Kwanini nchi za Afrika ikiwemo Tanzania bado maskini licha ya kupokea Misaada na Mikopo ya mamilioni ya Fedha kutoka nchi zilizoendelea? - Part I

Kwanini nchi za Afrika ikiwemo Tanzania bado maskini licha ya kupokea Misaada na Mikopo ya mamilioni ya Fedha kutoka nchi zilizoendelea? - Part I

Mmewapitisha kina BABTUTALE bila kupingwa mnategemea nini!?
 
Vietnam iko Afrika?
Ungetafakari japo kidogo basi. Ninazungumzia weupe na weusi. Ndiyo vita ilipo.

Kwa taarifa yako misaada waliyopewa Vietnam ni tofauti sana na ya Afrika kuanzia riba hadi masharti.
Kwa mfano, Tz inapewa msaada wa dola 5m. Masaharti ni pamoja na utaajiri baadhi ya wataalam kutoka kwa mtoa msaada, utanunua vifaa vyote kutoka kwake na si nchi nyingine. Sehemu ya fedha inaletwa kwa maelezo ishachotwa kulipa hao watumishi wa nje na mitambo toka kwao. Lakini riba ndo usiseme.

Mwisho wa siku utalipa riba hata hela aliyobaki nayo kulipa wataalam na mitambo, wakati hela hiyo haikugusa Tz ikaongeza mzunguko na hiyo mitambo huisha unapoisha mradi. Unabaki na nini zaidi ya deni? Wakati huohuo mradi si wa kuzalisha fedha bali ni wa matumizi tu.
We jamaa mweupe sana, unasikia hearsay za mtaani unazileta JF, kwa taarifa yako tu, nchi nyingi za nje ya Africa zimepitia dhoruba na madhila makubwa kuliko nchi yako hii ya Tz na ila zimenyanyuka na ni developed Kea kufanya kazi na elimu , Waafrica kinachowaangusha ni uvivu na kutokufikiri
 
Mkuu, usifikiri hilo la "Development Assistance" ni jipya na kwamba hata sisi wengine hatulijui. Tunalijua sana, ila hatukubaliani na wewe juu ya misaada hiyo kuleta maendeleo ndani ya nchi hizo unazotutolea kama mfano.
Basi katika mfano niliyotoa, ni Ujerumani baada ya uharibifu wa vita kuu ya pili. Kama unaijua, hongera! Hapo upigamizi ni kuhusu nini? Lete hoja!
 
Sekta ya kilimo tuliyoitilia mkazo tangu tumepata uhuru ilidorora kwa sababu nyingi tuu ambazo ziko nje ya uwezo wa serikali. Kwa mfano bei za mkonge ziliporomoka kwenye soko la dunia walipogundua katani feki. Kahawa tulikuwa ni moja ya wazalishaji wakubwa siku hizi mpaka China inalima kahawa tena inazalisha kahawa kuliko sisi. Pamba nayo ni vile vile. Korosho kidogo ina afadhali sasa. Labda serikali iwekeze sana kwenye kilimo cha korosho tuone tutafikia wapi.

Kwenye swala la elimu nakubaliana na wewe ila hata kama tungeboresha elimu, ajira ziko wapi? Vijana wetu hata wakienda kusoma nje ya nchi wakirudi wataajiriwa na nani? Wengi wanabakia kuhangaika na maisha bila kujua maisha yao yakoje huko mbele. Wanabakia kufanya kazi ambazo wangeweza kuzifanya bila ya familia zako kutumia au kukopa hela nyingi za kuwasomesha. Na hata serikali ingesema makampuni ya nje yote yanayowekeza hapa lazima yajiiri Watanzania tuu, bado kutakuwa na tatizo la ajira.

Halafu nchi za Afrika kuzilinganisha na nchi za Malaysia na Vietnam siyo sawa. Kihistoria hizo nchi hazikuongozwa kikabila kama nchi zetu. Sisi mfano wetu ni nchi kama Afghanistan au nchi kama Iraq. Kihistoria watu wa hizo nchi walikuwa wanaongozwa kikabila mpaka pale zilipotawaliwa na wakoloni. Kwa Afghanistan, Marekani imetumia zaidi ya dola trilioni moja, wamekaa miaka 20 na bado wameshindwa kuleta maendeleo kwenye nchi ya watu milioni 38 tuu. Maendeleo yameishia Kabul, sehemu zingine bado masikini.
Hakuna hata moja katika aya hizo tatu ulizoandika hapo.

Kilimo wewe unaangalia kuporomoka kwa katani, pamba wakati huo ndiyo kiwe kigezo cha kupuuzia kilimo? Si ndiyo hayo hayo niliyoandika humo kuhusu mipango isiyokuwa endelevu? Leo unagusa hiki, kukitokea tatizo kidogo unabwaga unakimbilia kingine, na chenyewe kikitetereka kidogo unakimbia? Nchi itaendelea vipi kwa mtindo huo wa utendaji.

Hata kama Mkonge na pamba na kahawa na chai, mazao yote hayo yalipata matatizo, lakini siyo kwamba yalikuwa hayauziki kabisa sokoni.
Maana ya kuwa na kilimo endelevu ni kwamba wakulima wa zao lolote lile wanapata uzalishaji wa hali ya juu na kuweza angalau kurudisha kiasi cha mtaji waliowekeza na faida kidogo ili waweze kuendelea na uzalishaji katika msimu ufatao, ambao pengine bei itakuwa nzuri zaidi.

Maana ya elimu sio ya kuapatia ajira pekee, na maana ya elimu siyo wingi wa wanaoipata (ingawa ni muhimu), lakini pia ubora wa elimu hiyo.
Elimu yetu tumeweka mkazo kwenye wingi wa wanaoipata na kusahau ubora wa elimu inayotolewa.

Kwa nini usilinganishe maendeleo ya nchi kama Malaysia, Thailand, Vietnam na nyinginezo na hizi zetu, kwa sababu tu ya mfumo wa kiutawala uliokuwepo kabla ya uhuru?
SAWA, hata kama isingekuwa maendeleo ya mlinganisho wa moja kwa moja na nchi hizo, miaka 60 ya kujipanga kiutawala bado inakuwa kama ndio tunaanza moja katika maendeleo? Na kwingineko hadi kurudi nyuma karibu na hali ya kabla ya uhuru?
Nchi ya Haiti imekuwepo karibia miaka 200 hivi ikiwa inajitawala. Usione ajabu kabisa miaka 200 tokea sasa ukibahatika kurudi Afrika, unaweza ukakutana na nchi kama ilivyo Haiti ya leo!
 
Basi katika mfano niliyotoa, ni Ujerumani baada ya uharibifu wa vita kuu ya pili. Kama unaijua, hongera! Hapo upigamizi ni kuhusu nini? Lete hoja!
Ujerumani ni nchi iliyokuwa imeendelea hata kuizidi Marekani kabla ya vita. Hali ilikuwa ni hivyohivyo kwa Japan.
Hii ina maana, uharibifu ulioletwa na vita na kuharibu miundombinu na sekta mbalimbali za uchumi, ilikuwa ni kazi tu ya kuirejesha na kuweka mingine.
Hiyo misaada ya "Marshall" unayoizungumzia, ilikuwa ni nyenzo tu ya kurudishia sehemu zilizoharibika na kuanzisha viwanda vilivyoharibiwa.Hawa watu tayari walikuwa wameendelea, siyo misaada iliyowaletea maendeleo.

Na sisi kama tuna dhamira ya kweli ya kupata maendeleo, ni lazima tujizatiti kuleta maendeleo hayo. Hii misaada kamwe haitaweza hata siku moja kutuletea maendeleo. Itatusaidia tu kama nyenzo ya kuyapata maendeleo hayo kwa bdii zetu wenyewe.

Juzi tumepata msaada (pesa ya bure) toka Ujerumani,; sijui bilioni ngapi zile. Na hii haikuwa mara ya kwanza benki hiyo kutoa msaada kama huo kwetu. Yalitolewa maelezo mareeeefu kuhusu malengo ya msaada huo, utakapotumika kiasi kwamba unasoma hadi unakaribia kupata usingizi!

Hawa watu wanajua fika, wananchi wetu wengi ni wakulima, tena wa kilimo hiki cha vieka vitano. Kila mwaka wanalia gharama za kununulia mbolea, mbegu bora hawapati, na mahitaji mengine ya kuwawezesha hivi viekari vyao vitano angalau vizalishe mazao ya kutosha. Hawa watoa misaada wanaijua vizuri sana hali hii duni inayowakabili wakulima wetu. Uliwahi kusikia hata mwaka mmoja akatokea mtoa msaada unawalenga wakulima hawa, wapate mbolea na mahitaji mengine ili kilimo chao kiwe cha tija?
 
Kwasababu bado zinapokea misaada wakati zina rasilimali za kutosha ila zinatumiwa ndivyo sivyo
 
Ujerumani ni nchi iliyokuwa imeendelea hata kuizidi Marekani kabla ya vita. Hali ilikuwa ni hivyohivyo kwa Japan.
Hii ina maana, uharibifu ulioletwa na vita na kuharibu miundombinu na sekta mbalimbali za uchumi, ilikuwa ni kazi tu ya kuirejesha na kuweka mingine.
Hiyo misaada ya "Marshall" unayoizungumzia, ilikuwa ni nyenzo tu ya kurudishia sehemu zilizoharibika na kuanzisha viwanda vilivyoharibiwa.Hawa watu tayari walikuwa wameendelea, siyo misaada iliyowaletea maendeleo.

Na sisi kama tuna dhamira ya kweli ya kupata maendeleo, ni lazima tujizatiti kuleta maendeleo hayo. Hii misaada kamwe haitaweza hata siku moja kutuletea maendeleo. Itatusaidia tu kama nyenzo ya kuyapata maendeleo hayo kwa bdii zetu wenyewe.

Juzi tumepata msaada (pesa ya bure) toka Ujerumani,; sijui bilioni ngapi zile. Na hii haikuwa mara ya kwanza benki hiyo kutoa msaada kama huo kwetu. Yalitolewa maelezo mareeeefu kuhusu malengo ya msaada huo, utakapotumika kiasi kwamba unasoma hadi unakaribia kupata usingizi!

Hawa watu wanajua fika, wananchi wetu wengi ni wakulima, tena wa kilimo hiki cha vieka vitano. Kila mwaka wanalia gharama za kununulia mbolea, mbegu bora hawapati, na mahitaji mengine ya kuwawezesha hivi viekari vyao vitano angalau vizalishe mazao ya kutosha. Hawa watoa misaada wanaijua vizuri sana hali hii duni inayowakabili wakulima wetu. Uliwahi kusikia hata mwaka mmoja akatokea mtoa msaada unawalenga wakulima hawa, wapate mbolea na mahitaji mengine ili kilimo chao kiwe cha tija?
Asante kwa jinbu lako, angalau mara moja moja kupata majadiliano ya maana!
Ndiyo nimesikia mara nyingi kuna miradi ya kulenga wakulima hasa.
Naona kuna sentensi moja muhimu kwako "Hawa watu tayari walikuwa wameendelea", yaani nakubali watu (the human factor) ni msingi wa maendeleo.
Ukiacha mfano wa nchi zilizoharibika baada ya vita kuu, tunaweza kuangalia pia tofauti ya maendeleo baina Asia na Afrika.
Maana mnamo 1950 mara nyingi uwezo wa kiuchumi (kwa vipimo vilivyopatikana) ulikuwa juu zaidi Afrika.
Maana Asia mara nyingi umaskininulikuwa mkali zaidi.
Leo ni tofauti. Machoni pako kwa nini?
 
Asante kwa jinbu lako, angalau mara moja moja kupata majadiliano ya maana!
Ndiyo nimesikia mara nyingi kuna miradi ya kulenga wakulima hasa.
Naona kuna sentensi moja muhimu kwako "Hawa watu tayari walikuwa wameendelea", yaani nakubali watu (the human factor) ni msingi wa maendeleo.
Ukiacha mfano wa nchi zilizoharibika baada ya vita kuu, tunaweza kuangalia pia tofauti ya maendeleo baina Asia na Afrika.
Maana mnamo 1950 mara nyingi uwezo wa kiuchumi (kwa vipimo vilivyopatikana) ulikuwa juu zaidi Afrika.
Maana Asia mara nyingi umaskininulikuwa mkali zaidi.
Leo ni tofauti. Machoni pako kwa nini?
Ni muhimu niseme yafuatayo nisije nikaeleweka vibaya:

Afrika kuna maendeleo yanafanyika hata kama yanaonekana kuwa ni ya polepole sana. Mabadiliko kati ya sasa na wakati nchi nyingi zinapata uhuru mtu huwezi kutoyaona na kuyatambua.

Kwa hiyo tusibeze sana mafanikio yaliyopatikana hadi sasa hata kama hayafikii kiwango tulichokitarajia.

Ni lazima pia niseme kwamba maendeleo ni mchakato (process), siyo kitu kinachomwagika kwa mara moja na nchi ikaonekana imeendelea ndani ya muda mfupi sana, hilo haliwezekani.

Kwa hiyo maendeleo yapo, hata kama tutapishana baina ya nchi na nchi. Kuna baadhi ya nchi zimepiga hatua haraka kuliko nchi nyingine kuelekea kwenye kuinua hali ya maisha ya wananchi wake..., kwa sababu mbalimbali (ambazo sitazitaja hapa).

Hata huko Asia, kuna nchi kama Malaysia, wameinuka haraka kuliko nchi nyingine, kama Burma (Mynmar), kwa mfano, kwa sababu mbalimbali pia.

Kwa hiyo niseme tu kwamba Tanzania tumo kwenye mchakato wa maendeleo, tunaendelea hatua kwa hatua, hata kama wakati mwingine hatua zetu za kwenda mbele zinakuwa hafifu zaidi kuliko nyakati zingine (kwa sababu mbalimbali pia).

Mwishowe tutafika kwenye 'critical point' (threshold), ambapo maendeleo yataanza kuonekana bayana na kutokea kwa haraka kuliko ilivyo sasa (Kama tusipotumbukia kwenye janga la kisiasa inakotupeleka CCM wakati huu).

Wakati huo unakuja, na hauko mbali sana kama tutajibidisha kuuhifadhi na kuutumia vizuri. Pato la mtu mmoja mmoja litaongezeka haraka, na uwezo wa kujifanyia mambo yetu wenyewe bila ya kutegemea misaada utaongezeka pia.

Sasa sijui kama nimejibu hoja yako uliyotaka niisemee hapo juu, au utaona kama nimeikwepa maksudi!
 
Niliuliza hili swali kupata maoni, sio hapa tu ni kwenye majukwaa mbalimbali, Asante kwa wote waliotoa maoni yao.

Lakini kwa ufupi misaada na Mikopo kihistoria vilianza miaka ya 1945 na ilikuwa baada ya vita kuu ya pili ya dunia kwa malengo mawili;

i) Kujenga miundombinu iliyoharibiwa wakati wa vita na jukumu hili ilipewa Benki ya Dunia.

(ii) Na lengo la pili lilikuwa ni kuharakisha maendeleo ikiwemo biashara na kudhibiti masuala yote yahusuyo Fedha Duniani, jukumu hili likawa ni la Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Shirika la Biashara Duniani.

Lakini kwa pamoja mashirika haya waliyaweka pia kwaajili ya kudhibiti ama kuzuia kutokea tena kwa mdororo wa uchumi (Great Economic Depression) uliowahi kutokea miaka ya 1930's (Hawa watu wana akili [emoji4], kumbuka Kati ya wadau 700 waliokuwa wanajadili haya, hakuna mdau hata mmoja aliyetoka Afrika kwa ujumla).

Mwaka 1946 na 1947 nchi za Ulaya zilichukua mikopo na misaada kutoka kwenye mashirika haya. Nchi kama Ufaransa, Denmark, Netherlands na Luxembourg waliweza kufanikisha kuunda upya nchi zao na kufuta uharibifu wote uliosababishwa na vita, pamoja na kujenga uchumi wao. Kwa kiasi kikubwa taasisi hizi za Kimataifa zilimudu kudhibiti na kuchochea Uchumi wa Dunia.

Sasa ni nini kilizikuta nchi za Afrika ikiwemo Tanzania ambapo nchi hizi zinaonekana kuwa na ugonjwa sugu wa Umaskini usiosikia dawa licha ya kupewa mikopo na misaada ya matrilioni ya Fedha? Tutaona Part (ii)

View attachment 1929403
Lile gari alilojisifia Polepole Vile ni la aina gani?
 
Hivi kwani bado tunapokea misaada kutoka kwa mabeberu?
Si tulishakuwaga uchumi wa kati na matajiri a.k a dona kantriii.
 
Misaada ina dumaza akili na ubunifu maana wanakupa msaada uku wameishakupa masharti na maelekezo ya vipi uutumie(hawataki wakupe msaada alafu wakuache utumie akili na ubunifu wako ni jinsi gani utumie huo msaada ili ujikomboe)
Wizi, rushwa na ubinafsi: hii nayo inachangia tusiendelee pamaoja na kupatiwa hio misaada maana mingi haifikii walengwa kama ilivyo pangwa. Pia waafrika wengi hatuna ushirikiano mzuri kati ya nchi na nchi, viongozi kwa viongozi na hii inawafanya wajanja watutumie kama fursa kupitia misaada yao.
Kukosekana ubunifu, akili na usimamizi wa rasilimali tulizonazo. Kama vya ndani tulivyopewa bure na Mungu tunashindwa kuvisimamia hivi vinavyotoka nje tutaweza kweli!?
 
Misaada ina dumaza akili na ubunifu maana wanakupa msaada uku wameishakupa masharti na maelekezo ya vipi uutumie(hawataki wakupe msaada alafu wakuache utumie akili na ubunifu wako ni jinsi gani utumie huo msaada ili ujikomboe)
Wizi, rushwa na ubinafsi: hii nayo inachangia tusiendelee pamaoja na kupatiwa hio misaada maana mingi haifikii walengwa kama ilivyo pangwa. Pia waafrika wengi hatuna ushirikiano mzuri kati ya nchi na nchi, viongozi kwa viongozi na hii inawafanya wajanja watutumie kama fursa kupitia misaada yao.
Kukosekana ubunifu, akili na usimamizi wa rasilimali tulizonazo. Kama vya ndani tulivyopewa bure na Mungu tunashindwa kuvisimamia hivi vinavyotoka nje tutaweza kweli!?
Umenena vyema mkuu
 
Tungekuwa ni watu makini (tuliomo JF) huu ungekuwa ni mjadala mahsusi, tena wenye ushahidi wa tarakimu kuonyesha matumizi makubwa kwa watumishi hawa.

Tungedadavua na faida za kuwa nao watu hao wote sehemu hizo walipo kuonyesha umuhimu wao.

Lakini muda wa kufanya hivyo hatuna, na badala yake tunapapasa tu na kwenda zetu.
Watawaka hata mjadala wa kitaifa wanauogopa
 
Tatizo kubwa la Africa ni uongozi mbaya, uongozi usio ja uwezo wa kuongozila, uongozi usio ja upei wala maono.

Mahali popote ukiona kuna failure, utambue kuwa ni failure ya uongozi. Watanzania hawa hawa wakipelekwa nchi yenye uongozi mzuri, hakuna atakayekuwa maskini.

Bahati mbaya kabisa, katika mataifa mengi ya Afrika, wale wenye akili kidogo, upeo mdogo, wasio na ustaarabu, ndiyo walioshika uongozi. Mfano mzuri ni wa hapa Tanzania. Utafiti ule wa TWAWEZA ulionesha kuwa ndani ya CCM ndiko walikojaa wajinga, na ndani ya upinzani ndiko walikojaa waelewa, LAKINI CCM ambayo imejaa wajinga, ndiyo inayoongoza nchi. Yaani wajinga wanawaongoza werevu.

Misaada na mikopo ni nyenzo muhimu sana katika kujenga uchumi na kupata maendeleo. Misaada na mikopo ni mbegu. Lakini kwa nchi nyingi za Afrika, misaada na mikopo inaliwa badala ya kupanda ili izalishe.

Ni misaada, mikopo na uwekezaji wa nje, ndivyo vilivyoiendeleza sana Ujerumani, South Korea, Botswana, Namibia, Afrika Kusini na China.

China chini ya Mao ilikuwa hoi bin taabani. Miaka ya karibuni, China ikafungua uchumi wake kwa Dunia, makampuni za Ulaya na America yakawekeza heavily China, uchumi wa China kwa karibu miaka 10 mfululizo ukawa unakua kwa 12%. Mpaka leo China ndiyo inayoongoza kwa kuvutia miraji ya kutoka Ulaya na America, Duniani. Sisi hapa kwetu, kwa ujinga wa wachache waliopo madarakani wanaamini kuwa uwekezaji wa nje siyo muhimu.

Rais Samia siyo super intelligent lakini atafanya vizuri kwa zaidi ya mara 100 ya Magufuli kwa kutambua tu kuwa tunahitaji sana uwekezaji wa nje, na hasa Ulaya na America (siyo China) ili kuhuisha uchumi wetu.

Baadhi ya nchi chache za Afrika, kama Botswana, zilizobahatika kuwa na viongozi wenye akili na upeo, zinasonga mbele kwa kasi kubwa katika maendeleo.
 
Bora hata Magu alivyokufa kwasababu
1. Alikuwa anazidi kukopa pesa hasa kwa wachina. Mchina ana roho mbaya sana. Amechukua bandari ya Sri Lanka miaka 100 baada ya kushindwa kulipa mkopo
2. Alifuta ajira Kuna sekta km Ualimu na madaktari walikuwa wanaajiriwa kila mwaka baada ya kuingia yeye tu, ajira akafuta
3. Alikuwa anatengeneza kundi la viongozi wasiofuata sheria na mgawanyo wa majukumu. Kina makonda, Sambaya n.k kiongozi anatoka ofisini anaenda kuchapa wanafunzi. Km anapenda kuchapa wanafunzi apangiwe shule ya kufundisha
4. Kuwepo kwa watu wasiojulikana. Ukikosoa serikali au ukazinguana na kiongozi wanakupiga risasi au wanakuteka. Watu wengi sana wamepotea.
5. Kubambikiwa kesi, mfano hai Rugamalira.
6. Hakuna posho, upandishwaji wa vyeo na hakuna nyongeza za mshahara kwa wafanyakazi wa umma
Kuna vifo ambavyo huwa ni furaha kwa wengine. Magufuli alitimiza hilo
socialism imeharibu sana watu akili, si chama chenu ndo kinakoleza moto wa misaada, magufuli alivoamua tuanze kujitegemea mkamuona diktetea kwa kifupi nyie mnatakiwa wote mumfuate mbowe ukonga ni janga kwa hii dunia
 
Bora hata Magu alivyokufa kwasababu
1. Alikuwa anazidi kukopa pesa hasa kwa wachina. Mchina ana roho mbaya sana. Amechukua bandari ya Sri Lanka miaka 100 baada ya kushindwa kulipa mkopo
2. Alifuta ajira Kuna sekta km Ualimu na madaktari walikuwa wanaajiriwa kila mwaka baada ya kuingia yeye tu, ajira akafuta
3. Alikuwa anatengeneza kundi la viongozi wasiofuata sheria na mgawanyo wa majukumu. Kina makonda, Sambaya n.k kiongozi anatoka ofisini anaenda kuchapa wanafunzi. Km anapenda kuchapa wanafunzi apangiwe shule ya kufundisha
4. Kuwepo kwa watu wasiojulikana. Ukikosoa serikali au ukazinguana na kiongozi wanakupiga risasi au wanakuteka. Watu wengi sana wamepotea.
5. Kubambikiwa kesi, mfano hai Rugamalira.
6. Hakuna posho, upandishwaji wa vyeo na hakuna nyongeza za mshahara kwa wafanyakazi wa umma
Kuna vifo ambavyo huwa ni furaha kwa wengine. Magufuli alitimiza hilo

1) National dept ya marekani mpaka tunapoongea saahv ni kiasi gan? uyo anaekupa ushauri usikope kwa mchina hajakopa kwake?
2) Mpaka magufuli anapoteza uhai hakuna kipindi watu hawajaajiriwa, kama ulitimuliwa hilo ni lako!
3) Nitajie sehem moja magufuli hakufuata sheria (ambayo ilikua na ulazima wa kufuatwa): na toka izo sheria zmewekwa mpaka leo zilipotufikisha nadhan hapahitaji maelezo zaidi
4) hata saaahv bado wapo, "Kosoa serikali kwa staha na utoe ushauri unaoeleweka"
5) Hilo alilifanya na ilikua kosa kubwa
6) sasa kupandishwa cheo ni kanuni?

Time isnt fixed, time is an illusion, somewhere in time your already dead, lets say someone living in year 2100 right now anajua umeshakufa na kufukiwa muda mrefu sana.

Kinachokupa kiburi ni muda unaoishi saaahv, you feel like you have a long time to live but somewhere ahead your already dead, and so what differentiates you and death is only TIME:

- someone living in 2019 right now anamuona magu akiwa hai and likewise to everyone else
 
Mbona povu sana?
1. Ktk raisi aliyekopa sana ni Magu
2. Ajira rasmi na fursa za kiuchumi (biashara) ndizo zinazofanya nchi ipate kodi na nchi kuwa na uchumi. Madini, mbuga za wanyama hiyo acha pembeni.
Ukishindwa kuajiri na kutengeneza fursa matokeo yake
1. utataka mpk mama anayeuza vitumbua alipie kodi
2. Tozo zimekuwa nyingi, unanunua umeme ulipe na pango ya mwenye nyumba.
3. Watu wasiokuwa na ajira wamekuwa wengi sana. Sasa hivi phd, degree hazina thamani tena.
Ktk maraisi ambao hawakupaswa kuongoza nchi ni Magu, alilijua hilo ndiyo maana aliondoka mapema.
Raisi anatakiwa atumie akili nyingi + katiba + sheria kuliko nguvu.
Najua sote tutakufa ila vifo vingine ni faida. Anakufa mtu unaenda kujipongeza kwanza.

1) National dept ya marekani mpaka tunapoongea saahv ni kiasi gan? uyo anaekupa ushauri usikope kwa mchina hajakopa kwake?
2) Mpaka magufuli anapoteza uhai hakuna kipindi watu hawajaajiriwa, kama ulitimuliwa hilo ni lako!
3) Nitajie sehem moja magufuli hakufuata sheria (ambayo ilikua na ulazima wa kufuatwa): na toka izo sheria zmewekwa mpaka leo zilipotufikisha nadhan hapahitaji maelezo zaidi
4) hata saaahv bado wapo, "Kosoa serikali kwa staha na utoe ushauri unaoeleweka"
5) Hilo alilifanya na ilikua kosa kubwa
6) sasa kupandishwa cheo ni kanuni?

Time isnt fixed, time is an illusion, somewhere in time your already dead, lets say someone living in year 2100 right now anajua umeshakufa na kufukiwa muda mrefu sana.

Kinachokupa kiburi ni muda unaoishi saaahv, you feel like you have a long time to live but somewhere ahead your already dead, and so what differentiates you and death is only TIME:

- someone living in 2019 right now anamuona magu akiwa hai and likewise to everyone else
 
Back
Top Bottom