Kwanini Mwalimu Nyerere hakujenga hospitali ya mkoa wa Mara? Ujenzi ulisimama kwa miaka 40 na sasa kukamilika mwaka huu!

Kwanini Mwalimu Nyerere hakujenga hospitali ya mkoa wa Mara? Ujenzi ulisimama kwa miaka 40 na sasa kukamilika mwaka huu!

Richard,
Bahati mbaya tu, kwa nia njema ya kuwakomboa ndugu zetu waganda vita vya kagera viliyumbisha sana uchumi wa nchi yetu.Ndio maana Mwl JKN alikwama kufanikisha mambo mengi tu.Pia fitina za mabeberu maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha South Africa,Zimbabwe na Namibia zinakuwa huru.

mkuu, hata zaire ilikuwa mstari wa mbele kuhakikisha namibia inakuwa huru pamoja na Africa ya kusini tena marekani ambaye ni mmoja wa hao mnaowaita mabeberu alitoa misaada mingi tu kwa zaire ikiwemo ya ki uchumi kutokana na juhudi za zaire kutetea uhuru , hata uganda pia ilikuwa mstari wa mbele kuhakikisha zimbabwe inakuwa huru tena amin ali propose military intervention kabisa lakini uchumi wa nchi hizi mbili ulikuwa imara kuliko sisi
ni wakati watanzania tuseme ukweli pale tulipokwama tuache kujificha kwenye kichaka cha kupambania uhuru


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ama kweli usilolijua ni sawa na usiku wa kiza.

Wakati wazo la kujenga hospitali linabuniwa wananchi walianza kuchangishwa pesa za ujenzi huo, siku ya kwanza michango ilihamasishwa na marehemu Joseph Kizurira Nyerere aliyekuwa mbunge akiwakilisha mkoa wa Mara, wakati huo kulikuwa na mfumo wa wabunge wa mikoa,mbali na wabunge wa majimbo.
Wananchi walichanga pesa pale uwanja wa Karume ,kila mtu kwa kiwango alichokuwa nacho,pia walikuwapo wafanyabiashara mbali mbali wa Musoma wakatoa michango yao.
Hapo ukaundwa mfuko wa ujenzi wa hospitali ya Mkoa ya Kwangwa,chini ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Ili kupata mapato zaidi ,bidhaa mbali mbali kama vile mafuta, vinywaji nk.viliongezwa bei kwa ajili ya kutunisha mfuko wa ujenzi wa hospitali na ujenzi ulianza,ila sijui serikali ilichangia kiasi gani kwa wakati huo.
Tatizo kubwa la ufisadi lilijitokeza, mfuko ulishambuliwa na mchwa hakuna mfano,na hapo ndio ujenzi ukayumba na hatimaye kusimama jumla.

Nashangaa sana,maelezo yote yametolewa lkn ukweli huu haujatajwa ,Mungu atusamehe.
Hatimaye makato mbali mbali kwa ajili ya ujenzi wa hospitali yalisimamishwa na ndio kikawa kifo rasmi cha ujenzi huo.

Wengi wa mafisadi waliolamba pesa ya ujenzi wa hospitali ya Kwanga walikwishatangulia mbele ya haki, natumahi wanaendelea kujibu huko kwa waliyoyatenda.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ama kweli usilolijua ni sawa na usiku wa kiza.

Wakati wazo la kujenga hospitali linabuniwa wananchi walianza kuchangishwa pesa za ujenzi huo, siku ya kwanza michango ilihamasishwa na marehemu Joseph Kizurira Nyerere aliyekuwa mbunge akiwakilisha mkoa wa Mara, wakati huo kulikuwa na mfumo wa wabunge wa mikoa,mbali na wabunge wa majimbo.
Wananchi walichanga pesa pale uwanja wa Karume ,kila mtu kwa kiwango alichokuwa nacho,pia walikuwapo wafanyabiashara mbali mbali wa Musoma wakatoa michango yao.
Hapo ukaundwa mfuko wa ujenzi wa hospitali ya Mkoa ya Kwangwa,chini ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Ili kupata mapato zaidi ,bidhaa mbali mbali kama vile mafuta, vinywaji nk.viliongezwa bei kwa ajili ya kutunisha mfuko wa ujenzi wa hospitali na ujenzi ulianza,ila sijui serikali ilichangia kiasi gani kwa wakati huo.
Tatizo kubwa la ufisadi lilijitokeza, mfuko ulishambuliwa na mchwa hakuna mfano,na hapo ndio ujenzi ukayumba na hatimaye kusimama jumla.

Nashangaa sana,maelezo yote yametolewa lkn ukweli huu haujatajwa ,Mungu atusamehe.
Hatimaye makato mbali mbali kwa ajili ya ujenzi wa hospitali yalisimamishwa na ndio kikawa kifo rasmi cha ujenzi huo.

Wengi wa mafisadi waliolamba pesa ya ujenzi wa hospitali ya Kwanga walikwishatangulia mbele ya haki, natumahi wanaendelea kujibu huko kwa waliyoyatenda.


Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa hiyo tunaanza kupata sababu :

1. Ubadhilifu na ufisadi.

Haya tuendelee...
 
Mkuu heshima kwako.

Mimi suali langu mantiki yake ni kwamba kila mkoa unatakiwa uwe na hospitali kuu au ya rufaa.

Hivyo, mkoa wa Mara kwa miaka takriban 40 imekosa huduma hiyo ya kuwa na hospitali ya rufaa na wagonjwa wengi wamekuwa wakipelekwa Bugando kwa miaka hiyohiyo takriban 40.

Hivyo si mbaya kujuzwa sababu mahsusi licha ya kwamba fedha hizo (kiasi kilichotolewa na serikali ya sasa) kingeweza kupatikana kw amuda mfupi ili kumalizia ujenzi wa hospitali hiyo.

Nadhani wanipatapata hapo.

..Je, mikoa yote Tz ina hospitali za mkoa?

..au wewe uko interested na mkoa wa Mara peke yake.
 
Kwangwa MWL Nyerere Memorial Medical centre kama inavyoitwa kwa sasa, ilianza kujengwa miaka ya 1977 kama wadau wengine walivyosema hapo juu, ujenzi ulianza kwa kutumia michango ya wananchi na watumishi wa umma nao walikua wakikatwa sehemu ya mshahara ili kufanikisha ujenzi.

Baadae ufisadi ulianza kwenye michango na kupelekea ujenzi kusimama kwa muda mrefu, kanisa Katoliki kiliingilia kati ili kuendeleza ujenzi lakini haikupata sapoti kubwa sana kutoka kwa serikali ili kuendeleza ujenzi.
Awamu ya kwanza wa Jakaya Kikwete, Lowasa akiwa waziri mkuu alipenda sana ujenzi wa Hospitali ya Kwangwa ijengwe na kumalizika lakini alipata kikwazo kutoka kwa Wanamgambo waliokua wakimpinga wakiongozwa na RIP Samwel Sita (Mungu amlaze panapostaili) kisa ni urais tu. Si unajua angeonekana amemaliza Hospitali kwao Nyerere bwana....credit
Figisu ilianza adi Washauri waliokua site na ujenzi ukiwa unaendelea ofisi ya RAS ambao ndo walikua Washitiri wakala Pesa ya mradi kilichopelekea Wing B kutokumalizika, Washauri wakatupiliwa mbali na wakaondoka na mradi ukasimama.....watu walipiga pesa ndefu kuliko pesa uliowekwa kwenye ujenzi....(RAS Mara walikua mafisadi balaa).

Mwaka 2017 mwanzoni TBA walipewa fungu ili waweze kumalizia Wing B, baada ya kumalizika kwa Wing B na Hospitali zote kurudishwa kua chini ya Wizara ya Afya ikaonekana kua Hospitali ya Kwangwa kwasasa haikidhi vigezo vya sera za sasa za Wizara wa Afya hivyo kuna sehemu lazima zibomolewe na kuifanyia marekebisho.
Mwaka 2018 TBA wakapewa fungu la kuendelea na ujenzi Phase VI kwa kuanza na Wing C kuifanya wudi ya wazazi, wataalama wakakaa na kuiboresha ili iendane na sera ya sasa ya Wizara ya Afya. Baada ya Phase IV kuisha sasa Wing A na B zinaendelea kujengwa na NHC kwa phase VIII.

Iwapo Hospitali zisingerudishwa kua chini ya Wizara ya Afya, Hospitali nyingi zisingeisha make ofisi za RAS bado zimejaa siasa na RUSHWA kubwakubwa sana.
 
Mngeweka picha ya hilo jengo ningewaelewa Zaidi
1585630047212.png
 
Richard,
Bahati mbaya tu, kwa nia njema ya kuwakomboa ndugu zetu waganda vita vya kagera viliyumbisha sana uchumi wa nchi yetu.Ndio maana Mwl JKN alikwama kufanikisha mambo mengi tu.Pia fitina za mabeberu maana alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha South Africa,Zimbabwe na Namibia zinakuwa huru.
Upo sahihi kabisa kumbuka budget ya nchi inaanza kutumika july sasa 1978tupo vitani 1980mpaka1982 Njaa 84 mkuu ana ng’atuka 85mpaka 95ruksa tupo kwenye mpito wa kiuchumi na kisiasa
Mimi nadhani baada ya Ruksa walio fuata wangeuliziwa lkn sio wezee wetu Mchonga na Ruksa
Lkn kanda ya ziwa kuna rufaa bugando wananchi walipata huduma,za juu kama vile kanda ya kaskazini kuna KCMc kanda ya nyanda za juu kuna Mbeya ruffaral hosp na pwani ni muhimbili kati kuna benjamin mkapa
Awamu ya Jk wapil yeye alideal sn na shule na maabara barabara mzee Jpm yeye ni hosp kwenye vijiji
 
mkuu, hata zaire ilikuwa mstari wa mbele kuhakikisha namibia inakuwa huru pamoja na Africa ya kusini tena marekani ambaye ni mmoja wa hao mnaowaita mabeberu alitoa misaada mingi tu kwa zaire ikiwemo ya ki uchumi kutokana na juhudi za zaire kutetea uhuru , hata uganda pia ilikuwa mstari wa mbele kuhakikisha zimbabwe inakuwa huru tena amin ali propose military intervention kabisa lakini uchumi wa nchi hizi mbili ulikuwa imara kuliko sisi
ni wakati watanzania tuseme ukweli pale tulipokwama tuache kujificha kwenye kichaka cha kupambania uhuru


Sent using Jamii Forums mobile app
Zaire ile ya Mobutu aliyemuu Patrice lumumba? Na uganda ile ya Amin iliyokuwa inachinja watu kama mbuzi? Au umekengeuka?
 
Kuna mambo ambayo serikali imekuwa ikiyafanya nchi hii yanashangaza sana.

Mchoro wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere yaani Kwangwa ulibuniwa mwaka 1975 na baadae mwaka 1977 ujenzi ulianza.

Baadae mwaka huo wa 77 ujenzi wa hospitali hii iliyoko Musoma, ulisimama na kendelea kidogo kabla ya kusimama rasmi mwaka 1980 na huo ndo ukawa mwisho wa kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Kukamilika kwa ujenzi wa hospitali hiyo kungeifanya kuwa moja ya hospitali kubwa za mkoa za Tanzania ikiwa na majengo makubwa matatu, jengo la wazazi yaani "Wing C" na jengo moja kubwa la "Wing B" lenye vitanda na jingo la "Wing A" ambalo litakuwa ni la matibabu maalum.

Ni miaka miwili ilopita ambapo raisi John Magufuli aliamua kuelekeza fedha kiasi cha shilingi bilioni 15 ili ujenzi wa hospitali hiyo ukamilishwe.

Na hiyo ilikuwa ni baada ya ushawishi wa mkuu wa mkoa Adam Malima na mkuu wake wa wilaya pamoja na ufuatiliaji wa Waziri Mkuui na wazri wa Afya.

Ujenzi huo unatarajia kukamilika rasmi mwezi August mwaka huu na ujenzi bado waendelea chini ya usimamizi wa shirika la nyumba la taifa NHC.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba imewachukua maraisi watano tangu ujenzi wa hospitali hii usimame yaani hayati raisi Nyerere mwenyewe, Ally Hassan Mwinyi, Benjaminui Mkapa, na raisi Kikwete ndipo raisi Magufuli aamue kutenga fedha za ujenzi huo.

Licha ya hivyo, wakuu wa mkoa wapatao 16 ambao wamepita kusimamia mkoa wa Mara bila hata kupata wazo la kutembelea gofu la hospitali hii na kuliacha kama lilivyo.

Jengo la "Wing C" linatarajia kukamilika hivi karibuni na litakuwa likihudumia mama na mtoto.

Hivyo, hatua ya Rais John Magufuli kuidhinisha fedha za kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo kiasi cha shilingi bilioni 15 ni ya kizalendo na inahitaji kupongezwa na kuungwa mkono.

Huduma ya Afya katika nchi yoyote ile hutegemea sana miundombinu ya hospitali na vituo bora vya afya.

Serikali imekuwa ikijitahdi kuelekeza fedha za maendeleo katika maeneo haya muhimu ya Afya na Elimu kwani masuala haya mawili ni moja ya mihimii ya ustawi wa taifa kimaendeleo na kiuerevu.

Hata yule mtu aliezaliwa mwaka 75 sasa hivi ana miaka 43!

Je, ni sababu zipi ziliwezesha kutokamilika kwa hospitali hii?

Je, wakuu wote hao wa mikoa waliiona jengo la gofu la hospitali hiyo na walichukua hatua gani?

Je, kutoendelea kwa ujenzi wa hospitali hii kumetokana na sababu za kisiasa?
Wakyura tupo imara hatuumwiumwi kizembe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mambo ambayo serikali imekuwa ikiyafanya nchi hii yanashangaza sana.

Mchoro wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere yaani Kwangwa ulibuniwa mwaka 1975 na baadae mwaka 1977 ujenzi ulianza.

Baadae mwaka huo wa 77 ujenzi wa hospitali hii iliyoko Musoma, ulisimama na kendelea kidogo kabla ya kusimama rasmi mwaka 1980 na huo ndo ukawa mwisho wa kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Kukamilika kwa ujenzi wa hospitali hiyo kungeifanya kuwa moja ya hospitali kubwa za mkoa za Tanzania ikiwa na majengo makubwa matatu, jengo la wazazi yaani "Wing C" na jengo moja kubwa la "Wing B" lenye vitanda na jingo la "Wing A" ambalo litakuwa ni la matibabu maalum.

Ni miaka miwili ilopita ambapo raisi John Magufuli aliamua kuelekeza fedha kiasi cha shilingi bilioni 15 ili ujenzi wa hospitali hiyo ukamilishwe.

Na hiyo ilikuwa ni baada ya ushawishi wa mkuu wa mkoa Adam Malima na mkuu wake wa wilaya pamoja na ufuatiliaji wa Waziri Mkuui na wazri wa Afya.

Ujenzi huo unatarajia kukamilika rasmi mwezi August mwaka huu na ujenzi bado waendelea chini ya usimamizi wa shirika la nyumba la taifa NHC.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba imewachukua maraisi watano tangu ujenzi wa hospitali hii usimame yaani hayati raisi Nyerere mwenyewe, Ally Hassan Mwinyi, Benjaminui Mkapa, na raisi Kikwete ndipo raisi Magufuli aamue kutenga fedha za ujenzi huo.

Licha ya hivyo, wakuu wa mkoa wapatao 16 ambao wamepita kusimamia mkoa wa Mara bila hata kupata wazo la kutembelea gofu la hospitali hii na kuliacha kama lilivyo.

Jengo la "Wing C" linatarajia kukamilika hivi karibuni na litakuwa likihudumia mama na mtoto.

Hivyo, hatua ya Rais John Magufuli kuidhinisha fedha za kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo kiasi cha shilingi bilioni 15 ni ya kizalendo na inahitaji kupongezwa na kuungwa mkono.

Huduma ya Afya katika nchi yoyote ile hutegemea sana miundombinu ya hospitali na vituo bora vya afya.

Serikali imekuwa ikijitahdi kuelekeza fedha za maendeleo katika maeneo haya muhimu ya Afya na Elimu kwani masuala haya mawili ni moja ya mihimii ya ustawi wa taifa kimaendeleo na kiuerevu.

Hata yule mtu aliezaliwa mwaka 75 sasa hivi ana miaka 43!

Je, ni sababu zipi ziliwezesha kutokamilika kwa hospitali hii?

Je, wakuu wote hao wa mikoa waliiona jengo la gofu la hospitali hiyo na walichukua hatua gani?

Je, kutoendelea kwa ujenzi wa hospitali hii kumetokana na sababu za kisiasa?
Maendeleo bora kabisa kwa Mtanzania

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
Marais waliofuata baada ya NYERERE km NYERERE mwenyewe waliangalia zaidi maslahi ya taifa..... huyu wa sasa ni aibu kubwa aliyonayo baada ya kuifanya chato km nchi kamili ili ionekane eti anakujali kwa BABA wa TAIFA kumbe anahalarisha uharamia wake........
Sio tu hospitaliz Nyerere hakujenga airport mara, hakujenga international airport, hakupele mbuga kijijini kwake, hakujenga ofisi za kisasa za tra wala hakuwahi kufanya utafiti wa kufungua tawi la benki kijijini kwake (rejea hotuba ya Kimei crdb walivolazimishwa kufungua tawi chato wkt hapafai).......haya yote kayafanya rais wa wanyonge ********....
 
Kuna mambo ambayo serikali imekuwa ikiyafanya nchi hii yanashangaza sana.

Mchoro wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere yaani Kwangwa ulibuniwa mwaka 1975 na baadae mwaka 1977 ujenzi ulianza.

Baadae mwaka huo wa 77 ujenzi wa hospitali hii iliyoko Musoma, ulisimama na kendelea kidogo kabla ya kusimama rasmi mwaka 1980 na huo ndo ukawa mwisho wa kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Kukamilika kwa ujenzi wa hospitali hiyo kungeifanya kuwa moja ya hospitali kubwa za mkoa za Tanzania ikiwa na majengo makubwa matatu, jengo la wazazi yaani "Wing C" na jengo moja kubwa la "Wing B" lenye vitanda na jingo la "Wing A" ambalo litakuwa ni la matibabu maalum.

Ni miaka miwili ilopita ambapo raisi John Magufuli aliamua kuelekeza fedha kiasi cha shilingi bilioni 15 ili ujenzi wa hospitali hiyo ukamilishwe.

Na hiyo ilikuwa ni baada ya ushawishi wa mkuu wa mkoa Adam Malima na mkuu wake wa wilaya pamoja na ufuatiliaji wa Waziri Mkuui na wazri wa Afya.

Ujenzi huo unatarajia kukamilika rasmi mwezi August mwaka huu na ujenzi bado waendelea chini ya usimamizi wa shirika la nyumba la taifa NHC.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba imewachukua maraisi watano tangu ujenzi wa hospitali hii usimame yaani hayati raisi Nyerere mwenyewe, Ally Hassan Mwinyi, Benjaminui Mkapa, na raisi Kikwete ndipo raisi Magufuli aamue kutenga fedha za ujenzi huo.

Licha ya hivyo, wakuu wa mkoa wapatao 16 ambao wamepita kusimamia mkoa wa Mara bila hata kupata wazo la kutembelea gofu la hospitali hii na kuliacha kama lilivyo.

Jengo la "Wing C" linatarajia kukamilika hivi karibuni na litakuwa likihudumia mama na mtoto.

Hivyo, hatua ya Rais John Magufuli kuidhinisha fedha za kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo kiasi cha shilingi bilioni 15 ni ya kizalendo na inahitaji kupongezwa na kuungwa mkono.

Huduma ya Afya katika nchi yoyote ile hutegemea sana miundombinu ya hospitali na vituo bora vya afya.

Serikali imekuwa ikijitahdi kuelekeza fedha za maendeleo katika maeneo haya muhimu ya Afya na Elimu kwani masuala haya mawili ni moja ya mihimii ya ustawi wa taifa kimaendeleo na kiuerevu.

Hata yule mtu aliezaliwa mwaka 75 sasa hivi ana miaka 43!

Je, ni sababu zipi ziliwezesha kutokamilika kwa hospitali hii?

Je, wakuu wote hao wa mikoa waliiona jengo la gofu la hospitali hiyo na walichukua hatua gani?

Je, kutoendelea kwa ujenzi wa hospitali hii kumetokana na sababu za kisiasa?
Vita ya Kagera ni moja ya sababu zilizopelekea Mwalimu Nyerere kutoendelea na ujenzi wa hiyo Hospitali maana nchi iliyumba sana kiuchumi hadi alipoingia Mzee Ruksa mwaka 1985 kidoogo kukawa na mabadiliko hadi kufikia akina Kikwete lkn nani alikuwa na habari hiyo badala ya kujenga Bandari Bagamoyo...!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtaandika mengi tu, lakini kwa ufupi ni kwamba ufisadi na ubadhirifu ndio ulikwamisha ujenzi wa hospitali hiyo,pesa ilikuwapo ikitokana na makato mbali mbali, badala ya kujenga hospitali wahusika wakajenga matumbo yao.

Mfano mzuri ni jinsi mashirika mengi ya umma yaliyoanzishwa kwa juhudi za serikali ya awamu ya kwanza yalivyotafunwa na wajanja wachache na kusababisha kufilisika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom