Kwanini Mh Rais hakutokea kwenye sherehe za siku ya wafanyakazi (Mei Mosi)

Kwanini Mh Rais hakutokea kwenye sherehe za siku ya wafanyakazi (Mei Mosi)

Watoto wamekataliwa na Taifa/Mamlaka kwa kutoboresha maslahi ya mwalimu. Waache liwe Taifa la watu mbumbumbu.
Sasa tutamwachia nani ajenge hii nchi kama tutaendelea kususiana
 
Unaweza kwenda kwa mtu anaekudai kama hunauwezo wa kulipa deni?
 
Habari ya kazi wakuu!!

Naomba kwenda moja kwa moja kwenye hoja.
Hili nimekaa nalo sana tangu tarehe moja hadi leo na kila siku linaniumiza, nikikaa na wafanyakazi wenzangu naona wanahoja tofauti tofauti sasa leo nimeamua kuja mbele yenu wanajukwaa mnisaidie hili.

Nimetonywa hapa kuwa katiba ya JMT inamtambua moja kwa moja Mh Rais kama ndiye mgeni rasmi kwenye sherehe zote za kitaifa so kwa uelewa wangu mdogo najua kuwa ata hasipopata mwaliko ila akiamua kwenda kwenye sherehe husika bado atakuwa mgeni rasmi.

Sasa katika sherehe za Mei Mosi 2024 pale Arusha kwa baba Keegan hatukumuona mama yetu mpendwa na badala yake alikuepo Daktari Mpango. Hii ilikuwa ni tofauti na matarajio yetu watumishi kwani kwa miaka yote tumekuwa tukishuudia uwepo wa Top 3 (sasa Top 4) ya serikali yote ktk sherehe hizi.

Tunajua ratiba ya Rais ni ngumu sana ila kiukweli watumishi tumefadhaika sana kwa kutokuwepo kwa mama yetu katika sherehe zetu kwa sababu:








Sasa wanajukwaa kwa kuwa mimi nipo Kijijini Kidologwai na sina chaji na solar hazichaji kwa sababu jua halitoi kutokana na mvua na mawingu mazito, na pia uhenda kuna taarifa ilitoka ila sikuipata wala kuisikia naomba niishie hapa kwa kuwauliza, kwanini Mh Rais hakutokea kwenye sherehe za Mei Mosi2024 pale Arusha??

Kwa sababu mwaka jana alitoa ahadi ya uongo, sura likamshuka mwaka huu akashindwa kuja kutoa uongo mwingine.
 
Aliogopa masuala ya Kikokotoo kwa Wastaafu. Kuna Ile Aibu kuwa ni kweli hawa Wazee wanadhulimiwa naweza kuwaFace? Eti unatunzia mstaafu 67% ukimpa kidogo kwa Miaka 12 na nusu. Pension wamenyimwa wanapewa Tu Ile lump-sum ya Kiinua mgongo.
 
Ni aibu sana! Hili ndo lilomkimbiza mana hasingeweza kulikwepa pale. Wazee wamefanya kazi kwa nguvu na muda wao wote sasa wanatakiwa kupumzika na familia zao lakini wanawapangia Cha kuwalipa na namna wakati ni michango yao. Inasikitisha na kuhuzunisha sana.
 
Back
Top Bottom