Kwanini Ratiba ya Mazishi inabadilika badilika hovyo?

Kwanini Ratiba ya Mazishi inabadilika badilika hovyo?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Nilishangaa mno ile ya mara ya Kwanza kuona Wakazi wa Zanzibar hawakupewa nafasi ya Mwili kwenda Kisiwani Kuagwa ila kwakuwa jana Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan (atokaye Zanzibar) Kaapishwa leo mmeiweka.

Kama kuna Upuuzi mkubwa niliouona katika Ratiba mpya (iliyobadilishwa) ni kuona tarehe 22 Mwili utakuwa Dodoma halafu tarehe 23 utakuwa Zanzibar na tarehe 24 utakuwa Mwanza.

Mlioipanga hii Ratiba Vichwani mwenu mko vizuri kweli? Yaani Mwili muutoe Dar es Salaam kisha muupeleke Dodoma halafu urudi Zanzibar (nyuma ya Dodoma Kijiografia) na baadae Mwanza?

Kwanini Mwili baada ya kuutoa Dar es Salaam kwasababu ya ukaribu wa Kijiografia usiende Zanzibar kisha ndiyo uende huko Dodoma, Mwanza na ukamalizie Kwao Chato Mkoani Geita?

Na kwanini hii (hiyo) Ratiba inabadilika mno? Mlishindwa nini tu Kujipanga na Kuipanga vyema ikaeleweka? Na nini kiliwafanya mwanzoni Wazanzibari mliwasahau Kuwajumuisha wakati nao ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Mlitusisitiza sana kuwa Marehemu atazikwa tarehe 25 na Ratiba yenu mpya ( mliyoibadili ) mnasema sasa atazikwa tarehe 26. Je, na Siku za Mapumziko nazo zimebaki zile zile Mbili au sasa baada ya Kuibadili tena Ratiba sasa kuna Siku ya Tatu ya Kupumzika / Mapumziko?
 
Kwa siku mbili tangu kuapishwa kwake nimeona mapungufu manne-
1. Kutangaza siku za maombolezo ya Rais kuwa siku 14 badala ya siku 21
2. Akiwa kwenye kikao cha baraza la mawaziri kupokea kalamu ya blue kusaini bàdala ya nyekundu
3. Ratiba ya mazishi kusahau kuingizwa Zanzibar, ili kuagwa
4. Kubadili tarehe ya mazishi kutoka tarehe 25 kwenda 26 na Watanzania walishakata tiketi kwenda Chato tarehe 25.
 
Kwa siku mbili tangu kuapishwa kwake nimeona mapungufu manne-
1. Kutangaza siku za maombolezo ya Rais kuwa siku 24 bàdala ya siku 21
2. Akiwa kwenye kikao cha baraza la mawaziri kupokea kalamu ya blue kusaini bàdala ya nyekundu
3. Ratiba ya mazishi kusahau kuingizwa zanzibar, ili kuagwa
4. Kubadili tarehe ya mazishi kutoka tarehe 25 kwenda 26 na watanzania walisha kata tiketi kwenda chato tarehe 25.
Hakujipanga kushika dola ya Tanzania.
 
Kwa siku mbili tangu kuapishwa kwake nimeona mapungufu manne-
1. Kutangaza siku za maombolezo ya Rais kuwa siku 24 bàdala ya siku 21
2. Akiwa kwenye kikao cha baraza la mawaziri kupokea kalamu ya blue kusaini bàdala ya nyekundu
3. Ratiba ya mazishi kusahau kuingizwa zanzibar, ili kuagwa
4. Kubadili tarehe ya mazishi kutoka tarehe 25 kwenda 26 na watanzania walisha kata tiketi kwenda chato tarehe 25.
Yaan upungufu wa ratiba za mazishi ndio uone kuwa RAIS ana mapungufu makubwa? Mbona NYERERE HATA HUKO ZANZIBAR hakupelekwa. TUMSIFIE KIDOGO KWA UJASIRI HUO.
 
Kwa hiyo ijumaa sio mapumziko tuanzie hapo kwanza hata mwili wa hayati JPM ukipelekwa kuagwa hadi ILEJE mimi sioni tatizo. Kwa hiyo mapumziko yamefutwa ya ijumaa au??????
 
Kwa hiyo ijumaa sio mapumziko tuanzie hapo kwanza hata mwili wa hayati JPM ukipelekwa kuagwa hadi ILEJE mimi sioni tatizo. Kwa hiyo mapumziko yamefutwa ya ijumaa au??????
 
Kwa hiyo ijumaa sio mapumziko tuanzie hapo kwanza hata mwili wa hayati JPM ukipelekwa kuagwa hadi ILEJE mimi sioni tatizo. Kwa hiyo mapumziko yamefutwa ya ijumaa au??????
 
Kwa hiyo ijumaa sio mapumziko tuanzie hapo kwanza hata mwili wa hayati JPM ukipelekwa kuagwa hadi ILEJE mimi sioni tatizo. Kwa hiyo mapumziko yamefutwa ya ijumaa au??????
 
Back
Top Bottom