Kwanini kipimo cha nguvu za Mungu maishani mwako kiko kichwani na kinywani mwako?

Kwanini kipimo cha nguvu za Mungu maishani mwako kiko kichwani na kinywani mwako?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Tofauti yako na yule ambaye unaona anamfaidi Mungu na nguvu zake iko kichwani na kinywani mwako.

Wote ambao akilini mwao wanaamini katika ufinyu na uhafifu wa uwezo wa Mungu watafaidi uhafifu na ufinyu huo.

Wale wanaoamini katika na kusadiki kabisa kuwa kwao Mungu ananguvu na uweza wote kuliko kitu chochote hao ndio watakaofaidi ukuu huo.
Kazi hii inafanyika kichwani mwako.

Unachokiamini kichwani sharti ukinene mdomoni. Ukisikia mtu anasema anaamini Mungu wakati mdomoni anatamka mambo ya shetani, uchawi, kulongwa, na kushindwa hali ya maneno yako ndio itakayokuzunguka.
Warumi 10:10
Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

Ni hayo tu.
 
Binadamu mnahangaika sana kumuongelea mungu kwa vile hayupo kujiongelea mwenyewe.

Mnahangaika sana kutetea kisicho kuwepo kwa vile hakipo kujitetea chenyewe.
 
Kwa waislam Allah ndo mwenye nguvu na kwa wakristo Yesu ndo mwenye nguvu.
Point ya msingi ni kwamba hata ukiabudu Mungu wa uongo ni sawa, usipoabudu pia ni sawa tu. Yaani kweli na uongo havina utofauti ndo maana waislam na wakristo wanaabudu miungu tofauti lkn wote wana matokeo yaliyo sawa, mkristo anasema kupitia Yesu maombi yake yanajibiwa na muislam nae anasema Allah anajibu maombi yao
 
Back
Top Bottom