Kwanini Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imevunjwa?

Kwanini Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imevunjwa?

Kwa hyo kutakuwa na jiji la Ilala? Bado sijaelewa huu ukurupukaji... Au walipokuwa wanaita jiji la Dar es salaam walimaanisha ni hao madiwani na mkrugenzi wao and nothing else
Jiji la Dar es Salaam bado lipo na Ilala sio jiji bali Ilala imepewa hadhi ya kuwa halmashauri ya jiji la Dar es Salaam. Kama alivyoelezea mtaalamu hapo kuwa halmashauri ya jiji awali ilikuepo lakini haina eneo la utawala kwahiyo imeondolewa na halmashauri ya manispaa ya Ilala imepewa hadhi ya halmashauri ya jiji.

Kwahiyo shughuli za halmashauri ya jiji zitafanywa na halmashauri ya manispaa ya Ilala na aliekua meya wa manispaa ya Ilala atakua meya wa manispaa ya jiji. Ukiangalia katika majiji mengine ndio iko hivi lakini DSM pekee nadhani ndio ilikua na halmashauri ya jiji ambayo uongozi wake sio halmashauri ya wilaya iliyo katikati ya jiji.
 
Bado sijaelewa kabisa... Dar kuvunjwa na Ilala kupandishwa kuwa Dar sasa kuna tofauti gani? Watumishi waliokuwa ofisini Dar watahamia Ilala, kuna tofauti hapo?

Si bora ningesikia kila manispaa ijisimamie yenyewe ila kwa sasa mkoa wa Dar jiji ni Ilala tu. Wale watumishi waliokuwa m/spaa ya Dar watapewa kaz ingine.
 
Copy and paste ya tundu lissu kuhusu majimbo ila wamebugi km elimu bure
 
Maana yake, sasa zitabaki halmashauri 5 tofauti na 6 za mwanzo...
 
Kweli nilikuwa sielewi chochote kuhusu hilo.

Kwani hivyo vitu vinaundwa na nani? Naona kama presidential candidate ni juu mno kushughulikia vitu hivyo.

Anyways ...sipangiwi..
 
Jiji la Dar es Salaam bado lipo na Ilala sio jiji bali Ilala imepewa hadhi ya kuwa halmashauri ya jiji la Dar es Salaam. Kama alivyoelezea mtaalamu hapo kuwa halmashauri ya jiji awali ilikuepo lakini haina eneo la utawala kwahiyo imeondolewa na halmashauri ya manispaa ya Ilala imepewa hadhi ya halmashauri ya jiji...
Mkuu iwe nzuri au mbaya swalil la msingi Ni kwamba haya maaamuzi yamezingatia ushirikishwaji wa wananchi na Viongozi wenzake ndani ya chama na Serikali na je ni kwa mujibu wa sheria? Utaratibu wa kisheria na kikanuni umezingatiwa? Ni maamuzi ya pamoja au Ni ya mtu mmoja kafanya huku akiwazodoa na kuwasengenya wenzake?

Kama Ni ya mtu mmoja yatudumu baada ya yeye kuondoka? Huoni kwamba haya majadiliano yanayofanyika sasa mitandaoni ndiyo ambayo yangepaswa kutangulia maamuzi haya makubwa aliyoyafanya? Je katika hili nafasi ya waziri husika na nafasi ya bunge Ni ipi? Kwa hiyo hivi vyombo vya maamuzi havina maana Tena Ila Ni mzee baba akilala akiamka anashusha tu kombora lililomjia akilini?!!!!!

Sasa hao madiwani waliozodolewa kuwa wana viherehere vya kugombea umeya na Kwamba hawakuchaguliwa na wananchi( Ni Madiwani batili) Ni wa chama gani? Na Kama hao Madiwani Ni batili, wabunge na Rais watakuwaje halali? Na je Nia za hao Madiwani kugombea umeya zilikuwa batili kisheria kiasi Cha wao kuzodolewa hadharani?
 
KWANINI HALMASHAURI YA JIJI LA DAR ES SALAAM IMEVUNJWA Ni Mawazo Yangu #Joseph #Yona

Kiutawala Jiji lilikuwa limegawanyika katika Halmashauri sita za Serikali za mitaa ambazo ni:
Nimependa umefafanua vizuri sana, siku zote nimekuwa sielewi kumbe kuna chombo kilikuwa kinafanyia kazi zake hewani kikimaliza mbawa zinakwenda kutua kwake, magurudumu kwake, mkia kwake cockpit nayo kwake na fuselage kwake
 
Mkuu iwe nzuri au mbaya swalil la msingi Ni kwamba haya maaamuzi yamezingatia ushirikishwaji wa wananchi na Viongozi wenzake ndani ya chama na Serikali na je ni kwa mujibu wa sheria? Utaratibu wa kisheria na kikanuni umezingatiwa? Ni maamuzi ya pamoja au Ni ya mtu mmoja kafanya huku akiwazodoa na kuwasengenya wenzake? Kama Ni ya mtu mmoja yatudumu baada ya yeye kuondoka?
Hii ni desturi kwa kila eneo la kiutawala, ushirikishwaji kwetu ni msumari wa moto, ndiyo hayo yanalalamikiwa kila kona kuhusu allocations ya vituo vya kutolea huduma kwa wananchi,
 
Kuanzia leo tar 25 February 2021ukizungumzia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam unazungumzia Wilaya ya Ilala pekee,Ila ukizungumzia mkoa wa Dar es Salaam unazungumzia muunganiko wa Wilaya za Temeke, Ubungo, Kigamboni, Kinondoni na Ilala.

Kabla ya leo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam liliongoza Halmashauri 6 huku ikiwa haina kata wala mtaa na Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam aliongoza Halmashauri zote 6;-

1.Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam
2. Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
3. Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni
4. Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
5. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo
6. Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni

Kuanzia leo tar 25 February 2021, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam itajiongoza yenyewe kama Ilala,na Mayor wa Ilala anakuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam mwenye mamlaka kwa Halmashauri ya Ilala na atakuwa na mamlaka kwa Halmashauri ya Jiji la Ilala tu ambayo inabeba "title" na hadhi ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,kabla ya leo Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa na ma-Mayor 6,watano kutoka kila Manispaa na wasita kutoka Halmashauri hewa ya Jiji la Dar es Salaam.

-Halmashauri hewa ya Jiji la Dar es Salaam.

Sasa Ukiangalia hapo juu kulikuwa kuna chombo tu kinaitwa Halmashauri ya Jiji la Dar es,lakini chombo hicho hakikuwa na eneo rasmi la kiutawala kwa maana nyingine halmashauri ya jiji haina kata wala mtaa inayoitawala,kwa maana hiyo inategemea vyanzo vya mapato kutoka halmashauri za manispaa ya Ilala, Kinondoni,Temeke,Kigamboni na Ubungo, Halmashauri hiyo ilikuwa kama kupe,kwa hiyo ilikuwa ni kama halmashauri hewa.

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilikuwa ina Meya wake na baraza lake huku halina vyanzo vya mapato wala haina kata wala mtaa inayotawala,lakini cha ajabu walikuwa na bajeti yao ya kuhudumia miradi hewa ambayo miradi watayoitaja utaikuta kwenye Halmashauri ya Ilala, Kinondoni, Kigamboni,Temeke na Ubungo,

Hivyo kulikuwa na matumizi mabaya ya pesa kwa kuwa ni kama unampa mtu pesa wakati hana matumizi nayo,Sasa alichofanya Rais Magufuli ni kuivunja Halmashauri hiyo kupe na kuichukua Halmashauri ya Ilala na kuiita Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,na Manispaa za Kigamboni, Kinondoni,Ubungo,Temeke zitabaki kama Manispaa.

Nimalizie kwa kusema japo vigogo wawili jana wamekosa kazi Mayor wa Jiji la Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam,awa kijiografia na kuitawala walikuwa na mamlaka ya Halmashauri 6 za Mkoa wa Dar es Salaam wakijihusisha na kushughulikia Serikali za Mitaa,huku Mkoa wa Dar es Salaam ukijihusisha na kushughulikia masuala ya Serikali Kuu,niwaombe wakubaliane nasi kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar ilikuwa kama urembo tu kwani haikuwepo kiuhalisia,haina tofauti na wafanyakazi hewa kwani wafanyakazi na wanasiasa walikuwa wanafaidi mihela,Kwa hiyo ile ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya zamani itavunjwa na itakuwa chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,hii itapunguza hela zilizokuwa zinatumika hovyo.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Jiji la Ilala.
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Naona umeweka na CV kabisa, umesahau jiwe alisema kuapisha ni kazi?
 
Hiyo unayoiita halmashauri hewa ukumbuke kwamba iliundwa na serikali ya CCM.
 
Nimerudia kwa kusoma mara saba sijaelewa naomba aliyeelewa anieleweshe ...

Au ndio ule usemi akimaliza kuwavuruga wa nje atarudi kuwavuruga wa ndani .utaratibu ni ule ule wa kupunguziana keki mpaka iwe inaliwa na mmoja

Wote tutaimba wimbo mmoja au nasema uongo ndugu zanguu
 
Back
Top Bottom