Kwanini dini zinazataka wanawake kuvaa vitambaa kufunika vichwa vyao?

Kwanini dini zinazataka wanawake kuvaa vitambaa kufunika vichwa vyao?

Sababu ya msingi ni kuihifadhi jamii na maovu, machafu na udhalilishaji wa kijinsia dhidi ya mwanamke, take an example ya jamii yetu, kwa asilimia kubwa sana wanawake wanaojihifadhi kwa kufunika kichwa wanaheshimika na wapo mbali na maudhi kutoka kwa vijana wa hovyo kama mlima ufuta, vishu mtata na uhurumoja, angalia watawa wa kikatoliki na wengine wenye kuficha vichwa vyao.

Imeandikwa kuwa mwili wa mwanamke ni pambo kwa mwanaume ko hata nywele pia ni sehemu ya pambo, na ndio maana si ajabu kukuta kijana amemzimikia mdada kwa kumuona na wigi au brichi ya pacome, au aina nyingine ya nywele.
 
Ko wewe

kwa akili yako unaamini hayo maneno ya philosopher???
Na kama ni ndio basi wewe ni mjinga wa kiwango cha international standard!
Kwa hiyo tusiwaamini wenye scientific proof Bali tumwamini ambaye hakusoma aliyekuwa anatoa ndoto na kusema imeshushwa?
 
Katika maandiko ya dini zote tatu za Uisalamu, Ukristo na Uyahudi suala la wanawake kujifunika vichwa vyao linazungumziwa japo kwa msisitizo tofauti.

Katika Ukristo mazingatio yake ni madogo sana mfano kwa masista wa Kikatoliki na kwa makanisa machache mfano kwa Kakobe, katika Uyahudi siku hizi msisitizo umebaki kwa wanawake kufunika kichwa katika ibada tu, kwa upande wa Uislamu hilo bado ni jambo muhimu sana na tena kwenye nchi nyingine ni shurti kabisa.

Kwa nini mungu katika hizi dini na maandiko yake aliweka hayo maelekezo na sababu za msingi hasa ni zipi?
Katika Ukristo kuna mahali pia inamtaka Mwanamke asalipo basi sharti afunike kichwa....ni katika Agano jipya
 
Sikia hivi mie kwa ufahamu wangu . Mi mkristo tunaambiwa tukiingia nyumbani mwa bwana tunatakiwa tujisitiri , tuvae nguo za heshima na tufunike vichwa vyetu tukiwa kanisani
 
Vijana mukishiba munaongea upuuzi ili muonekane kama mumesoma sana ila hebu nikuambie kitu Muogope sana Mungu uhai usikupe kibri
Unamaanisha Mungu yupi? Maana Kila dini Ina Mungu mwenye sifa tofauti na Mungu wengine

🔹 Mungu wa waarabu ni mwenye hasira , anayewaamrisha watu wake walipe kisasi ( khum il kisasa) ambaye hutegemea wafuasi wake kumpigania, Ambaye anawaamrisha wafuasi wake waachinje walioiasi dini hiyo ( murtad), anayetaka kueineza dini hiyo kwa nguvu na anayekataa alipishwe Kodi (Jizya), anayewaahidi wafuasi wake wanaume mabikira 72 wa kufanya nao uasherati huko wanapopaita ( jahna) pamoja na kuelewa chakari kwenye mito ya pombe. Ambapo kwake Majini bado ni waamini na wanasali pamoja na Wana ushirika na binaadamu wanaomfuata

🔹 Kuna Mungu Mwingine aitwaye Jehova ambaye anawaamrisha watu wake amani, na kuwakataza kulipa kisasa (samehe mara Saba sabini, mtu akikupiga shavu la kushoto usimrudishie), Mungu anayejiita ana nguvu, ni Mungu wa MAJESHI, wafuasi wake ndio humtegemea na Wala sio wafuasi wake humpigania yeye, Kwake hata wanaomfuasa wakimwacha hakuna kipengele Cha kumuua,Kwake yeye hata usipomfuata maelekezo yake hulipishwi Kodi, Kwenye mbingu yake hakuna kuoa Wala kuolewa ,hakuna uasherati Wala ulevi na yeye Kwake Majini yote ni mashetani yanasubiri kichomwa moto wa milele baada ya kumegeka kutoka kundi la malaika kwa kutokumtii Mungu.

BOSI NI MUNGU GANI ULIYEMZUNGUMZIA KATI YA HAO WAWILI WENYE SIFA TOFAUTI NA ZINAZOKINZANA?
 
Kwa hiyo tusiwaamini wenye scientific proof Bali tumwamini ambaye hakusoma aliyekuwa anatoa ndoto na kusema imeshushwa?
dini ni imani ya uwepo wa Mungu asiyeonekana na mwezeshaji wa ulimwengu na vilivyomo.

Kama unaamini kwenye dini, hao wanafalsafa hawana nafasi kiimani, ila wewe utawafuata kwa self interests.
 
Uhalisia ni kwamba kichwa kiasili sio rahisi kukaa wazi , aidha kiwe na nywele nyingi na kusukwa , kubandikwa mawigi , au kufunika .Kiufupi hakifai kuonekena ile shape yake yote kama wanaume ambao wananyoa mpaka upara.

Kisogo cha mwanamke na shape ya kichwa havitakiwi kuonekana tangu enzi za zamani.
 
Kwanini malaya wanaojiuza husuka nywele na kuziachia? Hilo ndio jibu... Huenda wanaume wakiona ka unywele wanafuata...
 
Kichwa cha mwanamke ni mume wake.

1 Wakorintho 11
3. Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.

Hakiongelewi kichwa hiki cha physically
Vipi wasokuwa na waume, kwa sababu yoyote ile?
 
Kufunika kichwa mpaka miguu itakusaidia nini kama huzishiki Amri za MUNGU?

Muhimu kuliko yote, kwanza shika Amri za MUNGU, kisha jisitiri kwa kufunika kichwa mpaka miguu yako.
 
Sio dini ni Mila na tamaduni za ki babarism za za kiyahudi na kiarabu ambazo kimsingi ni Mila za eneo Moja ambazo dini Tatu za kiyahudi, kiislamu na Kikristu zilichipukia.Mila hizo kwa kuwa ziliibuka katika kipindi Cha babarism ambapo mwanamke alionekana sio binaadamu sawa na mwanaume Bali ni Mnyama kazi anayeongea (Instrumentum vocale)

Basi mabwana walioleta Imani hizo walikuwa na hayo mamila Yao ambayo kimsingi yanagandamiza Sana haki za wanawake hata kwenye nyumba za ibada hawatakiwi wawe viongozi wasimame mbele ya wanaume.
Ndiyo maana hata mitume wa yeah hayupo ambaye ni mwanamke
 
Back
Top Bottom