Kwanini Mwalimu Nyerere hakujenga hospitali ya mkoa wa Mara? Ujenzi ulisimama kwa miaka 40 na sasa kukamilika mwaka huu!

Kwanini Mwalimu Nyerere hakujenga hospitali ya mkoa wa Mara? Ujenzi ulisimama kwa miaka 40 na sasa kukamilika mwaka huu!

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Kuna mambo ambayo serikali imekuwa ikiyafanya nchi hii yanashangaza sana.

Mchoro wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere yaani Kwangwa ulibuniwa mwaka 1975 na baadae mwaka 1977 ujenzi ulianza.

Baadae mwaka huo wa 77 ujenzi wa hospitali hii iliyoko Musoma, ulisimama na kendelea kidogo kabla ya kusimama rasmi mwaka 1980 na huo ndo ukawa mwisho wa kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Kukamilika kwa ujenzi wa hospitali hiyo kungeifanya kuwa moja ya hospitali kubwa za mkoa za Tanzania ikiwa na majengo makubwa matatu, jengo la wazazi yaani "Wing C" na jengo moja kubwa la "Wing B" lenye vitanda na jingo la "Wing A" ambalo litakuwa ni la matibabu maalum.

Ni miaka miwili ilopita ambapo raisi John Magufuli aliamua kuelekeza fedha kiasi cha shilingi bilioni 15 ili ujenzi wa hospitali hiyo ukamilishwe.

Na hiyo ilikuwa ni baada ya ushawishi wa mkuu wa mkoa Adam Malima na mkuu wake wa wilaya pamoja na ufuatiliaji wa Waziri Mkuui na wazri wa Afya.

Ujenzi huo unatarajia kukamilika rasmi mwezi August mwaka huu na ujenzi bado waendelea chini ya usimamizi wa shirika la nyumba la taifa NHC.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba imewachukua maraisi watano tangu ujenzi wa hospitali hii usimame yaani hayati raisi Nyerere mwenyewe, Ally Hassan Mwinyi, Benjaminui Mkapa, na raisi Kikwete ndipo raisi Magufuli aamue kutenga fedha za ujenzi huo.

Licha ya hivyo, wakuu wa mkoa wapatao 16 ambao wamepita kusimamia mkoa wa Mara bila hata kupata wazo la kutembelea gofu la hospitali hii na kuliacha kama lilivyo.

Jengo la "Wing C" linatarajia kukamilika hivi karibuni na litakuwa likihudumia mama na mtoto.

Hivyo, hatua ya Rais John Magufuli kuidhinisha fedha za kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo kiasi cha shilingi bilioni 15 ni ya kizalendo na inahitaji kupongezwa na kuungwa mkono.

Huduma ya Afya katika nchi yoyote ile hutegemea sana miundombinu ya hospitali na vituo bora vya afya.

Serikali imekuwa ikijitahdi kuelekeza fedha za maendeleo katika maeneo haya muhimu ya Afya na Elimu kwani masuala haya mawili ni moja ya mihimii ya ustawi wa taifa kimaendeleo na kiuerevu.

Hata yule mtu aliezaliwa mwaka 75 sasa hivi ana miaka 43!

Je, ni sababu zipi ziliwezesha kutokamilika kwa hospitali hii?

Je, wakuu wote hao wa mikoa waliiona jengo la gofu la hospitali hiyo na walichukua hatua gani?

Je, kutoendelea kwa ujenzi wa hospitali hii kumetokana na sababu za kisiasa?
 
Wengi wa viongozi waliopita wa mkoa huo walikua wakiumwa wanakimbizwa Bugando hospitali Mwanza .sasa wakimalizie hicho kiporo cha nini??

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu, ukisema hivyo bado unakuwa hujajibu suali.

Kwamba,

Je, ni sababu zipi ziliwezesha kutokamilika kwa hospitali hii?

Je, wakuu wote hao wa mikoa waliiona jengo la gofu la hospitali hiyo na walichukua hatua gani?

Je, kutoendelea kwa ujenzi wa hospitali hii kumetokana na sababu za kisiasa?
 
Richard,
Bahati mbaya tu, kwa nia njema ya kuwakomboa ndugu zetu waganda vita vya kagera viliyumbisha sana uchumi wa nchi yetu.Ndio maana Mwl JKN alikwama kufanikisha mambo mengi tu.Pia fitina za mabeberu maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha South Africa,Zimbabwe na Namibia zinakuwa huru.
 
sijui umesaliwa lini mwaka 1977 na kuendelea tulikuwa vitani kipindi cha miaaka ya 80 hali ya nchi ilikuwa mbaya sana baada ya mwalimu kutoka kila kiongozi aliyeingia alikuwa na vipaumbele vyake kwa hiyo hospital kutomalizika kipindi cha Nyerere siyo hoja
 
Richard,
Hapa unataka kumpigia Magu debe...Mwaka 2009 kanisa Katoliki liliingia mkataba na serikali kwa ajili ya kuanza ujenzi na kanisa Katoliki liliweka bilioni mbili katika mkataba wa Awali...Ujenzi ulifanyika kidogo...lkn kilichokuja kufanyika ni kwamba kuna wananchi ambao walidai fidia ya kuondolewa katika eneo hilo.

hivyo zilihitajika Tsh 70 milioni ili walipwe fidia..kwa vile hosptali za mikoa na rufaa zinatekelezwa na wizara ya afya ...wizara ya afya kipindi hicho haikuwa tyr kulipa fidia na halmashauri ya manispaa ya musoma haikuwa tyr kulipa.

Siwezi kuacha kuipongeza serikali kuendeleza ujenzi huu ila kwa Marais waliopita waliendeleza miradi mingine mikubwa iliyoachwa ..issue ni vipaumbile na FEDHA tu...
 
Richard,
Bahati mbaya tu, kwa nia njema ya kuwakomboa ndugu zetu waganda vita vya kagera viliyumbisha sana uchumi wa nchi yetu.Ndio maana Mwl JKN alikwama kufanikisha mambo mengi tu.Pia fitina za mabeberu maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha South Africa,Zimbabwe na Namibia zinakuwa huru.
Umenena sawa kabisa.
 
Wabongo bana eti wanauliza nani alikwamisha ujenzi ?

Kwani tokea wakati huo kuna Serikali nyingine zaidi ya CCM ,ilikuwa madarakani.?

Matatizo mengi ya nchi hii yameletwa na serikali ya CCM sababu ya ufisadi uliojikita ndani ya CCM.
 
Nyerere hakutawaliwa na ubinafsi na kwetu kwanza,hakujengwa na lugha wewe kabila gani bali wewe Mtanzania
 
Aliyoyafanya Hayati Baba wa Taifa ni mengi sana kuliko kiongozi yeyote yule,Kwani baada ya Nyerere Nchi ilikuwa haina Uongozi? Waziri mkuu alitoka huko,Wakuu wa Majeshi,Mawaziri kibao,Wabunge ndio usiseme,Wakuu wa Mikoa na Wilaya yaani wote hao walishindwa kuibana Selikali ikamilishe Hospitali? Viongozi wakitaifa wakifanya ziara huko kwanini hawapelekwi kuiona hiyo hospitali? Mwacheni Mwl.Nyerere Apumzike.
 
Richard,

..labda ungeuliza kati ya 1977 na 2017 hospitali ngapi za mikoa / rufaa zilijengwa hapa nchini.

..pia katika kipindo hichohicho ni miradi gani ya afya ilitekelezwa hapa nchini, and particularly, mkoani Mara.

..pia miradi gani ya ujenzi ya maendeleo ilifanyika ktk kipindi hicho mkoani Mara. Je, kuna mradi ambao ulipatiwa fedha lakini haukuwa na umuhimu kulinganisha hospitali ya mkoa wa Mara?

..wakati mwingine mambo hayo hutegemea upatikanaji wa FEDHA na VIPAUMBELE ktk awamu husika ya uongozi.
 
Richard,

..labda ungeuliza kati ya 1977 na 2017 hospitali ngapi za mikoa / rufaa zilijengwa hapa nchini.

..pia katika kipindo hichohicho ni miradi gani ya afya ilitekelezwa hapa nchini, and particularly, mkoani Mara.

..pia miradi gani ya ujenzi ya maendeleo ilifanyika ktk kipindi hicho mkoani Mara. Je, kuna mradi ambao ulipatiwa fedha lakini haukuwa na umuhimu kulinganisha hospitali ya mkoa wa Mara?

..wakati mwingine mambo hayo hutegemea upatikanaji wa FEDHA na VIPAUMBELE ktk awamu husika ya uongozi.

Mkuu heshima kwako.

Mimi suali langu mantiki yake ni kwamba kila mkoa unatakiwa uwe na hospitali kuu au ya rufaa.

Hivyo, mkoa wa Mara kwa miaka takriban 40 imekosa huduma hiyo ya kuwa na hospitali ya rufaa na wagonjwa wengi wamekuwa wakipelekwa Bugando kwa miaka hiyohiyo takriban 40.

Hivyo si mbaya kujuzwa sababu mahsusi licha ya kwamba fedha hizo (kiasi kilichotolewa na serikali ya sasa) kingeweza kupatikana kw amuda mfupi ili kumalizia ujenzi wa hospitali hiyo.

Nadhani wanipatapata hapo.
 
Richard,
Hapa unataka kumpigia Magu debe...Mwaka 2009 kanisa Katoliki liliingia mkataba na serikali kwa ajili ya kuanza ujenzi na kanisa Katoliki liliweka bilioni mbili katika mkataba wa Awali...Ujenzi ulifanyika kidogo...lkn kilichokuja kufanyika ni kwamba kuna wananchi ambao walidai fidia ya kuondolewa katika eneo hilo.

hivyo zilihitajika Tsh 70 milioni ili walipwe fidia..kwa vile hosptali za mikoa na rufaa zinatekelezwa na wizara ya afya ...wizara ya afya kipindi hicho haikuwa tyr kulipa fidia na halmashauri ya manispaa ya musoma haikuwa tyr kulipa.

Siwezi kuacha kuipongeza serikali kuendeleza ujenzi huu ila kwa Marais waliopita waliendeleza miradi mingine mikubwa iliyoachwa ..issue ni vipaumbile na FEDHA tu...
Mkuu umezungumza sawia kabisa. Mimi nimeishi Kigera na Lwamlimi maeneo jirani na mradi huo wa hospitali. Na hiyo MoU baina ya Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma na serikali iko namna hiyo ulivyozungumza.

Ila mtoa post anataka kuwakweza watu hapa kwa sababu anazozijua mwenyewe. Sisi wana Mara hatudanganyiki na mapambio yenu kwa stone.
 
Mkuu umezungumza sawia kabisa. Mimi nimeishi Kigera na Lwamlimi maeneo jirani na mradi huo wa hospitali. Na hiyo MoU baina ya Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma na serikali iko namna hiyo ulivyozungumza.

Ila mtoa post anataka kuwakweza watu hapa kwa sababu anazozijua mwenyewe. Sisi wana Mara hatudanganyiki na mapambio yenu kwa stone.

Kujenga hospitali kubwa ya rufaa ya mkoa, ichukue miaka zaidi ya 40?

Tuseme tunamwondoa hayati Mwalimu twasema tuanzie mwaka 1985 hadi leo ni miaka 35, bado wazungumzia vipaumbele?
 
Back
Top Bottom