Kwanini Lugha ya wanajeshi huko Congo ni Kiswahili na sio Lugha zao za asili?

Tanzania tutumie kishwahili ku influence mahashariki ya Kongo.
 
Kiswahili kipo Kongo miaka na miaka, kama kuna mwanaccm alikuambia kuwa kiswahili ni lugha yetu alikudanganya. Kongo, Rwanda na Burundi zipo lugha za makabila mengi ila yote yanaunganishwa na kiswahili na si kwa wanajeshi tu kama unavyodai.
Muziki wa Kongo mpaka miaka ya sitini uliimbwa kwa kiswahili zaidi na kina Mwenda J. Bosco.
 
Kiswahili kilisambaa kwenda congo miaka mingi sana kwa njia za kibiashara , pia kuna lahaja za kiswahili hadi madagaska ndiposa unaambiwa kiswahili ni kibantu japo mimi ninadhani ni lugha chotara. Chimbuko lake ni uswahilini (kenya kwa wangozi) kisha kikateremka kusini katika upwa wa afrika mashariki yote
 
Kwa sababu Kiswahili sio lugha ndogo km unavyofikiria wewe bwana mdogo Kiswahili ni lugha kubwa inayotumika mataifa mengi duniani kote
 
Lugha inayozungumzwa Drc mashariki ni kiswahili
 
Historia ya kiswahili ifuatiliwe upya, hao jamaa wanatumia sana kiswahili si ajabu kilianzia kwao.

"kiswahili ni kiarabu"

Kiswahili sio kiarabu .
Hata maandishi yake hayafanani.
Lakini pia kuna nchi kama Omani wananchi wake wengi wanaongea kiswahili kwa sababu waliishi ukanda wa Afrika mashariki hasa Kilwa ,Zanzibar ,Tanga, Mikindani,Lindi , Tabora ,Kigoma n.k. Wakarudi kwao wakiwa wanaongea kiswahili maana walikaa zaidi ya karne mbili . Hata wajerumani wangekaa Tanganyika karne mbili leo pangekuwa na muingiliano mkubwa sana wa Kiswahili na lugha ya kijerumani .

Kiarabu ni Kiarabu na Kiswahili ni Kiswahili . Kuingiliana kwa baadhi maneno ni kwa sababu ni jamii iliyowahi kuishi pamoja na kufanya biashara pamoja .
 
Kwa maana hiyo basi wewe msimamo wako kiswahili ni lugha chotara
 
Kwasabu kwa wenzetu africa mashariki ili uonrkane msomi itakubidi uzungumze kiswahili japo maeneo ya goma na kiv wengi wanaongea kiswahili kile cha kikongomani
Hata Rais wao LKabila alikuwa anawahutubia kwa Kiswahili
 
Kiswahili hakijaanza congo. Nadharia inayosema kiswahili ni ki congo ina madhaifu makubwa. Kiswahili kinatokana na wabantu. Wabantu chimbuko lao ni Cameroon wakashuka kusini walikuja mafungu mafungu katika upwa wa africa mashariki wakawakuta waarabu .(waarabu walikuja africa mashariki kabla ya sisi wabantu) wabantu walebwaliochangamana na waarabu kikazaliwa kiswahili Kwa wangozi (kenya) baadaye waingereza wakasanifisha moja ya lahaja za kiswahili (kiunguja ) kuwa kiswahili sanifu. Kwa vyovyote vile kiswahili kilichosanifishwa kiliwekwa upya kutengenezwa upya kwa baadhi ya maneno. Mfano Moya ikawa moja , Cai ikawa chai na meneno mengine kibao. Kwa ufupi usanifidhaji uliharibu kwa namna fulani historia ya kiswahili ndiposa tunaweza kusema hiki kiswahili sanifu tunachoongea na kuandika kimetengenezwa
 
Mkuu umeeleza vyema yaani kama ulikuwepo vile.
 
Tanzania kuna lugha za asili, kwanini tunatumia kiswahili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…