Kwanini Comedians wa MIZENGWE wanapotezewa sana?

Kwanini Comedians wa MIZENGWE wanapotezewa sana?

Kwani Lazima kuiga kila kitu? Sababu Mr Bean kafanya vile imekua sheria kwamba hata wachekeshaji wabongo waige? Halafu Mr Bean ni vitendo wakati Hart ni maneno huoni kwamba unaji contradict mwenyewe vipi watu wasioelewa lugha anayotumia Hart(English). Unajidai wa mbele wakati unaishi Ombokoro
[emoji23] [emoji23]
 
Majibu yake ni marahisi kama siyo mepesi sana Mkuu....

Hawa ' Jamaa '....

  1. Hawajui ' kujipendekeza ' wala ' kujikomba ' kwa Mtu na hawaendekezi sana ' njaa '.
  2. Wanapambana sana na kujituma mno wenyewe.
  3. Hawataki kujihusisha na kuwa ' mabegi ' ya Drugs barons wa Tanzania kama wanavyofanyiwa wengine.
  4. Wanaridhika na kumshukuru Mwenyezi Mungu sana kwa chochote kile anachowapa kwa ' Jasho ' lao na kamwe hawapendi ' magumashi ' kama wenzao wengi.
  5. Tungo zao nyingi tena 100% ni za ukweli mtupu na usisahau kuwa 100% ya Watanzania hatupendi kuambiwa ukweli.
Ulichofanya hapa ni sawa na kupongeza Watu/Kikundi/Kampuni kwa poor PR.

Au mwisho wa mwaka una nusu ya bidhaa dukani zimeisha muda wake, alafu ukiulizwa unajisifu 'mimi huwa sihangaiki kutangaza biashara yangu, Wateja wasipokuja basi nakaa tu'.

Moja ya kazi za sanaa ni kuhabarisha, kama Redio, Magazeti n.k, sasa kuna haja gani kuchapisha Gazeti kila siku kama huna Wasomaji wa kutosha? ni lazima mfanye bidii ili jamii ijue uwepo wenu...kuwa maarufu sio lazima kutokane na kufanya mambo ya kijinga.

Milard Ayo hafanyi ujinga lakini ni jamii kubwa sasa wanafuatilia anachofanya, na ndio inamrahisishia kazi yake ambayo ni kuhabarisha...hata kundi la Sanaa lazima likuwe, liwe na Wafuatiliaji wengi wa ndani na nje ya nchi kadri inavyowezekana.

Watu kama kina Oprah walifika walipofika kwa kufanya bidii ya kufikia watu na sio kujifungia sehemu moja na kudhani kwamba audience ndio yenye wajibu wa kukutafuta.

Sio kila kitu ni cha kupongeza, poor PR ni uzembe na kukosa ubunifu...tuwahimize wakuwe...hakuna mtu anasema wafanye anachofanya Gigy money au Masogange ili ndio sanaa yao ijulikane, la hasha.
 
Jamaa wanajitahidi sana...haswa Sumaku ni moja Waigizaji wanaonivutia ndio maana huwa nafuatilia huu mchezo, ila nadhani Sumaku hatumiki fully kwa uwezo alio nao.

Huwa namsikia hata kwenye michezo mingi ya redio kwenye redio tofauti tofauti...kwa sasa kuna mchezo wa redio RFA namsikia unaitwa 'kumekucha' I think.

ILA UKWELI LAZIMA USEMWE JAPO NI MCHUNGU

Hawa jamaa wananikera sana...wapo hewani kwa muda mrefu, zaidi ya miaka kumi sasa kama sikosei lakini sioni maendeleo yoyote haswa kwenye sanaa wanayoifanya...production bado ni poor na ya kimasikini sana.

Inakera kuona kipindi kikongwe na waigizaji wakongwe wa kiwango kile kutengeneza mchezo unaohitaji kuonyesha tukio la siku tofauti na Waigizaji wanashindwa hata kubadili nguo..ile sio stage play, ingawa hata stage play wanafanya zaidi ya hapo.

Production kwa sehemu kubwa inafanywa nje (outdoor) kwa lengo kubwa la kukwepa gharama, haya si ya kufanywa na kundi kama lile tena wanaofanya kazi na TV kubwa kama ITV. Tatizo ni nini? vifaa? sasa kama wao inawashinda hao underground wataweza vipi iwapo watasema tunataka kuwa kama Mizengwe?

Kuna mdau hapo juu naona ameshauri waongezewe muda...nadhani ameshindwa kunotice kwamba jamaa hawana 'content' inayotosheleza, ubunifu unagotea hapo na kwamba wanategemea sana uwezo wa Muigizaji binafsi kusukuma muda, ndio maana utaona huwa wanavuta muda sana kabla kuanza kipindi ili walau wafikie muda..kile kipindi ni cha nusu saa kutoka tatu kamili au na dakika mpaka tatu na nusu, lakini hawajazi huo muda wewe unasema waongezewe.

Sasa sijui tatizo lao haswa ni nini, huwa mpaka najiuliza kama Mzee mengi kweli huwa anajali ni nini kinafanyika kwenye kampuni yake. Labda wanakosa washauri wazuri au wao wenyewe hawana cha kushauriana na kampuni yao (ITV)

Sifa kuu ya binadamu/kazi/biashara yoyote ni kukua kutoka ulivyokuwa awali, hata binaadamu asiye 'grow' hana lolote la kufunza wengine.....Wanaofuatilia Isidingo hapa hebu waniambie jinsi inavyoenda ikibadilika, sio lazima waigizaji wabadilishwe lakini walau production, mandhari n.k.
Umeeleza changamoto zao vzur vipi sasa solutions ?
 
Baada ya Uzi huu naamini idadi ya wafuatiliaji wa kipindi itaongezeka
 
Umeeleza changamoto zao vzur vipi sasa solutions ?
Ukisoma vizuri nilichoeleza kama tatizo ndicho kinachotakiwa kurekebishwa.

Wajipe muda wa kutosha kuandaa kazi zao, wafanye mazoezi ya kutosha (rehearsal), Waboreshe production...huwezi kuniambia hata tu kubadili costume ili kuashiria scene ni ya siku nyingine inahitaji ushauri wa Watu wengine ili hali wao ni Wasanii wa muda mrefu.

Mtu yoyote ukifuatilia michezo yao unagundua kabisa 'wanalipua' kwa maana ya production na muda...au basi watuambie changamoto zinazowakabili ili tuelewe kabisa, otherwise ni ngumu sana kuwaelewa tatizo lao ni nini.
 
Ulichofanya hapa ni sawa na kupongeza Watu/Kikundi/Kampuni kwa poor PR.

Au mwisho wa mwaka una nusu ya bidhaa dukani zimeisha muda wake, alafu ukiulizwa unajisifu 'mimi huwa sihangaiki kutangaza biashara yangu, Wateja wasipokuja basi nakaa tu'.

Moja ya kazi za sanaa ni kuhabarisha, kama Redio, Magazeti n.k, sasa kuna haja gani kuchapisha Gazeti kila siku kama huna Wasomaji wa kutosha? ni lazima mfanye bidii ili jamii ijue uwepo wenu...kuwa maarufu sio lazima kutokane na kufanya mambo ya kijinga.

Milard Ayo hafanyi ujinga lakini ni jamii kubwa sasa wanafuatilia anachofanya, na ndio inamrahisishia kazi yake ambayo ni kuhabarisha...hata kundi la Sanaa lazima likuwe, liwe na Wafuatiliaji wengi wa ndani na nje ya nchi kadri inavyowezekana.

Watu kama kina Oprah walifika walipofika kwa kufanya bidii ya kufikia watu na sio kujifungia sehemu moja na kudhani kwamba audience ndio yenye wajibu wa kukutafuta.

Sio kila kitu ni cha kupongeza, poor PR ni uzembe na kukosa ubunifu...tuwahimize wakuwe...hakuna mtu anasema wafanye anachofanya Gigy money au Masogange ili ndio sanaa yao ijulikane, la hasha.

Likes nilizopata tu kwa nilichokiandika na ambazo hadi sasa zinazidi tu kumiminika na zimefikia 25 zinapingana na aina ya ' u.p.u.m.b.a.v.u. ' wako wa ' kutukuka ' uliouandika hapa na sishangai ndiyo maana tokea uandike huu ' uharo ' wako hadi sasa hujapata ' like ' hata moja tu. Na ukiona Mtu hanielewi nini huwa naandika humu JF jua anastahili kuwepo Hospitali ya Wagonjwa wa ' akili ' ya Mirembe Mkoani Dodoma.
 
Kwani tanzania kuna Comedian?
hahaaaaa wajifunze kwa wenzao basi
sio kuchekesha maneno bali vitendo. kama maneno kwa asiejua lugha hiyo je?
hawaoni wanavochekeaha wenzao kina Mr Bean kina Chaplain au Kelvn Hart...
ndomaana me siangaliagi utumbo huo wa Mizengwe nk.
Kevin Hart huwa haongei mkuu? Au huyo wa Nanjilinji?!
 
Kwani tanzania kuna Comedian?
hahaaaaa wajifunze kwa wenzao basi
sio kuchekesha maneno bali vitendo. kama maneno kwa asiejua lugha hiyo je?
hawaoni wanavochekeaha wenzao kina Mr Bean kina Chaplain au Kelvn Hart...
ndomaana me siangaliagi utumbo huo wa Mizengwe nk.
Utumwa wa akili na kuwa brainwashed na umagharibi ni kitu kibaya sana!
 
Likes nilizopata tu kwa nilichokiandika na ambazo hadi sasa zinazidi tu kumiminika na zimefikia 25 zinapingana na aina ya ' u.p.u.m.b.a.v.u. ' wako wa ' kutukuka ' uliouandika hapa na sishangai ndiyo maana tokea uandike huu ' uharo ' wako hadi sasa hujapata ' like ' hata moja tu. Na ukiona Mtu hanielewi nini huwa naandika humu JF jua anastahili kuwepo Hospitali ya Wagonjwa wa ' akili ' ya Mirembe Mkoani Dodoma.
Sidhani kama likes ni kiashiria kuwa ulichoongea ni cha maana au ndio ukweli...kama nipo kwenye show ya ya Afande alafu akavua nguo na uwanja mzima ukashangilia kasoro mimi haimaanishi kuwa alichofanya ni sahihi.

We ukihara watu wakakushangilia basi ndio unaongeza bidii mpake udhurike msamba?...nani kakwambia huko kushangilia kunamaanisha unafanya cha maana?

Usiogope kusema ukweli kwa kuhofia kukosa likes...na msimamo wangu ni ule ule huwezi kusifia poor PR kama ushujaa, lazima muwahimize Wenzenu wajitangaze wafike mbali..wawe 'talk of the town'
 
Majibu yake ni marahisi kama siyo mepesi sana Mkuu....

Hawa ' Jamaa '....

  1. Hawajui ' kujipendekeza ' wala ' kujikomba ' kwa Mtu na hawaendekezi sana ' njaa '.
  2. Wanapambana sana na kujituma mno wenyewe.
  3. Hawataki kujihusisha na kuwa ' mabegi ' ya Drugs barons wa Tanzania kama wanavyofanyiwa wengine.
  4. Wanaridhika na kumshukuru Mwenyezi Mungu sana kwa chochote kile anachowapa kwa ' Jasho ' lao na kamwe hawapendi ' magumashi ' kama wenzao wengi.
  5. Tungo zao nyingi tena 100% ni za ukweli mtupu na usisahau kuwa 100% ya Watanzania hatupendi kuambiwa ukweli.
uchambuzi safi..
 
Ulichofanya hapa ni sawa na kupongeza Watu/Kikundi/Kampuni kwa poor PR.

Au mwisho wa mwaka una nusu ya bidhaa dukani zimeisha muda wake, alafu ukiulizwa unajisifu 'mimi huwa sihangaiki kutangaza biashara yangu, Wateja wasipokuja basi nakaa tu'.

Moja ya kazi za sanaa ni kuhabarisha, kama Redio, Magazeti n.k, sasa kuna haja gani kuchapisha Gazeti kila siku kama huna Wasomaji wa kutosha? ni lazima mfanye bidii ili jamii ijue uwepo wenu...kuwa maarufu sio lazima kutokane na kufanya mambo ya kijinga.

Milard Ayo hafanyi ujinga lakini ni jamii kubwa sasa wanafuatilia anachofanya, na ndio inamrahisishia kazi yake ambayo ni kuhabarisha...hata kundi la Sanaa lazima likuwe, liwe na Wafuatiliaji wengi wa ndani na nje ya nchi kadri inavyowezekana.

Watu kama kina Oprah walifika walipofika kwa kufanya bidii ya kufikia watu na sio kujifungia sehemu moja na kudhani kwamba audience ndio yenye wajibu wa kukutafuta.

Sio kila kitu ni cha kupongeza, poor PR ni uzembe na kukosa ubunifu...tuwahimize wakuwe...hakuna mtu anasema wafanye anachofanya Gigy money au Masogange ili ndio sanaa yao ijulikane, la hasha.
mkuu mizengwe inafuatiliwa sana, haswa na watu wazima na wanaojielewa mara nyingi nikiwa ofisini au kwenye mizunguko yangu siku ya jumatatu hua nasikia wakisemwa kwa kazi nzuri wanayofanya siku ya jumapili.. Kitu kinachofanya hawa jamaa wasivume ni kutokuwa active kwenye social network.. ie instagram, facebook, twitter.. Kazi wanafanya vizuri na Tanzania hakuna wacheshi wa ukweli na wazuri kama hawa, udhaifu wao wamekosa management nzuri ya kuwapa kiki, na kuwaweka katika high classic ila wanafuatiliwa sana na watu(VIPAJI WANAVYO VIKUBWA SANA ZAIDI YA WALE WAVAA MAWIGI NA KUJIPAKA WANJA MADUME WAZIMA)
 
mkuu mizengwe inafuatiliwa sana, haswa na watu wazima na wanaojielewa mara nyingi nikiwa ofisini au kwenye mizunguko yangu siku ya jumatatu hua nasikia wakisemwa kwa kazi nzuri wanayofanya siku ya jumapili.. Kitu kinachofanya hawa jamaa wasivume ni kutokuwa active kwenye social network.. ie instagram, facebook, twitter.. Kazi wanafanya vizuri na Tanzania hakuna wacheshi wa ukweli na wazuri kama hawa, udhaifu wao wamekosa management nzuri ya kuwapa kiki, na kuwaweka katika high classic ila wanafuatiliwa sana na watu(VIPAJI WANAVYO VIKUBWA SANA ZAIDI YA WALE WAVAA MAWIGI NA KUJIPAKA WANJA MADUME WAZIMA)
Ni vizuri kusikia wanafuatiliwa kwani hata mimi nimfuatiliaji ndio maana nimeona niainishe yale ninayodhani ni mapungufu yanayoonekana wazi yapo ndani ya uwezo wao iwapo tu watatulia.

Na ningetamani nione wamekuwa wakubwa na kujulikana mbali kuliko ilivyo sasa.

Wasijifungie tu na kukubali sifa za kuwa wao hawajishughulishi kutafuta umaarufu/audience...sio sifa nzuri hata kidogo hiyo..asikwambie Mtu msanii yeyote moja ya sifa yake kuu ni kujulikana/kupendwa na kuwa midomoni mwa Watu wengi kadri inavyowezekana, na hilo ni jukumu lao na si la mwingine yeyote kwani hata manufaa watakayopata yatabaki kuwa ni ya kwao.
 
Majibu yake ni marahisi kama siyo mepesi sana Mkuu....

Hawa ' Jamaa '....

  1. Hawajui ' kujipendekeza ' wala ' kujikomba ' kwa Mtu na hawaendekezi sana ' njaa '.
  2. Wanapambana sana na kujituma mno wenyewe.
  3. Hawataki kujihusisha na kuwa ' mabegi ' ya Drugs barons wa Tanzania kama wanavyofanyiwa wengine.
  4. Wanaridhika na kumshukuru Mwenyezi Mungu sana kwa chochote kile anachowapa kwa ' Jasho ' lao na kamwe hawapendi ' magumashi ' kama wenzao wengi.
  5. Tungo zao nyingi tena 100% ni za ukweli mtupu na usisahau kuwa 100% ya Watanzania hatupendi kuambiwa ukweli.
You nailed it Mkuu[emoji16]
 
Sidhani kama likes ni kiashiria kuwa ulichoongea ni cha maana au ndio ukweli...kama nipo kwenye show ya ya Afande alafu akavua nguo na uwanja mzima ukashangilia kasoro mimi haimaanishi kuwa alichofanya ni sahihi.

We ukihara watu wakakushangilia basi ndio unaongeza bidii mpake udhurike msamba?...nani kakwambia huko kushangilia kunamaanisha unafanya cha maana?

Usiogope kusema ukweli kwa kuhofia kukosa likes...na msimamo wangu ni ule ule huwezi kusifia poor PR kama ushujaa, lazima muwahimize Wenzenu wajitangaze wafike mbali..wawe 'talk of the town'

Sioni kwanini nipoteze muda na Wewe wakati hata ID yako tu inatosha kueleza kuwa hata nifanyeje huwezi kunielewa hasa ukizingatia kuwa Wewe ni ' fyatu ' kweli.
 
Back
Top Bottom