Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naomba tujadili hii hoja
Ukimuuliza mtanzania swali tegemea kuulizwa swali kabla hata hajakujibu swali ulilomuulizaWewe unadhani ni kwa sababu gani?
Hivi nursing na uhasibu kwa level ya form four na ualimu wapi wanachukuliwa wenye marks chafu? Chunguza utaona kimbilio la walio feli ni uhasibu na nursing, walimu wanachukuliwa wenye 4 ya 26 na 28 wakati nursing hadi 30 ilimradi awe na D ya Bios, pia CBE pale Dodoma wanadahiliwa hadi wenye Zero za mwanzo yani 4 negative!
System ya kuchukua hata watu waliofeli wakasome ualimu mwisho wa siku inaonekana ni profession ya watu wasiojiweza kielimu, watu wanachukulia tumefeli ndo maana ni walimu.
wengi ni magumashi tu elimu zao hazieleweki hata vyeti vya form four hawana ila ni walimu, siku msako ukipita ndo watajua kumbe walimu hakuna.
sijui kwa sababu ya kupata kazi kimagumashi ndo maana hata haki zetu hatuzijui, sijui ndo nidhamu ya ki ualimu mi sielewi,
tunafanyishwa vikazi hata bila malipo wakati inatakiwa tulipwe ukiuliza eti ni oder kutoka juu, juu mbinguni au?
mishahara midogo, mazingira ya kazi ovyo n.k n.k
idara ya elimu ubabaishaji mwingi tofauti na kada zingine ndo maana mambo ni ovyo
Kwani waalimu mnalipwa sh. Ngap? Ili tujue mshahara wenu kweli mdogo!!
mi naona kuwa msahara mdogo we angalia mwalimu mwenye shahada analipwa na anapitwa na daktari au injinia mwenye diploma!