Kwanini naupenda mti huu

Kwanini naupenda mti huu

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Kwanini naupenda mti huu.
Bujibuji X Mas Tree.jpg

Kuna historia kubwa sana ya mazingira niliyoishi kwenye udogo wangu .

Miti mingi ilikua ni hii , wenyewe tuliita mi Krismas

Kuchanua kwake kuliashiria holiday-sikukuu imekaribia ,
Na shule inakaribia kufungwa ,
Vilevile Krismas haikua mbali hivyo nguo , viatu vipya vinanukia .

Ni miti maalumu sana ,
Nikiona inachanua nafarijika kukumbuka mambo kemkem yaliyo burudisha maisha yangu zama hizo .

Kiimani .
Mti huu kwangu unafumbo la imani kwa waliokata tamaa.
Mti huu hunyauka kabisa kuanzia Julai , Agost , Septemba na Octoba ....ni mti ambao hukwepa ukali wa jua na ukame kwakuruhusu kupukutisha majani yote .
Huungua kabisa na hutia huruma .

Inapofika wiki ya 3 ya Octoba miti hiyo huchanua maua , na maua huendelea kuufunika mti usio na majani .

Kiimani ,
Mungu husema nasi kupitia mazingira kuwa katikati ya dhiki uskate tamaa .

Katikati ya mateso usikose tumaini ,

Hata unahisi dunia inakuelemea Mungu huleta faraja zake kwa namna aitakayo na apendavyo.

Mti huu kwangu hunifunza uvumilivu , kusamehe na kutojiumiza kwa mambo yaliyo nje ya uwezo wangu.
Heshima kwa Samson Mwasakafyuka Ndwanga
 

Attachments

  • Bujibuji X Mas Tree.jpg
    Bujibuji X Mas Tree.jpg
    109.2 KB · Views: 8
Kwanini naupenda mti huu.
View attachment 2415649
Kuna historia kubwa sana ya mazingira niliyoishi kwenye udogo wangu .

Miti mingi ilikua ni hii , wenyewe tuliita mi Krismas

Kuchanua kwake kuliashiria holiday-sikukuu imekaribia ,
Na shule inakaribia kufungwa ,
Vilevile Krismas haikua mbali hivyo nguo , viatu vipya vinanukia .

Ni miti maalumu sana ,
Nikiona inachanua nafarijika kukumbuka mambo kemkem yaliyo burudisha maisha yangu zama hizo .

Kiimani .
Mti huu kwangu unafumbo la imani kwa waliokata tamaa.
Mti huu hunyauka kabisa kuanzia Julai , Agost , Septemba na Octoba ....ni mti ambao hukwepa ukali wa jua na ukame kwakuruhusu kupukutisha majani yote .
Huungua kabisa na hutia huruma .

Inapofika wiki ya 3 ya Octoba miti hiyo huchanua maua , na maua huendelea kuufunika mti usio na majani .

Kiimani ,
Mungu husema nasi kupitia mazingira kuwa katikati ya dhiki uskate tamaa .

Katikati ya mateso usikose tumaini ,

Hata unahisi dunia inakuelemea Mungu huleta faraja zake kwa namna aitakayo na apendavyo.

Mti huu kwangu hunifunza uvumilivu , kusamehe na kutojiumiza kwa mambo yaliyo nje ya uwezo wangu.
Heshima kwa Samson Mwasakafyuka Ndwanga
Dakika hii unaweza kua umeokoa nafsi nyingi sana kwa uzi wako mwanana! Hapo ulipo agiza ya baridi kabisa ntalipa kwa 'lipa namba'
 
Back
Top Bottom