Kwanini DPP Feleshi anatakiwa kuleta mashtaka dhidi ya RA na YM na wengin juu ya Kagoda

Kwanini DPP Feleshi anatakiwa kuleta mashtaka dhidi ya RA na YM na wengin juu ya Kagoda

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Mkurugenzi wa Mashtaka amepewa dokezo kuwa kuna uhalifu umefanyika na ni uhalifu ambao unagusa taasisi mbalimbali nyeti na hata watu ambao tunaweza kusema ni watu maarufu. Tuhuma ambazo zimetolewa jana si ngeni lakini kilichodokezwa zaidi ni madai kwamba kilichofanyika hakikuwa wizi wa ulaghai tu bali ulikuwa ni uhalifu dhidi ya uchumi na taasisi zetu. Hivyo ameombwa kuchunguza na kuleta mashtaka.

Nimeambatanisha hapa sheria mbili (kwenye sheria ya NPS angalia ibara hasa ya 16) na nyingine mtu anaweza kujisomea kuwa hakuna mtu mwenye uwezo na madaraka ya kuleta uchunguzi wa kihalifu (criminal investigation) kama Feleshi. Aangalie ushahidi uliopo na aliambie Taifa kuwa hakukuwa na uhalifu wowote uliofanyika na kama hakuna uhalifu wale wote wanaohusishwa na Kagoda warudishiwe 'fedha zao'. ..

Soma pia Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kwa ufupi.. Feleshi alitakiwa kufanya haya yote yeye mwenyewe na binafsi naamini anatakiwa kumteua Public Prosecutor chini ya article 22 ya NPSA. Sheria ya Anti-Money Laundering nayo imeambatanishwa kuwasaidia watu kupima madai yaliyotolewa..

Ndugu zangu, kama Feleshi angekuwa anatumia madaraka yake ipasavyo kusingekuwa na haja za kina Hosea na Kamati Teule. Binafsi ninaamini mmoja watu ambao kutokana na madaraka yake amekuwa ni sehemu iliyohalalisha kukua na kukomaa kwa ufisadi nchini. Nimewahi kuandika hili kwa kirefu huko nyuma na katika Kagoda tunalirudia tu kwani angekuwa ni mtu anayetumia madaraka yake vizuri na ipasavyo hata tume ya EPA isingeundwa wala Luhanjo asingemchunguza Jairo!

Wakati umefika wa kuanza kutaka huyu jamaa aliyeapa kufanya kazi hii aaifanye kama hawezi ni bora ajiuzulu ili mtu mwingine mwenye nia na uwezo wa kusimamia sheria zetu kufanya kazi hiyo.

Kama yeye mwenyewe anaona hawezi kuchunguza jambo hili au anaona kwamba hawezi kuwa impartial ana uwezo wa kumchagua independent prosecutor kufanya uchunguzi - kuanzia na hizi nyaraka zilizowekwa jana - na hatimaye kuleta mashtaka yapasayo.
 

Attachments

Mkurugenzi wa Mashtaka amepewa dokezo kuwa kuna uhalifu umefanyika na ni uhalifu ambao unagusa taasisi mbalimbali nyeti na hata watu ambao tunaweza kusema ni watu maarufu. Tuhuma ambazo zimetolewa jana si ngeni lakini kilichodokezwa zaidi ni madai kwamba kilichofanyika hakikuwa wizi wa ulaghai tu bali ulikuwa ni uhalifu dhidi ya uchumi na taasisi zetu. Hivyo ameombwa kuchunguza na kuleta mashtaka.

Nimeambatanisha hapa sheria mbili (kwenye sheria ya NPS angalia ibara hasa ya 16) na nyingine mtu anaweza kujisomea kuwa hakuna mtu mwenye uwezo na madaraka ya kuleta uchunguzi wa kihalifu (criminal investigation) kama Feleshi. Aangalie ushahidi uliopo na aliambie Taifa kuwa hakukuwa na uhalifu wowote uliofanyika na kama hakuna uhalifu wale wote wanaohusishwa na Kagoda warudishiwe 'fedha zao'. ..

Kwa ufupi.. Feleshi alitakiwa kufanya haya yote yeye mwenyewe na binafsi naamini anatakiwa kumteua Public Prosecutor chini ya article 22 ya NPSA. Sheria ya Anti-Money Laundering nayo imeambatanishwa kuwasaidia watu kupima madai yaliyotolewa..

Unachosema ni sawa lakini siamini kuwa DPP haelewi haya unayoyasema. Kinachowasumbua wenzetu tuliowapa mamlaka ya kusimamia haki ni kuwa wamelewa mvinyo wa madaraka ambao mning'inio (hangover) wake ni mgumu sana kuuondoa. Hawana tofauti na Ghadafi ambaye mpaka sasa anaamini kuwa atashinda vita pamoja na kuwa dalili zote zinaonyesha kuwa ameshindwa tayari na kinachosubiriwa ni kumkamata tu na kumpeleka mahakamani.
 
Kuna mtu aliuliza kama inawezekana kwa wanaharakati kuwafungulia mashtaka watuhumiwa wa ufisadi badala ya kuwasubiri kina Feleshi wafanye kazi hiyo.Kwa jinsi hali ilivyo sidhani kama RA na Manji wanaweza kufikishwa popote na sana sana wao ndo wanaoweza kumfix yeyote atakayejaribu kuwafuata fuata.
 
kwa vyovyote vile ni lazima DPP arespond juu ya ushahidi huu. Ukichukulia mfano kama Misri kulikuwa na matatizo ya kiutawala lakini kuna baadhi ya taasisi zilikuwa bado zinaaminiwa na wananchi amabyo ilisaidia nchi isitetereke sana ila kwa Libya taasisi zote zilionekana kumuunga mkono Ghadafi na tofauti ni kuwa Misri aliondoka rais tu na taasisi nyingine zikaendelea kufanya kazi lakini Libya wanajenga upya!
Kwa maana hiyo hizi ofisi kama za DPP, CAG, AG nk lolote likitokea (hakuna ajuaye siku wala saa-kama yupo muulize Ghadafi) zitapoteza uhalali wake na wanaozisimamia watakuwa wameandikwa vibaya (negative) nkatika historia ya nchi kwa kuchangia kurudisha/kujenga umaskini, kupalilia injustice na kuhujumu uchumi wa nchi.
Unachosema ni sawa lakini siamini kuwa DPP haelewi haya unayoyasema. Kinachowasumbua wenzetu tuliowapa mamlaka ya kusimamia haki ni kuwa wamelewa mvinyo wa madaraka ambao mning'inio (hangover) wake ni mgumu sana kuuondoa. Hawana tofauti na Ghadafi ambaye mpaka sasa anaamini kuwa atashinda vita pamoja na kuwa dalili zote zinaonyesha kuwa ameshindwa tayari na kinachosubiriwa ni kumkamata tu na kumpeleka mahakamani.
 
Hivi utaratibu ukoje nchi zingine? Mbona huwa nasikia kuna waendesha mashtaka binafsi. Hivi Tanzania hatuna watu kama Ken Starr? Au ni katiba hairusuhu?
 
Kama yeye DPP anaona hawezi kufanya hiyo kazi au uchunguzi anaweza kuchagua independent prosecutor akampa wajibu huo - kitu ambacho binafsi ningekipenda zaidi. Kwa sababu kama angetaka kutumia madaraka yake angeweza kuyatumia lakini ana woga wa aina fulani sijui ni wa nini hasa.. kuanzia suala la Chenge hadi leo hii hajafanya lolote la kuonesha anaweza kutumia madaraka yake kuongoza vita dhidi ya ufisadi.

Kama nilivyowahi kuandika huko nyuma kwa nchi yetu he is the most powerful law enforcer in the country. Ndio maana binafsi sikushabikia kabisa kitendo cha Bunge kujivika madaraka hata ya kuonekana kuchunguza uhalifu wakati mtu aliyepewa madaraka hayo yupo anakula bata na mbatata!
 
Hivi utaratibu ukoje nchi zingine? Mbona huwa nasikia kuna waendesha mashtaka binafsi. Hivi Tanzania hatuna watu kama Ken Starr? Au ni katiba hairusuhu?

Ndio maana tumeweka hizo sheria umechukua muda kuzisoma? Feleshi akitaka anaweza kuchagua Independent Prosecutor or Investigator kama Ken Starr
 
Saisa zinaendesha kila jambo Tanzania mkuu. Tunashuhudia watumishi wengi wa umma wenye profession zao wakiogopa kufanya chochote hata wanapobaini kuwa wanapaswa kuchukua hatua kutokana na nafasi zao, kwa kusubiri orders kutoka kwa viongozi wa kisiasa haswa Rais na mawaziri. Huu ni udumavu. Taifa halitaendelea. Na hapana haja ya kuajiri wataalamu kwa kuwa hawautumii utaalamu wao.
Fait accompli.
 
Ndio maana tumeweka hizo sheria umechukua muda kuzisoma? Feleshi akitaka anaweza kuchagua Independent Prosecutor or Investigator kama Ken Starr

Mkuu hapa naona kuna tatizo. Ni kama akitaka na asipotaka basi anafanya yeye?!! Kwa hiyo Msemakweli hawezi kutoka na ushahidi wake na kufungua kesi mahakamani? Nadhani ni vyema tukawa na independent prosecutors ili kuondoa mawingu kama haya.
 
Jamani mimi nimechoka na hizi Sarakasi za Serikali inayowakumbatia mafisadi, Imeshafikia wakati sasa wakuchukuwa hatua dhidi ya hii Serikali ya ukandamizaji na unyanyasaji wa Watanzania kuwatoa madarakani hata kwa gharama yoyote ile kama ikibidi ili tuweze kulinusuru hili Taifa letu linadhidi kudidimia na sisi tupo tunabakia kulalamika badala ya kuchukuwa hatua. Tutakuja kuchapwa viboko na Wajukuu zetu kama tusipolitetea Taifa lao la Kesho na kulinda Rasilimali zao. Tutakuja kujilaumu hapo baadaye kama Hatua hazitochukuliwa, Mchakato wa kuwango'a Mafisadi uanze mapema na haraka uwezekanavyo.
 
..Moja ya sababu za Ubutu wa DPP ni kutokana na Katiba hii tulionayo, huyu nae ni Presidential Appointee kama alivyo CAG, kama alivyo DG wa PCCB. Wanafanya kazi zao kwa Vimemo kutoka juu ambavyo Ujumbe wake always utasomeka hivi🙁fanya hivi, mtoe huyu, muweke huyu, achana na huyu, mchunguze huyu, mwache huyu).
Tunahitaji Katiba Mpya, Katiba ambayo DPP, CAG na DG-PCCB watakuwa huru kufanya kazi zao kwa mujibu wa Sheria ambayo imeunda Taasisi wanazozisimamia.
Mungu ibariki Tanzania
 
Unajua Ken Starr aliteuliwa na nani?

Mkuu sikumbuki aliteuliwa na nani na kwa wakati huo sikujua aliteuliwa na nani. Ila nchi kama hii ya kwetu tatizo ni siasa kama alivyosema hapo juu #12 (Pokola). Wanataaluma wetu wengi wanasukumwa na siasa. Siamini na hakuna mtu yeyote atanifanya niamini kwamba Feleshi hana hicho ambacho Msemakweli amekionyesha na kukisema jana, ni kwa nini haku act? Siasa. Sasa kusema kwamba ateue independent prosecutor katika hali kama hii naona kama ndoto vile!! Wewe mwenyewe umesema kwamba bunge linajivika mamlaka ya kuchunguza wahalifu. Hapa tatizo ni ombwe la wanataaluma waliomo serikalini!! Ama hawfanyi kazi kwa weledi au wanaminywa wasifanye kazi zao kwa weledi.

Ndio nataka niisome hiyo sheria ya NPS ila sijui security of tenure ya DPP ikoje. Haya matatizo tutaendelea nayo hadi tutakapopata katiba mpya na kufanya overhaul ya organs zetu za serikali kama wanavyofanya wenzetu wa hapo Kenya.
 
Ndio maana kuna comment nimesema kwa sababu serikali yetu ina wepesi wa kubinasfisha basi washauariwe kubinafsisha majukumu ya DPP. Yanni ziwepo kampuni binafsi ambazo zitakuwa Private directorate of Public prosecution. Kama kweli wana lengo la utawala bora wa haki na sheria hawatalikataa.

Then pale ambapo kina DPP serikali ikiona hakuna ulazima wa kushataki lakini hizi kampuni binafsi za mashataa zikijirdhisha kuna kesi basi ziwe na nafasi ya kuendesha mashataka. wakishidwa kesi inakula kwao na wakishinda kesi basi serikali inawalipa......

Binafsi niliondokewa na imani pale kwa suala la EPA niliposikia ofisi ya DPP inaomba msaada kwa wananchi wenye ushahidi. As if uhalifu uliofanyika ni wa wa mtu kuchomwa kisu njiani au kuvamiwa na majambazi.
 
Mkurugenzi wa Mashtaka amepewa dokezo kuwa kuna uhalifu umefanyika na ni uhalifu ambao unagusa taasisi mbalimbali nyeti na hata watu ambao tunaweza kusema ni watu maarufu. Tuhuma ambazo zimetolewa jana si ngeni lakini kilichodokezwa zaidi ni madai kwamba kilichofanyika hakikuwa wizi wa ulaghai tu bali ulikuwa ni uhalifu dhidi ya uchumi na taasisi zetu. Hivyo ameombwa kuchunguza na kuleta mashtaka.

Nimeambatanisha hapa sheria mbili (kwenye sheria ya NPS angalia ibara hasa ya 16) na nyingine mtu anaweza kujisomea kuwa hakuna mtu mwenye uwezo na madaraka ya kuleta uchunguzi wa kihalifu (criminal investigation) kama Feleshi. Aangalie ushahidi uliopo na aliambie Taifa kuwa hakukuwa na uhalifu wowote uliofanyika na kama hakuna uhalifu wale wote wanaohusishwa na Kagoda warudishiwe 'fedha zao'. ..

Kwa ufupi.. Feleshi alitakiwa kufanya haya yote yeye mwenyewe na binafsi naamini anatakiwa kumteua Public Prosecutor chini ya article 22 ya NPSA. Sheria ya Anti-Money Laundering nayo imeambatanishwa kuwasaidia watu kupima madai yaliyotolewa..

Ndugu zangu, kama Feleshi angekuwa anatumia madaraka yake ipasavyo kusingekuwa na haja za kina Hosea na Kamati Teule. Binafsi ninaamini mmoja watu ambao kutokana na madaraka yake amekuwa ni sehemu iliyohalalisha kukua na kukomaa kwa ufisadi nchini. Nimewahi kuandika hili kwa kirefu huko nyuma na katika Kagoda tunalirudia tu kwani angekuwa ni mtu anayetumia madaraka yake vizuri na ipasavyo hata tume ya EPA isingeundwa wala Luhanjo asingemchunguza Jairo!

Wakati umefika wa kuanza kutaka huyu jamaa aliyeapa kufanya kazi hii aaifanye kama hawezi ni bora ajiuzulu ili mtu mwingine mwenye nia na uwezo wa kusimamia sheria zetu kufanya kazi hiyo.

Kama yeye mwenyewe anaona hawezi kuchunguza jambo hili au anaona kwamba hawezi kuwa impartial ana uwezo wa kumchagua independent prosecutor kufanya uchunguzi - kuanzia na hizi nyaraka zilizowekwa jana - na hatimaye kuleta mashtaka yapasayo.
Mwanakijiji you have raised a very important point. mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi hayatakuwa na mafanikio kama system iliyopo sasa haitaweza kuamshwa na kupewa sababu ya kuanza kuuma kwa kutumia meno iliyonayo. Na kama tunataka kulisaidia Taifa, imefika mahali sasa, watu wanaokalia ofisi za umma wakakumbushwa kuwa tunajua wanatakiwa kufanya nini. Hatutaweza kufanya hivyo kama sisi hatujasoma na kuelimika na kuamua kuwa wazalendo.
 
Huu mziki umepigwa muda mrefu lakini wenyewe wameamua kukaa kimya labda kutusahaulisha? Tuendelee kuimba au labda kuna Plan C?
 
Back
Top Bottom