Kwanini msemaji wa Club ya Simba anatangaza bidhaa za pinzani kibiashara? Inawezekana vipi?

MURUSI

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
4,537
Reaction score
8,824
Kuna kitu sijakielewa na hiki ni vigumu sana kukiona kwenye nchi zilizo endelea hasa Ulaya huko.

Haji Manara ni Msemaji wa Club ya Simba na Mdhamini au mmiliki wa Club ni Mo,
Mo ana bidhaa zake nyingi sana kama maji, aina mbalimbali za vinywaji, unga wa ngano kwa kifupi ana product nyingi sana na ziko hadi kwenye jezi za timu.

Ila hii ya Manara kutangaza product za Azam sielewi inawezekana vipi, how come? Anayejua anisaidie kwamba inawezekana vipi? Na product anazotangaza ni the same na zinazozalishwa na Bosi wake.

Kwa wenzetu hiki hakiwezekani Milele.

 
Hiyo ni akaunti binafsi ya Haji Manara na sio akaunti ya Simba! Kwa maana nyingine, anayetangaza hiyo bidhaa sio Msemaji wa Simba bali Haji Manara! Na kwa maana nyingine, hata Mo anaweza kutangaziwa bidhaa zake na Haji Manara lakini atatakiwa kumlipa Haji yeye binafsi, na malipo hayo hayataingia kwenye vitabu vya Simba!!! Na kwa maana nyingine tena ya msisitizo, hata GSM nao wanaweza kutangaziwa bidhaa zao na huyo huyo Haji Manara kwenye akaunti hiyo hiyo ya Haji Manara kama ambavyo Mo Dewji anavyoweza kutangaziwa bidhaa zake kwenye akaunti binafsi ya Antonio Nugaz!!

Na pia usisahau, kuna Kampuni ya Azam na Azam FC! Na pia kuna Simba SC na Mohamed Enterprises!!Nazi ni za Azam (kampuni) na sio za Azam FC!! Mshindani wa Simba SC ni Azam FC na sio Azam Kampuni! Na Mshindani wa Mohamed Enterprises sio Azam FC bali Azam Kampuni!!
 
Hiyo ni akaunti binafsi ya Haji Manara na sio akaunti ya Simba! Kwa maana nyingine, anayetangaza hiyo bidhaa sio Msemaji wa Simba bali Haji Manara!
Kwahiyo tumkute mwanaccm anapost Mambo ya Chadema kwenye account Yake kisa ni account binafsi.

Unajua terms and conditions za mkataba kuhusu conflict of interest ?
 
Umezingua, hata kama ni account binafsi,
Huyu anafaa kufukuzwa kazi anahihujumu timu,
 
Acheni uchawi Watanzania wenzangu, hamtaki mwenzenu awe na side income?
Yeye ni msemaji wa Simba sio wa Mwamedi Enteplaizi. Simba ina mdhamini mmoja tu? Kwa hiyo mnataka Manara awajibike kwa kila aliyewekeza Simba?
Hapo chacha!!! Hiyo nayo ni another strong point; Haji ni Msemaji/Mwajiriwa wa Simba na sio wa Mo!! Na isitoshe, Haji anatangaza bidhaa za Azam na sio za Azam FC!
 
Manara Ni wahed Simba imempa mapembe kaamua kuongezea mkia na manara nje ya Simba Ni mtu wa KAWAIDA tu leo itokee manara out mtakuja kushangaa wenyewe eti akaunti binafsi kama ni hivyo Leo Dkt. Kakurwa katibu mkuu CCM aitangaze chadema kwenye akaunti yke binafsi hivi unamtofautisha vipi manara na kwa wakati upi?
 
Hii haiko sawa..
 
Ni hujuma Sana tena iko wazi, ataanzaje kutangaza bidhaa za jirani wakati boss wake nae anabidhaa kama izzo, bidhaa za boss wake zisipo toka atawalipa Nini.?
Bosi wa Haji Manara ni Simba na sio Mo Dewji au METL!! Club ya Simba haina biashara ya nazi!! Isitoshe, Manara anatangaza nazi za kampuni ya Azam na sio Azam FC!! Na mambo yangekuwa yanaendeshwa kama mnavyotaka, basi hiyo Simba isingetangazwa kabisa pale Azam TV!!!
 
Hiyo haiko sawa mkuu.

Siku zote manara husema kwamba simba ni brand,
Na yeye popote anapokuwepo kuzungumza jambo lolote basi anakuwa amebeba brand ya simba.

Sasa iweje leo atangaze biashara za Azam?
Tena timu ambayo ni shindani kwenye ligi?
Kama kunaweza kufanywa mazungumzo ya kibiashara za matangazo kati ya Azam na manara,,
Watashindwaje kufanya mazungumzo ya kuuziana mechi?

Hapo kuna tatizo,,, nadhani jamaa kabugi sana kwa hilo.
 
Bosi wa Haji Manara ni Simba na sio Mo Dewji au METL!! Club ya Simba haina biashara ya nazi!! Isitoshe, Manara anatangaza biashara ya Azam na sio Azam FC!! Hali ingekuwa kama mnavyotaka, basi hiyo Simba isingetangazwa kabisa pale Azam TV!!!
Bado hata kama boss wake ni Simba, kutangaza bidhaa za Azam ni tatizo , Azam Fc, Simba Fc, Ni Bora angetangaza bidhaa za Simba tela,
 
Sasa iweje leo atangaze biashara za Azam?
Tena timu ambayo ni shindani kwenye ligi?
Haji Manara ametangaza nazi za Kampuni ya Azam na sio Azam FC! Msichanganye mambo!!! Ina maana leo hii Azam TV haiwezi kutangaza bidhaa za Simba kwa sababu Azam TV na Azam FC zote zinatokana na kampuni mama ya Azam, na Simba ni mshindani wa Azam FC?
 
Bado hata kama boss wake ni Simba, kutangaza bidhaa za Azam ni tatizo , Azam Fc, Simba Fc, Ni Bora angetangaza bidhaa za Simba tela,
Wewe ndo unaona ni tatizo lakini mwajiri wake hajaona hilo tatizo kwa sababu wanajua hakuna tatizo!!! Hivi kwa ufahamu wako, leo hii Mo Dewji amiliki TV Stations unaamini hatatangaza bidhaa za Yanga?! Au unataka kusema Azam TV hawawezi kutangaza bidhaa za Simba?!
 
Haji Manara ametangaza nazi za Kampuni ya Azam na sio Azam FC! Msichanganye mambo!!! Ina maana leo hii Azam TV haiwezi kutangaza bidhaa za Simba kwa sababu Azam TV na Azam FC zote zinatokana na kampuni mama ya Azam, na Simba ni mshindani wa Azam FC?
Utakauka koo broo bure.... Hawa hawaelewi
 
Haji Manara ametangaza nazi za Kampuni ya Azam na sio Azam FC! Msichanganye mambo!!! Ina maana leo hii Azam TV haiwezi kutangaza bidhaa za Simba kwa sababu Azam TV na Azam FC zote zinatokana na kampuni mama ya Azam, na Simba ni mshindani wa Azam FC?
Hivi muheshimiwa mbowe anaweza kutangaza kofia na mashati ya ccm ?
Halafu ikajengwa hoja ya kumtenganisha mbowe na chadema?

Kwanini watanzania tunakubali kufanywa wapuuzi kwa hoja za kipuuzi?

Hivi manara popote pale utamtambulisha kama msemaji wa simba,,?
Au utamtambulisha kama nani?

Hapo mwambieni kakosea,,,angeweza kutangaza zingine na sio brand za watu ambao wapo kwenye ligi moja.

Kumbuka azam pia ni brand.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…