Kwanini Mhe. Nape asijiari? Amekiri mabadiliko ya baadhi ya mawaziri yalifanya awashe AC kwa hofu; maana yake anafahamu kwamba hayupo pale kwa merits

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Waziri Nape amekiri aliposikia mkeka wa mabadiliko ya Mawaziri umetoka ilibidi aongeze AC kwa hofu aliyokuwa nayo. The same minister wakati wa Magufuli alimtafuta hadi Mama Maria Nyerere amwombee msamaha kwa JPM;

Mtu kama huyu kwanini asijifunze kujitegemea? Kwanini asijiajiri ili afanye kazi kwa uhuru aidha akiwa ameteuliwa au akikosa uteuzi?

Lini tutakuwa na watu wanaoweza kusimama bila kutegemea kusimamishwa? Hixi kauli zake siyo ishara kwamba anapaswa kutumbuliwa?
 
Nape ni debe tupu kama walivyo nguruwe wengi ccm.
 
Waziri Nape amekiri aliposikia mkeka wa mabadiliko ya Mawaziri umetoka ilibidi aongeze AC kwa hofu aliyokuwa nayo. The same minister wakati wa Magufuli alimtafuta hadi Mama Maria Nyerere amwombee msamaha kwa JPM;
Angekuwa mcheza mpira basi yule mchezaji wa kubutua kula pasi anayopewa
 
Hapo wanamsikia pia wananchi wake ambao maji wala umeme hawana hana leso ya kujipepea joto hawana (alafu anazungumzia kuwasha AC) ?!!! Huo muda wa kutoa hii statement angetumia kutafakari kwanini tangia aingie kwenye hii wizara Bundle limeendelea kutoshikika
 
Kuwepo Kwa merit,hofu au kujiajiri mbona mambo mengi hayaeleweki?

Kwani ukiwepo Kwa merit unakuwa na hati miliki? Hiyo merit unayo peke yako?
 
Hivi Watumishi wa serikali huwa Wana akili za kujiajiri,hao wamegeuza Ofisi za umma kuwa Mali yao wao na watoto zao na marafiki zao.
Na ndiyo maaana wakioneshwa pesa ya Rushwa wanachukua wakiamini watakuwa Matajiri maaana kanuni ya kutafuta utajiri hawaijui!
 
Kuwepo Kwa merit,hofu au kujiajiri mbona mambo mengi hayaeleweki?

Kwani ukiwepo Kwa merit unakuwa na hati miliki? Hiyo merit unayo peke yako?
Ukiwa na sifa na ukasoma katiba utagundua hakuna cheo cha kudumu; hakuna exit plan; hivyo muda mwingi utaishi wewe kama wewe na siyo kuwategemea wakubwa

Hivi huyu mtu ikitokea akazingua kazini nakutakiwa kujiuzulu unadhani atathubutu?tuache kuchukulia madaraka kama maji mwilini au damu kwamba vikipungua tutakufa au kudhoofu
 
Nape hawezi kujiajiri! Kazoe maisha ya dezo Sana. Anadhani uongozi Ni Haki yake.
 
Unafikiri kujiajiri mchezo🤣🤣
Washazoea pesa za bure bure za kuhangaika hawataki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…