Kwanini mbunge Musukuma anapenda kuwadharau wasomi wetu?

Yani wewe ujipeleke wizi wa mafuta uungue asilimia 95 utegemee ku solve aisee mbona ni impossible kabisa hyo.
Pia ili uweze kutoa dawa kwa ufasaha lazima uwe na shule pia
 
Tatizo letu kubwa Watanzania ni zaidi ya huyo Msukuma, tatizo hasa ni chama tawala, CCM.

CCM imewekeza sana kwenye ujinga kama mtaji wake mkubwa katika jitihada zake za kung’ang’ania madaraka.

Ni kweli tunao wasomi lakini wengi wao ni wale ambao ukiondoa walichochuma darasani, kichwani ni watupu.

Makundi hayo mawili ni mtaji mkubwa sana kwa CCM na tofauti yao kubwa ni kiwango cha ujinga au akili ya kuzaliwa

Yawezekana kuwa Msukuma hana akili ya darasani lakini akajaaliwa ile ya kuzaliwa inayotutofautisha na wanyama.

Haya makundi mawili, CCM inawahitaji sana kwa sababu mapungufu yao kwa namna fulani yanashabahiana.

Kwanza wote ni wajinga…kundi moja kwa kutokwenda shule na lingine, pamoja na kwenda shule, kutoelimika.

Mfano mzuri ni mwendazake…pamoja na kudaiwa alikwenda shule hadi kiwango cha uPhD, alikuwa mshenzi (primitive)

Ushenzi wake ulijionesha katika utendaji wake na teuzi zake za kuwakumbatia wanaoshabahiana naye kitabia.

Mshenzi hana hekima wala busara katika maamuzi na badala yake hujikita katika matumizi ya nguvu na ubabe.

Mshenzi hajaelimika na hivyo sheria, kanuni na taratibu ni ngeni kwake na uhuru, haki na usawa hazina maana yoyote kwake.

Katika bunge letu la sasa uwanja umebaki wao wakipambana wenyewe kwa wenyewe kwa hoja za nguvu, nani mkali zaidi!
 
Fact.
 
Msukuma anasema ukweli, tatizo tuna wasomi wengi wa makaratasi anachofanya msukuma ni kuwapa changamoto. Angalia waliokuwa wakijiita mabingwa wa uchumi kina mwigulu bajeti wanayotengeneza hivi unaweza kusifia usomi wao.
Msomi wa kweli huwa anajionyesha kwa vitendo na sio kulalamika kama mleta mada.
 
Prof; kabudi alipaita UDSM Jalalani..msukuma unataka aseme nini?
Wasomi february walisema TZ hakuna CORONA..leo June wanasema tuvae barakoa..
Msukuma aseme nini?
Muuza mkaa wasomi wanataka awe na EFD Machine...msukuma awaitaje?
TZ HAKUNA WASOMI..
 
Haina majibu hiyo.
Wenye akili wote hawabishani nae.
That will make them come down to his level. Mambo yanaendekea kila mtu anashiba
Wangelkua na hakili kama usemavyo mwanya wa kusemwa usingelikuepo, maajabu chanya katika elimu zao isingekua siri
 
Mkuu hiyo para ya mwisho ndio imetoa mwanga dhatibi, wasomi wetu hata mimi wa darasa la Nane wa mtihani wa Cambridge nawaona ni bure kabisa, HAWAJIAMINI, Msukuma amesoma gepu, hana cha kupoteza kwenye ubunge wala nafasi ya kuteuliwa. Kwa hiyo anawalipua atakavyo na hawana chakumfanya. Wanajikomba mno.
 
"Wanajikomba mno" hii ina sum up wasomi wetu na tabia zao.
wakiwa nje ya siasa wanaonyesha umahiri. ngoja wapewe vyeo sasa
 
Sasa kama mwendazake alikuwa na PHD kwa nini wasidharauliwe?
 
Wasomi wenyewe Akina nani.....msukuma yuko sahihi
 
Mama wa Elimu nae pia yumo, japo namkubali sana.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…