Kwanini IMF na Benki ya Dunia wameitenga Tanzania katika mgao wa fedha za Corona? Au ule utani kwamba sisi matajiri, wao wametuibia, uliwachukiza?

Majibu kutoka kwa mataka a.k.a nyumbu za lumumba yatakua hivi...

... Misaada yao ina masharti hatuna shida nayo!

...Hao ni mabeberu na wezi.

... wanataka tufwate ushoga wao tuka kataa!!

... Usiepende misaada (wakati wamesahau juzi tu walipokea msaada kutoka WB)

... Wametunyima kwa sababu tuliwabana kwenye madini!!

...

Nakwakikishia haya ndio yatakua majibu yao hawa lumumba buku saba!! Ngoja waje uone akili zao zilivyo ndogo!!
 
Msaada!? Kutoka Word Bank na IMF?!!! Sio charity organisations zile. Ndio mambo Magufuli aliyoyakataa. Wanakupa mkopo wa harakaharaka halafu unafurahia eti umesaidiwa. Kama ni msaada wasamehe walizokupa maana kwao ndio ingekua rahisi zaidi
 
Kwani ule ulikua ni utani?

😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Donar Country
 
Jiulize kwa nini Ghadaff walimua ndio jibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona 'utani' kwenu ni kila kitu.
Hata mnapowasweka jela au kuwapiga risasi wenzenu mnacheka na kuwaambia ni watani wenu!

Huu 'utani' unaipaisha Tanzania kimataifa katika nyanja ya maendeleo.
 
Ukiona Mabeberu yanakunyima msaada ujue umeyabinya makende

Tanzania, Venezuela i na iran tunanyanyasika sana mbele ya Mabeberu ila tutapindua meza kibabe
 
LOoooh, unaelewa unachokiandika kweli?
 
Sie ACACIA wakitulipa trilion zetu,mambo yatakuwa mswano.

Sent using iphone pro max
 
Mkuu ambacho nafikiri hujakielewa ni kwamba hao mabeberu hawatoi msaada bali wanatoa mkopo mwenye riba hata hizo nchi zilizopewa fedha huo ni mkopo ndugu Na sio msaada, sasa la msingi na kuangalia hapa ni je,tunahitaji huo mkopo sana hasa katika kipindi hiki Cha matatizo ya corona au ni bora tusipate huo mkopo ili kujiondoa katika utumwa wa kutumikia deni?

Na hata nafikiria mh. Magufuli aliwajibu kiaina na kwa akili sana hao jamaa kwa kuwaambia badala ya kutuongezea mkopo katika hiki kipindi kigumu ni bora wangeweza kusamehe baadhi ya madeni ili hizo hela wanazolipwa kila mwezi kama marejesho basi wazitumie katika mapambano haya.

Kwa mtazamo wangu naona hatuhitaji huo mkopo wa fedha katika kipindi hiki maana ni kujiongezea janga jingine baada ya kupita hii corona na janga lenyewe litakuwa ni utumwa wa kulipa mkopo ambao mabeberu wameubatiza jina la “MSAADA”.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…