Super Sub Steve
JF-Expert Member
- Jul 9, 2011
- 17,404
- 10,900
Maelezo ya mdomo tu wanatoasasa hawa si ra di bi hawakunipa na sidhani kama wanawapa wateja wao hii cover note, wao wanakata juu kwa juu tu unapewa maelezo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Maelezo ya mdomo tu wanatoasasa hawa si ra di bi hawakunipa na sidhani kama wanawapa wateja wao hii cover note, wao wanakata juu kwa juu tu unapewa maelezo
Hivi Processing fee Huwa wanamaanisha nini?Sio bima tu kuna kitu wanaita processing fee nayo ni wizi mtupu. Tena wanakata hela ndefu sana. Serikali iingilie kati, wananchi wanadhulumiwa na mabenki.
Kwanini hiyo processing fee wasiijumlishe kwenye riba wanayotoza?Processing fee kwa upande mwingine ni gharama inayolipwa na mkopaji kwa ajili ya shughuli mbalimbali zinazohitajika kukamilisha mkopo
Kwa haraka haraka nafikiri gharama zake ni kama vile stationeries, travel here and there, kuja kufanya uhakiki ( kwa baadhi ya aina ya mikopo), na vinginevyo
Hapa kinachoonekana Kuna kaujanja wanakafanya hao watu wa benki.is this true? nani ananiwekea sign huko kampuni za bima kwamba nimelipa mimi?
Ukikata bima ya moto au ya gari na gari isipate ajali mwaka huo ,unarudishiwa hela yako? Sijawahi kuona. Kila mwaka tunalipia hata kama hatujapata ajaliHabari zenu wanajamvi
Miaka sita (6) iliyopita nilichukua mkopo bank ya CRDB kwa dhamana ya utumishi na marejesho yakiwa yanakatwa moja kwa moja kwenye mshahara, moja ya masharti ya ule mkopo ilikuwa ni lazma ukatiwe bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu, maafisa mikopo wa CRDB walinielimisha vizuri sana kuhusu hii bima amabayo wanaikata kwenye kile kiasi ulichoomba mkopo, nadhani ni kama 200k+ kama sikosei.wakanielieza kwamba
Kile kiasi cha pesa kilichokatwa kwenye mkopo nilioomba kama Bima kinasimamia upotevu wa fedha,mali iliyokatiwa Bima kutokana na kutokuwepo kwa uaminifu kutoka kwa waajiri wakati wafanyakazi wakiwa kazini. Bima hii pia inasimamia usalama wamali iliyochukuliwa kama dhamana. Wakaendelea kusema,
Bima hiyo inalipia hasara ya fedha anayoipata mkopeshaji ( ambao ni wao CRDB Bank) kutokana na matatizo aliyopata mdeni kufuatia majanga ya kifo au ulemavu wa kudumu kabla hajamaliza kulipa deni. Husaidia kupunguza hasara ikilinganishwa na dhamana iliyowekwa. Kwa wakopaji wasio na dhamana za kazi Bima hii ina hakikisha familia ya mhanga haiachwi bila makazi au mzigo wa kuendelea kulipia deni linalodaiwa pale mkopaji anapofariki au kupata ulemavu wa kudumu.
HOJA YANGU
Deni langu lilikuwa la miaka mitano (5) na mwaka jana nilimalizana na hili deni, yaani hawanidai tena tangu mwaka jana, nilitegemea baada ya deni kumalizika hawa CRDB bank wanirudishie ile pesa yangu Zaidi ya 200K kwa vile mkopo wao tayari nimeurudisha wote pamoja na riba na bila usumbufu, mwanzoni mwa mwaka huu niliwatumia barua kuwakumbusha kuhusu kunirejeshea hii pesa hawajanijibu hadi leo, jana nimewatumia email kupitia kwa DG wao bado pia naona kimya.
Hii kitu imeekaaje kwa hapa bongo, au ndo bank inadhulumu wateja wao…, nakumbuka nilikopaga pesa stanbic bank nikiwa Kenya kwa mda wa mwaka mmoja na baada ya mkopo kuisha nikarejesehewa hii pesa tena wakani email kabisa kunitaarifu.
Najua wakopaji kwenye hizi taasisi za kifedha wako wengi na najua na wao hawajui kama wanatakiwa kurudishiwa hii pesa baada ya mikopo kumalizika , naombeni kujulishwa kama hapa bongo hii pesa huwa hairudi hata kama deni lao umemaliza lote?
Uko sawa mkuu. umeelimisha vyemaHakuna bima inayorudishwa duaniani kanuni kuu ya bima ni wengi kuchangia kidogo kidogo ili mmojawapo anapopata janga basi Fidia inatoka kwenye pool ambayo wote mmechangia. Unaweza wewe binafsi usipate janga ila ulichokatwa kimemchangia mwenzako. Kwa logic hiyo hata chako kidogo kimetumika na wengine na huwezi kurudishiwa. Hiyo ndio logic kuu ya bima. Hizo nyingine ni categories tu za bima lakini msingi mkuu wa bima ni kuchangia kidogo kidogo ili mmoja akipata janga anafidiwa kutoka kwenye michango ya wenzake
Nimetumia lugha rahisi ili nipate kueleweka hata na layman
bima ya afya na hii na bima ya mkopo ni vitu viwili tofauti mkuu.Tangu lini bima ikarudishwa? Kwa wale wanaotumia bima ya afya watanielewa Bima ni mchango ambao hutolewa kabla kwa lengo la kutatua jambo husika endapo litatokea na ikumbukwe mteja anaweza pata tatizo ambalo litagharimu fedha nyingi kuliko kiasi alicho changia, hapa inamaanisha bima ni mchango ambao kwa namna unavyo fanya kazi inategemea michango ya wengi kutatua matatizo ya wachache! So Bima its some inafanana kidogo na gumbling
Ukikata bima ya moto au ya gari na gari isipate ajali mwaka huo ,unarudishiwa hela yako? Sijawahi kuona. Kila mwaka tunalipia hata kama hatujapata ajali
bima ya gari na hii na bima ya mkopo ni vitu viwili tofauti mkuu.Ukikata bima ya moto au ya gari na gari isipate ajali mwaka huo ,unarudishiwa hela yako? Sijawahi kuona. Kila mwaka tunalipia hata kama hatujapata ajali
Nakubaliana na wewe mkuu lakini bado nadhani haya mabank yanatupiga hapa na kwa vile Akili za wabongo wengi zinachukulia vitu kirahisi sana na ndio maana wajanja wanatumia huo mwanya kutengeneza pesa , kama ulivyosema unavyokopa Bank ndio wanaingia mkataba na bima na Kwa sababu hao ndio wanafahamiana kwa hiyo Mimi mkopaji nisingetakiwa kuhusika na kulipa bima inatakiwa watu wa benki ndio walipe hiyo pesa ya bima kwa sababu hao ndio wenye wasiwasi wa kupotea kwa pesa yao iliyokopwa na mteja Basi ni jukumu lao kulipia bima.Niongezee kitu kingine; unapokatwa credit life premium unatakiwa kujazishwa terms and conditions za hizo insurance.
Ikitokea hujajaza haimanishi cover haipo ila inamanisha benki wamekusanya hizo premiums wakaenda kukata kwa niaba. Lakini there must be a clause in the documentations you have signed kuonesha ulilipia credit life.
Alternatively, benki inaweza kukuambia tutahitaji uwe na credit life insurance kwa hiyo nenda kakata unapotaka wewe then tuletee cover note ikiwa umeweka benki kama part ya beneficiary kwenye proceeds za insurance
Wengine wana life insurance zao binafsi so wanaweza pia kuweka benki kama beneficiary wa hizo proceeds zao pia ingawa ni lazima wafuatilie kujua kama ina room ya kutosha
ujinga ni kujifanya unajua kila kitu mkuuWell said. Umemaliza mkuu
CASE CLOSED kama kuna mbishi aende darasani kusoma kuhusu bima.
Ila watanzania wengi sana wana uelewa mdogo mtu anashindwa hata kujua bima inafanyaje kazi anakuja kusema alikopa Kenya alivyomaliza akarudishiwa bima, hamna kitu kama hicho ELIMU ELIMU ELIMU. Tujifunze kuhusu vitu kama security, bond, insurance, collateral n.k ni mambo ya finance, uchumi na hata sharia za mikataba. Tutumie mitandao vizuri haya mambo yamejaa humu tena bureee. Tunashinda insta tu kupigana vijembe wakati internet ina kila kitu cha kukukomboa kiakili na kukutoa kwenye ujinga
Mkuu, unajua lakini bima inavyofanya kazi?. Maana naona unachanganya mambo hapa na si vinginevyo.ujinga ni kujifanya unajua kila kitu mkuu
kinachoonekana wabongo wengi ukiwemo wewe tunachukulia vitu kirahisi sana na ndio maana wajanja wanatumia huo mwanya kutengeneza pesa Kuna, unavyokopa Bank ndio wanaingia mkataba na bima na Kwa sababu hao ndio wanafahamiana kwa hiyo Mimi mkopaji nisingetakiwa kuhusika na kulipa bima inatakiwa watu wa benki ndio walipe hiyo pesa ya bima kwa sababu hao ndio wenye wasiwasi wa kupotea kwa pesa yao iliyokopwa na mteja Basi ni jukumu lao kulipia bima.
Ila kwa vile wabongo huwa hatufuatilii masuala muhimu yanayotuhusu utakuta unakubali kwa haraka haraka kila sharti utakalopewa kwa sababu ya kuharakisha kuipata pesa ya mkopo na hapo ndio watu wa benki wanacheza na hiyo weakness.
Ufafanuzi hivi hii ni kitu mfano mtu unaandika 300k K husimama badala ya nini ? Naomba kufahamu chiefhivi mkuu nikiweka bond simu kwako ukanipa 120K kwa makubaliano nikilipa deni lako na riba uliyonipa unirudishie simu yangu, nikimaliza deni utakatalia simu yangu?
Mkuu, unajua lakini bima inavyofanya kazi?. Maana naona unachanganya mambo hapa na si vinginevyo.
Bima inafanya kazi kama sehemu ya kumitigate/kuzia risks/majanga endapo tukio fulani litajitokeza na kuathiri mali ya yule anayekata bima. Ukiingia ndani zaidi ni kwamba bima zinafanya kazi katika utaratibu wa kukusanya fedha kidogo kidogo toka kwa watu wengi na kisha kuwafidia wale watakao pata matatizo katika kipindi bima ikiwa hai/valid.
Tafsiri yao sio wote watapata majanga kwa mara moja, na wakati mwingine miongoni mwa wengi ni wachache tu ndio watakaopata majanga katika kipindi cha uhai wa bima, hivyo hawa wachache watalipwa kutokana na kile ambacho kililipwa na wengi.
Unachopaswa kujua bima ni biashara, na bima ni shughuli inayoitaji utaalamu wa juu sana. Usiichukulie kwa lugha za mtaani kuwa bima ni kuweka bondi/dhamana. Hivi ni vitu viwili tofauti kwa muktadha wa masuala ya fedha.
Nikirudi kwenye mada yako, katika hali ya kawaida kabisa na wewe ukiwa ni muelewa, ulikopa huo mkopa na kisha ukakatiwa bima ya mkopo kama unavyosema 200k. Assume ni mkopo tu hata wa milioni 5. Ukalipa marejesho mawili, bahati mbaya ukapata ulemavu wa kudumu/total disability au ukafariki dunia. Kwa akili ya kawaida, deni lililobaki nani anapaswa kulipa?.
Jibu ni rahisi. Taratibu zitafuatwa kuhakikisha taarifa muhimu za marehemu/mlemavu zinapatikana na kisha benki wataenda kudai/claim kiasi chote cha mkopo pamoja na riba kilichobaki kutoka shirika la bima. Bima wakiona kila kitu kiko sawa basi watawalipa benki fedha yao. Na benki haitokaa imsumbue aliyepata majanga au ndugu za marehemu juu ya ulipaji wa deni husika. Huu ndo utaratibu unaotumika na ni lugha nyepesi kabisa jinsi bima inavyofanya kazi.
Mifano ni mingi, watu wanakata comprehensive insurance/bima kubwa tuseme kwa gari ya milioni 20, mfano analipa milioni + kama ada ya bima/premium. Mtu huyu huyu gari ikipata mzinga na ikawa total loss, analipwa fedha inayolingana na thamani ya gari (aliyoitaja bima kipindi anakata bima) toa uchakavu. Tuchukulie mtu kalipwa na bima milioni 15. Sasa jiulize, kwamba hizo zingine wamezitoa wapi mpaka wakaweza mlipa.
Kwa kifupi fedha ya bima huwa hairudishwi, na bima ya mkopo iko kihalali ili kulinda/safeguards maslahi ya pande zote mbili endapo majanga yatatokea.
Mwisho kabisa kumbuka fedha iliyoko benki ni akiba za watu hivyo wakati wowote zinapaswa kuwa salama hata kama zitatumika kukopeshwa.
Hiyo k husimama badala ya sifuri tatu, hivyo 10k ni sawa na shilingi 10,000Ufafanuzi hivi hii ni kitu mfano mtu unaandika 300k K husimama badala ya nini ? Naomba kufahamu chief
Katika hali ya kawaida kabisa kila bima ina vitu inavyokinga na hii kiuhalisia ndio mipaka ya bima husika. Bima ya mkopo au mara nyingi huitwa credit life insurance ni bima inayokatwa dhidi ya majanga kama kifo au ulemavu wa kudumu kama vitamkumba yule anayekatiwa bima/insured.Umeelezea vzuri sana kiongozi,
Swali langu,je bima wanalipa pia kwa mtu aliyeacha kazi bila kufuata tatatibu(kutoroka)?
Na Je,Bima wanafanya kazi pia na taasisi ndogo ndogo za kifedha i.e Bayport and the like?
Kiongozi hakuna bima ya kukatwa kwa maneno, unapaswa ujue hilo. Mimi nadhani ni vyema watu tujifunze au kuuliza kuliko kuyasemea mambo yaliyo ya kitaalam kwa kuchanganya na story za huko mtaani.mkuu kuna vitu unachanganya bima ya gari ni tofauti kabisa na hii na hata ulipaji wake, hii bima wanakata bank na makubaliano ni ya maneno hakuna documentation inayoonesha umelipia... mkopo wako ukitoka wao wanakata moja kwa moja kinachoitwa bima ya mkopo kwenye huo mkopo wako, hapa ina maana hii pesa inarudi kwao bank wenyewe na haiendi kwa kampuni wala taasisi za bima
Hichi unacho kizungumza hakipo mkuu. Labda kama walicho kurudishia ni aina fulani ya tozo waliyoifanya wakati wa kukupa mkopo, na mwisho ukilipa na kumaliza basi wanarudisha.mkuu roho ipi ya kwa nini? hiyo 200K sio ndogo ingekuwa ndogo wasingechukua..., stanbic bank branch ya kenya wao mbona walinirudishia mkuu...na kumbuka hao wanaoweka bond nyumba lakini pia wanakatwa hii bima kwenye mikopo wanayochukua sasa why wasirudishiwe pesa yao wanapomaliza deni lao