Kwanini Kenya wamefuta Mitihani ya Taifa kwenye Mtaala mpya?

Kwanini Kenya wamefuta Mitihani ya Taifa kwenye Mtaala mpya?

Elim inahitaji reshaffle kubwa sana hii tabia ya kumpima mtoto na mitihan ya taifa ifeee!!!!!

Ulaya USA hakuna hii kitu chek kipaji cha mtoto mpeleke huko huko
Ronald,mess,pogba,na wengine ni mabilionea lakn hawana hata masters degree
Si kweli ulaya hakuna mitihani, ipo, sema kuna options nyingi za assessment, mtoto anachagua option anayotaka
 
Si kweli ulaya hakuna mitihani, ipo, sema kuna options nyingi za assessment, mtoto anachagua option anayotaka

Watu wanapenda kudanganyana. Halafu wengi ukiangalia ni ushabiki tu. Hakuna hata hoja ya maana wanayojenga au kuonesha.
Wee tangu lini mtoto aanze darasa la kwanza mpaka anamaliza level hiyo bila kupimwa kama alielewa yale aliyokuwa amefundishwa?? Na kipimo cha kuelewa duniani kote ni mtihani ama uwe wa kuandika au wa kuzungumza.
Mpaka mmoja anadiriki kudanganya kwamba ulaya hakuna mitihani wakati si kweli. Huyu mbarika atafute kitu kinaitwa ects ajionee kama kweli ulaya hakuna mitihani.
Mitihani haikosi, hata mataifa ya Asian Tiger tunayoyaonea tamaa, wana mitihani. Ambayo lengo lake ni kupima uelewa wa wanafunzi. Kuboresha elimu ili ionekane ina tija zaidi kwa jamii, ni kuangalia kama yale yanayofundishwa na namna wanavyofundishwa yana saidia katika kuleta maendeleo chanya ya jamii na nchi kwa ujumla. Kwa hiyo tuangalie elimu kwa ujumla wake, na si kuangalia kipengele kidogo sana cha mitihani.
 
Watu wanapenda kudanganyana. Halafu wengi ukiangalia ni ushabiki tu. Hakuna hata hoja ya maana wanayojenga au kuonesha.
Wee tangu lini mtoto aanze darasa la kwanza mpaka anamaliza level hiyo bila kupimwa kama alielewa yale aliyokuwa amefundishwa?? Na kipimo cha kuelewa duniani kote ni mtihani ama uwe wa kuandika au wa kuzungumza.
Mpaka mmoja anadiriki kudanganya kwamba ulaya hakuna mitihani wakati si kweli. Huyu mbarika atafute kitu kinaitwa ects ajionee kama kweli ulaya hakuna mitihani.
Mitihani haikosi, hata mataifa ya Asian Tiger tunayoyaonea tamaa, wana mitihani. Ambayo lengo lake ni kupima uelewa wa wanafunzi. Kuboresha elimu ili ionekane ina tija zaidi kwa jamii, ni kuangalia kama yale yanayofundishwa na namna wanavyofundishwa yana saidia katika kuleta maendeleo chanya ya jamii na nchi kwa ujumla. Kwa hiyo tuangalie elimu kwa ujumla wake, na si kuangalia kipengele kidogo sana cha mitihani.
atakuwa form IV failure ukiangalia maandishi yake ni mtu amekata tamaa anataka pa kutokea!
 
Mwanangu mdogo yupo kwenye huu mtaala wa CBC, ila kiukweli ni shughuli, namna wanavyofunzwa, wanavyoshughulishwa, na pia sisi wazazi tunavyoshughulishwa yaani tu, mwanzoni nilikua mojawapo wa waliosuasua lakini hadi hapo nimetokea kuupenda. Uzuri ni mtaala ulioandaliwa na watalaam waliochukua muda wao kudadavua mfumo wote wa elimu Kenya na bara lote na mahitaji ya dunia ya leo.
Hongera sana wazalendo wetu mliofanikisha hili.
 
img-20220117-wa0138-jpg.2085700
 
Mwanangu mdogo yupo kwenye huu mtaala wa CBC, ila kiukweli ni shughuli, namna wanavyofunzwa, wanavyoshughulishwa, na pia sisi wazazi tunavyoshughulishwa yaani tu, mwanzoni nilikua mojawapo wa waliosuasua lakini hadi hapo nimetokea kuupenda. Uzuri ni mtaala ulioandaliwa na watalaam waliochukua muda wao kudadavua mfumo wote wa elimu Kenya na bara lote na mahitaji ya dunia ya leo.
Hongera sana wazalendo wetu mliofanikisha hili.
Tunaomba mtusaidie, Kenya wamerejea mfumo wa nchi gani ambao wameona umefanikiwa hapa duniani, au Ndio kwanza wameugundua hapo Kenya?, Kama ni ugunduzi wao, basi tunahitaji muda wa kufanyia majaribio Kama kweli ni Bora kuliko huu wa mitihani.
 
Mwanangu mdogo yupo kwenye huu mtaala wa CBC, ila kiukweli ni shughuli, namna wanavyofunzwa, wanavyoshughulishwa, na pia sisi wazazi tunavyoshughulishwa yaani tu, mwanzoni nilikua mojawapo wa waliosuasua lakini hadi hapo nimetokea kuupenda. Uzuri ni mtaala ulioandaliwa na watalaam waliochukua muda wao kudadavua mfumo wote wa elimu Kenya na bara lote na mahitaji ya dunia ya leo.
Hongera sana wazalendo wetu mliofanikisha hili.
Mimi niliipenda CBC tangia siku ya kwanza. Wala sikunung'unika hata siku moja ndugu yangu. Kuhusishwa moja kwa moja, yaani 'hands-on', kwenye shughuli za kielimu za mwanangu imekuwa baraka kubwa sana. Sio tu kielimu kwa mwanangu, imeleta faida tele kwangu, kwa familia yangu kwa ujumla na kwenye shughuli yote ya kutekeleza majukumu yangu kama mzazi. Hujakosea ulipowaita wazalendo, hao waliofanikisha mtaala huu. Hongera zao.
 
Mitihani ikifutwa kuna watu watashindwa kuhalalisha uwepo wao.

Wengi mnakurupuka bila kutulia muelewe mfumo wenyewe, ifahamike ni mtaala ulioandaliwa kwa kuzingatia mambo mengi sana na iliwachukua wataalam muda ikiwemo kuwashirikisha wadau wote, kwa hivyo sio kitu cha kupuuza kizembe bila kushirikisha ubongo.
Mitihani itakuwepo ila sio ya kiushindani kama ilivyo kwa mtaala wa kitambo, lengo la mitihani itakua kumsaidia mwanafunzi achangamkie fani iliyo bora kwake.
Na mtihani hautakua kama huu wa sasa wa mpigo mmoja, itakua kama ilivyo vyuoni ambapo tulifanya CAT, matokeo yanaangaliwa kuanzia ulipoanza shule mpaka unamaliza msingi ili ieleweke nini utasomeshwa kwenye kila daraja. Samaki afunzwe kuogelea, naye gedere aonyeshwe ukweaji wa miti, kila mmoja aelekee kunakomhusu.

Mtihani wa leo kwenye mtaala wa kitambo, miaka yote ya shule ya msingi inaweza ikaharibiwa na tukio la siku tatu ambazo mnafanya mtihani, ukiwa na tatizo lolote, iwe labda umepanic, au umeumwa au issue yoyote tu, vikusababishe uteleze kwenye kujibu maswali ndio imekula kwako, na hapo kwanza mnashindanishwa na wenzako, mtu wa St. Kayumba unapambanishwa na wale wa Feza shool bila kuzingatia chochote.
Mambo kama hayo yanasababisha taarifa kama hizi hapa chini, itazame hii video ya kusikitisha.

 
Wengi mnakurupuka bila kutulia muelewe mfumo wenyewe, ifahamike ni mtaala ulioandaliwa kwa kuzingatia mambo mengi sana na iliwachukua wataalam muda ikiwemo kuwashirikisha wadau wote, kwa hivyo sio kitu cha kupuuza kizembe bila kushirikisha ubongo.
Mitihani itakuwepo ila sio ya kiushindani kama ilivyo kwa mtaala wa kitambo, lengo la mitihani itakua kumsaidia mwanafunzi achangamkie fani iliyo bora kwake.
Na mtihani hautakua kama huu wa sasa wa mpigo mmoja, itakua kama ilivyo vyuoni ambapo tulifanya CAT, matokeo yanaangaliwa kuanzia ulipoanza shule mpaka unamaliza msingi ili ieleweke nini utasomeshwa kwenye kila daraja. Samaki afunzwe kuogelea, naye gedere aonyeshwe ukweaji wa miti, kila mmoja aelekee kunakomhusu.

Mtihani wa leo kwenye mtaala wa kitambo, miaka yote ya shule ya msingi inaweza ikaharibiwa na tukio la siku tatu ambazo mnafanya mtihani, ukiwa na tatizo lolote, iwe labda umepanic, au umeumwa au issue yoyote tu, vikusababishe uteleze kwenye kujibu maswali ndio imekula kwako, na hapo kwanza mnashindanishwa na wenzako, mtu wa St. Kayumba unapambanishwa na wale wa Feza shool bila kuzingatia chochote.
Mambo kama hayo yanasababisha taarifa kama hizi hapa chini, itazame hii video ya kusikitisha.

Inaonekana wazi hili ni Jambo jipya ambalo linaonekana kuwa ni Bora kinadharia, Je Kuna nchi yoyote ambayo Kenya imejifunza toka kwao au ndio mwanzo hapo Kenya?, Kama ndio mwanzo, basi ngoja kidogo tuone ufanisi wake, ni mapema mno kupinga au kupongeza mfumo huu.
 
Great answer.

Naomba mfano wa wawili au watatu ambao kwa sasa wanatoa ajira au hata sehemu walipo!.
Akimtaja unitag mkuu!!Mi sijaona hata Mimi ni graduate LAKINI nazalisha ajira za house girl tu na kuuza duka out of the professional yangu!!!
 
Mimi niliipenda CBC tangia siku ya kwanza. Wala sikunung'unika hata siku moja ndugu yangu. Kuhusishwa moja kwa moja, yaani 'hands-on', kwenye shughuli za kielimu za mwanangu imekuwa baraka kubwa sana. Sio tu kielimu kwa mwanangu, imeleta faida tele kwangu, kwa familia yangu kwa ujumla na kwenye shughuli yote ya kutekeleza majukumu yangu kama mzazi. Hujakosea ulipowaita wazalendo, hao waliofanikisha mtaala huu. Hongera zao.

Bado hujaeleza kinaga ubaga nini ni faida ya mfumo huu mpya, ukilinganisha na mfumo wa zamani. Ndiyo ni baraka, lkn ni baraka zipi hizo!?
 
Mtoa mada taarifa yako haijakamilika vzuri,au haujaifanyia uchunguzi,si kweli kwamba hakuna mitihani Kenya,Ipo tena mingi mno,
 
Bado hujaeleza kinaga ubaga nini ni faida ya mfumo huu mpya, ukilinganisha na mfumo wa zamani. Ndiyo ni baraka, lkn ni baraka zipi hizo!?
Kama unataka kujua mengi zaidi kuhusu mtaala wenyewe fanya risechi yako mwenyewe. Sio jukumu langu kukuelimisha, acha uvivu.
 
Longolongo nyingi. Ili mtu awe competent lazima awe na knowledge. Knowledge is acquired through: 1. REFLECTION 2. IMITATION 3. EXPERIENCE
Hapo sasa, mtaala huo mpya wa CBC unatilia mkazo kwenye 'competence'. Yaani uwezo wa mwanafunzi 'ku-apply' hiyo 'knowledge' aliyoipata shuleni kwenye maisha ya kawaida. Sio tu kwenye shughuli ya kupita mitihani ya 'kitaifa'. Ambayo sasa itatupiliwa mbali na nafasi yake kujazwa na mitihani kadhaa(assessments). Ambazo zitakuwa zinafanywa mara kwa mara, sio tu mwisho wa mwaka au labda baada ya miaka 6 ya elimu ya shule ya msingi/miaka 6 ya shule ya upili.
 
Back
Top Bottom