Kwanini Jude Bellingham amepewa Kadi nyekundu na mchezo ulikuwa umekwisha malizika?

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2012
Posts
11,622
Reaction score
26,005
Refareee Jesús Gil Manzano amemuonesha kadi nyekundu Mchezaji wa Real Madrid Jude Bellingham kwenye mechi iliyokuwa inachezwa kati ya Real Madrid na Valencia.

Mzozo Huo ulitokea baada ya Refa kumaliza Mchezo wakati mpira Ulikuwa Hewani na baada ya mpira kutua ukatua Nyavuni na Refa kukataa Goli hilo na ndipo Mchezaji huyo akatoa maneno yaliyomchukiza Refa.

Bila kujali kuwa mchezo umeisha akampachika Kadi nyekundu..

Kwa wachambuzi na Waelewa hii kitu iko sawa kweli

 
Alijiona Superstar kwenye hakuna
 
Unamaanisha hiyo kadi alipewa nje ya uwanja? yani mfano ingekuwa pale lupaso kwa mkapa wapeane kadi nje kule viwanja vya duce au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…