Kwanini kushindwa kuowa kwa binamu yangu ilikuwa ni faraja kwa mama yake mzazi (shangazi)

Mwizukulu mgikuru

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2021
Posts
5,715
Reaction score
13,739
Habari zenu wakuu, kuna jambo lilikuwa likiniacha njia panda sana,

Kuna binamu yangu umri wake kwa sasa ni 33 to 34 hajaowa mpaka sasa na amekuwa akipambana kujiweka sawa kiuchumi na huku akitafuta mwenza wa maisha yake.

Baba yake mzazi amekuwa akimshauri mwanae umri umekwenda na muda mwingine hufikia kumwambia binamu yangu kama anahitaji msaada wa hali na mali basi aseme ili aweze kuowa.

Lakini kwa upande wa mama yake mzazi yaani shangazi yangu kila jamaa anapojitahidi kupiga hatua ili afikie lengo lake na akaferi basi shangazi huonekana kama anafurahia ile hali na muda mwingine huwa mgumu wa kutoa hata ushauri kwa huyo binamu.

Hili jambo tumeshindwa kufahamu tatizo ni nini au ni laana?
 
Apelekwe Buza Kwa lulenge ukutane na kiboko ya wachawi

USSR
 
Kushindwa kufanya nini kwa binamu yako?
 
Um
Umri wake ni 33-34 lkn hajafanya nini?
 
Ili
Ili aweze kufanya nini?
 
huyo mama msimwone ni mmbaya,,anamwonea huruma mwanae,manake anajua wanake walivo hasa wanawake hawa wa leo ukichukulia na yeye ni mwanamke na amekula chumvi nyingi anajua alichokuwa akimfanya mumewe,na pia anajua wanawake wenzake wanachowafanyia waume zao mpaka kuwaloga na kuwavuruga kisaikolojia kimakusudi manake wanasimuliana,,ndoa nyingi siku izi ni mateso makubwa sana!!!! hamna ndoa salama,,mauaji ya wanandoa yamezidi,umesikia juzi kuna mdada kaachana na mumewe na kwenda kupanga ,mumewe kamnyatia kamuua na kumzika kwenye kinyesi!!!,,,,so musimlaumu huyu mama,,,ndo manake HASHRAF HAKIM yule mchezaji wa ulaya,alimwandikisha mama yake mali zake zote,,,so mkewe alipomshtaki kwenda mahakamani ikaonekana msela hana k2!!! MSIMLAUMU!!
 
Huyo mama itakuwa kataa ndoa πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
point ipo hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…