Kwanini mikate mingi ina mchanga siku hizi?

Kwanini mikate mingi ina mchanga siku hizi?

Mnapenda sana na kuendekeza anasa kwa kula kula mikate hovyo hovyo wakati kuna mbadala magimbi, mihogo na viazi. Endeleeni tu kuparamia iyo mikate mwishowe appendix itajaa michanga mtaingia matatizoni na gharama kwenda kutoa appendix.

Badilikeni aseeh!
Kuna mda kula mikate ni dalili ya kuficha umasikini. Mkate wa buku unauwakika wa kula siku 3-4 ila magimbi/gombi la buku unaweza kula siku 1-2 kwa maeneo ya mjini.
 
Mnapenda sana na kuendekeza anasa kwa kula kula mikate hovyo hovyo wakati kuna mbadala magimbi, mihogo na viazi. Endeleeni tu kuparamia iyo mikate mwishowe appendix itajaa michanga mtaingia matatizoni na gharama kwenda kutoa appendix.

Badilikeni aseeh!
Tatizo mda wa kupika hayo magimbi
 
Viwanda vya Mikate saiv NI mingi Sana ,na ubora upo chini Sana ,kwanza ni michachu,inavunjika hovyo,ukifungua tu mkate bac kesho huwez ukaula Tena inawahi haribika.mkate mzuri ni ile brand ya zamani adi Sasa ipo.
 
Wakuu habarini za usiku,

Ni muda nimekuwa mtumiaji mzuri wa mkate katika kifungua kinywa cha asubuhi, lakini nime-kutana na changamoto ya kitafunwa hichi kuwa na chembe chembe za michanga ndani yake. Nimejaribu kubadili brand mbali mbali lakini naona hali ni ile ile.

Je, hali hii inasabishwa na mazingira ya uandaji wa mikate hii kabla ya kumfikia mlaji, au ni ngano wakati wa kuvuna na kusaga, au ni viwanda bubu vya mtaani ambavyo havina mazingira rafiki ya uzalishaji, au ni vyombo vinavyotumika huko viwandani au shida ni nini, au ni mamlaka husika kutokufanya ukaguzi kwenye viwanda!?

Kuna haja ya mamlaka ya chakula kufatilia hili, maana imekuwa kero kuanzia shida ya meno mpaka afya kiujumla.

Nawasilisha
Bidhaa nyingi za ndani ziko chini ya kiwango ukilinganisha na zile za Kenya.
 
Itakuwa ile tekinolojia ya zamani ya kukandia miguu imerudi.

Umeme hamna kila wakati unakatika. Mwenye kiwanda atafanya nn hata ungekuwa wewe.

Japo napenda sikonsi sijui nifanyeje duuuu
 
Mkate hautafunwi..
Unachovya kwenye kikombe cha chai au maziwa ukilainika unaufyonza na kuuweka sawa usawa wa njia ya koromeo na kumeza
 
Mihogo inanunuliwa!

Navyojua, mtu anang'oa shambani kwake na kuja kuchemsha.

Hili la kununua sijawahi lisikia mie!
Hahaaaaaa hahaaaaaa.
Kwani kila mtu analima mkuu???
Hujawahi kwenda masokoni ukaona mihogo inauzwa?
Kama unavyonunua mchele dukani, hata mihogo inauzwa sokoni na vibandani (au na mchele unajilimia?)
Dar wanakula mihogo inayotoka sehemu za pwani, Tanga, Lindi na Mtwara.
Duuuh sikutegemea kama mpo.
 
backary zimekuwa nyingi mno alafu unakuta baadhi yao mazingira ya uandaaji ni local sana mtu ana fanya backing ya vipande vya mkate alafu anaweka zakafuni ambapo hapaeleweki ki vile unategemea nini wanacho angalia ni fedha na wala si afya za walaji ndio maana mambo ndio kama haya.Cha msingi kabla ya kununua fanya utafiti wa kampuni ya waandaaji yenye viwango kama unataka kuepuka hayo.
 
Ni kweli si jambo jipya ila hapo kilicholeta mshtuko ni uhusiano wa huo mchanga na kukandia miguu...kwamba mtu anatoka kukanyaga mchanga moja kwa moja anaingia kwenye unga?
Umetoka kwenye mazoezi ya mpira kisha unapitia bekari kwenye kibarua cha kukanda unga, unaosha miguu kisha unatembea mpaka kwenye bafu la kukandia unga, hapo ndipo unapobeba mchanga.
 
Mnapenda sana na kuendekeza anasa kwa kula kula mikate hovyo hovyo wakati kuna mbadala magimbi, mihogo na viazi. Endeleeni tu kuparamia iyo mikate mwishowe appendix itajaa michanga mtaingia matatizoni na gharama kwenda kutoa appendix.

Badilikeni aseeh!
Mbona kama umekuja na povu badala ya suluhisho la alichouliza mleta mada?
 
Tbs wapo, tfda wapo, afisa afya wapo hakuna kinachofanyika..
 
Back
Top Bottom