Kwanini niliamua kuwa raster man[why do i choose to be raster man]

Kwanini niliamua kuwa raster man[why do i choose to be raster man]

B'REAL

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2010
Posts
4,443
Reaction score
3,002
Wagwan rasta.....selasiii i,i & i in the name of jah, i salute you wana zengo wa jamii forum.Leo nataka kuongelea kuhusu imani ya kirastafari na kwanini nilichagua kuwa rastafari japo sijazaliwa kwenye misingi ya imani ya kirastafari.

tuanze na kujifunza nini maana ya rastafari na imetoka wapi.
kidogo

Rastafari (wakati mwingine huitwa Urastafari) ni diniiliyoanzishwa huko Jamaika miaka ya 1930. Wakati mwingine dini hii hutambuliwa pia kuwa mfumo wa maisha na vuguvugu la kitamaduni.
Rastafari inarejelea imani zao, ambazo zinategemea ufafanuzi maalum wa Biblia, kama "Rastaloji". Msingi wake ni imani ya Mungu mmoja ambaye anajulikana kama Yahu (Jah) ambaye anaishi ndani ya kila mtu.

Mfalme wa zamani wa Ethiopia, Haile Selassie, anapewa umuhimu wa pekee. Marasta wengi humuona kama mwili wa Jah duniani na kama ujio wa pili wa Yesu Kristo. Wengine humwona kama nabii wa kibinadamu ambaye alitambua kikamilifu uungu wa ndani ya kila mtu.
Rastafari inatilia mkazo Afrika, na Afrika ya ughaibuni ambayo wanaamini kuwa inanyanyaswa ndani ya jamii ya Magharibi, au "Babeli". Marasta wengi wanasisitiza wito kwa Waafrika walioko nchi za magharibi wa kurudi Afrika, hasa Ethiopia. Wanaamini kuwa bara la Afrika ni Nchi ya Ahadi ya "Sayuni".

Marasta huita mfumo wao wa maisha "uhai" (livity). Ibada zao huita "misingi" (groundations), na hujumuisha muziki, kuimba, majadiliano na bangi, ambayo huonekana kama sakramenti.

Marasta wengi hula vyakula vya asili bila nyama wala chumvi (vyakula hivi huitwa itali), wanaacha nywele zao kukua bila kuchanwa au kukatwa (dreadlocks).
Inaaminika kuwa kuna wastani wa Rasta milioni 1 duniani.

Rastafari ilitokea miongoni mwa jumuiya za Wajamaika weusi maskini katika miaka ya 1930. Itikadi yake ya Uafrika ilikuwa jibu dhidi ya utamaduni wa kikoloni wa Jamaika. Imani hii ilitiwa chachu na itikadi za Uethiopia na Vuguvugu la Kurudi Afrika lililotokana na falsafa za Marcus Garvey.
Imani ilikua baada ya wahubiri kama Leonard Howell kutangaza kuwa kuvikwa taji la ufalme kwa Haile Selassie kama Mfalme wa Ethiopia mwaka 1930 kulitimiza unabii wa Biblia.

Katika miaka ya 1950, hali ya kupambana na utamaduni wa Rastafari ilisababisha harakati kuwa mgogoro na jamii pana ya Jamaika, ikiwa ni pamoja na mapigano ya vurugu na utekelezaji wa sheria.
Katika miaka ya 1960 na 1970 ilipata heshima zaidi ndani ya Jamaika na kujulikana zaidi nje ya nchi kwa njia ya umaarufu wa wanamuziki wa Rasta walioumbwa na Rasta kama Bob Marley.
Jitihada za Rastafari zilipungua katika miaka ya 1980, kufuatia vifo vya Haile Selassie na Marley.
Rastafari ina madhehebu kadhaa ̈(Nyumba za Rastafari). Madhehebu maarufu ni Nyahbinghi, Bobo Ashanti, Kanisa la Sayuni Koptiki la Ethiopia (Ethiopian Zion Coptic Church) na Makabila 12 ya Israeli (Twelve Tribes of Israel) ambayo yana tafsiri tofauti kuhusu imani ya Rastafari.
ITAENDELEA...
 
Binafsi nimezaliwa kwenye familia yenye itakadi ya dini ya kisilamu, japo sio siasa kali sana.ila nimepita pita madrasaa, ila katika kukuwa kwangu nilikua mtukutu sana mpaka na maliza darasa lasaba mwaka 1997 nilikua nishaanza kuvuta marujuana, so nilipo maliza shule ya msingi nilijichanganya na watoto wengine wa kihuni tukakimbilia mererari kwenda kutafta pesa, sababu kipindi hicho wanapolo ndo ilikua habari ya arusha.nakumbuka siku agaa nyumbani nilitoroka.

Kweli tulifika mererani kwani wezangu walikuwa washawai kwenda mara kazaa, rasimi nikaanza unyokaa sasa, kaziangu ilikuwa kutumwa majii,sigara,kununua kwa pusha ganja na kuwarolia[kuwasokotea ma braza wakubwa] alhamdulilaaah nilikuwa napata pataa vipesa maana kuna ma braza walikuwa wakizama chini[manta]wananiachia mzigo yao unakuta kuna tanzanite na hifadhi mpaka watoke then wakienda kuuza napewa kiaina au wengine na wachikichia naenda kuuza.

kutokana na tabia yangu ya ujanjaa, ushapuu na kutokuwa na kiereeree,ilinifanya ma bro wengi kunipenda na kuuza kushuka chini manta rasmi, nikiwa kama nyoka wa mchorongaji mkuu, kaziangu ilikuwa ni kushusha diga na kupandisha.kikweli maisha yalikuwa matamu sana shimoni.

familia yangu ilipata tarifa niko machimboni, ila hawajui mgodi gani,so kuna bro alikuwa broka aliambiwa anitafte anirudishe ili niende shule,nilipo kutana na yule bro akaniambia jioni tunaondoka wote nikaona ananichezea ikawa mi nashinda shimoni tu, nikipanda nikuja kula diko na shuka chini.maisha ya niendelea na mnamo mwaka 1998.
 
Nakufatilia kwa karibu sana bandiko lako chief,,
Binafsi nimezaliwa kwenye familia yenye itakadi ya dini ya kisilamu, japo sio siasa kali sana.ila nimepita pita madrasaa, ila katika kukuwa kwangu nilikua mtukutu sana mpaka na maliza darasa lasaba mwaka 1997 nilikua nishaanza kuvuta marujuana, so nilipo maliza shule ya msingi nilijichanganya na watoto wengine wa kihuni tukakimbilia mererari kwenda kutafta pesa, sababu kipindi hicho wanapolo ndo ilikua habari ya arusha.nakumbuka siku agaa nyumbani nilitoroka.

Kweli tulifika mererani kwani wezangu walikuwa washawai kwenda mara kazaa, rasimi nikaanza unyokaa sasa, kaziangu ilikuwa kutumwa majii,sigara,kununua kwa pusha ganja na kuwarolia[kuwasokotea ma braza wakubwa] alhamdulilaaah nilikuwa napata pataa vipesa maana kuna ma braza walikuwa wakizama chini[manta]wananiachia mzigo yao unakuta kuna tanzanite na hifadhi mpaka watoke then wakienda kuuza napewa kiaina au wengine na wachikichia naenda kuuza.

kutokana na tabia yangu ya ujanjaa, ushapuu na kutokuwa na kiereeree,ilinifanya ma bro wengi kunipenda na kuuza kushuka chini manta rasmi, nikiwa kama nyoka wa mchorongaji mkuu, kaziangu ilikuwa ni kushusha diga na kupandisha.kikweli maisha yalikuwa matamu sana shimoni.

familia yangu ilipata tarifa niko machimboni, ila hawajui mgodi gani,so kuna bro alikuwa broka aliambiwa anitafte anirudishe ili niende shule,nilipo kutana na yule bro akaniambia jioni tunaondoka wote nikaona ananichezea ikawa mi nashinda shimoni tu, nikipanda nikuja kula diko na shuka chini.maisha ya niendelea na mnamo mwaka 1998.
 
Mwaka 1998 yalikuja mashirika mengi sana mererani ku hamashisha kuzuiwa kwa ajira za watoto,nakumbuka walitukusanya manyokaa wengi sana na mamijusi,wakatupa semina pale ila wapi kama walikuwa wanampigia mbuzi gitaa na wao walikuwa wanaogopa maana mererani ya miaka hiyo ilikuwa ya vichaaa, watu tumepinda balaa,ila kuna maneno yalikuwa yanajirudia rudia kichwani kwangu, nakumbuka mwezi wa kumi mwaka 1998 niliamua kurudi nyumbani,kikweli nilikuwa na tabia tofauti sana tena mbaya, bangi ilikuwa ishanitawala na niliaza kujifunza viroba kipindi hiyo kulikuwa na totii au NQ.

niliwaomba wazazi msamaha na nikawaambia nataka kurudi shule,japo ilikuwa ngumu kwani nilishazoea kushika helaa nyingi,nakumbuka hela yangu ya kwanza kipindi hiyo nilipiga milioni tatu, nakumbuka nilinunua mafulii jeans, masendoo makali Caterpillar kuna duka moja liko pale arusha metro linaitwa LAST IMAGE ndo lilikua duka la Wana angaaa appolo jazz, na kukodisha bajaa kuja kushumbua arusha, hahah

Mwaka 1999 january niliaza shule rasimi kidato cha kwanza private, shule moja iko kilimanjaro[bording skull], hapa ndo nili badili mfumo wangu wote wa maishaa hadi leo.
 
nilikutana na bro wawili walikua na imani kali sana za kirastafari mmoja alikuwa form 4 mwingine 6,walipenda sana kutengeneza culture[bracelet],nilianza kuvutiwa na mienendo yao, walikuwa wakimya sana, wasio na makuu na asilimia 97% walikuwa wanapendwa na wanafunzi na walimu,taratibu niliaza kuingiwa na imani za kirasta,nakumbuka kilicho nivutia zaidi ni life style ya kirastafari,ilikuwa kila jioni naenda nakaanao wanasoma bibilia sana,tunaongea mawili matatu, maneno ya hekima sanaa.

niliaza kubadilisha maisha taratibu kutoka mtoto mtu kutu to good boy, nilipendelea sana nyakati za mchana baada ya masomo kukaa bustanini kujisomea makala tofauti za imani ya kirastafari.nakumbuka kuna siku nilikuja moshi town,baada ya hawa ma bro kumaliza shule kuja kuwatembelea, moshi kama unaenda msikiti wariadha pale kuna rastarman anaduka na vinyago na vitu vya culture anauza kwa watalii.so hawa washikaji ndo walikuwa wako nae pale.

Sikuiyo ilikuwa ni jmosi kumbe ilikuwa siku ya ibada ya kirastafari inafanyika nyumbani kwa huyo mkushi wenye duka, jamaa wakaniambia twende japo nilikuwa sina dread ila mavyazi yangu,boshori nililovyaa na maculture culture utajua mi ni raster.

siku hiyo ndo siku rasimi niliamua kuwa Rastafarian baada ya kuskia ma teaching from the elders, consensus na ilikuwa ina kunaubiriwa Amani na Upendo.
 
KWA NINI SASA NIMEAMUA KUWA RASTER.

kuwa Rastafarian kunaitaji uwe na upendo sio tu kwa ndugu zako na kwawengine

Niimani inayo spread sana upendo kuliko vita

Rastafarian ni ibada,na ibada sio ya kufanyika machoni ila pia moyoni mwako ukiri kuubiri amani na upendo

Sio kila mwenye Dreadlock ni rasterman[Rastafarian], to be Rastafarian ni zaidi ya kuwa na nywele, yakupasak kunyenyekea, kujali hisia za wengine, kuwapenda wengine na kuwa na busara
 
nilikaa nikajitasimini nini nataka kunye maisha yangu....nikagundua ni furaha,na hiyo furaha nita ipataje ni kufanya wengine wawenafuraha.nimiaka 21 sasa niko kwenye imani hi,nafuraiya na ninapenda sana
 
mimi nataka kuwa na imani hii,tatizo linakuja kazi ninayofanya kwa kufuga nywele itakuwa ngumu,je naweza kuwa rasta na nywele fupi?kwa Dar wanapatikana wapi makanisa yao
kaka Rastafarian ni imani inayotoka kwenye moyo,unaweza kuwa kama utaishi ndani ya miiko ya Rastafarian.sio mwenyeji sana Dar ila kuna ma kaka wako hapo tabata bima wana kidoksi kinauza uza culture na batiki,hawa ni real wakushi unaweza kuwaona
 
asante nitawafatilia
kaka Rastafarian ni imani inayotoka kwenye moyo,unaweza kuwa kama utaishi ndani ya miiko ya Rastafarian.sio mwenyeji sana Dar ila kuna ma kaka wako hapo tabata bima wana kidoksi kinauza uza culture na batiki,hawa ni real wakushi unaweza kuwaona
 
nilikaa nikajitasimini nini nataka kunye maisha yangu....nikagundua ni furaha,na hiyo furaha nita ipataje ni kufanya wengine wawenafuraha.nimiaka 21 sasa niko kwenye imani hi,nafuraiya na ninapenda sana
The world would have been a better place kama watu angalau robo ya population ya dunia ingekua na imani kama hii. Big up brother!!! Jah guide and bless you
 
eah, yeah, yeah - ragga so ragga

You don't ha fi dread to be rasta (don't ha fi dread)
This is not a dreadlocks thing
Divine conception of the heart, well
(repeat)

Oh, it's a life of a livity
Lived by the fathers of our history
Uphold the ancient and prophecy
Trust in the power of the Trinity, yeah
Got to believe in His Majesty
Oh yes, his lineage an divinity
The first step is serenity
Knowing one self's true royalty, yeah

You don't ha fi dread to be Rasta, yeah
(don't ha fi dread)
This is not a dreadlocks thing
Divine conception of the heart, well
(repeat)

Don't be afraid of Jah ever burning fire
Trust in Jah fire and you never get burn
The fire that reigns over heat, air and water
No water can put out Jah fire
Jah fire gonna lift Rasta higher
 
morgan hertage
eah, yeah, yeah - ragga so ragga

You don't ha fi dread to be rasta (don't ha fi dread)
This is not a dreadlocks thing
Divine conception of the heart, well
(repeat)

Oh, it's a life of a livity
Lived by the fathers of our history
Uphold the ancient and prophecy
Trust in the power of the Trinity, yeah
Got to believe in His Majesty
Oh yes, his lineage an divinity
The first step is serenity
Knowing one self's true royalty, yeah

You don't ha fi dread to be Rasta, yeah
(don't ha fi dread)
This is not a dreadlocks thing
Divine conception of the heart, well
(repeat)

Don't be afraid of Jah ever burning fire
Trust in Jah fire and you never get burn
The fire that reigns over heat, air and water
No water can put out Jah fire
Jah fire gonna lift Rasta higher
 
Back
Top Bottom