kuwalaani Waisraeli
Mwanzo 49
5 Simeoni na Lawi ni ndugu;Panga zao ni silaha za jeuri.
6 Nafsi yangu, usiingie katika siri yao,Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao,Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu,Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng?ombe;
7 Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali,Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma.Nitawagawa katika Yakobo,Nitawatawanya katika Israeli


Mkuu hapa vp mbona kuna waisrael wamelaaniwa hapa ama kwa kuwa imetoka kwa Muisrael mwenzao?? Ikiwa na maana muisrael akimlaani muisrael mwenzake its ok ila mtu asiye musirael akimlaani muisrael ndio haifanyi kazi??

Simply una maana waisrael ndio wenye haki pekee ya kulaani mtu??
 
Mwanzo 49
5 Simeoni na Lawi ni ndugu;Panga zao ni silaha za jeuri.
6 Nafsi yangu, usiingie katika siri yao,Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao,Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu,Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng?ombe;
7 Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali,Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma.Nitawagawa katika Yakobo,Nitawatawanya katika Israeli


Mkuu hapa vp mbona kuna waisrael wamelaaniwa hapa ama kwa kuwa imetoka kwa Muisrael mwenzao?? Ikiwa na maana muisrael akimlaani muisrael mwenzake its ok ila mtu asiye musirael akimlaani muisrael ndio haifanyi kazi??

Simply una maana waisrael ndio wenye haki pekee ya kulaani mtu??
Mkuu ukisoma mwanzo 49 unaona kwamba yakobo ambae ndo israel mwenyewe anawakusanya wanae anawaambia yatakayowatokea siku za mwisho angalau baraka haziwezi kuwa sawa ndomana hata YUSUPH na alipewa makabila mawili EFRAIMUnaMANASE na pia kama umekosea utapewa kinachostairi, lakini katika kule kuwa wana wa yakobo ni baraka tosha ndomanai wote waligawiwa nchi na YOSHUA walivyorudi kanani
 
hapo naona hii ni historia tu na kwenye historia error haiwezi kosekana aliyeleta huu ujumbe kwa mara ya kwanza inform of written document huenda alikoseaga na waliofuata kukopi maandishi haya either waliyadadavua na kuyatafsiri hivyo wakayaharibu zaidi na ndio mpaka sasa kuna mkanganyiko kwenye swala hili pia hapa huwezi pata jibu labda utafute vitabu vya kidini vya kale kabisa vyenye lugha mama ya kipindi hicho ndipo ujarbu kufanya translation kwa yaliyoandikwa hapo utapata jibu halisi

pamoja kiongozi zitto jr maada hii nzuri
 
Mkuu ukisoma mwanzo 49 unaona kwamba yakobo ambae ndo israel mwenyewe anawakusanya wanae anawaambia yatakayowatokea siku za mwisho angalau baraka haziwezi kuwa sawa ndomana hata YUSUPH na alipewa makabila mawili EFRAIMUnaMANASE na pia kama umekosea utapewa kinachostairi, lakini katika kule kuwa wana wa yakobo ni baraka tosha ndomanai wote waligawiwa nchi na YOSHUA walivyorudi kanani
Mkuu maelezo yako nimeyaelewa ila Son of Gamba alisema HAKUN mtu anaweza mlaani muisraeli yeyote na hiyo laana ikafanya kazi ndio nkamuuliza mbona Musiraeli Huyo lawi na shimeon walilaaniwa?? Yeye amesema wenye nguvu ya kulaani Israel ni MUNGU pekee ndio nikauliza je hapa Muisrael (LAWI) alipolaaniwa na baba yake ina maana waisraeli wanaweza kufanya kazi ya Mungu??

Hapo ndio sijamuelewa mkuu
 
hapo naona hii ni historia tu na kwenye historia error haiwezi kosekana aliyeleta huu ujumbe kwa mara ya kwanza inform of written document huenda alikoseaga na waliofuata kukopi maandishi haya either waliyadadavua na kuyatafsiri hivyo wakayaharibu zaidi na ndio mpaka sasa kuna mkanganyiko kwenye swala hili pia hapa huwezi pata jibu labda utafute vitabu vya kidini vya kale kabisa vyenye lugha mama ya kipindi hicho ndipo ujarbu kufanya translation kwa yaliyoandikwa hapo utapata jibu halisi

pamoja kiongozi zitto jr maada hii nzuri
Nimekusoma..... Pamoja sana mkuu
 
Mwanzo 49
5 Simeoni na Lawi ni ndugu;Panga zao ni silaha za jeuri.
6 Nafsi yangu, usiingie katika siri yao,Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao,Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu,Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng?ombe;
7 Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali,Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma.Nitawagawa katika Yakobo,Nitawatawanya katika Israeli


Mkuu hapa vp mbona kuna waisrael wamelaaniwa hapa ama kwa kuwa imetoka kwa Muisrael mwenzao?? Ikiwa na maana muisrael akimlaani muisrael mwenzake its ok ila mtu asiye musirael akimlaani muisrael ndio haifanyi kazi??

Simply una maana waisrael ndio wenye haki pekee ya kulaani mtu??
Duuh hii security sio ya kawaida
 
Ndio maana Mungu anasema anawalehemu maelfu elfu wampendao na kuzishika amri zake
Kwa mfano ukizaliwa katika familia inayo abudu sanamu dhambi ya familia itakuwa na wewe lakini ukiamua kuitafata kweli ukaifata kiroho umejitenga na uovu wa familia hiyo kwamaana hiyo utakuwa ni familia ya wana wa Mungu
I smell ignorance he ni mfumo fair kuumba gumfumo gwa kunisumbua kwa maovu ya baba wakati kila MTU atahukumiwa kivyake
 
Hebu ni saidie kwa nini nnangangania hapo temple mount? Kama sehemu muhimu ya kihistoria?
Japo umerudisha swali ntakusaidia kidogo..

Kushushwa kwa Quran na Kuhusu Habari ya Msikiti wa Al Aqsa ambao upo Jerusalem ni vitu viwili tofauti kabisa..

Quran imepokelewa Saudia si Jerusalem..
 
Mkuu zitto junior ili uweze kuelewa ni kwanini Nuhu alimlaani Caanan na siyo Ham aliyetenda kosa, kwanza unatakiwa ulielewa na kuliamini NENO la MUNGU. Ili ulielewe NENO la MUNGU, kwanza lazima uliamini. Binadamu hatuwezi kumwelewa MUNGU, lakini tunaweza kulielewa NENO lake ambalo ametupa ili litusaidie katika maisha ya sasa na yale yajayo.

Tatizo linakuja pale ambapo watu walio wengi hawataki kuielewa Biblia wala kuiamini, wengi wanaona kile kilichoandikwa kwenye Biblia ni kama hadithi tu, ni kama porojo tu ambazo hazina maana. Ukweli ni kwamba, Biblia ni zaidi ya hadithi, ni zaidi ya Historia, na ni zaidi ya Unabii ambao umekuwa ukitimia kila siku. Kwa kulitambua hili, mimi nitakupa majibu ya Kibiblia ni kwanini Nuhu alimlaani Caanani badala ya Ham. Majibu yote yapo ndani ya Biblia na nje ya Biblia huwezi kupata majibu.

Iko hivi; zamani zile Wazazi hasa baba walikuwa wanatoa baraka au laana kwa kizazi cha watoto wao na siyo kwa mtu mmoja peke yake. Kama ni baraka, baba alikuwa anatoa baraka hizi kwa watoto wake wa kiume na vizazi vyao vyote vinavyofuata kwa sababu walikuwa wanaamini kuwa kizazi hakiishii kwa watoto, bali kinaendelea na kuendelea. Pia huu ndiyo ulikuwa utaratibu waliojifunza kutoka kwa BWANA MUNGU, pale alipotoa laana ya kwanza kwa mwanadamu na nyoka;

"nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino". MWANZO 3:15

Hapo juu utaona hiyo laana siyo kwa Eva na nyoka peke yao, bali ni kwa uzao wao wote utakaotokea duniani. Hii inaonekana kuwa wazee wale wa kale walijifunza pia kutoa laana au baraka kwa kizazi na kizazi. Hebu tuone baraka ya Isaka kwa Yakobo.

"Mataifa na wakutumikie, na makabila wakusujudie. Uwe bwana wa ndugu zako, na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakaye kulaani, alaaniwe na atakayekubariki, abarikiwe". MWANZO 27:29

Hapa pia utaona Yakobo anabarikiwa na baba yake, tena siyo baraka kwa ajili yake tu katika maisha yake yeye kama Yakobo, bali ni kwa ajili yake na uzao wake wote utakaofuatia baada yake. Hivi ndivyo ilivyokuwa, hivi ndivyo wanadamu walijifunza kutoa baraka kwa wana wao au laana. Pia unaweza ukasoma kitabu hicho cha MWANZO sura ya 49, na utaona jinsi ambavyo na yeye Yakobo alivyotoa baraka kwa watoto wake 12.

Tukirudi upande wa BWANA MUNGU, pia tutaona jinsi alivyombariki mzee Ibrahimu, hakumbariki yeye tu kwa wakati ule, bali alimbariki yeye na uzao wake wote utakaofuatia baadaye.

"Nami nitakufanya wewe kuwa Taifa kubwa na kukubariki, na kulikuza jina lako nawe uwe baraka. Nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia zitabarikiwa". MWANZO 12:2-3

Mpaka hapa tutakuwa tumeona jinsi baraka na laana zilivyokuwa zinatolewa na inaonekana wazi kabisa namna ya kutoa baraka au laana, Wanadamu wa kale akiwemo mzee Nuhu walijifunza kutoka kwa MUNGU. Tukumbuke kuwa Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, na aliongea na MUNGU mara nyingi tu katika njozi na maono. Hivyo basi Hamu alipokosea kwa kumwangalia baba yake akiwa uchi na kumcheka, alilaaniwa Caanani ambaye alikuwa ni uzao wa Hamu, yaani kizazi chote cha Hamu kikawa kimelaaniwa.

Huo ndiyo ulikuwa utaratibu wa kutoa laana au baraka, tena ni utaratibu ambao ulikuwa na baraka zote toka kwa MUNGU. Caanan hakumcheka Nuhu, lakini alilaaniwa sababu yeye alikuwa ni uzao wa Hamu, Caanan alikuwa anabeba damu ya Hamu ndani yake na alipaswa kulaaniwa. Pia tukumbuke jinsi MUNGU alivyosema katika zile Amri kumi;

".........nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu". KUTOKA 20:5-6

Nuhu hakukosea kumlaani Caanan, nasema hakukosea sababu Nuhu alifuata utaratibu uliokuwepo. Utaratibu ambao hata BWANA MUNGU aliutumia kwa mara ya kwanza pale Eva alipokula matunda ya mti aliokatazwa asile. Tukihoji kwanini Nuhu Nabii wa MUNGU alimlaani Caanan kwa makosa ya baba yake, itakuwa kama tunataka kuhoji pia ni kwanini sisi leo hii tunabeba laana ya Eva na Adamu wakati siyo sisi tuliokula tunda. Nafikiri hakuna mwanadamu anayeweza kusimama na kumuuliza MUNGU kwanini ulifanya hivyo, kwanini ulitulaani sisi? (Soma ISAYA 45:9 au WARUMI 9:14-21)

MUNGU hakosei na wala MUNGU hamuonei mtu wala kumpendelea mtu. Nuhu alikuwa ni Nabii wa MUNGU, hivyo basi laana ya Nuhu kwa Caanan ilipata baraka zote toka kwa MUNGU. Kama Nuhu angekuwa ametoa laana kwa uonevu bila kufuata utaratibu unaokubalika na MUNGU; basi MUNGU asingekubali Caanan alaanike, angeizuia hiyo laana isitokee.

Nina imani kwa maelezo hayo, utakuwa umeelewa ni kwanini Caanan alibeba laana ya baba yake, tena siyo Caanan tu, bali ni yeye na uzao wake wote uliofuatia. Hata sisi Waafrika tunabeba laana hiyo mpaka leo, lakini tukumbuke kwamba MUNGU aliyetupiga kwa laana, ndiye YEYE huyo huyo aliyetuletea UKOMBOZI kupitia kwa Mwanawe YESU KRISTO.


"Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam Mimi ndiye, wala hapana MUNGU mwingine ila Mimi; naua Mimi, naponya Mimi, nimejeruhi tena nimeponya; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu". KUMBUKUMBU LA TORATI 32:39
Mkuu zitto junior hatuwezi kumwelewa MUNGU hata siku moja, akili zake, wala mawazo yake, hayachunguziki na Mwanadamu wala Malaika. Lakini tunaweza kulielewa NENO lake, kuliamini na kumtii Yeye kama MUUMBA wetu.
NA KWANINI AWE KAANI PEKE YAKE ILIHALI HAM ANAWATOTO WANNE. KWA NADHARIA YAKO HII LAANA ILIBIDI IENDE KWA WATOTO WOTE WA 4. SIO KWA KAANANI PEKE YAKE
 
Lakini caanan hakufa kwenye gharika!
According to Quran mkuu Kanaan alifia kwenye gharika baada ya kukataa kuingia kwenye safina ya Nuhu na akaishia kwenda milimani soma Surat Hud nzima utakuta habari za mkasa huu ila kibiblia Kanaan yupo baada ya gharika ila kikubwa Quran inasema kanaan alikuwa mtoto wa Nuhu yaani mtoto wa mke wa Nuhu hivo inaweza tupa mwanga zaidi ya canaan alitokea wapi?? So huenda ni kweli alikuwa baba yake ni Ham na mama yake ni mke wa Nuhu!!!! Kwa assumption ya sura hii ya Quran
 
Back
Top Bottom