Mhandisi Mzalendo
JF-Expert Member
- Aug 23, 2010
- 6,682
- 11,461
- Thread starter
- #21
Asante kwa jibu murua...First of all let me dealer interest mimi ni afisa kilimo hivyo ngoja nikujibu kitaalam kidogo!
Pana mambo kama mawili au matatu hivi yaliyokua yanasababisha hiyo hali unayoiona lakini kubwa kabisa ni kilimo kutokua cha KIBIASHARA.
Utakubaliana na mimi kua kwa miaka ya hivi karibuni atleast watanzania tumeanza kukiona kilimo kwa mtazamo tofauti, na kuanza kulima kibiashara sasa hii imepelekea wakulima kuanza kulima si tu kwa kutegemea msimu wa mvua bali kwa kumwagilia kwa njia mbali mbali kuanzia visima, kumwagilia kwa kutegea maji mtoni mpaka kwa njia ya matone ikiwa ni mapinduzi ya kisayansi mpaka sasa katika sekta yetu ya kilimo.
Sababu nyingne kubwa zaidi ni uwepo wa mbegu za kisasa za mazao mbali mbali ikiwemo na hizo za matikiti kwani haya ya kisasa yamekuja na sifa ambazo zile mbegu zetu za asili hayakua na uwezo wa kua nazo ndo mana yakafanya zao hili kutokua maarufu!.
Mbegu za kisasa zmekuja na sifa za kukomaa mapema ndani ya siku 60 - 75 tayari linakua limekomaa tayari kwa kupelekwa sokoni pia matikiti yake yanakua makubwa (baadhi ya varieties zinaenda mpaka kilo 7 - 10 Kwa tunda moja) kitu ambacho matikiti yetu ya asili hayakua na uwezo huo wa kua makubwa kwa kiasi hiko pia varieties za kisasa matikiti yake ni matamu sana (sina haja ya kulielezea hili sote tunafahamu) na per one acre unaweza kuvuna zaidi ya tani 20
Kwa sababu hizi nadhani utakua umenipata!
Kwa hiyo sasa tunakula tikiti chotara la maabara na asili, kama ilivyo btoiler chicken, ng'ombe wa kisasa n.k..
Hizi afya zetu zipo matatani...