Kwanini nchi za Afrika ikiwemo Tanzania bado maskini licha ya kupokea Misaada na Mikopo ya mamilioni ya Fedha kutoka nchi zilizoendelea? - Part I

Kwanini nchi za Afrika ikiwemo Tanzania bado maskini licha ya kupokea Misaada na Mikopo ya mamilioni ya Fedha kutoka nchi zilizoendelea? - Part I

Wanananchi wengi hawana akili
Kama huna akili ni wewe tu.

Soma historia za maendeleo ya ulaya, Afrika na mambo yaliyojitokeza kabla ya ukoloni, wakati wa ukoloni na baada ya ukoloni. Jifunze uhusiano uliopo kati ya watawala wetu na sisi watawaliwa wao.

Mzungu halali, anafikiria namna ya kuinyonya Afrika. Anatumia hela nyingi kutengeneza mifumo ya kiunyonyaji ili tu awe mbele ya Afrika all the time.

Tatizo lilianzia pale teknolojia ya Afrika kupigwa marufuku na kuonekana ya kishenzi. Tukapokea dini zao zikitoa misaada bure ikatulemaza.

Hali hii hadi leo bado ipo. Afrika ikigundua kitu, wazungu hutafuta namna ya kuifanya ionekane haina ubora. Wakiona ina manufaa kwao, mgunduzi watamchukua aende kwao. Akiwa mbishi wanamwua.

Wanataka Afrika liendelee kuwa soko na siyo chanzo cha ugunduzi wa maendeleo kwa namna yoyote.

Kifupi matatizo ya nchi za Afrika ni planned na weupe. Halafu wewe unasema hatuna akili. Kama huna akili ni wewe.
 
Hiyo misaada haifiki chini inapigwa juu kwa juu na watawala kisha wanarudi kuficha mabenk ya ulaya.
 
Pamoja na jibu lako zuri, ambalo kimsingi naliunga mkono, sikubaliani nawe katika mlinganisho huo wa nchi za ulaya na hizi zetu, hasa Tanzania.

Tumepata uhuru takribani miaka sitini sasa. Ndio, tulianzia chini sana, na uwezo wetu ulikuwa mdogo sana, lakini muda huo ni muda mzuri na wa kutosha sana kuleta mabadiliko chanya kuliko haya tuliyofikia sasa hivi kama tungekuwa makini na kufanya mambo yetu kwa ueledi na uhakika zaidi.
Leo hii, hata yale mambo mazuri tuliyokuwa tumekwishayatimiza, ni kama tunarudi nyuma, kwa sababu hatuna tabia ya kuwa na kumbukumbu ya mazuri tuliyokwishafanya na kuyaendeleza ili tusigharimie tena kuyafanya upya. Ni kama serikali yetu haina kumbukumbu, pamoja na kwamba ni chama kilekile kinachounda serikali hizo. Wakati mwingine, serikali hiyo hiyo inarudia tena makosa yale yale yaliyofanyika huko nyuma.
Utapataje maendeleo kwa hali ya namna hiyo!

Pili, sisi haitulazimu tena tukagundue kurudumu upya. Kuna mambo mengi sana tunayotakiwa kugezea tu yalivyofanywa na wengine ili nasi tufaidike nayo. Hata kama ikilazimu kubadili kidogo ili yalingane na hali yetu ilivyo, isingekuwa vigumu na kutuchukua muda mrefu namna hii kuleta mabadiliko ya maisha ya wananchi wetu.

Jambo ninalojua ni moja. Tunakosa kiongozi mwenye dira na usimamizi wa dira hiyo ili kutufikisha kwenye hayo anayoamini nchi yetu inayahitaji.

Chukulia mfano wa kilimo na elimu tu, maeneo mawili ambayo mimi naamini yangeweza kutubadilisha haraka sana kama nchi kama yangewekewa mkazo unaostahiri. Sisemi kamwe hapa kwamba mengine yote yataachwa, lakini haya mawili yawe na kipa umbele cha ziada katika uongozi wa kiongozi shupavu na imara ndani ya miaka kumi.
Kilimo ambacho wananchi wetu wengi ndiko wanakopatia ridhiki yao, wakapata mbegu bora, vitendea kazi na ushauri mahususi juu ya kazi zao; na serikali ikafanya kila iwezalo kuwasaidia kutafuta soko la mazao yao..., hali itakuwaje ndani ya miaka kumi?

Elimu yetu inaonekana kama tunarudi kinyumenyume. Tunakuwa na wasomi wengi, lakini thamani ya wasomi hawa inakuwa haijionyeshi katika jamii. Ni hawa hawa wahitimu wetu ndio tunaowategemea wasaidie kuleta mabadiliko ndani ya jamii zetu. Lakini sasa angalia tunavyokwenda, hata mashirika ya Vodacom na Tigo hawawezi kabisa kupata watu ndani ya nchi hii wa kuendesha vikampuni hivi, baada ya miaka sitini ya kufundisha watu wetu wenyewe?

Mkuu Bepari2020, nakumbuka mara ya mwisho tulikutana kule kwa Kagame na Rwanda yake. Pamoja na kwamba hatukuweza kukubaliana katika yale mambo huko, leo hii nitakubali katika hili moja la yeye kuwa na dira, basi.

Umetolea mfano wa nchi za Ulaya, sijui utasemaje kuhusu nchi kama Malaysia, Vietnam na nyingine ambazo nazo zimeibuka kutoka kwenye umaskini miaka kadhaa baada ya kuwa huru.
Sawa mkuu. Lakini unadhani viongozi wetu wanapenda kushindwa?

Rais anaingia madarakani akiwa na mipango mizuri sana ya maendeleo. Analojaribu kuitekeleza, anakumbana na vikwazo hadi vya kifo. Mwoga huishia kufuata maagizo ya watishiaji na jasiri kama Gaddaf na Magufuli huishia hapo walipoishia.

Dunia ina siri nyingi, wahusika hawasemi. Ni mropokaji Magufuli tu alijaribu kusema ya ndani na mwisho wake tumeuona.

Mama anapepea na kilemba si kwa kupenda. Anafuata maagizo ya ndani na nje ili aishi.
 
Njia pekee ya kuisaidia afrika sio kuwapa pesa bali wao ndo waje wafanye hitaji watukabidhi na sio kuwapa pesa watawala zinaliwa juu kwa juu
Waje wajenge vyuo,shule,vituo vya afya,visima, barabara na wakabidhi kama afanyavyo Japan.
 
Kama huna akili ni wewe tu.

Soma historia za maendeleo ya ulaya, Afrika na mambo yaliyojitokeza kabla ya ukoloni, wakati wa ukoloni na baada ya ukoloni. Jifunze uhusiano uliopo kati ya watawala wetu na sisi watawaliwa wao.

Mzungu halali, anafikiria namna ya kuinyonya Afrika. Anatumia hela nyingi kutengeneza mifumo ya kiunyonyaji ili tu awe mbele ya Afrika all the time.

Tatizo lilianzia pale teknolojia ya Afrika kupigwa marufuku na kuonekana ya kishenzi. Tukapokea dini zao zikitoa misaada bure ikatulemaza.

Hali hii hadi leo bado ipo. Afrika ikigundua kitu, wazungu hutafuta namna ya kuifanya ionekane haina ubora. Wakiona ina manufaa kwao, mgunduzi watamchukua aende kwao. Akiwa mbishi wanamwua.

Wanataka Afrika liendelee kuwa soko na siyo chanzo cha ugunduzi wa maendeleo kwa namna yoyote.

Kifupi matatizo ya nchi za Afrika ni planned na weupe. Halafu wewe unasema hatuna akili. Kama huna akili ni wewe.
Mfano halisi wa Tanzania aside na akili ni were, Africa ndio pekee iliyotawaliwa? Nchi za Korea, Vietnam, Singapore,India n.k hazikutawaliwa na kupewa misaada baadae na wakoloni?

Watu wenye akili watakubali vipi na teknolojia Yao ipigwe marufuku?
Kwenye global trade Sub Sahara Africa hai account hata 0.5% ya manunuzi ya bidhaa, sasa nani awategemee kwa soko masikini wakubwa kama hawa?
Soma kwanza historia ya Dunia, na uchumi wa Dunia sio kuamini propaganda za akina Polepole
 
Misaada haisaidii
Imagine unapewa msaada then unapangiwa ukanunue chanjo ya corona
Uongo utakuuwa dogo, chanjo tumepewa bure kama ambavyo tunapewa bure kondomu, vyandarua, kujengewe vyoo kwa msaada wa Marekani etc etc by the way unajua maana ya Aids, Grants & loans??
 
Misaada inakuja na masharti mfano
Nunua chanjo ya corona
Masuala ya jinsia
Usijenge kiwanda nunua dawa toka kwao
Pia mikopo inakuja na masharti pia
Na asilimia kubwa ya mikopo inaishia nje ya malengo.kwenye matumbo ya wanasiasa
 
Mkuu 'FM WOLLE', kukusaidia kupata jibu sahihi kwa swali lako, nami ningependa nikuulize wewe na wasomaji wako wengine swali, ambalo kama mnaweza kulijibu kwa usahihi, basi swali lako nalo litakuwa limepata jibu:

Kuna nchi ngapi duniani ambazo zilishapata maendeleo kutokana na misaada?

Usikimbilie kujibu hili swali bila ya tafakuri makini juu yake, kama kweli nia yako ya kutaka jibu ya swali lako ni halali.
Ni ngumu mno kuendelea kwa kutumia misaada yenye masharti uzitumiaje bila kusahau riba.
Wazungu wakiona kiongozi hataki misaada wanamtafutia zengwe mf. Gadafi,JPM nk.
Hata waswahili husema mtegemea Cha nduguye hufa maskini.
 
socialism imeharibu sana watu akili, si chama chenu ndo kinakoleza moto wa misaada, magufuli alivoamua tuanze kujitegemea mkamuona diktetea kwa kifupi nyie mnatakiwa wote mumfuate mbowe ukonga ni janga kwa hii dunia
Kwani wewe umemfuata kaburini kwake au kuzikwa naye?
 
Chanjo sio bure go and check your source
Uongo utakuuwa dogo, chanjo tumepewa bure kama ambavyo tunapewa bure kondomu, vyandarua, kujengewe vyoo kwa msaada wa Marekani etc etc by the way unajua maana ya Aids, Grants & loans??
 
Kuna koo Zimeendele kama za akina Dewji, Mengi, Bakhersa nk

Unadhani kwa nini ukoo wako ni choka Mbaya kimaisha? Ni uongozi mbaya ndani ya ukoo wenu, ubinafsi, uvivu na ufisadi wa viongozi wako wa ukoo?
Nazungumzia maendeleo ya jumla sizungumzii kuchomoka kwa mtu mmoja mmoja.
Kwann nchi za afrika ya weupe wao angalau wameendelea kwa ujumla kuliko afrika ya weusi.
Kama wakoloni kwa mda mfupi wao waliweza tuletea maendeleo makubwa Sana nyie ccm mmeshindwa vipi.Soon tunaingia jubilee miaka100 tukiendelea kusaidia kujengewa vyoo vya shule.
 
Ni ngumu mno kuendelea kwa kutumia misaada yenye masharti uzitumiaje bila kusahau riba.
Wazungu wakiona kiongozi hataki misaada wanamtafutia zengwe mf. Gadafi,JPM nk.
Hata waswahili husema mtegemea Cha nduguye hufa maskini.
Hayo ni mawazo ya kikomunist,mbona ulaya, Asia, latin america mbona wao wameendelea kwa misaada hio hio wanayopewa afrika.
 
Wenzetu waliwekeza kwenye uchumi wa familia Kwanza kwa kulazimisha Kila familia kuwa na idadi ya watoto wachache watakaoweza kujiimarisha kiuchumi mfano China, Nchi za Ulaya idadi ya watoto haizidi wanne hivyo uchumi wa familia umezingatiwa Kwanza Ili kuiacha serikali ipambane na uchumi wa Nchi na ustawi wa mazingira mazuri ya Kila huduma za jamii.
Sio kweli idadi ya watoto iwe kikwazo cha kutoendelea
 
Mkuu 'FM WOLLE', kukusaidia kupata jibu sahihi kwa swali lako, nami ningependa nikuulize wewe na wasomaji wako wengine swali, ambalo kama mnaweza kulijibu kwa usahihi, basi swali lako nalo litakuwa limepata jibu:

Kuna nchi ngapi duniani ambazo zilishapata maendeleo kutokana na misaada?

Usikimbilie kujibu hili swali bila ya tafakuri makini juu yake, kama kweli nia yako ya kutaka jibu ya swali lako ni halali.
Misaada sio kwa ajili ya afrika pekee hata nchi za ulaya zinapewa misaada.Misaada sio tatizo tatizo inaishia wapi?
 
Back
Top Bottom