Kwanini hatuna teknolojia?

Kwanini hatuna teknolojia?

Naomba niongee kidogo kuhusu suala la vyuo na Technology tunayo itaka, kiukweli tanzania ya sasa tumesha haribiwa kiakili, sio kwamba elimu tunayopewa haifai la hasha ila wanaopewa elimu ndio matatizo, dronedrake nadhani utakuwa shahidi kwa upande wa career ambayo upo ni wanafunzi wangapi wanamaliza hawajui hata resistor na nini na wanatoa pesa kufanyiwa projects za mwaka wa mwisho. Kingine nimeshiriki sana baadhi ya mashindani ya Makisatu, Feed the Future na mengine na ni watu kibao wanapewa mapesa kibao lakini after hapo wanapotea na hawasikiki tena, kikubwa kwa upande wangu ninachokiona ni vijana hatutaki kujishughurisha na wazee hawataki tujishughulishe na wanafunzi hawataki kujifunza wao wanachotaka ni cheti tu. Kuna watu ukiwaambia wanasingizia vifaa ila kiukweli uzembe wa kujifunza na kufatilia ndio unafanya tuone upatikanaji wa vifaa ni mgumu. Ila vifaa upatikanaji ni rahisi na wa gharama nafuu kama una nia na unachotaka kukifanya. Hayo ni maoni yangu tu

Serikali haijaweka mazingira mazuri, wanawaza uchaguzi.
 
kitambo nilifanya kazi kama fundi-umeme, kiwanda flani maarufu tu Dar

na kulikua hao 'injiniaz' wa kutosha kadhaa , umeme na mekaniko

kilichonishangaza ni kwamba, ukimuita ni lazima ( by-law ) uanze na neno Eng. flani or ana haki ya kutoikia wito na wewe ukawajibishwa

aisee, kilichonishangaza zaidi, output za hao 'injiniaz' hakuna, hata ku-solder hajui, kushika 'screw-driver' hajui, zaidi ya ku jaza log-book kila mda wa kuondoka,

likitokea tatizo siriaz sana kwenye 'mashine', engineers wa kikenya wanakua 'contracted' kuja kutatua

nikabaki nasikitika sana
Hii ndio shida kubwa iliyopo, mimi nipo chuo fulani hapa nnchini na sio kwamba najua vitu vingi sana ila kiukweli wanafunzi tuna visingizio vingi sana, kikubwa huwa tunasema upatikanaji wa vifaa na kingine huwa hatuna shida sana ya kujua vitu kwakuwa wanaotufundisha pia huwa Hawajui, na ninarudia hili neno Hawajui na kisingizio ni kuwa wamesoma zamani ivyo wanasahau 😂😂😂😂😂 , kitu ambacho hakijawai tokea duniani kusahau kitu unacho fundisha. Ivo kiukweli tuna Engineers majina na tusijivunie kwani mimi naonaga wakati mwingine tunapoteza tu pesa kutoa mikopo bora tujenze shule za msingi
 
Kitu kikiwa kimetengenezwa Tanzania watu awawezi kukiamini mtu ni kheri avae nguo kutoka china lakini sio cha ya Tanzania
Sio kweli, kitu kinacho tusumbua ni fikira zetu za watanionaje au wataniaminije, kopa gas si ilikuwa ya mtanzania kabla ya kuuzwa na kuna propotype kibao zinapewa pesa ila zinapotea, shida ya tanzania ni njaa na ujinga ila sio serikali, nasema ivo maana nipo kwenye kitengo cha innovation na nina record ya zaidi ya 350M watu kupewa na hawajulikani walikoenda
 
Sio kweli, kitu kinacho tusumbua ni fikira zetu za watanionaje au wataniaminije, kopa gas si ilikuwa ya mtanzania kabla ya kuuzwa na kuna propotype kibao zinapewa pesa ila zinapotea, shida ya tanzania ni njaa na ujinga ila sio serikali, nasema ivo maana nipo kwenye kitengo cha innovation na nina record ya zaidi ya 350M watu kupewa na hawajulikani walikoenda

Mkuu Serikali ndo tatizo yani tunakila kitu hapa kwetu ila maendeleo ni 0 mpka leo tunatumia vitu vilivyo achwa na mkoloni,mfano reli, magereza, vitu kibao sasa wataweza kuleta kuwaletea wanachi tecnologia
 
Wewe unadhani nini kinasababisha wanafunzi wetu wasijifunze kwa lugha ya Kiswahili? Kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu?
Darasani penyewe unajibu mtihani kwa kiingereza lakini unawaza kwa kiswahili.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣,Kwamba tunawaza kwa kiswahili
 
changes inatakiwa ianze na sisi na sio serikali kijana, elewa kwanza hapo

Hapana sasa sisi tunanguvu gani ya kuleta hiyo tecnology kama serikali haijweka njia rahisi, tunashindwa vipi hata kutengeneza hata pikipiki tuwauzie wanachi kwa bei rahisi.
 
changes inatakiwa ianze na sisi na sio serikali kijana, elewa kwanza hapo

Serikali ni kama Baba kwenye Familia,Uwezi kuwaumu watoto wakati huyo Baba hata Baiskeli ya Miti hana.
 
Inovation inaanzia mbali sana.
Kwanza hakikisha una basic
1.uwe nakazi yakuingizia kipato
2.uwe umejitosheleza kiMalazi
3.usiwe unategemewa na watu wengi..
Hii ya mwisho itakusaidia sana akili iwe imetulia
Ukitimiza haya hata akili ya inovation inapatikana kwakua kupitia kipato unachopata utaweka endeleza malengo yako otherwise utasubiri serikali daima ..innovator wengi hawakusaidiwa na serikali. ..never
 
Back
Top Bottom