Kwanini mnawapangia wanawake ukomo wa umri wa kuolewa?

Kwanini mnawapangia wanawake ukomo wa umri wa kuolewa?

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Kuna katabia kapo hata sijui aliyekaanzisha nani aisee, ka kuamini kila mwanamke anataka kuolewa na ndio lengo au ndoto za maisha yake.

Utakuta wanaume wanamtongoza mwanamke akikataa wanaanza kusema anaringa kwa kuwa bado umri haujaenda, ukienda ataokota yoyote aliye mbele yake ili aolewe, wakati huo jua lishazama.

Wakikataa wanakutana na maneno kama; kalenda inaenda wewe changamka, unaringa wakati una miaka 30? Unaringa hujui mwanamke anazeeka haraka! Unaringa na jua lishazama? Endelea kuringa utakosa soko wewe! Una miaka miwili tu ya kupata mtoto hapo si uolewe?!

Kwani aliyewaambia huyo mwanamke anataka kuolewa nani? Tamaa zenu tu ndio zinawafanya muwapangie wanawake wakifika umri fulani waolewe, matokeo yake pressure wanayopewa wanakubali yoyote hata wasiomtaka.

Kwa hiyo mnataka binti ajizolee yoyote ili mradi kuuwahi umri? Kwanza nani kawaambia lazima kila binti aolewe? Kwani asipoolewa ataumwa au atakufa kwa kutokuolewa? Mwacheni dada wa watu atimize malengo yake, ataolewa hata na miaka 70 kama akitaka kuolewa. Kwani hakuna wanaoolewa na miaka 80?

Acheni kuwapa pressure ya ndoa wanawake kwa kigezo cha umri, nao wana malengo na ndoto zao za kutimiza kabla ya kuingia kwenye hizo ndoa.
 
Kuna katabia kapo hata sijui aliyekaanzisha nani aisee, ka kuamini kila mwanamke anataka kuolewa na ndio lengo au ndoto za maisha yake.

Utakuta wanaume wanamtongoza mwanamke akikataa wanaanza kusema anaringa kwa kuwa bado umri haujaenda, ukienda ataokota yoyote aliye mbele yake ili aolewe, wakati huo jua lishazama.
Unakuta tunasema hvyo tu ila unakuta lengo ilikua ni kula mbususu tu [emoji12]
 
Nawajua Wamama kede kede wameolewa kwenye 40s, 50s, 60s.... hakuna kikomo cha Ndoa tena kwenye Uzee Wanaume ndio wanahitaji zaidi Wanawake.

Ila suala la Kuzaa kama Mwanamke anataka watoto ni bora azae mapema maana baada ya 35 uzazi unaanza kuleta mushkeli.
 
Kwasababu Muumba amekwisha wapangia umri wa kubeba mimba na sisi hatupendi muwe single mothers Mkuu.

Angalia wimbi kubwa la wanawake wanaotafuta wachumba JF na mtaani wengi umri wao ni machweo 30+ na hata vigezo vyao sio vikali, tofauti kabsa na wa miaka 20+ hapa JF na huko mtaani.
 
Nawajua Wamama kede kede wameolewa kwenye 40s, 50s, 60s.... hakuna kikomo cha Ndoa tena kwenye Uzee Wanaume ndio wanahitaji zaidi Wanawake,
Je, unawajua pia Wanawake ambao kwenye huo Umri wamejaa Makanisani, Mitandaoni wanatafuta Wanaume wa kuwaoa na hawapati? na wakipata Mwanaume wanatoa na uShuhuda, wanaona kama ni Miujiza.

Pia Ulishawahi kumuoa Binti wa miaka 20-27 yuko huko Makanisani, Mitandaoni anatafuta Mwanaume wa kumuoa?
 
Je, unawajua pia Wanawake ambao kwenye huo Umri wamejaa Makanisani, Mitandaoni wanatafuta Wanaume wa kuwaoa na hawapati? na wakipata Mwanaume wanatoa na uShuhuda, wanaona kama ni Miujiza.

Pia Ulishawahi kumuoa Binti wa miaka 20-27 yuko huko Makanisani, Mitandaoni anatafuta Mwanaume wa kumuoa?
Vipi kama hao waliojazana huko ni kwa sababu ya shinikizo mnalowapa kuona kuwa wamechelewa?
 
Kuna katabia kapo hata sijui aliyekaanzisha nani aisee, ka kuamini kila mwanamke anataka kuolewa na ndio lengo au ndoto za maisha yake.

Utakuta wanaume wanamtongoza mwanamke akikataa wanaanza kusema anaringa kwa kuwa bado umri haujaenda, ukienda ataokota yoyote aliye mbele yake ili aolewe, wakati huo jua lishazama.

Wakikataa wanakutana na maneno kama; kalenda inaenda wewe changamka, unaringa wakati una miaka 30? Unaringa hujui mwanamke anazeeka haraka! Unaringa na jua lishazama? Endelea kuringa utakosa soko wewe! Una miaka miwili tu ya kupata mtoto hapo si uolewe?!

Kwani aliyewaambia huyo mwanamke anataka kuolewa nani? Tamaa zenu tu ndio zinawafanya muwapangie wanawake wakifika umri fulani waolewe, matokeo yake pressure wanayopewa wanakubali yoyote hata wasiomtaka.

Kwa hiyo mnataka binti ajizolee yoyote ili mradi kuuwahi umri? Kwanza nani kawaambia lazima kila binti aolewe? Kwani asipoolewa ataumwa au atakufa kwa kutokuolewa? Mwacheni dada wa watu atimize malengo yake, ataolewa hata na miaka 70 kama akitaka kuolewa. Kwani hakuna wanaoolewa na miaka 80?

Acheni kuwapa pressure ya ndoa wanawake kwa kigezo cha umri, nao wana malengo na ndoto zao za kutimiza kabla ya kuingia kwenye hizo ndoa.
Kuhusu umri ni sawa ila kuhusu maamuzi ni ya kwake binafsi
 
Kwanini Me tukiwatongoza Ke huwa mnatukejeli kuwa "si type yangu" mkitushusha juu hadi chini kwa midomo iliyopinda afu mkifika miaka 30 mnajazana kwa Mwamposa kutafuta Me yeyote awaoe hata kama ana sura gome kama Chimpanzee?
Screenshot_2023-01-08-21-00-53-92_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg
 
Mwanamke akishafikisha umri was 30+ afu awe Hana mtoto Wala mume mtarajiwa,huwa Anachanganyikiwa Sana kwa kweli.

Wengi huwa wanahisi wamerogwa kumbe waliyataka wenyewe kwa kuwa too much selective.Wanajistukia umri umewatupa then wanaanza kujazana kwenye mitandao kutafuta " mwanaume yeyote" wa kuwaoa.
 
Mwanamke akishafikisha umri was 30+ afu awe Hana mtoto Wala mume mtarajiwa,huwa Anachanganyikiwa Sana kwa kweli.

Wengi huwa wanahisi wamerogwa kumbe waliyataka wenyewe kwa kuwa too much selective.Wanajistukia umri umewatupa then wanaanza kujazana kwenye mitandao kutafuta " mwanaume yeyote" wa kuwaoa.
Kuolewa mwisho miak mingapi?
 
Back
Top Bottom