Uchaguzi 2020 Kwanini nitasikitika na kufurahi kwa pamoja wapinzani wa kweli wakikosa mbunge hata mmoja?

Uchaguzi 2020 Kwanini nitasikitika na kufurahi kwa pamoja wapinzani wa kweli wakikosa mbunge hata mmoja?

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2011
Posts
1,684
Reaction score
2,156
Kwanza nitasikitika kwasababu naipenda nchi yangu hivyo Kama mzalendo na agent wa maendeleo siwezi kufurahi kuona nchi yangu inadumaa kwa kukosa mawazo mbadala.

Pili nitafurahi wapinzani makini wakikosa wabunge ambao miaka yote ndio wamekuwa wasemaji wakubwa wa shida za wananchi lakini wananchi hao hao wamekuwa nyuma kuwatetea wasemaji wao hata pale wanapoonewa hadharani.

Mtoto anayemjali Mzazi wake hawezi kuvumilia anaposhuhudia Mzazi wake anadhalilishwa hadharani bila sababu.

Nitafurahi pia kwasababu tangu upinzani uanze kuminywa nchini imekuwa sala yangu kuu kwamba wakae pembeni kidogo ili raia waonje utamu wa nchi hii kutawaliwa bila mawazo mbadala. Labda somo likiwa kwa vitendo litaeleweka kirahisi zaidi.

Nitafurahi tena ili CCM wajionee uhalisia wa nini wapinzani walikuwa wanasaidia na kipi walikuwa hawasaidii katika ku push maendeleo ya nchi hii.

Binafsi naamini Kuna mkakati mahususi wa kuwaondoa wote ndiomaana wameanzia kwa Mbowe.

Laana ni kwa wote waliokubali kwa akili zao timamu kuhusika kupindua matokeo hasa hasa walimu wanaolia shida kila siku lakini kwasababu ya posho ya kusimamia uchaguzi wamesahau vilio vyao na kukubali kuwa sehemu ya kupindua meza.

Labda tukikaa miaka hii mitano bila kelele za wapinzani tutajua ubaya na uzuri wao.
 
Ukirudisha swali kwa viongozi wa upinzani, wanompiganinia ni nani?
Jibu ni watanzania wasio jielewa,

Sasa ngoja tuangalie kama wasiojielewa walioamua kuwapitisha wanao wataka
 
Mawakala waaminifu walikuwepo na wanakubali kwamba Uchaguzi ulikuwa huru na haki.
 
Wapinzani wapuuzi, walijisahau mno, wao walikuwa wanaikiri Bungeni ni sehemu ya kupiga tu kelele na kuacha wananchi wao masikini.
 
Usijal wapinzani watakuwa wawili zitto & Msigwa hao ndo wanaweza kutoboa wengine omba shetani atende mujiza
 
Wadhalimu malipo yao yanajulikana tu! Muda utasema! Jana ni miongoni siku ya hovyo kwenye siasa za Tanganyika tangu ipate uhuru
 
Usijal wapinzani watakuwa wawili zitto & Msigwa hao ndo wanaweza kutoboa wengine omba shetani atende mujiza

Hata hao wameliwa vichwa. Hakuna jiwe kusalia juu ya jiwe safari hii.
 
Naendelea kusisitiza japo watakuwa wamekosa kazi Kama chanzo halisi cha mapato kwao, ila binafsi niliwahi kutamani wanasiasa wote wa upinzani wakae pembeni wawaachie hao wanaccm wanaodhani nchi ni yao ili akili zitukae sawa kwanza
 
Mtoa maada upo sahihi kabisa! hii ni mbaya sana kwa CCM na mkuu wao nadhani watamaliza kwa aibu sana, kutakua na mpasuko mkubwa ndani ya CCM yenyewe! vita itakuwa wenye kwa wenyewe sasa.
 
Back
Top Bottom