Kwanini ni Mbowe na sio Lissu na kwanini CHADEMA haifi?

Sijaweza kusoma bandicoot lako refu. Inawezekana una hoja nzuri tu. Lakini unaonaje kama hizi hoja mngejadiliana ndani ya vikao vyenu vya chama? Sisi tusio wanachama inatusaidiaje? Lakini je ni Lisu na Mbowe tu ndio wenye uwezo kwenye chama chenu? Kwanini msiwaamini wengine? Ningekuwa mimi ndiye mshauri wenu basi ningeshauri kuwa Mbowe na Lisu wote wapigwe chini. Achaguliwe kiongozi asiye na makundi. Kwanini msijifunze kwa CCM?
 
Naunga mkono hoja
 
Chawa tu huyo wengine wanasema ni mtumishi nyeti
 

Tuko pamoja mkuu.

Cc: imhotep, binti kiziwi
 
Ni kweli kuna uwezekano wa Lisu kutuingiza kwenye machafuko kutokana na majeraha uake ya moyo yaliyotokana na kupigwa risasi. Lakini kama machafuko hayo yataleta Katiba mpya hakuna ubaya!
 
Wewe ni mtu au robot? Kwa akili hizo hata ukiitwa sokwe 🦍 sitashangaa!
 
Mwamba tunakupenda sana, hebu kaa rafakari, ni 20 years sasa, muachie Lissu amyooshe huyu Kizimkazi na Mkwe wake wanataka kuiba na Uchaguzi MKUU ujao.

Siasa chini ya Lissu tutazifanyia Mabarabarani Gen Z style.✌️✌️✌️

Lissu atamwaga Petroli ya kisiasa na kuamsha Vijana halafu Uchaguzi Mkuu ujao ndio "Spark" hawa CCM hawana Legitimacy ya kututawala kwa kuiba Chaguzi.
 
Mkuu alafu huyu eti ni mwandishi,amekuwa biased, kamsema lisu mabaya yake,tu bila kusema na ya Mbowe, audui wa taifa hili vijana wa chadema pia hafai, kabisa chawa
 
Ukitaka uvuliwe nguo na wana Chadema kindakindaki hata kama ulikuwa unakula nao na unalala nao, gombea Uwenyekiti wa Chadema Taifa. Yaani nguli Lissu ndio wa kuanza kuvuliwa nguo kiasi hiki? Hii ni salami kwa akina Boniyai, Lema, Heche, Mnyika na wengineo kuwa hicho kiti hakigusiki! Idumu demokrasia ya Chadema!!!
 
Uzuri moyo wako unajua fika kuwa unaunga mkono Umachame wenu na sio hatma ya CDM🤣🤣
 
Boniyai ni vhawa namba 1 wa mtafuna chadema
 
Acha uoga,kura zipigwe mshindi atangazwe kwa haki,ila kama Lisu anatumika kukiuwa chama hataweza kamwe,haiwezekani kamwe CHADEMA kuangushwa na mtu(Kila aliyethubutu alianguka yeye).
 
Yani mtu mwenyewe unaabudu mizimu nani atakuamini. Unasema Lissu ametumwa na maccm hivi unajua mmoja wapo wa waanzilishi wa chadema ni Daudi Balali ambaye ni ccm???. Unajua kuna Team mbowe wengi ambao ni wanachama halali wa chadema lakini wakati huo huo ni ccm?

Kama lissu hana mandate ya kuongoza chama kwa sifa unazozitaja kwanini mlimpitisha kuwania urais, maamuzi ambayo Mbowe mwenyewe mwenyekiti wako unaempigia debe ali approve na akampigia kampeni, kama Lissu hakuwa na sifa vipi kuhusu hao walimpigia kampeni mtu asiye na sifa???
Ngoja nipate lunch nitakurudia muabudu mizimu wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…