Kwanini naupenda mti huu

Kwanini naupenda mti huu

A
Kwanini naupenda mti huu.
View attachment 2415649
Kuna historia kubwa sana ya mazingira niliyoishi kwenye udogo wangu .

Miti mingi ilikua ni hii , wenyewe tuliita mi Krismas

Kuchanua kwake kuliashiria holiday-sikukuu imekaribia ,
Na shule inakaribia kufungwa ,
Vilevile Krismas haikua mbali hivyo nguo , viatu vipya vinanukia .

Ni miti maalumu sana ,
Nikiona inachanua nafarijika kukumbuka mambo kemkem yaliyo burudisha maisha yangu zama hizo .

Kiimani .
Mti huu kwangu unafumbo la imani kwa waliokata tamaa.
Mti huu hunyauka kabisa kuanzia Julai , Agost , Septemba na Octoba ....ni mti ambao hukwepa ukali wa jua na ukame kwakuruhusu kupukutisha majani yote .
Huungua kabisa na hutia huruma .

Inapofika wiki ya 3 ya Octoba miti hiyo huchanua maua , na maua huendelea kuufunika mti usio na majani .

Kiimani ,
Mungu husema nasi kupitia mazingira kuwa katikati ya dhiki uskate tamaa .

Katikati ya mateso usikose tumaini ,

Hata unahisi dunia inakuelemea Mungu huleta faraja zake kwa namna aitakayo na apendavyo.

Mti huu kwangu hunifunza uvumilivu , kusamehe na kutojiumiza kwa mambo yaliyo nje ya uwezo wangu.
Heshima kwa Samson Mwasakafyuka Ndwanga
Amina
 

Attachments

  • 1668355320949.png
    1668355320949.png
    505.7 KB · Views: 4
Kwanini naupenda mti huu.
View attachment 2415649
Kuna historia kubwa sana ya mazingira niliyoishi kwenye udogo wangu .

Miti mingi ilikua ni hii , wenyewe tuliita mi Krismas

Kuchanua kwake kuliashiria holiday-sikukuu imekaribia ,
Na shule inakaribia kufungwa ,
Vilevile Krismas haikua mbali hivyo nguo , viatu vipya vinanukia .

Ni miti maalumu sana ,
Nikiona inachanua nafarijika kukumbuka mambo kemkem yaliyo burudisha maisha yangu zama hizo .

Kiimani .
Mti huu kwangu unafumbo la imani kwa waliokata tamaa.
Mti huu hunyauka kabisa kuanzia Julai , Agost , Septemba na Octoba ....ni mti ambao hukwepa ukali wa jua na ukame kwakuruhusu kupukutisha majani yote .
Huungua kabisa na hutia huruma .

Inapofika wiki ya 3 ya Octoba miti hiyo huchanua maua , na maua huendelea kuufunika mti usio na majani .

Kiimani ,
Mungu husema nasi kupitia mazingira kuwa katikati ya dhiki uskate tamaa .

Katikati ya mateso usikose tumaini ,

Hata unahisi dunia inakuelemea Mungu huleta faraja zake kwa namna aitakayo na apendavyo.

Mti huu kwangu hunifunza uvumilivu , kusamehe na kutojiumiza kwa mambo yaliyo nje ya uwezo wangu.
Heshima kwa Samson Mwasakafyuka Ndwanga
huu mti jina lake unaitwaje
 
Back
Top Bottom