Ni kweli ukataji miti holela kwa ajili ya kuni na mkaa ni janga la kitaifa na lina madhara makubwa na ya muda mrefu.
Lakini, tatizo la ukataji miti hapa nchini sio la leo wala jana. Ni tatizo la miaka nenda rudi. Ni tatizo lililokuwepo hata kabla ya uhuru wa nchi hii.
Tofauti ni kwamba tatizo halikuonekana wakati huo sababu population ilikuwa ndogo ukilinganisha na sasa.
Tukija kwenye ukame, dunia nzima kwa sasa inakabiliwa na ukame wa kutisha. Mwaka huu pekee nchi za Ulaya na Amerika zilikuwa na kiwango kikubwa sana cha joto ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya nchi hizo.
Mvua nazo zimekuwa kwa kiwango kidogo sana au hakuna kabisa maeneo mbali mbali ya dunia. Mfano huko California, USA, ambako ndiko kunafanyika shughuli nyingi za kilimo, mwaka huu hakuna walichofanya sababu hakuna mvua!!
Ripoti ya maswala ya hali ya hewa kwa bara la Africa inaonesha kwamba nchi za pembe ya Africa, Africa mashariki, na kusini kutakuwa na ukame mkubwa sana ambao unaweza kudumu kwa zaidi ya miaka 3. Taarifa hiyo inaonesha kwamba ukame huo ulianza tangu mwaka jana.
Binafsi sikubaliani na uongozi wa Samia na Makamu wake, lakini kwa hili la ukame it is something out of their reach. Tukiwalaumu wao ni kuwaonea wakati wamekaa madarakani kwa mwaka mmoja tu!!!!
Hata hivyo kwa namna fulani Samia na Serikali yake wanabeba lawama kwa kutokuwa proactive. Walipaswa kusoma alama za nyakati mapema tu walipoingia madarakani na wangewekeza nguvu kubwa sana kwenye nishati ya gesi asilia ambayo tunayo ya kutosha hapa nchini.
Kwa kumalizia, elewa kwamba matatizo ya ukame ni ya dunia nzima. Shirika la chakula duniani walishatoa angalizo kuwa miaka 2 ijayo dunia itakuwa na uhaba mkubwa sana wa chakula ambao haujawahi kuonekana katika historia ya dunia hii na yote hiyo ni sababu ya ukame!!!
Kwa sisi WAKRISTO WA KANISA LA KWELI LA MUNGU, tunafahamu hayo hayana budi kutokea kipindi hichi maana yote yametabiriwa kwenye kitabu cha UFUNUO, DANIELI na MATHAYO.
Ukame huu, Vita vya Urusi na Ukraine, milipuko ya magonjwa yasiyokuwa na tiba, kupanda kwa gharama za maisha, watu kuuana hovyo hovyo, nk, yote hayo ni maandalizi tu ya ile DHIKI KUU ambayo itaikumba dunia nzima miaka michache ijayo.
We are getting very close to the end of ages!!
Mwenye kusoma na afahamu, mwenye masikio na asikie.