Kwanini injili ya Barnabas iliteketezwa?

Kwanini injili ya Barnabas iliteketezwa?

Majibu hayo aliyotoa mbona nilishauliza swali lake mkuu , sijajibiwa wewe rejea comments zangu
Mkuu nimesoma post zote kutafuta ulipojibu post #25 nimeona umejaribu ktk post #35 lakini kiukweli hujamjibu hizo hoja zake hata moja.
Bali yeye amekujibu au kukuonesha sababu za watu hao wa kanisa kuiona injili ya Barnaba alie andika ameghushi mambo.

Mfano anapo andika mtu historia ya Nyerere aseme alikufa wakati wa awamu ya nne, utaona stori yote ina walakini na batili.

Mtu anaposema alipanda meli Arusha akaenda Moshi utaona hiyo kitu ni tatizo
 
Mkuu nimesoma post zote kutafuta ulipojibu post #25 nimeona umejaribu ktk post #35 lakini kiukweli hujamjibu hizo hoja zake hata moja.
Bali yeye amekujibu au kukuonesha sababu za watu hao wa kanisa kuiona injili ya Barnaba alie andika ameghushi mambo.

Mfano anapo andika mtu historia ya Nyerere aseme alikufa wakati wa awamu ya nne, utaona stori yote ina walakini na batili.

Mtu anaposema alipanda meli Arusha akaenda Moshi utaona hiyo kitu ni tatizo
Ni tatizo akiandika barnaba tu au hata wakiandika wengine?
 
Ni tatizo akiandika barnaba tu au hata wakiandika wengine?
Injiri ya Barnaba ni tofauti kabisa na Injiri za kwanye biblia kwakuwa Injiri zote za kwenye biblia zinakubaliana kwa pamoja kuwa.
Yesu wa Nazaleti ndiye-
[emoji116]

-Pekee Kristo na Masihi.
-Bwana na Mwokozi wa watu wote wa ulimwenguni.
-Njia, Kweli na Uzima.
-Alitoka Mbinguni, akauvaa mwili wa binadamu, akaja duniani kupitia bikira maria, akahubiri, akateswa, akafa, akafufuka siku ya tatu, akapaa mbinguni, atakuja kuwahukumu wazima na wafu siku ya kiama.
-Ana mamlaka ya duniani na mbinguni.
Hajafa hadi leo na yupo anatawala mbinguni na duniani.
-Ni mwana wa Mungu.
-Anauweza wote, ni muumbaji wa vitu vyote.
-Ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.
-Amri alizotuagiza kuzifanya ndio za mwisho hakuna amri na maagizo mengine mapya.
-Alikuwepo kabla ya ulimwengu kuwapo.
-Injiri yoyote itakayoonekana ikipingana na Injiri yake basi ni feki na aliyeileta amelaaniwa.
-Atakuja kutufufua siku ya Mwisho na kutupeleka kwake mbinguni sisi tunaomwamini na kufuata maagizo yake kama agizo la UBATIZO.
-Mashetani, ma Ibilisi, ma Jini, Mapepo, na wafuasi wao ni jamii ya giza na yamelaaniwa yanasubiri kutupwa jehanam siku ya kiyama, hakuna JINI JEMA.
-Yesu Kristo Ndiye Masihi, Mungu Mkuu na Mwokozi wa watu wote.

[emoji115]
Hayo maelezo hapo juu ni baadhi ya maneno ambayo Injiri zote za kwenye biblia zinayasisitiza kwa uzito kubwa.
Tofauti ipo kwa,
Injiri ya kwenye kitabu cha Muhammadi (Qurani) na ya kitabu cha Barnaba, hayo mambo hayapo kabisa.
Injiri ya Qurani na Barnaba kwa pamoja zinasema
[emoji116]
-Muhammadi ndiye Nabii wa kumfuata kwa sasa.
-Yesu ni mtume tu kama Muhammadi.
-Yesu Kristo hakuwahi kuteswa, kusulubiwa wala kufa msalabani wala kufufuka.
-Yesu sio Mungu wala Mwana wa Mungu.
-Mungu hawezi kuwa na mwana kwakuwa hana mke.
-Uislamu ni Dini, na asiye mwislamu hawezi kufika mbinguni kwakuwa ni kafiri.
-Maagizo aliyo agiza mtume Muhammadi ndiyo ya msingi kufuatwa na watu wote.
-Mtume Muhamadi ndiye mtume wa mwisho, hakutatokea mtume mwingine mwenye kitabu na maagizo mengine.
[emoji115]
Hayo ni baadhi ya maagizo yanayosisitizwa sana, kwenye kitabu cha Qurani na kitabu cha Injiri ya Barnaba.
.....................................................

Hivyo msibishane hadi kutoana ngeu wewe Masudi Mshahala na wenzako.
Mjue kuwa,
Wakristo tuna Injiri yetu iliyopo kwenye Biblia.
Na ninyi Waislamu muna Injiri yenu iliyopo kwenye kitabu cha Qurani na kwenye kitabu cha Barnaba.

Tusilazimishane wala kuvutana kila mtu aifuate Injiri yake anayoiamini na mtume wake.

Tuonane siku ya KIYAMA.
Siku hiyo tutajua mbichi na mbivu .
Wasalaam.
 
Kuna wakristo biblia yao una vitabu 72, wengine 66, waethiopia vitabu 82 na wote wanasema waliongizwa na roho mtakatifu kukusanya hiv vitabu nanu yupo sahihi?? Na kwanini uww hivyo?
 
Ni tatizo akiandika barnaba tu au hata wakiandika wengine?
Mkuu tatizo sio nani kaandika ni bali nini kaandika?

Unaposema alisafiri kwa meli/mashua sehemu ambayo ni nchi kavu tu kama Dar kwenda Morogoro utasema huyo mtu anaongea ukweli?

Mimi nimekufafanulia huo mfano mmoja tu, wewe nenda karudie kapitie hoja zote zaidi ya 8 alizozitoa mdau Che mittoga pale juuu.
 
Kuna wakristo biblia yao una vitabu 72, wengine 66, waethiopia vitabu 82 na wote wanasema waliongizwa na roho mtakatifu kukusanya hiv vitabu nanu yupo sahihi?? Na kwanini uww hivyo?
Hiyo ni mada mpya.
Kwasasa tunajadili injiri ya Barnaba.
Hata Qurani inayotumiwa na
Wa-Suni na Wa-Shia zinatofautiana.
Ndio mana hawa wanafunga Ramadhani leo na wengine kesho yake.
Leo tunajadili kwanza umuhimu wa Injiri ya Barnaba.
Ukitaka kwingine anzisha mada yake maalum.
Kuleta mada nyingine ni kushindwa hoja ya msingi.
 
Ni tatizo akiandika barnaba tu au hata wakiandika wengine?
Tatizo akiandika mtu yeyote yule hata yesu kama akiandika vitu vya kutatanisha mfano kusafiri meli nchi kavu au tarehe tofauti kabisa za wakati wa kuishi mtu flani.

Hivi umesoma vizuri hoja za jamaa au unataka kubishana kama watu wa mitaani vijiwe vya kahawa?
 
Baada ya kuonekana iko tofauti sana na injili nyingine ndo mana ikapigwa marufuku. Hiyo injili huumiwa sana na waislam katika baadhi ya mandiko ku support Quran kwani yaongelea ujio wa mtume Muhhamadi na kutouliwa kwa Yesu msalabani.

Kama umuelewa unaeza gundua hizi dini ni miradi ya watu ili kutuweka akili zetu ndani ya BOX.
Hata kama sijawahi kuyaona maandishi ya huyu mtume Barnaba but hapo kwenye bold sidhani kama unasema kweli, nina hakika humfahamu vizuri Barnabas, Barnabas ndio mtume (kwanza tafsiri ya hilo jina lake ni mwana wa faraja and he was walking his name) ambaye kusema kweli ndiye aliye m sharp mtume Paul hata kawa vile alivyokua, Paul bada ya kumwamini Yesu alijikuta anakataliwa na jamii zote, jamii ya mafarisayo ambayo ndio alikotokea na jamii ya waamini wa Kristo, sababu ilikua ni hi, Mafarisayo waliona "amesariti imani yao" na so walimuona kama ni muasi regarding usomi aliokua nao through elimu yao na pia jamii ya waamini (kina Petro, Paul alipenda sana kumwita Petro kwa jina la Kefa) ilimtenga kwasababu walikua na mashaka nae kama ni kweli kaamua kuingia katika IMANI ya Yesu Kristo, remember wakati mwanafunzi wa kwanza wa Yesu anauawa (Stefano/Steven) Paul ndio alikua ana supervise mauaji hayo na story hi ilijulikana vizuri sana kwa waumini wa YEsu na mitume wake akiwepo Petro, BArnaba mwenyewe nk. Ni Barnaba ndio aliyemtia moyo sana Paul na kumsika mkono na kumfundisha mambo mengi yahusuyo Kristo na hatimae akawa ndio mtume aliye andika nyaraka nyingi kuliko mtume yeyote. Again PAul akiwa sasa kaanza kuhubiri Injili sehemu tofauti tofauti, kwenye team yake miongoni mwa watu waliokua nae ni Marko Yohana (Mark John), Luka na Barnaba mwenyewe, siku moja Marko Yohana (ndiye aliye andika Injili ya Marko) aliahirisha safari zao na kurudi Jerusalem kwa mama yake (umri wa huyu kijana ilikua ni tatizo, he was too young compered with others). Tukio hili lilimuudhi sana Paul na akaamua kutokuendelea nae kwenye safari zake za kimisheni, alimwondoa na kijana huyu akaonesha kukata tama sana, is Barnaba again who took care of him hadi akafikia hatua ya kuandika Injili hiyo ya Marko (kitabu cha pili tu ndani ya agano jipya) With saying so, kama huyu ndio aliyekua mwalimu wa Paul na ulimwengu wa Kiislam unamchukia sana mtume Paul, how comes alioyafundisha kwa Paul yawe tofauti na alicho kuja kuandika!? Hilo moja, lingne ni hili, wakati Barnaba yupo duniani na hadi anakufa, Uislamu na kitabu chake havikuwepo duniani kabisa, yaani hakukua na kitu kinaitwa UISLAM na au Quran duniani by that time, so how comes awe ni supporte wa kitu ambacho hakipo!? Mtume aliyeishi miaka mingi sana ni Yohana, nae alikufa miaka ya 96 baada ya Kristo, wenzie wote kina Petro, Paul, Barnaba mwenyewe, Mathayo, Luka nk walikua wameisha KUFA kitambo sana, uislamu umeanza mwaka 640 BK
 
Hata kama sijawahi kuyaona maandishi ya huyu mtume Barnaba but hapo kwenye bold sidhani kama unasema kweli, nina hakika humfahamu vizuri Barnabas, Barnabas ndio mtume (kwanza tafsiri ya hilo jina lake ni mwana wa faraja and he was walking his name) ambaye kusema kweli ndiye aliye m sharp mtume Paul hata kawa vile alivyokua, Paul bada ya kumwamini Yesu alijikuta anakataliwa na jamii zote, jamii ya mafarisayo ambayo ndio alikotokea na jamii ya waamini wa Kristo, sababu ilikua ni hi, Mafarisayo waliona "amesariti imani yao" na so walimuona kama ni muasi regarding usomi aliokua nao through elimu yao na pia jamii ya waamini (kina Petro, Paul alipenda sana kumwita Petro kwa jina la Kefa) ilimtenga kwasababu walikua na mashaka nae kama ni kweli kaamua kuingia katika IMANI ya Yesu Kristo, remember wakati mwanafunzi wa kwanza wa Yesu anauawa (Stefano/Steven) Paul ndio alikua ana supervise mauaji hayo na story hi ilijulikana vizuri sana kwa waumini wa YEsu na mitume wake akiwepo Petro, BArnaba mwenyewe nk. Ni Barnaba ndio aliyemtia moyo sana Paul na kumsika mkono na kumfundisha mambo mengi yahusuyo Kristo na hatimae akawa ndio mtume aliye andika nyaraka nyingi kuliko mtume yeyote. Again PAul akiwa sasa kaanza kuhubiri Injili sehemu tofauti tofauti, kwenye team yake miongoni mwa watu waliokua nae ni Marko Yohana (Mark John), Luka na Barnaba mwenyewe, siku moja Marko Yohana (ndiye aliye andika Injili ya Marko) aliahirisha safari zao na kurudi Jerusalem kwa mama yake (umri wa huyu kijana ilikua ni tatizo, he was too young compered with others). Tukio hili lilimuudhi sana Paul na akaamua kutokuendelea nae kwenye safari zake za kimisheni, alimwondoa na kijana huyu akaonesha kukata tama sana, is Barnaba again who took care of him hadi akafikia hatua ya kuandika Injili hiyo ya Marko (kitabu cha pili tu ndani ya agano jipya) With saying so, kama huyu ndio aliyekua mwalimu wa Paul na ulimwengu wa Kiislam unamchukia sana mtume Paul, how comes alioyafundisha kwa Paul yawe tofauti na alicho kuja kuandika!? Hilo moja, lingne ni hili, wakati Barnaba yupo duniani na hadi anakufa, Uislamu na kitabu chake havikuwepo duniani kabisa, yaani hakukua na kitu kinaitwa UISLAM na au Quran duniani by that time, so how comes awe ni supporte wa kitu ambacho hakipo!? Mtume aliyeishi miaka mingi sana ni Yohana, nae alikufa miaka ya 96 baada ya Kristo, wenzie wote kina Petro, Paul, Barnaba mwenyewe, Mathayo, Luka nk walikua wameisha KUFA kitambo sana, uislamu umeanza mwaka 640 BK
Umeandika vema,..ila umewachanganya Barnaba wawili tofauti mkuu
 
Injiri ya Barnaba Sio Injiri ya Kristo na haiendani na Theolojia ya Kristo hivyo haina mashiko kwa Wakristo.
Machache kati ya hayo ni kwamba.
-Mwandishi wake alikuwa na uelewa mdogo sana kuhusu jiografia ya Upalestina.
-Katika sura ya 99:21 mwandishi anaeleza alipanda kwa miguu kuelekea kijiji cha Kapernaumu, wakati kijiji hicho kipo zaidi ya mita 200 chini ya usawa wa bahari.
-katika sura ya 100 mwandishi anaeleza kuwa Yesu Kristo alienda Nazareti kwa mashua wakati kijiji hicho kipo mita 500 juu ya usawa wa bahari,
-Katika sura ya 151 anasema pia kuwa Yesu alienda Yerusalemu kwa mashua ukiangalia ramani inapingana na huo usemi.
-Barnaba ndiye pekee aliyeandika kuwa Mamajusi waliompelekea zawadi mtoto Yesu, walikuwa watu watatu tu, tofauti na Injiri ya Yesu ambayo haijataja idadi ya Mamajusi bali imetaja idadi ya zawadi tatu walizopeleka (uvumba, manemane na dhahabu)
-Katika sura 40:41 Barnaba analitaja jina la tunda la mti wa mema na mabaya kuwa ni tunda la Tofaa, lile alilokula Hawa ktk bustani ya Edeni, wakati kitabu cha mwanzo na Biblia kwa ujumla ambayo ndiyo chanzo pekee cha habari hii, haijataja popote jina la tunda la Tufaa ktk maelezo yake.
-Katika sura ya 54 Barnaba ameitaja Dinari kuwa ina Minuti 60, bila kujua kuwa Minuti ilikuwa fedha ya Uhispania iliyoanza kutumika mwaka 685 baada ya Kristo wakati wa utawala wa Khalifa Abdul Malaki. Enzi za Yesu hiyo fedha haikuwepo.
- Katika sura ya 150 Barnaba anaeleza kuwa Yesu Kristo alizaliwa wakati wa utawala wa Pontio Pilato akiwa kiongozi, wakati ukweli ni kwamba utawala wa Pilato ulianza mwaka 26 na 27 baada ya Kristo kuzaliwa.
-Katika sura ya 97 Barnaba anamtaja Mtume Muhammad kuwa ni Masihi na Yesu anamwita Kristo bila kujua kuwa neno Kristo ni kwa Kigiriki na Masihi ni kwa Kiebrania yakiwa na maana moja.
-Katika sura ya 222 Barnaba anaeleza kuwa Yesu Kristo hakusulubiwa, aliondolewa na Malaika, kisha Yuda alisulubiwa badala yake.
-Katika sura ya 44 Barnaba anaeleza kuwa Ibrahimu alimtoa Ishmaeli awe sadaka katika madhabahu, na anamwita Mungu wa Ibrahimu, Ishmaeli na Yakobo, tofauti kabisa na Mwanzo 22.
-Katika sura ya 192 Barnaba anasema Mwishmaeli ndiye aliyeiandika Torati.
-Barnaba anamweka mtume Muhammadi kama mbadala wa Yesu kristo, angalia sura ya 44, 45, 9, 112, 39 na nyinginezo ktk kitabu hicho.
{ hii ndiyo injili mnayoipigania iwekwe kwenye Biblia takatifu ? }
Katika ukweli huu mchache nadhani wasomaji mmeelewa mlengo wa Injiri ya Barnaba wala sina haja ya kuwaambia.
Injiri iliyowekwa katika biblia inaeleza wazo moja (maudhui yanafanana) ingawa inatofautiana maneno kutokana na mazingira ya kila mwandishi alivyofunuliwa na Yesu mwenyewe, tofauti na Injiri ya Barnaba.
[ Ndio maana kuna msemaji mmoja hapo juu nimemwambia, kama anaihitaji Injiri ya Barnaba, inapatikana madukani, akainunue na kuitumia ]

Hapo zamani za kale, kuna mtume mmoja alitokewa na kiumbe asichokijua, kwenye pango, na bila ya kujitambulisha kwamba kiumbe hicho ni kiumbe gani. Ghafla kikamkaba Koo na kumwambia " SOMA "
Asante zikufikie.
 
Baada ya kuonekana iko tofauti sana na injili nyingine ndo mana ikapigwa marufuku. Hiyo injili huumiwa sana na waislam katika baadhi ya mandiko ku support Quran kwani yaongelea ujio wa mtume Muhhamadi na kutouliwa kwa Yesu msalabani.

Kama umuelewa unaeza gundua hizi dini ni miradi ya watu ili kutuweka akili zetu ndani ya BOX.
Waislamu huwa ukataa utume wa Paulo kwa kigezo kwamba " Paulo hakuwa miongoni mwa wale wanafunzi 12 wa Yesu ". Kutokuwa moja wa wale thenashara inamfanya Paulo asiwe mtume, na kama si mtume maandiko yake si sahihi kwa maana hakuwa na hiyo mamlaka ya kiutume kuandika hivyo vitabu vikawekwa kwenye Biblia.

Barnaba hakuwa miongoni mwa wanafunzi kumi na mbili, na alikuwa rafiki yake Paulo, kila sehemu alipokwenda Paulo, Baranaba alikuwepo, lakini Waislam kwa akili zao kubwa kupita kiasi wanaona kuwa Barnaba ni mtume na maandishi yake wanapaswa kutumia hadi na Waislamu. Huwa ninajiuliza, kwanini Paulo ambaye hakuwa miongoni mwa thenashara asiwe mtume, na Barnaba ambaye pia hakuwa mmoja wa thenashara ( wanafunzi 12 ) amekuwa mtume hadi anaaandika kitabu kinachopendwa na Waislamu?????. Barnaba ana kitu gani cha ziada????.

Kwa watu wenye akili hawawezi kuamini kile Waislamu wanachokiita "Injili ya Barnaba" kwa sababu Barnaba, mtume Mkristo, hakufundisha vitu vingine vilivyokuwa vinatofautiana na mitume wengine kama akina Paulo, Petro, Yohana n.k. nitatoa ushaudi wa kwamba Barnaba hawezi kufundisha kitu tofauti na Mtume Paulo ( asiyekuwa mtume kwa Waislamu ) ambaye waliongozana kwenda kuhubiri katika miji ya wayunani na pia kubishana na wayahudi wenye imani kali.

1. Paulo alipoongoka kwa mara ya kwanza, alikwenda kanisani Yerusalemu ambapo waumini wote walimkimbia, lakini BARNABA alimchukua akampeleka kwa mitume ( Petro, Yakobo na Yohana )huko huko Yerusalemu. ( Matendo ya Mitume 9:26-27).

2. Kanisa huko Yerusalemu waliposikia ya kwamba mataifa wanaliamini neno la Mungu wakamtuma BARNABA aende Antiokia kuiona hiyo neema, lakini Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Sauli ( Paulo ) akamleta Antiokia, wakakaa wakihubiri na kulifundisha pamoja kwa mwaka mmoja. ( Matendo ya mitume 11:19-26).

3. BARNABA na Paulo walibishana na wayahudi waliokuwa wanataka kuwapotosha wakristo. Mtazamo wa Baranaba na Paulo ulikuwa ni mmoja kuhusu kile walichokuwa wanakiamini ( Matendo ya Mitume 15: 2 ).

4. Paulo analiambia kanisa la Galatia kwamba "Paulo na BARNABA walipokwenda Yerusalemu kwa mitume Petro, Yakobo na Yohana, mitume hawa waliwapa mkono wa kiume wa shirika ili waende kwa mataifa na hao mitume wabaki kwa Wayahudi ( Wagalatia 2:9-10)

5. Baraza la kwanza la mitume wote lilipokaa Yerusalemu, wakapitisha baadhi ya sheria kwa watu wa mataifa, waliwapa Paulo na BARNABA hizo nyaraka wazisambaze kwa makanisa mbalimbali. ( Matendo ya mitume 15:1-35 ).

Kwa mifano hiyo hiyo ni dhahiri kabisa kuwa BARNABA hawezi kuja na injili inayopingana na mafundisho yaliyoko kwenye nyaraka za Paulo, Yakobo, Petro na Yohana. Hiyo Injili ya Barnabas imeandikwa baada ya miaka mingi kupita wakati huo Barnaba alikuwa ameshakufa. Injili ya Barnaba inasadikika kuandikwa mwaka 120 AD, wakati Mtume wa mwisho kufa alikuwa Yohana aliyekufa mwaka 100AD.

Hii injili ya Barnabas iliandikwa na Waislamu wenyewe ili waitumie kupotosha Wakristo wasiojielimisha.
 
Hata Qurani inayotumiwa na
Wa-Suni na Wa-Shia zinatofautiana.
SIO KWELI
Ndio mana hawa wanafunga Ramadhani leo na wengine kesho yake.
Leo tunajadili kwanza umuhimu wa Injiri ya Barnaba.
.
Hilo wala halina uhusiano wowote na u-Shia au u-Sunni na wala halijazungumzwa popote kwenye Quran!

Haya, tuendelee Mkuu na hoja ya Barnaba! Nilitaka tu kukurekesbisha hapo juu manake Bwana Yesu anakemea kusema uongo! Nahisi ulisema uongo kwa kutofahamu na ndio maana nimekurekebisha!
 
naomba kujua kwanini injili ya barnaba iliteketezwa ni karatasi mbili pekee ndizo zilizosalia moja ilikua imeandikwa kwa lugha kihispania na moja kwa kitaliano je sababu zilikua ni zipi kwani barnaba hakua mwanafunzi wa yesu au kuna vitu tunafichwa tusivijue?
nilikua nasoma nakala moja inasemekana injili hiyo wakati wa pope glacious aliiteketeza na aliipiga marufuku kutumika kwanini?
Nilibahatika kusoma nakala ya injili hiyo na kwa kiasi kikubwa inakubaliana na mafunzo ya Quran. Huenda ni kwa sababu hiyo ndo ikazuiwa isisomwe ili watu wasijewakaona hakuna kupingana katika mafunzo ya imani mbili hizi.
 
natumaini wote wazima ndugu zangu wa jf intelligence,
bila kupoteza muda naomba niende moja kwa moja kwenye kichwa husika cha mada

kwanza kabisa naomba kujua kwanini injili ya barnaba iliteketezwa ni karatasi mbili pekee ndizo zilizosalia moja ilikua imeandikwa kwa lugha kihispania na moja kwa kitaliano je sababu zilikua ni zipi kwani barnaba hakua mwanafunzi wa yesu au kuna vitu tunafichwa tusivijue?
nilikua nasoma nakala moja inasemekana injili hiyo wakati wa pope glacious aliiteketeza na aliipiga marufuku kutumika kwanini?
na kwanini vitabu vingine vya injili havijajumuishwa kwenye bible?
pili nimekua nikisoma tu bible ila kuna vitabu vya watu wengi ambao ndio waliokua wanafunzi wa yesu lakini je ni wote walioteuliwa kuandika injili na yesu? kwa maana nyingine ni nani aliyeteuliwa na yesu mwenyewe aandike injili?

natumaini maswali yangu yameeleweka kama nitakua nimekosea mahala basi turekebishane kwa kua wote tupo kujifunza naomba wajuzi wa mambo mnisaidie kupata hayo majibu ya hayo maswali husika ufia dini tuweke pembeni

nawasilisha
Injili iliyofichwa sio ya barinaba tu hata ya Yesu mwenyewe aliyo andika kwa mkono wake imefichwa haiwezekani Mungu ampe Yesu injili alafu iandikwe na wengine yeye mwenyewe asiandika
Kuna andiko moja Yesu anasema
TUBUNI NA KUIAMINI INJILI HII hivyo inaonyesha yake aliandika mwenyewe ila imefichwa ili kuwapoteza watu
 
ukurasa wa.70 hicho Kitabu Anakwambia Malaika woote watakufa
emoji38.png
emoji38.png
halafu muisilamu wanaamini hicho Kitabu ni sahihi
emoji12.png
Mkuu kwani wewe una maoni tofauti? NI YEPI BASI?
 
Uhalisia unaonesha cc ni wamoja lakini inaonekana kuna wanaong'ang'ania tuwe tufauti.
 
Back
Top Bottom