Kwanini China bado inabaki ni kitendawili baada ya miaka 100

Kwanini China bado inabaki ni kitendawili baada ya miaka 100

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111337169773.jpg

Hivi majuzi tu Chama cha Kikomunisti cha China CPC kimesherehekea kutimiza miaka 100 tangu kiasisiwe mwaka 1949. Ambapo kililazimika kusubiri kwa miaka 28 hadi kuingia madarakani na toka hapo kimeongoza watu bilioni 1.4.

Katika miaka 100, chama na nchi imepitia vita vya wenyewe kwa wenyewe, mapinduzi ya kiutamaduni, mageuzi na ufunguaji mlango, China kurejeshewa Hong Kong na Macau na kumalizika kwa vita baridi.

Ukitembelea vijiji na miji mikubwa ya China kama vile Shanghai, utapata kuona nchini imefikia wapi. Licha ya zama za ustaarabu wa China, nchi inaonekana kuwa kitendawili kwa nchi za Magharibi na hata kwetu sisi pia. Kweli tunaweza kutegua kitendawili cha China?

Kama umesikiliza hotuba za viongozi wa China, basi kila mara utasikia wakitaja alama kubwa za siku za nyuma kama vile Ukuta Mkuu wa China. Nchi inapata msukumo wake kutokana na vitu vya nyuma.

Kama China imeweza kujilinda na wavamizi kwa kujenga ukuta wenye urefu wa kilomita 700, kweli itashindwa kuchukua hatua kama hiyo hivi leo, yaani kusimama kidete dhidi ya nchi za Magharibi?

Kwa miaka mingi China imekuwa na shida kadha wa kadha, kama vile vita vya kasumba na uvamizi wa Japan wakati wa Vita vya Pili vya Dunia. Inawezekana kuwa sasa imeazimia kuhakikisha kwamba matukio kama hayo hayarejei tena. Uhusiano wa China na matukio ya nyuma unaokena kwenye ujenzi wa makumbusho. Kwa kupata msukumo wa nyuma, China inakabili siku za mbele kwa kujiamini.

Ingawa wasomi wa Magharibi na wachambuzi wa sera wanaishutumu China kwa kuchagua vitu vizuri tu ambavyo vilisisitizwa zamani, lakini hawana tofauti na watu wengine. Kwa mfano sisi Wakenya tunasisitiza ukoloni lakini tunasahau ustaarabu mkubwa uliokuwepo kabla ya hapo. Kila jamii ya Wakenya ilikuwa na mfumo wake wa kisiasa na sheria ambao uliendelea kwa karne kadhaa. Lakini mfumo huo umeondolewa na ukoloni. Kwanini tusichanganye na utamaduni wetu?

China imefanya hivyo, imechanganya tamaduni zake na mambo ya kisasa. Wachina wanaongea Kichina cha Mandarini, Wachina wanaohamia nchi za Magaharibi mara nyingi wanachagua majina ya Kiingereza ili kutoa urahisi. Lakini hayo hayakuizuia China kurusha chombo cha anga ya juu na kutua kwenye mwezi. China sasa ni kiongozi wa akili bandia AI na sayansi za aina nyingine, hadi Wamarekani wameanzisha sheria maalumu ya kupambana na ukuaji wa kushangaza wa China.

Ukuaji wa China pia upo kwenye msingi wa kutumia sayansi na teknolojia. Hata viongozi nao pia wamo. Angalia historia ya marais wengi wa China akiwemo wa hivi sasa, wengi wao ni wahandisi au wanasayansi. Rais Xi Jinping amesomea uhandisi wa kemikali katika chuo kikuu cha Tsinghua. Wanafunzi wa China hawaendi nchi za magharibi kusomea elimu ya binadamu (anthropolojia) au sayansi ya siasa. Bali wanasomea sayansi, teknolojia, uhandisi, na hesabati (STEM) na kurejea nyumbani.

Wachina wanaonekana kujua kwamba masomo haya ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hesabati lazima yatakuwa na mhimili wa falsafa au itikadi.

Itikadi za magharibi zinasisitiza uhuru wa mtu binafsi, ambao umetekelezwa tangu kipindi cha kuchipuka upya. Lakini China ilifuata upande tofauti, kudhibiti maisha ya mtu binafsi ikiwa ni pamoja na idadi ya watoto wanaozaliwa. Hivi sasa imelegeza sheria hiyo ili kupata nguvu kazi za kukuza uchumi katika siku za mbele.

China inataka kuepuka mtego wa nchi za Magharibi wa kupunguza idadi ya watu, ambao imevuta wahamiaji. Kinachoifanya China iwe ni kitendawili ni kwamba wakati uchumi wake unapokuwa, tulitegemea na demokrasia itakua pia. Hilo halijatokea. China inaonekana kujua “hatari ya kuharakisha demokrasia” Mimi naona siku moja China itakuwa nchi ya kidemokrasia lakini sio katika wakati ambao tunautarajia.

Hatimaye, China inaonekana kwamba karibuni tu itakuwa nchi yenye nguvu kubwa duniani ikisaidiwa na mafanikio yake katika kugeuza wimbi la COVID-19. Lakini itafanya kwa kasi yake yenyewe, ambayo inaweza kufadhaisha juhudi za nchi za Magharibi na kupelekea kuipunguza kasi. Kwa nchi nyingine hasa za Afrika zinaweza kuiangalia China inavyoinuka na kujifunza kutoka kwake.
 
China tayri ni giant duniani hakuna wa kumstopisha hakuna wa kumuogopa ndyo maana marekani anaangaika Tu kuweka vikwazo kwenye makampuni yake Ila stage alivyofika China marekani kashachelewa maana teknolojia, ushawishi, pesa vyote amevishika na kibaya zaidi ni Kwa bei nafuu bidhaa zake unazipata
 
China tayri ni giant duniani hakuna wa kumstopisha hakuna wa kumuogopa ndyo maana marekani anaangaika Tu kuweka vikwazo kwenye makampuni yake Ila stage alivyofika China marekani kashachelewa maana teknolojia, ushawishi, pesa vyote amevishika na kibaya zaidi ni Kwa bei nafuu bidhaa zake unazipata
Ndio hivyo China ni Kama kariako ya dunia sasa hivi anahangaika kushik soko la semiconductor, akishaafanikwa basi TSMC ni lazim afunge kiwanda maa chip zitakuwa zinapatikana kwa bei rahis
 
View attachment 1852342
Hivi majuzi tu Chama cha Kikomunisti cha China CPC kimesherehekea kutimiza miaka 100 tangu kiasisiwe mwaka 1949. Ambapo kililazimika kusubiri kwa miaka 28 hadi kuingia madarakani na toka hapo kimeongoza watu bilioni 1.4.

Katika miaka 100, chama na nchi imepitia vita vya wenyewe kwa wenyewe, mapinduzi ya kiutamaduni, mageuzi na ufunguaji mlango, China kurejeshewa Hong Kong na Macau na kumalizika kwa vita baridi.

Ukitembelea vijiji na miji mikubwa ya China kama vile Shanghai, utapata kuona nchini imefikia wapi. Licha ya zama za ustaarabu wa China, nchi inaonekana kuwa kitendawili kwa nchi za Magharibi na hata kwetu sisi pia. Kweli tunaweza kutegua kitendawili cha China?

Kama umesikiliza hotuba za viongozi wa China, basi kila mara utasikia wakitaja alama kubwa za siku za nyuma kama vile Ukuta Mkuu wa China. Nchi inapata msukumo wake kutokana na vitu vya nyuma.

Kama China imeweza kujilinda na wavamizi kwa kujenga ukuta wenye urefu wa kilomita 700, kweli itashindwa kuchukua hatua kama hiyo hivi leo, yaani kusimama kidete dhidi ya nchi za Magharibi?

Kwa miaka mingi China imekuwa na shida kadha wa kadha, kama vile vita vya kasumba na uvamizi wa Japan wakati wa Vita vya Pili vya Dunia. Inawezekana kuwa sasa imeazimia kuhakikisha kwamba matukio kama hayo hayarejei tena. Uhusiano wa China na matukio ya nyuma unaokena kwenye ujenzi wa makumbusho. Kwa kupata msukumo wa nyuma, China inakabili siku za mbele kwa kujiamini.

Ingawa wasomi wa Magharibi na wachambuzi wa sera wanaishutumu China kwa kuchagua vitu vizuri tu ambavyo vilisisitizwa zamani, lakini hawana tofauti na watu wengine. Kwa mfano sisi Wakenya tunasisitiza ukoloni lakini tunasahau ustaarabu mkubwa uliokuwepo kabla ya hapo. Kila jamii ya Wakenya ilikuwa na mfumo wake wa kisiasa na sheria ambao uliendelea kwa karne kadhaa. Lakini mfumo huo umeondolewa na ukoloni. Kwanini tusichanganye na utamaduni wetu?

China imefanya hivyo, imechanganya tamaduni zake na mambo ya kisasa. Wachina wanaongea Kichina cha Mandarini, Wachina wanaohamia nchi za Magaharibi mara nyingi wanachagua majina ya Kiingereza ili kutoa urahisi. Lakini hayo hayakuizuia China kurusha chombo cha anga ya juu na kutua kwenye mwezi. China sasa ni kiongozi wa akili bandia AI na sayansi za aina nyingine, hadi Wamarekani wameanzisha sheria maalumu ya kupambana na ukuaji wa kushangaza wa China.

Ukuaji wa China pia upo kwenye msingi wa kutumia sayansi na teknolojia. Hata viongozi nao pia wamo. Angalia historia ya marais wengi wa China akiwemo wa hivi sasa, wengi wao ni wahandisi au wanasayansi. Rais Xi Jinping amesomea uhandisi wa kemikali katika chuo kikuu cha Tsinghua. Wanafunzi wa China hawaendi nchi za magharibi kusomea elimu ya binadamu (anthropolojia) au sayansi ya siasa. Bali wanasomea sayansi, teknolojia, uhandisi, na hesabati (STEM) na kurejea nyumbani.

Wachina wanaonekana kujua kwamba masomo haya ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hesabati lazima yatakuwa na mhimili wa falsafa au itikadi.

Itikadi za magharibi zinasisitiza uhuru wa mtu binafsi, ambao umetekelezwa tangu kipindi cha kuchipuka upya. Lakini China ilifuata upande tofauti, kudhibiti maisha ya mtu binafsi ikiwa ni pamoja na idadi ya watoto wanaozaliwa. Hivi sasa imelegeza sheria hiyo ili kupata nguvu kazi za kukuza uchumi katika siku za mbele.

China inataka kuepuka mtego wa nchi za Magharibi wa kupunguza idadi ya watu, ambao imevuta wahamiaji. Kinachoifanya China iwe ni kitendawili ni kwamba wakati uchumi wake unapokuwa, tulitegemea na demokrasia itakua pia. Hilo halijatokea. China inaonekana kujua “hatari ya kuharakisha demokrasia” Mimi naona siku moja China itakuwa nchi ya kidemokrasia lakini sio katika wakati ambao tunautarajia.

Hatimaye, China inaonekana kwamba karibuni tu itakuwa nchi yenye nguvu kubwa duniani ikisaidiwa na mafanikio yake katika kugeuza wimbi la COVID-19. Lakini itafanya kwa kasi yake yenyewe, ambayo inaweza kufadhaisha juhudi za nchi za Magharibi na kupelekea kuipunguza kasi. Kwa nchi nyingine hasa za Afrika zinaweza kuiangalia China inavyoinuka na kujifunza kutoka kwake.
Mnaongea habari za ushabiki technologically china hawajafika hata Kwa wajapan ila Kwa sababu tupo Africa na sisi tunatumia bidhaa zao sawa
 
Ofcourse ...USA kwa sasa hana pa kumshika CHINA kwa level aliyofika coz hawa jamaa ,,,soon wataliteka soko la dunia
GDP ya USA na china Hazifanani kaka kwenye maswala ya kijeshi Bado USA ni giant ila kinachonifikirisha Mimi sana ni wameweza vip kupiga hatua Kwa haraka
 
GDP ya USA na china Hazifanani kaka kwenye maswala ya kijeshi Bado USA ni giant ila kinachonifikirisha Mimi sana ni wameweza vip kupiga hatua Kwa haraka
Hujaelewa mkuu .......up to know bado USA ni Giant .......but tunasema ......kwa speed aliyonayo China ........sio mda atakuwa giant zaid ya USA
 
Hujaelewa mkuu .......up to know bado USA ni Giant .......but tunasema ......kwa speed aliyonayo China ........sio mda atakuwa giant zaid ya USA
Nimememuelewa lakin hata biashashara za china hizi zinazomfanya apige hatua over time ata face constraints nyingi
 
Kama Mmarekani anapata taabu kumdhibiti hakuna kitakacho mrudisha nyuma mchina
Watu wanashinndwa kuelewa watu ndo wanamfuata machina kwa Kuwa wanaona fursa ,kila kampuni ikiangalia ili iendelee kusurvive lazima ifikiria soko la China apple sio mjinga kwenda kuwekeza kule
 
GDP ya USA na china Hazifanani kaka kwenye maswala ya kijeshi Bado USA ni giant ila kinachonifikirisha Mimi sana ni wameweza vip kupiga hatua Kwa haraka
Bajati ya USA Kwenye sector ya heshi ni kwakuwa usa anautsources kazi nyingi za kijeshi lakin gharama za maisha ziko juu kwao ,kwa mfano gharam za kutengezeneza B-2 ni karibia usd 2b ilihali hiyo ndege ikitengenzewa china ni Kama usd 900m
 
Mnaongea habari za ushabiki technologically china hawajafika hata Kwa wajapan ila Kwa sababu tupo Africa na sisi tunatumia bidhaa zao sawa
Mkuu, teknolojia ya fani gani unayoizungumzia hasa? labda tuanzie hapo - ninacho kijuwa mimi ni kwamba, Uchina hipo nyuma kidogo kwenye teknolojia ya ku-master packing density kubwa za cmoses na bipolar kwenye size ndogo zaidi in terms of nanometers,as I said unlike:Japan,Taiwan(TMSC),Samsung na kampuni za Merikani zinazo zalisha semiconductors.

Tatizo linatokana kwamba kwa hivi sasa Wachina hawana mashine za ku-fabricate VLSIC zenye unene mdogo sana na packing density kubwa ya kufikia kiwango cha mataifa tajwa hapo juu, lakini hilo ni suala la muda tu nina uhakika ndani ya miaka mitano China ndio itakuwa inaongoza kwa uzalishaji mkubwa wa semiconductors za kiwango cha juu Duniani, watatafuta mbinu za kila aina kuunda mashine zao wenyewe badala ya kutegemea mashine za kutoka Japan na Merikani ambazo Serikali ya Merikani inaweka masharti magumu/kataza kuziuza uchina.

In short Uchina hivi sasa hipo mbali sana katika masuala ya sayansi na teknolojia,kiuchumi pamoja na kijeshi save uzalishaji wa semiconductors, lakini kama nilivyo sema tangu mwanzo hilo ni suala la muda tu lakini wata catch up eventually sooner than you think - my opinion.
 
Mkuu, teknolojia ya fani gani unayoizungumzia hasa? labda tuanzie hapo - ninacho kijuwa mimi ni kwamba, Uchina hipo nyuma kidogo kwenye teknolojia ya ku-master packing density kubwa za cmoses na bipolar kwenye size ndogo zaidi in terms of nanometers,as I said unlike:Japan,Taiwan(TMSC),Samsung na kampuni za Merikani zinazo zalisha semiconductors.

Tatizo linatokana kwamba kwa hivi sasa Wachina hawana mashine za ku-fabricate VLSIC zenye unene mdogo sana na packing density kubwa ya kufikia kiwango cha mataifa tajwa hapo juu, lakini hilo ni suala la muda tu nina uhakika ndani ya miaka mitano China ndio itakuwa inaongoza kwa uzalishaji mkubwa wa semiconductors za kiwango cha juu Duniani, watatafuta mbinu za kila aina kuunda mashine zao wenyewe badala ya kutegemea mashine za kutoka Japan na Merikani ambazo Serikali ya Merikani inaweka masharti magumu/kataza kuziuza uchina.

In short Uchina hivi sasa hipo mbali sana katika masuala ya sayansi na teknolojia,kiuchumi pamoja na kijeshi save uzalishaji wa semiconductors, lakini kama nilivyo sema tangu mwanzo hilo ni suala la muda tu lakini wata catch up eventually sooner than you think - my opinion.
Wako Kwenye 14nm .. kidogo kidogo tu wanaindia mwkani watakuwa 7nm which is enough to run any application
 
Mkuu, teknolojia ya fani gani unayoizungumzia hasa? labda tuanzie hapo - ninacho kijuwa mimi ni kwamba, Uchina hipo nyuma kidogo kwenye teknolojia ya ku-master packing density kubwa za cmoses na bipolar kwenye size ndogo zaidi in terms of nanometers,as I said unlike:Japan,Taiwan(TMSC),Samsung na kampuni za Merikani zinazo zalisha semiconductors.

Tatizo linatokana kwamba kwa hivi sasa Wachina hawana mashine za ku-fabricate VLSIC zenye unene mdogo sana na packing density kubwa ya kufikia kiwango cha mataifa tajwa hapo juu, lakini hilo ni suala la muda tu nina uhakika ndani ya miaka mitano China ndio itakuwa inaongoza kwa uzalishaji mkubwa wa semiconductors za kiwango cha juu Duniani, watatafuta mbinu za kila aina kuunda mashine zao wenyewe badala ya kutegemea mashine za kutoka Japan na Merikani ambazo Serikali ya Merikani inaweka masharti magumu/kataza kuziuza uchina.

In short Uchina hivi sasa hipo mbali sana katika masuala ya sayansi na teknolojia,kiuchumi pamoja na kijeshi save uzalishaji wa semiconductors, lakini kama nilivyo sema tangu mwanzo hilo ni suala la muda tu lakini wata catch up eventually sooner than you think - my opinion.
Brother unajua huja study swala la international trade practically solo la bidhaa za kichina ni Africa. Kwa miaka ya karibuni competition dhid ya wachina kuteka soko la ki Africa imekuwa kali mno mfano tuchukulie mfano wa automobile company china ameanza kuteka soko la magari Africa lakin hujasikia makampuni kama scania ford Mitsubishi Rover na wengineo tayari Wana sub branch za ku assamble magari Africa
 
Mkuu, teknolojia ya fani gani unayoizungumzia hasa? labda tuanzie hapo - ninacho kijuwa mimi ni kwamba, Uchina hipo nyuma kidogo kwenye teknolojia ya ku-master packing density kubwa za cmoses na bipolar kwenye size ndogo zaidi in terms of nanometers,as I said unlike:Japan,Taiwan(TMSC),Samsung na kampuni za Merikani zinazo zalisha semiconductors.

Tatizo linatokana kwamba kwa hivi sasa Wachina hawana mashine za ku-fabricate VLSIC zenye unene mdogo sana na packing density kubwa ya kufikia kiwango cha mataifa tajwa hapo juu, lakini hilo ni suala la muda tu nina uhakika ndani ya miaka mitano China ndio itakuwa inaongoza kwa uzalishaji mkubwa wa semiconductors za kiwango cha juu Duniani, watatafuta mbinu za kila aina kuunda mashine zao wenyewe badala ya kutegemea mashine za kutoka Japan na Merikani ambazo Serikali ya Merikani inaweka masharti magumu/kataza kuziuza uchina.

In short Uchina hivi sasa hipo mbali sana katika masuala ya sayansi na teknolojia,kiuchumi pamoja na kijeshi save uzalishaji wa semiconductors, lakini kama nilivyo sema tangu mwanzo hilo ni suala la muda tu lakini wata catch up eventually sooner than you think - my opinion.
Bado usisahau kuwa waafrica nao hajaridhika wanatafuta namba what if nchi za kiafrica zikawa industrialized machina atakuwa ktk position gan
 
Brother unajua huja study swala la international trade practically solo la bidhaa za kichina ni Africa. Kwa miaka ya karibuni competition dhid ya wachina kuteka soko la ki Africa imekuwa kali mno mfano tuchukulie mfano wa automobile company china ameanza kuteka soko la magari Africa lakin hujasikia makampuni kama scania ford Mitsubishi Rover na wengineo tayari Wana sub branch za ku assamble magari Africa
Mchina anauza bidhaa dunia nzima
 
Back
Top Bottom