Kwanini Mabenki hayarudishi pesa wanazokata kama " Bima ya mkopo pindi deni la mhusika linapoisha

Kwanini Mabenki hayarudishi pesa wanazokata kama " Bima ya mkopo pindi deni la mhusika linapoisha

Ndo leo nasikia eti bima inarudishwa. Ina maana utakuwa bima ni nini? Bima sio deposit. Hiyo pesa inakuwa imeshachukuliwa na Insurer. Ni sawa uende uakadai bima ya afya makato yako sababu hukuumwa mwaka mzima. Si wehu huo.
 
Ndo leo nasikia eti bima inarudishwa. Ina maana utakuwa bima ni nini? Bima sio deposit. Hiyo pesa inakuwa imeshachukuliwa na Insurer. Ni sawa uende uakadai bima ya afya makato yako sababu hukuumwa mwaka mzima. Si wehu huo.
Mkuu tafadhari tofautisha bima ya mkopo na hizi bima zingine.... Inawezekana na wewe ukawa mwehu mkuu
 
hivi mkuu nikiweka bond simu kwako ukanipa 120K kwa makubaliano nikilipa deni lako na riba uliyonipa unirudishie simu yangu, nikimaliza deni utakatalia simu yangu?

Huu mfano wako hauendani, bima wao wamechukua risk ya kulipa mkopo wa 5M(mfano) km ikitokea umeshindwa kulipa, sasa ukisema wakulipe faida yao ni nini? Maana yake hiyo 200k ni gharama ya wao kubeba risk ya kulipia hilo deni Incase umeshindwa kulipa. Na hiyo ndo biashara ya bima ilivyo
 
Niliwahi chukua mkopo toka benki moja (jina kapuni) na marejesho yake yalikuwa ni miaka mitatu. Baada ya mwaka mmoja, mwajiri akasitisha mkataba hivyo nikawa sina uwezo wa kulipa mkopo. Benki wakaja juu wanataka hela yao, tukakaa mezani nami nikawaambia sina kazi ya kunipa kipato cha kurejesha mkopo. Hatukuelewana, wakampa debt collector kazi ya kunidai.

Uzuri wake waliponipa mkopo walinipa na cover note ya insurance, nikampa huyo debt collector wao, nakala ya insurance cover note na barua yangu ya kuvunjwa mkataba wa kazi, nikamuomba tuonane mahakamani. Sikuwaona tena.

Ushauri wa bure: Wakikukata bima ya mkopo,wewe dai wakupe insurance cover note, likitokea la kutokea, wao wakapambane na kampuni ya bima. ILA mkopo ukiisha kwa mujibu wa mkataba, bima ya mkopo HAIRUDISHWI kwako mteja.

Asante, nafikiri wengi hawaelewi maana ya bima.
 
Bima hairudishwi mkuu, tafasiri nyepesi ni kuwa wakati wewe umerejesha mkopo smooth, kuna mwingine hakurejesha kabisa labda kafariki, kwa hiyo kiasi ulichotoa wewe na mwingine na mwingine kama bima kinaenda kufidia deni la yule ambaye hakurejesha kwa sababu hizo. Mfano bima ya afya, usipougua wewe katika kipindi hicho cha bima haina maana kuwa pesa yako utarudishiwa, kwani kuna mwingine kanufaika kupitia pesa yako ( kwa kupata matibabu zaidi ya kile alichochangia katika bima yake.
Sio kwamba ukifariki au kupata tatizo deni halijaisha wanakata kwenye mafao?
 
Habari zenu wanajamvi
Miaka sita (6) iliyopita nilichukua mkopo bank ya CRDB kwa dhamana ya utumishi na marejesho yakiwa yanakatwa moja kwa moja kwenye mshahara, moja ya masharti ya ule mkopo ilikuwa ni lazma ukatiwe bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu, maafisa mikopo wa CRDB walinielimisha vizuri sana kuhusu hii bima amabayo wanaikata kwenye kile kiasi ulichoomba mkopo, nadhani ni kama 200k+ kama sikosei.wakanielieza kwamba

Kile kiasi cha pesa kilichokatwa kwenye mkopo nilioomba kama Bima kinasimamia upotevu wa fedha,mali iliyokatiwa Bima kutokana na kutokuwepo kwa uaminifu kutoka kwa waajiri wakati wafanyakazi wakiwa kazini. Bima hii pia inasimamia usalama wamali iliyochukuliwa kama dhamana. Wakaendelea kusema,

Bima hiyo inalipia hasara ya fedha anayoipata mkopeshaji ( ambao ni wao CRDB Bank) kutokana na matatizo aliyopata mdeni kufuatia majanga ya kifo au ulemavu wa kudumu kabla hajamaliza kulipa deni. Husaidia kupunguza hasara ikilinganishwa na dhamana iliyowekwa. Kwa wakopaji wasio na dhamana za kazi Bima hii ina hakikisha familia ya mhanga haiachwi bila makazi au mzigo wa kuendelea kulipia deni linalodaiwa pale mkopaji anapofariki au kupata ulemavu wa kudumu.

HOJA YANGU
Deni langu lilikuwa la miaka mitano (5) na mwaka jana nilimalizana na hili deni, yaani hawanidai tena tangu mwaka jana, nilitegemea baada ya deni kumalizika hawa CRDB bank wanirudishie ile pesa yangu Zaidi ya 200K kwa vile mkopo wao tayari nimeurudisha wote pamoja na riba na bila usumbufu, mwanzoni mwa mwaka huu niliwatumia barua kuwakumbusha kuhusu kunirejeshea hii pesa hawajanijibu hadi leo, jana nimewatumia email kupitia kwa DG wao bado pia naona kimya.

Hii kitu imeekaaje kwa hapa bongo, au ndo bank inadhulumu wateja wao…, nakumbuka nilikopaga pesa stanbic bank nikiwa Kenya kwa mda wa mwaka mmoja na baada ya mkopo kuisha nikarejesehewa hii pesa tena wakani email kabisa kunitaarifu.

Najua wakopaji kwenye hizi taasisi za kifedha wako wengi na najua na wao hawajui kama wanatakiwa kurudishiwa hii pesa baada ya mikopo kumalizika , naombeni kujulishwa kama hapa bongo hii pesa huwa hairudi hata kama deni lao umemaliza lote?
sijawahi sikia bima inarudisha fedha kama janga lilitegemewa halija tokea, mfano mimi nikikata bima ya gari na gari yangu ikawa haija pata ajali hadi inachakaa unataka nirudishiwe pesa si ndo hivyo
 
sijawahi sikia bima inarudisha fedha kama janga lilitegemewa halija tokea, mfano mimi nikikata bima ya gari na gari yangu ikawa haija pata ajali hadi inachakaa unataka nirudishiwe pesa si ndo hivyo
Hapana mkuu bima ya mkopo na gari tofauti.... Hebu soma terms and conditions zao....
 
sijawahi sikia bima inarudisha fedha kama janga lilitegemewa halija tokea, mfano mimi nikikata bima ya gari na gari yangu ikawa haija pata ajali hadi inachakaa unataka nirudishiwe pesa si ndo hivyo
Hapana mkuu bima ya mkopo na gari tofauti.... Hebu soma terms and conditions zao....
 
Huu mfano wako hauendani, bima wao wamechukua risk ya kulipa mkopo wa 5M(mfano) km ikitokea umeshindwa kulipa, sasa ukisema wakulipe faida yao ni nini? Maana yake hiyo 200k ni gharama ya wao kubeba risk ya kulipia hilo deni Incase umeshindwa kulipa. Na hiyo ndo biashara ya bima ilivyo
،ukiniuliza faida yao ni nini, nashindwa kukuelewa maana Mimi sikuingia mkataba na wa watu WA bima na wala sikuwahi kuonana nao, niliingia mkataba na bank na wao wana wajibu wa
 
ndio mkuu lazma warudishe, vinginevyo watakuwa wanawaibia wateja wao
ndio maana kuna baadhi ya wanawachuoni wa kiislamu wanatoa fatwa kwamba bima za namna hiyo ni haramu kwa sababu BIMA NI KAMARI YA KISASA HIYO.

ukiwa halijatokea haki kila mtu apate pesa yake, lakini dhulma ni kuwa hata kama halikutokea pesa hairudi, ni kama kamari y biko na mzuka tu
 
Nakushauri hili bandiko lako lipeleke pia Twitter, kwani ni issue muhimu sana na kule Twitter CRDB wana account yao na wanajibu papo kwa papo maswali ya wateja...
 
Nakushauri hili bandiko lako lipeleke pia Twitter, kwani ni issue muhimu sana na kule Twitter CRDB wana account yao na wanajibu papo kwa papo maswali ya wateja...
Sawa mkuu
 
hivi mkuu nikiweka bond simu kwako ukanipa 120K kwa makubaliano nikilipa deni lako na riba uliyonipa unirudishie simu yangu, nikimaliza deni utakatalia simu yangu?
Tofautisha kati ya bima na kuweka kitu kama dhamana(bond).

Bima hairudishwi kama tatizo halijatokea.
Ukipata tatizo wanalipa pesa nyingo kuliko uliyolipua bima, sasa jiulize hiyo pesa wanatoa wapi na faida wanatoa wapi?

Bima ni kama biashara ya bahati nasibu/kamari(betting) au kama forex trading au biashara ya stock market.
 
hivi mkuu nikiweka bond simu kwako ukanipa 120K kwa makubaliano nikilipa deni lako na riba uliyonipa unirudishie simu yangu, nikimaliza deni utakatalia simu yangu?
Bima sio bond.

Hivi zile bima za magari huwa wanaturudishia muda wake ukimalizika?
 
Bima hairudishwi mkuu, tafasiri nyepesi ni kuwa wakati wewe umerejesha mkopo smooth, kuna mwingine hakurejesha kabisa labda kafariki, kwa hiyo kiasi ulichotoa wewe na mwingine na mwingine kama bima kinaenda kufidia deni la yule ambaye hakurejesha kwa sababu hizo. Mfano bima ya afya, usipougua wewe katika kipindi hicho cha bima haina maana kuwa pesa yako utarudishiwa, kwani kuna mwingine kanufaika kupitia pesa yako ( kwa kupata matibabu zaidi ya kile alichochangia katika bima yake.
Unaweza fikiria humu tuna watu wengi ambao ama hawajaenda kabisa shule na pia sio hata watumishi.

Lakini unanakuta wanaolalamika ndiyo watu wanaokatwa NHIF lakin huwaoni wakidai.

Itabidi bima ifundishwe kama somo walau kuanzia darasa 5.
 
Bima katika mikopo ni nzuri sana.

Jirani yangu alikopa kama 30m, baada ya miezi 3 akafariki.

Tulipopeleka cheti cha kifo benki haikumdai mke wa marehemu na nyumba yao waliyoweka bond ikasalimika.

Mama na watoto wakabaki salama na mtaji umeongezeka dukani.

Shikamoo bima.
 
mkuu kuna vitu unachanganya bima ya gari ni tofauti kabisa na hii na hata ulipaji wake, hii bima wanakata bank na makubaliano ni ya maneno hakuna documentation inayoonesha umelipia... mkopo wako ukitoka wao wanakata moja kwa moja kinachoitwa bima ya mkopo kwenye huo mkopo wako, hapa ina maana hii pesa inarudi kwao bank wenyewe na haiendi kwa kampuni wala taasisi za bima
Mkopo ni sheria msikubali makubaliano ya mdomo bila maandishi, ikiwa hakuna documentation hilo deni una liwasilishaje sasa?! Unalipia hupewi receipt na haiko kwenye mkataba wa deni sasa unalipaje na una daije?!
 
Back
Top Bottom