Kwanini Mungu alituumba sisi wanadamu, iwapo alijua kuwa tutamuasi na atatupeleka motoni?

2-Hatatuchoma milele na milele, MUNGU sio mkatili ki hivo atatuchoma na kuteketeza dhambi, ziki isha kazi ya moto imemalizika na dunia itachipuka upya pasina dhambi.

4- Ukimcha MUNGU kwa kuogopa adhabu ya moto hutoboi mkuu, mpende kwanza, then kumcha kutakuja automatically, ndo maana anasema
Ndo maana anasema mkinipenda mimi mtazishika amri zangu,
wala nira yangu sio nzito na mzigo wangu ni mwepesi, .....kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo.
So mkuu, shetani anatufanye tuone maisha ya Anasa ndio maisha while hata kama kusingekua na moto, mwisho wa anasa ni majuto matupu mkuu.
 
Ukifatilia kwa kina habari zinazohusu Mungu utagundua ni uongo tu
 
Mleta mada Unapoteza muda kutuuliza sisi kaongee na Mungu Mwenyewe
 
Ninavyojua mimi adhabu yq moto n8 kama kurefresh dunia then wabaki waliochaguliwa kuishi milele amabo inasemekana walishateuliwa hata kabla dunia haijaumbwa, kwa hiyo kwenda kanisani na msikitin na kujifanya mfia dini ni kujitesa maana wateule walishapangwa. Yaani mechi tayari matokeo yapo mezani maisha yako ni ushahidi tu.
 
1)Mungu akituchoma sisi kwenye moto wa milele, ataongezeka nini, na kufaidiwa nini? Asipotuchoma atapungukiwa nini?



3)Asingetuumba kuna mtu angemuuliza kwanini hajatuumba wakati yeye ni muweza wa yote?
1- MUNGU hafurahii kuona mtu akipotea yeye mwenyewe anasema, mimi MUNGU sifurahii kufa kwake mdhambi nia yake wadhambi wote wafikirie toba.
2-Hakuumba kwa makusudi mabaya ila yupo alifanya uchaguzi mbaya, wazazi wetu wa kwanza.

Mkuu shetani anatumia mbinu kubwa sana inayofanikiwa these days, kutufanya tuamini hatuwezi kumtii na madai yake ya MUNGU ni dictator yanapata sana mashiko, lakini hayuko hivo, Tazama stori ya Yona na mji wa Ninawi, haya Sodoma na Gomora, mpaka kuangamizwa kwa Jerusalem mwaka 78.

Mwisho mkuu
“Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;

— Kumbukumbu la Torati 30:19 (Biblia Takatifu).
 
Hakuna aliyechaguliwa mkuu, bali sisi ndio tunafanya chaguzi kila siku za kuishi kwetu.
 
Wakati fulani ukifikiria kwa kina utagundua kuna mambo Mungu anasingiziwa ili kuwapa makasisi fursa ya kutoa upepo, fikiria mtu anasema Mungu ana wivu, Mungu amewaua watu kwa gharika, Mungu anataka tumpe, mbona yeye ana full control ya kila kitu kwanini ajipe taabu kutusubiri tumpe kwa kusuasua? Si achukue tu kama anavyochukua uhai?
 
Mkuu Nanukuu ".......labda kuna vitu ambavyo sivijui."
Yeah .. hujasema kwamba ni kwa Upendo tu Mungu alituumba i.e hakushurutishwa na yeyote bali ni kwa Upendo wake tu; na tena alituumba kwa mfano na sura yake. Isitoshe Mungu huyo huyo kwa Upendo wake huo huo, alituweka Huru i.e. tufanye mambo kwa Utashi wetu wenyewe -unaamua unachotaka.
Kwa hiyo Mtu kwa utashi wake anachagua kuelekea sehemu kunakoitwa motoni au mahali panapoitwa mbinguni. (Mbinguni/Motoni - Hayo ni majina tu na hayana uhusiano na kilichopo mahali hapo/huko).
Mungu hapeleki watu motoni au mbinguni kumbuka kwenda kwako mbinguni au motoni hakumwongezei au kumpunguzia chochote) Huko tunakwenda kwa Hiari yetu wenyewe- Tunajichagulia twende wapi. Mfano; Uko Moro na unataka kwenda Dar. Halafu unapata maelekezo, Unaambiwa barabara ya Dar ni hii inayoelekea mashariki lakini hii inayoelekea magharibi ni ya kwenda Iringa. Wewe unataka kwenda Dar lakini kwa hiari yako unaelekea Magharibi. Kwa kutumia Hiari yako vibaya Kamwe hutofika Dar. Kwa mfano huo basi; Kwa hiyo Tenda mema uende kuwa raia wa nchi inayoitwa Mbinguni; au fanya ukorofi na kutenda mabaya ujitwalie uraia wa nchi inayoitwa Motoni. Kwani shida iko wapi? Tunajisajili wenyewe kwa hiari bila shuruti.
 
Usiamini upuuzi toka kwa vitabu vilivyorungwa na binadamu kama wewe na kuaminishwa kuwa ni vya Mungu. Hivi wewe kama ni mzazi kweli unaweza choma moto wanao kisa hawakusikilizi? Na kama Yesu kafa msalabani kufuta dhambi zetu kwanini Mungu akusudie kutuchoma moto baada ya kufa ikiwa mwanawe alishalipa tayari? Tatizo la hizi dini ni ushetani mtupu tu na ndiyo maana unaona hata wenyewe Waarab na Wayahudi kila kukicha wanauana japo wanaamini Mungu mmoja. Sisi Waafrika tunaanza baguana kwa kuwa na dini tofauti tofauti zisizotuhusu sisi, si ujinga huu? Hizi dini ni laana tupu kwetu Waafrika.
 
Hizo ni Nadharia tu za kututawala na kututia hofu.

Mimi ni mzazi pamoja na mapungufu yangu yote, siwezi kumchoma mwanangu moyo.

Mungu amejaa Upendo hawezi kuwachoma watu wake kwa moto wa milele.
Moto hakuna hiyo ni habar ya kusadikika tu isipokuwa watenda zambi hawatauona ufufuo na hawatakaa meza moja pamoja na bwana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…