Kwanini huolewi? Au una kasoro?

Kwanini huolewi? Au una kasoro?

Umri wako sasa hivi ndio wa kutafuta mchumba uolewe, kuwahi kuolewa wakati mwingine sio kuzuri unashindwa kufanya mambo mengine ya maisha sababu ya majukumu ya kulea familia,usife moyo mwambie mama mume wako ataletwa na mungu wakati ukifika
 
Kwa jamii ya kiafrica ni kawaida sana maswali kama hayo hasa umri unapofika miaka 30 kwa wasichana.

Unajua zamani walikuwa wanaolewa fasta fasta na mambo ya career woman walikuwa hawana.

Muombe Mungu sana dada yangu ili akuletee mume mwema, au hupendi kuolewa??.
 
haolewi kwasababu bado mdogo au hajampata bado wa kumuoa c unajua wanawake ni wengi kuliko wanaume
 
cku hiz kuolewa cyo inshu tafuta m2 au ntafute mimi nikutie mimba ukishajifungua lea mtoto wako mwenyewe .....maisha yanaendelea
 
Habari wanajamvi.
Kwa kweli hilo swali huwa linanisononesha sana.
Nina umri wa miaka 30, sijaolewa, sina mchumba wala mpenzi yapata mwaka na miezi kadhaa sasa.
Mdogo wangu anayenifuatia ana miaka 27 aliolewa akiwa na miaka 24 na ana watoto wawili sasa.
Familia yangu na jamii inayonizunguka hainielewi na mara nyingi nakutana na hilo swali
"Mbona wenzako wanaolewa wewe huolewi, au una tatizo?"
Kiukweli hua napata ugumu sana kujibu hilo swali kwa sababu sina cha kuwajibu.
Labda ningesema nina tatizo au kasoro lakini kati ya niliowahi kuwa nao kimahusiano hakuna alieoa hadi sasa japo wote walinizidi umri na kuna wawili walikua na watoto tayari na mpaka sasa hawajaoa.
Hivi kwa jamii yetu mwanamke kutoolewa ni kasoro?
Maana kuna rafiki yangu naye anapata usumbufu kama wangu kutoka kwa familia yake.
Vipi kama mwanaume ninayempata yeye hana wazo la kuoa nifanyeje?
Na wanaume huwa wanaulizwa na kuonekana wana matatizo kama wanawake?

wewe unaonaje??au wewe unatakaje?
kama huoni ni tatizo uwe na amani..lakini kama na wewe linakuletea shida ni wakati wa kuchukua hatua muafaka (yaani kukaa mkao wa kuolewa)
 
cku hiz kuolewa cyo inshu tafuta m2 au ntafute mimi nikutie mimba ukishajifungua lea mtoto wako mwenyewe .....maisha yanaendelea
Chwechwe unasambaza mbegu tu,malezi watahangaika nayo wenyewe we kiboko...
 
usijilazimishie kuolewa tena hiyo miaka sio tishio kiivyo.
Mwombe Mungu utapata wa kukufaa.
 
Sisi wakristo tunaamini kila jambo mungu hulifanya kwa kusudio lake. Ona ndoa ngapi zinafungwa na baada ya muda mfupi zinavunjika au ni ngapi hazidumu. Wewe zidi kumwomba mungu usikate tamaa atakuonyesha wakwako tu. Usijaribu kufanya hivyo kunufaisha watu utapata matatizo makubwa kama si MARADHI basi manyanyaso.
 
Pole sana Da Pretty hiyo ni moja ya maisha. Kikubwa ongea na mama yako aelewe huna tatizo lolote, halafu wewe mwenye jiamini fanya mambo yako ya maendeleo. mie mwenyewe yamenikuta lakini nasonga mbele na maisha sisikilizi wanayosema wanadamu maana ni kawaida yao. ninachofanya nikujitahidi kuwa na maisha mazuri na mengine yatakuja kwa wakati uliopangwa
 
Usijali Da Pretty wakai ukifika utaolewa tu na pia endelea kumuomba Mungu akujalie upate mume mwema.
 
Dada angu pole sana kwa mawazo mabaya ulojiwekea na unawaza sana sababu wewe mwenyewe unapenda upate mchumba uolewe lakini inakuwa sivyo, embu jiulize maswali kwanza kwa nini unaokuwa nao hawakukuuliza swali hilo? pengine kuna kitu kinawakwaza bila ya wewe mwenyewe kujua, relax kila kitu kitakuja chenyewe wakati ukifika wala usiumie roho kuona mdogo wako alishaolewa, pia siku hizi kutaka kusoma kwanza wasichana wengi wamejikuta wana madegree kibao then wanatafuta wachumba wa kuwaoa miaka inakuwa imeenda sana mwishoni unajikuta kwenye situation ambayo unajiona umechelewa. mimi naona umri wako bado upo freshutapata tu mchumba

Wala usiwaze miaka 30 bado kabisa. Ila nakushauri isizidi miaka 35 kwa kuwa unahitaji kupata watoto angalau ukiwa na umri chini ya miaka 35.
 
Dada Pretty miaka 30 ni mingi ndugu yangu mtu asikudanganye na anekuambia kuolewa sio issue inamaana anataka uwe malaya au utembee na wanaume za watu? kutokana na maelezo yako Kama unavyodai majamaa zako wa nyuma wote bado hawajaoa mimi navyoona huo ni mkosi au nuksi shost kukutana na mijinaume ambayo sio mioaji mfululizo mhh! sasa fata ushauri naokwambia Kama nikuomba mungu omba mungu akuondolee nuksi ya kutokuolewa kwanza ikishatoka ndio uombe mungu akuchagulie mume, pili nina wasiwasi una jini mahaba lina kupeleka kwa wanaume wasiofaa ambao pia wao wana hayo majini shost piga vizuri Kama wewe ni mkristo kemea jini mahaba kwa kwenda mbele mama la sivyo unazeeka kumbuka kuna kuna kuzaa na watoto ni hazina maishani usijidanganye ukazaa bila kuolewa huko nikujidhalilisha yaani ukae miaka yote hiyo 30 halafu uje uzae bila kuolewa usikubali wanaume wapo kibao wanatafuta wanawake wa kuoa hawawaoni kwani una kasoro gani chakarika mwaka huu usiishe shost
 
usijilazimishie kuolewa tena hiyo miaka sio tishio kiivyo.
Mwombe Mungu utapata wa kukufaa.

Sijilazimishi mpenzi na sio kwamba suala la kuolewa linanisumbua.
Tatizo kukitokea mkusanyiko wowote wa ndugu basi lazima wanijadili.
Ndio maana najiuliza ni kwa nini?
Hilo la maswali ndio linalonikera, na hadi kuandika hapa ni kwa vile wanaoniandama ni watu wangu wa Karibu, wangekua wa mbali kama majirani na watu aki wala nisingekerwa na hil swali.
 
wengine micharuko huko kuolewa watakusikia ktk kitchen parts tu!
 
pole,hata hivyo usikate tamaa bado wakati wako aliokupangia mungu haujafika,wakati ukifika mchumba mungu atakuletea mtu ambaye mtapendana na mtaoana,jamii nyingi zina mawazo potofu lakini wewe unatakiwa uwaelimishe jamii ili wasiendelee kukusumbua
 
Back
Top Bottom