Mzee Mwanakijiji, hili la DPP kufungua mashitaka dhidi ya Kagoda haliwezi kufanyika kamwe, unless otherwise!
Natumaini umesoma mamlaka ya DPP,
Naomba nikuwekee na kifungu chenyewe ili tuelewane.
Part II Sec 9,-(1) (a) decide to prosecute or not to prosecute in relation to an offence;
Ni kwa kutumia kifungu hicho, DPP anaweza kufungua mashitaka, ama anaweza asifungue na hakuna wa kumuuliza sababu, hata rais hawezi. Siku zote nimekuwa naimba haka kawimbo cha madaraka ya ajabu ya DPP. Kwa lugha nyepesi, hata kama jinai imetendeka na ushahidi upo kwa asilimia 100%, DPP ana mamlaka kuendesha kesi au kutokuendesha na hakuna mamlaka ya kuuliza ni kwa nini.
Kuna kipindi cha nyuma, Ijumaa moja, mtoto ambaye ni mwana pekee wa kiume wa kigogo mmoja, ilichukua bastola ya baba yake akamiminia risasi 6 adui yake mmoja na kufa papo hapo. Mtoto huyo alichukuliwa na kulazwa polisi, Jumatatu asubuhi mtoto alifikishwa mahamani kusomewa shitaka la mauaji. Jioni ya siku hiyo DPP alipeleka Nolle Prosequi, Jumanne kesi ikafutwa, mtoto akaachiwa na kupelekwa nje ya nchi, baba kigogo wakayamaliuza na familia ya marehemu, kesi ikaishia hapo.
Powers hizo za DPP kupeleka Nolle, pia hazihojiwa na mamlaka yoyote, wala DPP hapaswi kutoa sababu zozote za nolle kwa yoyote.
Sababu za DPP kutoanzisha mashitaka dhidi ya Kagoda, nimezieleza kwenye thread yangu ya 'Kagoda Kamwe Haitafikishwa Mahakamani!'
Pasco.