Kwanini mvua imnyeshee Waziri Jafo huku mgeni wake akifunikwa na mwamvuli? Ukoloni mamboleo

Kwanini mvua imnyeshee Waziri Jafo huku mgeni wake akifunikwa na mwamvuli? Ukoloni mamboleo

Teko Modise

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2017
Posts
2,331
Reaction score
7,733
Hapa ni Airport wakati waziri Jafo akimpokea mgeni kutoka falme za kiarabu.

Waziri kulowa na mvua ruksa ila mgeni hapana?

Hii hapana kwangu mimi.
8B49EB15-2CBE-4468-AD8D-D6CDB971A0EB.jpeg
 
Kama mwamvuli ulikua mmoja sioni tatizo hapo, au Bora wangeacha tu wote wapigwe na mvua

Ila wangemkinga jafo afu wamuache mgeni hapo ndo ingekua na ukakasi


Mwendo wa kutembeza bakuli tu
 
Hapa ni Airport wakati waziri Jafo akimpokea mgeni kutoka falme za kiarabu.

Waziri kulowa na mvua ruksa ila mgeni hapana?

Hii hapana kwangu mimi.
View attachment 2510667
Utumwa ni hatari hasa unapoingia vichwani na matumboni. Hapa kwanini wasitudharau na kutuibia hawa wezi tunaowanyenyekea na kuwaabudia? Jafo hana ujanja. Mali wanazo lakini wamezikalia na kushikilia kuomba na kukopa. Mtakuja kugeuzwa shauri yenu.
 
Mwanamfalme wa familia ya kifalme .Hujamuona waziri dkt.Pindi Chana au ni mahaba tu kwa Jafo yamekutia upofu?
 
Nimejikuta nimekumbuka mbali!!

Wakati hayati Kigoma Malima anaagwa pale Viwanja vya Mnazi Mmoja ili akazijwe huko kwao, ghafla manyunyu yakaanza wakati wanajiandaa kubeba jeneza lenye mwili kupakia kwenye gari.

Rais Salmin Amour "Komandoo" alikuwa ni mmoja ya waombolezaji na hakusita kujumuika na wananchi waliojitokeza kutoa heshima zao za mwisho pale Mnazi Mmoja.

Sasa kwakuwa kuna manyunyu, mlinzi wa Rais, akatoa mwamvuli na kumkinga Rais Salmin na manyunyu ya mvua.

Kitendo hiko kikapingwa na Sheikh Ponda akisema iweje wengine mkingwe na mvua na wengine tuloe hali ya kuwa wote ni binadamu na tupo msibani.

Basi Salmin Amour akamuamrisha mlinzi wake ashushe mwamvuli na aloe kama wengine!!

Hapo ndipo macho na masikio ya watanzania walipoanza kumjua Sheikh Ponda!!
 
Back
Top Bottom