Kwanini msemaji wa Club ya Simba anatangaza bidhaa za pinzani kibiashara? Inawezekana vipi?

Mkuu lakini pia Azam na Simba ni Baba na Shangazi wote ndugu...na pia Yeye Haji ameingia mkataba na Simba kua msemaji na hajaingia na Mo kumtangazia biashara zake.
Now you talk!!!!

Hapo kwenye simba na Azam ni ndugu .
 
Simuombei mabaya GSM.
Ila siku mungu akiamua kumchukua.
Urafiki wa yanga na GSM nao unakufaaa.
Anayeisaidia yanga Ni gharib sio kampuni ya GSM.
Mana hata mkataba hamna na GSM Ni kama mnasaidiwa tu.
GSM kampuni haiwatambui YANGA [emoji16][emoji16][emoji16].

Siwezi bishana nawe, Id yako tu yatosha kunituliza
 
Hao wote wanalipwa na nani?
 
Haji kaajiriwa na simba sc holding company. (Wadaawa) sio Mo kwahyo hatangazi kampuni nyingine. Mfano ulaya Messi ni ambassador wa Adidas anatangaza Adidas ila Barca ni Nike.
 
Hivi dogo Haji Manara si ni mtu mzima mwenye maamuzi yake mwenyewe? Kama anatangaza bidhaa za biashara kutoka kwenye account yake yeye binafsi kuna tatizo gani hapa? Mwacheni Manara na mambo yake binafsi.
 
Mbona Wasafi Media huwa wanaitangaza Azam media...hiyo ni business tu haihusishi mambo binafsi.
 
hivi hawa wasanii wetu wanaushawishi kweli kwa mtu mpaka anunue bidhaa😎😎😎
 
Mkuu jezi za Barcelona sponsor ni Nike ila Messi kwenye account zake za Instagram anapost kavaa t-shirt za adidas ana post viatu vipya vya Adidas. Nafikiri hamna shida hapo

Kingine kwa wenzetu mamlaka makubwa anakuwa nayo kocha, kocha ndo anazungumza 90% ya mambo public ya team, 5% inshu ikiwa critical sana ndo utamuona CEO au President, 5% ambazo mara nyingi huwa ni marudio tu ya aliyosema kocha na kutangaza siku za mechi utaona kwenye TV za club na social media zao, huo upuuzi upo Africa tu na nahisi kwa Simba umezidi.

Ningetamani kwenye transformation ya Yanga hiko kitu kipunguziwe madaraka, maana eti inshu critical ya mikataba ya wachezaji mfano Morisson anatafutwa Bumbuli, swala la mchezaji kuchelewa kambini anatafutwa haji badala ya Sven
 
Anachofanya Haji sio kosa bali kwa ajili ya kuondoa kitu wahaya wanaita "conflict of Interest" inabidi mikataba ya wafanyakazi woote wa Simba ibadilishwe na iwekewe kipengele hicho cha kuzuia kujihusisha na bidhaa zinazofanana na za mdhamini au mmiliki wa club. Mfano mshabiki wa Simba anaweza kuacha kunywa maji ya Mo akawa anakunywa ya uhai tu kisa kaona Haji anatangaza akidhani kuwa akinywa hayo maji anaiunga mkono Simba...
 
Anatangazaga vitu vingi kama unga wa ngano na maji
 
Haji Manara ametangaza nazi za Kampuni ya Azam na sio Azam FC! Msichanganye mambo!!! Ina maana leo hii Azam TV haiwezi kutangaza bidhaa za Simba kwa sababu Azam TV na Azam FC zote zinatokana na kampuni mama ya Azam, na Simba ni mshindani wa Azam FC?
Huwa anatangaza maji ya Uhai, na Unga wa ngano wa Azam, MO pia ana maji ya kunywa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…