Kwanini huwa tunaamini kuwa wazungu ndiyo wametudumaza tusiendelee?

Kwanini huwa tunaamini kuwa wazungu ndiyo wametudumaza tusiendelee?

Victim hood mindset kutafuta sehemu ya kutupia lawama.

Waafrika adui yetu ni uvivu, ulalamikaji, ulafi na umimi hasa ukabila

Hata wachina na wahindi waliwahi kutawaliwa na wazungu, Leo wahindi ndio kundi linaloongoza kwa kuwa na jamii yenye familia zenye kipato cha juu zaidi Marekani, Wachina wameipigisha nchi yao hatua kwa spidi ya radi
 
Mpaka Leo Bado Kwa sehemu kubwa wanasiasa wetu wanaonesha kwa maneno na matendo yao kuwa wazungu ndiyo ama wanasababisha tusiendelee au wao ndiyo walisababisha tusiendelee.

Kwa nini tunaamini hivyo??

Kwa sababu ni kweli!!….
Dhana nzima ipo kwene ukoloni mamboleo! Ni rahis sana mtu kubeza hili kama hajui ukoloni mambo leo!!….
-Usione kuna mapinduzi ya kijeshi ( fatilia utakuta aliyepindua alipata mafunzo USA, sijui Europe-Je bado una hisi ni coincedence)

-Mikataba mibovu isiyo na masilahi-(Economic Hitman)
-Madikteta wa muda mrefu ambao wanasave maslah ya wazungu ( kwa kigezo cha kuachwa madarakani muda mrefu)

-kuuliwa kwa viongozi wenye maono na watetezi wa raia wa nchi zao ie Patric Lumumba,Thomas sankara etc

-Kutumia organization kubwa kucontrol uchumi ie IMF,World bank
-Mikopo yenye mashart magumu ie IMF nk

INGAWA KUNA PART AMBAYO VIONGOZI WETU NAO WANAHUSIKA,,, lakin pia na jamaa wametukalia pabaya
 
Ni mjinga pekee ndo anayo mawazo ya kijinga kama hayo,utakuta msomi mzima anatumia kitabu Cha Water Rodney ku-justify kuto endelea kwa Waafrika,kumbe mchawi wa maendeleo ya bara la Afrika ni mwafrika mwenyewe.

Rais wa awamu ya tatu wa Tanzania BWM. kwenye kitabu chake,anakiri wazi kutumia pesa ya umma kugharamia kampeni za uchaguzi za CCM ,sasa hizi ni akili au ujinga wa mtu mweusi au alishauri na wazungu?

Hivi ni mzungu ndo huwa anawashauri watawala wa kiafrika kuiba pesa za umma na kupeleka kwenye ma-bank ya ughaibuni,kama alivyofanya San Abacha wa Nigeria,hapa kwetu tu ni shida mara Tegeta-Esrow,EPA, Richmond nk.

Hivi ni mzungu ndo hutoa ushauri kwa watawala wa kiafrika kuandaa maigizo na ujinga wa kisiasa wa kuandaa chaguzi za marudio,ambapo pesa nyingi hupotea uko, mfano ni kipindi cha JPM katika ile hatua ya "kuunga mkono juhudi".

Hivi mzungu ndo huingia mikataba ya hovyo ya kuuza rasilimali hovyo za taifa,mfano Mzee Mwinyi na kashfa ya kuuza Loliondo,Kikwete- gesi na Samia-bandari.

NB: wazungu hujenga matundu ya vyoo katika shule za waafrika ambapo watawala wameshindwa,lakini muda huo huo watawa wa kiafrika wanaagiza magari ya kifahari ya V8 ,toka Japan.
 
Kwa hii nchi ilivyo bora itawaliwe tena tu maana tumeshindwa kujitawala wenyewe...
 
Mpaka Leo Bado Kwa sehemu kubwa wanasiasa wetu wanaonesha kwa maneno na matendo yao kuwa wazungu ndiyo ama wanasababisha tusiendelee au wao ndiyo walisababisha tusiendelee.

Kwa nini tunaamini hivyo??
Waafrika wengi hawana akili ni matahira
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Victim hood mindset kutafuta sehemu ya kutupia lawama.

Waafrika adui yetu ni uvivu, ulalamikaji, ulafi na umimi hasa ukabila

Hata wachina na wahindi waliwahi kutawaliwa na wazungu, Leo wahindi ndio kundi linaloongoza kwa kuwa na jamii yenye familia zenye kipato cha juu zaidi Marekani, Wachina wameipigisha nchi yao hatua kwa spidi ya radi
Mchina katawaliwa lini na mzungu?
 
Hivi chama kama ccm kinatawala nchi miaka nenda rudi kwa kuiba na kupora kura huku hakina kabisa mkakati wowote wa kuleta maendeleo sasa hapo mtu unakuja kumlaumu mzungu kwa lipi.

Unakuta mtu aliishastaafu urais lakini bado anarudi kuwa "power behind the throne" kwa kulazimisha fikra zake ndizo zitumike kuendesha nchi ili tu kukidhi maslahi yake na rais mwandamizi naye anakubali kwa sababu hana uwezo wa uongozi kwani ameukwaa uongozi kwa sababu tu ya kufa kufaana.

Afrika hatuna uongozi wa kuweza kulifanya bara hili liondokane na taswira ya kuwa "The laughing stock of the world."
 
Back
Top Bottom