Kwanini ng'ombe anaficha maziwa wakati wa kukamua?

Kwanini ng'ombe anaficha maziwa wakati wa kukamua?

Gaddaf i06

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2022
Posts
1,770
Reaction score
2,841
Naombeni mwongozo: kwani ng'ombe anaficha maziwa?

ni ng'ombe mwenye maziwa mengi tu lakini ana tabia ya "kubana" ukiwa unakamua. Sijuwi ni kwanini?!

mwenye uelewa kuhusu hili anisaidie jamani
 
Naombeni mwongozo: kwani ng'ombe anaficha maziwa?

ni ng'ombe mwenye maziwa mengi tu lakini ana tabia ya "kubana" ukiwa unakamua. Sijuwi ni kwanini?!

mwenye uelewa kuhusu hili anisaidie jamani
Nadhani utakuwa si mfugaji mbobezi.

Ng'ombe wengine huwa wanamjua yupi mwenye uhalali wa kuwakamua maziwa la sivyo tofauti na hapo hutathubutu hata kuwasogelea watavyokuchangamkia kukupiga mapembe.

Ng'ombe hafichi maziwa isipokuwa inategemea unamzoeza vipi hadi kufikia hatua aelewe kukamuliwa maziwa ni kawaida kwake.
 
Naombeni mwongozo: kwani ng'ombe anaficha maziwa?

ni ng'ombe mwenye maziwa mengi tu lakini ana tabia ya "kubana" ukiwa unakamua. Sijuwi ni kwanini?!

mwenye uelewa kuhusu hili anisaidie jamani
Ng'ombe anajua maziwa ni ya ndama, sasa anaapokuona baba mwenye mandevu yako komavu unajidai ndama, hapo ndipo anapo changanyikiwa
 
Nadhani utakuwa si mfugaji mbobezi.

Ng'ombe wengine huwa wanamjua yupi mwenye uhalali wa kuwakamua maziwa la sivyo tofauti na hapo hutathubutu hata kuwasogelea watavyokuchangamkia kukupiga mapembe.

Ng'ombe hafichi maziwa isipokuwa inategemea unamzoeza vipi hadi kufikia hatua aelewe kukamuliwa maziwa ni kawaida kwake.
mbona akikamuliwa na mtu mwingne,hata awe mgeni hafanyi hvyo?
 
Nilishakukataza utoto huo please! Utakua lini bujibuji?
Maswali ya kitoto yanahitaji majibu ya kitoto. Tukiendekeza watu kutoshirikisha akili zao vyema, matokeo yake tutakuwa na taifa la ajabu kabisa.

Ninapenda ifike wakati, JF pawe ni sehemu ya kuuliza maswali ambayo umeshindwa kuyapata sehemu yoyote ile. Umetafuta Google umekosa, umetafuta mtaani kwako umekosa, sasa ndipo unakuja kuuliza hapa.

Ndugu yangu ninaye kupenda sana Retired, nakuahidi, sitaacha kuwajibu watu wanaouliza maswali ya kijinga ipasavyo.

Naamini umenielewa. Asante.
 
Naombeni mwongozo: kwani ng'ombe anaficha maziwa?

ni ng'ombe mwenye maziwa mengi tu lakini ana tabia ya "kubana" ukiwa unakamua. Sijuwi ni kwanini?!

mwenye uelewa kuhusu hili anisaidie jamani
Mkuu ni kweli kuwa Ng'ombe anaweza kuamua kuficha maziwa hadi pale atakapoona baadhi kama siyo yote, mahitaji yake muhimu amepatiwa

ila kabla ya kumlalamikia anaficha maziwa, inabidi uwe unajua exactly uwezo wake wa kutoa maziwa at maximum ni upi na katika minimum ni upi

Kwanza kabisa sababu namba 1 ambayo inaweza kufanya Ng'ombe akapunguza maziwa ni Maradhi, tukisema Maradhi basi tunamaanisha maradhi yoyote yale, ila angalia zaidi maradhi ya kiwele

Je ana Mimba na kama anayo ina umri gani Hadi muda huu ambao amepunguza utoaji wa maziwa

Baada ya hapo anza kuchunguza kipi kimebadirika hadi atoke kwenye maziwa labda Lita 7 hadi 3

Unaweza kuanza na kucheki mabadiriko ya msosi, kama umebadiri kitu chochote kwenye chakula chake either kwa kuongeza au kupunguza

Angalia milking boost unayotumia hivi sasa ndio ile ile uliyokuwa unatumia kipindi anatoa maziwa mengi au umebadirisha? Angalia mchanganyiko wa chakula chake je umeongeza au kupunguza kipi

Njoo kwenye mkamuaji je anaekamua ndio yule yule au kuna mabadiriko? Ng'ombe pia huzoea mtu anaemkamua ambao hujiskia huru mbele yake, na wakamuaji wengine hawajui kukamua wanamuumiza Ng'ombe

All in all fata taratibu nzuri za ukamuaji, kama kuosha kiwele pamoja na chuchu kwa kutumia maji yamoto, na pia tumia mafuta ya kukamulia na sio unakamulia mafuta ya Kula au mafuta ya kupaka
 
Shukrani sana Anigrain [emoji120][emoji120]

kuna jirani yangu ameniambia kwamba sijuwi kukamua! Je ni utaalamu gani labda unatumika kwenye ukamuaji licha kutumia mafuta ya kukamulia??
 
Back
Top Bottom