Kwanini CWT inatesa Waalimu na kuiba fedha zao kila uchao?

Kwanini CWT inatesa Waalimu na kuiba fedha zao kila uchao?

JET SALLI

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2014
Posts
2,392
Reaction score
1,578
Ndugu za wanaJamiiForums, nimepata taarifa leo hii kwamba kumbe CWT ambacho kimekuwa chama cha walimu kwa muda mrefu sasa kimepata chama mwenza ambacho ni chama cha CHAKUHAWATA. Taarifa hii nimeambiwa na mwalimu mmoja leo hii.

Mwalimu huyo amesikitika kuona kwamba pamoja na yeye kujiungana na chama kipya cha CHAKUHAWATA eti amekatwa mara mbili kwa maana ya kwamba CWT wamemkata na CHAKUHAWATA wamemkata, mwalimu amedai kwamba sheria mpya ya Ajira na mahusiano kazini inampa mtumishi nafasi ya kuchagua chama cha wafanyakazi anachotaka yeye ili kujiunga nacho na si kuchaguliwa chama au kulazimishwa kujiunga na chama fulani.

Ameendelea kusema kwamba hakuna sheria inayomruhusu Afisa Utumishi kupitisha makato ya aina mbili kwa chama cha wafanyakazi bila ridhaa ya mwajiriwa

Sasa nasikia leo mishahara ya walimu na watumishi wengine imetoka lkn cha kushangaza wale walimu waliojiunga na chama kipya cha CHAKUHAWATA wamekatwa na CWT kinyume na Sheria za Utumishi.

Hebu Basi tunaojua kudadavua hizi Sheria za utumishi mtusaidie tupate Elimu kidogo au kwa upana zaidi maana JamiiForums ni kisima cha great thinkers.
 
CWT wanalindwa na Serikali ya CCM! Ukiwauliza kwa nini mpaka leo wanawakata walimu 2% ya basic salary zao, hawana majibu ya kueleweka! Wizi mtupu.

Yaani kila mwanachama eti anakatwa kulingana na mshahara wake, tena ule ghafi! kana kwamba wenye makato makubwa ndiyo wanatetewa zaidi! Kumbe ni wizi tu. Hela nyingi wanazitumia kulipana posho! Msaada kwa walimu ni 0!

CWT ni takataka tu 🚮
 
Kwa sababu waalimu wamekubali kuliwa hela zao kimasihara. Hakuna watu waoga kama waalimu wa Tanzania. Imagine hata mjumbe wa CCM wa kijiji akija shuleni waalimu matumbo joto
 
Hicho ni chanzo cha ulaji la kundi fulani ili liendelee kuwepo na kuhakikisha walimu wanadhibitiwa na kutumika.
 
Hela za cwt ndio zinasaidia kile chama cha kijani muda wa kuiba kura na kufanya chochote kubakia madarakani
 
Mtumishi ana haki ya kujiunga na chama chochote cha wafanyakazi kwa hiari yake bila kushurutishwa hivyo ni haki yako ya msingi kuchagua kati ya Cwt au chakamwata na unapaswa kukatwa mara moja tu na sio mara mbili

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Ukitaka kujiunga na chama kingine hakikisha makato ya kwanza yamesitishwa.

Fuatilia, kama ulipeleka fomu ya kuzuia CWT kukata na nakala unayo shitaki afisa utumishi.

Atakuwa amefanya uzembe au njama ovu kwako.
 
Ushauri kwa walimu,ikiwa sheria iko wazi namna kama ilivyo Basi ni wazi kabisa kwamba Afisa utumishi atakayeingiza makato mara mbili Basi huyo ni kilaza aliye ofisin asiye na uwezo wa kutafsiri Sheria na hivyo ni mzigo kwa Serikali na hivyo hatoshi kwenye nafasi hiyo.
 
Ndugu za wanaJamiiForums, nimepata taarifa leo hii kwamba kumbe CWT ambacho kimekuwa chama cha walimu kwa muda mrefu sasa kimepata chama mwenza ambacho ni chama cha CHAKUHAWATA. Taarifa hii nimeambiwa na mwalimu mmoja leo hii.

Mwalimu huyo amesikitika kuona kwamba pamoja na yeye kujiungana na chama kipya cha CHAKUHAWATA eti amekatwa mara mbili kwa maana ya kwamba CWT wamemkata na CHAKUHAWATA wamemkata, mwalimu amedai kwamba sheria mpya ya Ajira na mahusiano kazini inampa mtumishi nafasi ya kuchagua chama cha wafanyakazi anachotaka yeye ili kujiunga nacho na si kuchaguliwa chama au kulazimishwa kujiunga na chama fulani.

Ameendelea kusema kwamba hakuna sheria inayomruhusu Afisa Utumishi kupitisha makato ya aina mbili kwa chama cha wafanyakazi bila ridhaa ya mwajiriwa

Sasa nasikia leo mishahara ya walimu na watumishi wengine imetoka lkn cha kushangaza wale walimu waliojiunga na chama kipya cha CHAKUHAWATA wamekatwa na CWT kinyume na Sheria za Utumishi.

Hebu Basi tunaojua kudadavua hizi Sheria za utumishi mtusaidie tupate Elimu kidogo au kwa upana zaidi maana JamiiForums ni kisima cha great thinkers.
Walimu Hawa wanaodai 2025 ni Samia
Wacha waibiwe tu
 
WAJINGA+HAWANA UMOJA.

KAMA ANAYEKUIBIA UNAMUONA TENA MKIKUTANA UNAMCHEKEA, WEWE SIO MJINGA?
 
Kiuhalisia walimu wengi waoga. Yaani hata wakitembelewa na afisa utamaduni wa kata, wanahaha sana. Sheria iko wazi kujiunga na chama ni hiari lakin wakifika kwa mkurugenzi ni kutetemeka tu na kusaini bila kuhoji wala kuhitaji elimu ya chama cha cwt. Hili kundi linalofundsha wanafunzi wajiamini ndo lilistahili kufundishwa kwanza kujiamini.
 
CWT kiliwekwa kudhibiti walimu... Serikali haiwezi kutaka kuona walimu wana chama cha wafanyakazi chenye ngubu.

Walimu mpaka leo ndio wanaongoza kwa kunyonywa na mabenki na taasisi za kifedha za kihuni wakati wana benki yao
 
Watu wako ktk ofisi za serikali na hawawez kutafsiri sheria za nchi,je wanafaa kwa kitu gani.
 
LEO NIMEPATA TAARIFA kutoka huko SUMBAWANGA MANISPAA kwamba ETI BAADHI YA WALIMU waliojitoa CWT AFISA UTUMISHI WA MANISPAA YA SUMBAWANGA ameingiza MAKATO MARA MBILI katika mishahara yao yaani CWT wamekata Fedha na CHAKUHAWATA wamekata Fedha na baada ya walimu hao kufuatilia, Mkurugenzi anadai CWT wamepeleka waraka mpya kutoka ofisi ya mwanasheria Mkuu wa serikali.WITO wangu kwa serikali hebu wasaidieni walimu wanateseka sana,wengi wao Wana mishahara midogo sana,kama Sheria ziko wazi Basi Sheria zilizotungwa na Bunge ziheshimike na kama tuna tuna Afisa utumishi kama huyo wa kule Sumbawanga ambaye hawezi kutafsiri sheria Basi tumfukuze kazi.Wale wajuvi wa sheria Toeni ufafanuzi wa kina watu pamoja na walimu waliomo humu jamii forum waelewe ili wasiendelee kuonewa.
 
KWA WATU WA SERIKALI MLIOMO HUMU JAMII FORUM ni kwa nn walimu wanaendelea kuteseka na wanaendelea kukatwa mishahara ya na vyama viwili Kule Sumbawanga hii kitu inaendelea.Serikali fuatilieni kule Sumbawanga Kuna kitu cha hovyo kinaendelea kule.walimu wanaendelea kukatwa
 
Back
Top Bottom