Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Mkurugenzi wa Mashtaka amepewa dokezo kuwa kuna uhalifu umefanyika na ni uhalifu ambao unagusa taasisi mbalimbali nyeti na hata watu ambao tunaweza kusema ni watu maarufu. Tuhuma ambazo zimetolewa jana si ngeni lakini kilichodokezwa zaidi ni madai kwamba kilichofanyika hakikuwa wizi wa ulaghai tu bali ulikuwa ni uhalifu dhidi ya uchumi na taasisi zetu. Hivyo ameombwa kuchunguza na kuleta mashtaka.
Nimeambatanisha hapa sheria mbili (kwenye sheria ya NPS angalia ibara hasa ya 16) na nyingine mtu anaweza kujisomea kuwa hakuna mtu mwenye uwezo na madaraka ya kuleta uchunguzi wa kihalifu (criminal investigation) kama Feleshi. Aangalie ushahidi uliopo na aliambie Taifa kuwa hakukuwa na uhalifu wowote uliofanyika na kama hakuna uhalifu wale wote wanaohusishwa na Kagoda warudishiwe 'fedha zao'. ..
Soma pia Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal
Kwa ufupi.. Feleshi alitakiwa kufanya haya yote yeye mwenyewe na binafsi naamini anatakiwa kumteua Public Prosecutor chini ya article 22 ya NPSA. Sheria ya Anti-Money Laundering nayo imeambatanishwa kuwasaidia watu kupima madai yaliyotolewa..
Ndugu zangu, kama Feleshi angekuwa anatumia madaraka yake ipasavyo kusingekuwa na haja za kina Hosea na Kamati Teule. Binafsi ninaamini mmoja watu ambao kutokana na madaraka yake amekuwa ni sehemu iliyohalalisha kukua na kukomaa kwa ufisadi nchini. Nimewahi kuandika hili kwa kirefu huko nyuma na katika Kagoda tunalirudia tu kwani angekuwa ni mtu anayetumia madaraka yake vizuri na ipasavyo hata tume ya EPA isingeundwa wala Luhanjo asingemchunguza Jairo!
Wakati umefika wa kuanza kutaka huyu jamaa aliyeapa kufanya kazi hii aaifanye kama hawezi ni bora ajiuzulu ili mtu mwingine mwenye nia na uwezo wa kusimamia sheria zetu kufanya kazi hiyo.
Kama yeye mwenyewe anaona hawezi kuchunguza jambo hili au anaona kwamba hawezi kuwa impartial ana uwezo wa kumchagua independent prosecutor kufanya uchunguzi - kuanzia na hizi nyaraka zilizowekwa jana - na hatimaye kuleta mashtaka yapasayo.
Nimeambatanisha hapa sheria mbili (kwenye sheria ya NPS angalia ibara hasa ya 16) na nyingine mtu anaweza kujisomea kuwa hakuna mtu mwenye uwezo na madaraka ya kuleta uchunguzi wa kihalifu (criminal investigation) kama Feleshi. Aangalie ushahidi uliopo na aliambie Taifa kuwa hakukuwa na uhalifu wowote uliofanyika na kama hakuna uhalifu wale wote wanaohusishwa na Kagoda warudishiwe 'fedha zao'. ..
Soma pia Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal
Kwa ufupi.. Feleshi alitakiwa kufanya haya yote yeye mwenyewe na binafsi naamini anatakiwa kumteua Public Prosecutor chini ya article 22 ya NPSA. Sheria ya Anti-Money Laundering nayo imeambatanishwa kuwasaidia watu kupima madai yaliyotolewa..
Ndugu zangu, kama Feleshi angekuwa anatumia madaraka yake ipasavyo kusingekuwa na haja za kina Hosea na Kamati Teule. Binafsi ninaamini mmoja watu ambao kutokana na madaraka yake amekuwa ni sehemu iliyohalalisha kukua na kukomaa kwa ufisadi nchini. Nimewahi kuandika hili kwa kirefu huko nyuma na katika Kagoda tunalirudia tu kwani angekuwa ni mtu anayetumia madaraka yake vizuri na ipasavyo hata tume ya EPA isingeundwa wala Luhanjo asingemchunguza Jairo!
Wakati umefika wa kuanza kutaka huyu jamaa aliyeapa kufanya kazi hii aaifanye kama hawezi ni bora ajiuzulu ili mtu mwingine mwenye nia na uwezo wa kusimamia sheria zetu kufanya kazi hiyo.
Kama yeye mwenyewe anaona hawezi kuchunguza jambo hili au anaona kwamba hawezi kuwa impartial ana uwezo wa kumchagua independent prosecutor kufanya uchunguzi - kuanzia na hizi nyaraka zilizowekwa jana - na hatimaye kuleta mashtaka yapasayo.