Binafsi namuona ni soloist bora baada ya Dally Kimoko “King” hapa duniani na hususani kwenye Congolese music scene!!
Haikuwa na haja ya kuimbwa au kutajwa kwenye nyimbo alizohusika maana alipopewa jina la Tchakou yaani “kasuku” sababu gitaa lake liliongea lenyewe[emoji4]. Kitu cha ziada alichowazidi Dally na Diblo ni uwezo wa kupiga gitaa zote 3 kwa ufasaha wa hali ya juu. Pia alikuwa ni music arranger bora sana, jaribu kusikiza wimbo wa Massapa wa Alain Kounkou utajua uwezo wake hasa namna aliyopangilia rhythm ya nyimbo nzima.
Watu waliomtaja sana kwenye tungo mbalimbali alizoshiriki ni msanii mwenye vipaji vingi kuliko wote ndani ya Soukous Stars namuongelea “SHIMITA EL DIEGO” na atalaku / animator bora zaidi katika Congolese music scene yaani “3615 Code Niawu” au “Cherry Niawu” au “Papa na Renzo”[emoji23]
RIP NENE TCHAKOU “Papa na Melody”.
GENTA hebu sikiliza solo ya Muchana.
Masahihisho: Kwenye Bazo solo guitar lilipigwa na Dally Kimoko.