Kwanini Rwanda wametuzidi katika hili?

Kwanini Rwanda wametuzidi katika hili?

...jasusi.....ukifatilia huu uzi utadhihirisha ule usemi wa siku hizi kuwa...anaeonekana kuzungumzia madhaifu ya TZ ya leo anaonekana msaliti....ama si mzalendo.....ukweli huu unajidhirisha kwenye uzi huu kwa michango ya watu....na ndio sababu hata kupambana na mambo kama ufisadi...ama biashara chafu za unga inakua shida nchi hii...maana lazima watatoka wapuuzi wengi kutetea uchuro uliotufanya kufika hapa kama nchi....tena wanatetea kwa kigezo cha kipubavu...eti watu wanakosa uzalendo....hapa ndipo tumefika kama nchi....na inasikitisha unakuta hawa na graduates ambapo wanategemewa kesho waijenge TZ......

.....Tukija kwenye issue ya Rwanda na maendeleo yao ya haraka ukilinganisha na wengine(kama TZ)...hawa wanaosema kuwa Rwanda wanaendelea kwa kutumia raslimali wanazopora DRC...mbona hawajiulizi kwanini basi TZ isiendlee kwa raslimali tele ilizonazo???...ama nazo zinaporwa na Rwanda????.....ujinga huu wa kifikra.....

....Ukweli unabaki pale pale kuwa Rwanda wanaongozwa na kiongozi ambae anaongoza kwa ideology ya "self dependency ..as a country"...as opposed to mtawala wa TZ(JK)...ambaye anaendesha nchi kwa ideology ya "begging for survival".....huu ni ukweli mchungu....na ndio tofauti kubwa kati ya uongozi wa Rwanda na TZ.....

....In fact tofauti kwenye ideology za kiuongozi inaweza kuwa ndicho kikwazo kikubwa kinachofanya TZ ionekane kama inatengwa kwenye issue za EAC.....pamoja na kuwa watu wengi wamekazia kuwa yote yanatokana na ugomvi wa PG na JK...mimi naona ugomvi huu ni catalyst tu ya issue zilizojificha....ambazo(unfortunately)watu hawaziongelei......

...Pale ambapo PG na marais wengine karibu wote wa EAC wanapita na kuhuburi "self dependency as countries"....ni JK pekee kati ya wote ambae anapita dunia nzima bila aibu(tena openly)akihubiri "begging for survival as a country"....Huu ni ukweli usiofichika na ndio umeiweka TZ katika hali iliyopo.....na sioni kwanini usiifanye TZ kutengwa na wengine....pamoja na resources zilizopo.....Ni wajinga pekee watabeza maendeleo ya Rwanda...huku wakisahau uchuro uliopo TZ unaofanywa na watawala wao.....

.....Hata kule Zimbabwe kwa Mugabe...ambae JK na ccm yake wanamtumia kama role model.....yeye naye Mugabe ideology yake kiutawala pia ni "self dependency as a country"...na ndio imemfanya hata atengwe na nchi za magharibi....lakini utashangaa serikali ya ccm wanatoka kinafiki na kujifanya eti waumini wa sera za Mugabe.....wakati si kweli kimsingi......Tofauti kubwa ya PG na JK kiutawala ni kuwa mmoja ni "self dependent leader"....na mwingine ni "world begger"......huu ni ukweli mchungu kwa wajinga wengi TZ........

Ndugu yangu asante sana kwa hili. Mimi nimeitwa mamluki kwenye mtandao mmoja kwa sababu ya msimamo wangu na pia nikaulizwa mbona nimekuwa mkali naikandia nchi yangu sioni chochote kizuri kinachofanyika? Afadhali niitwe majina lakini siwezi kukaa kimya wakati naona nchi yangu inakwenda mrama. Kuna Wamarekani waliitwa wasaliti kwa kupinga vita ya Vietnam, lakini leo historia imewaonyesha kuwa walikuwa wazalendo kweli kweli. Ile vita ilikuwa ya maafa makubwa kwa taifa la Marekani. Vivyo hivyo leo kumsifia Kikwete wakati anaipeleka nchi kusikojulikana si uzalendo hata kidogo. Miaka minane sasa mamlakani alituahidi tatizo la umeme litakuwa historia kufikia Desemba 2007. Sote tunajua mgao wa umeme unaendelea kama kawa. Alituahidi atafanya mabadiliko kwenye mikataba ya madini ili kuwepo win win situation. Bado tuko kwenye win lose situation sisi tukiwa losers. Hapana, nitakubali kuitwa majina ya kila aina lakini hakuna mtu mwenye haki ya kuhoji uzalendo wangu. Asante sana kwa mchango wako ambao umeniongezea ari.
 
Uchumi utakuwaje wakat % kubwa ya fungu la bajeti linatengwa kwa matumiz binafsi na sio kwa maendeleo? Pia hata linalotengwa kwa maendeleo huwa no return hapo uchumi utakuwa kwel
 
Uchumi gani unaosema na wewe mbulula nyie warwanda wa ajabu sana mnaiba madini congo bila ushuru halafu leo mseme uchumi unakua kwenda zako na lwanda yako.
Unatokwa povu tu na uzushi wenu, lini uliona wanaiba madini, mtazusha wenzenu wanasonga mbele. Nyinyi c mmeridhika na biashara ya sembe
 
Kupitia taarifa ya Habari ITV saa 2, taarifa imesema katika utafiti uliofanyika na benki ya dunia katika nchi 100 Rwanda imekuwa nchi ya 7 kati ya 100 ambayo uchumi wake unakuwa kwa kasi kila mwaka na mfumuko wa bei umeshuka kwa kasi sana,
Najua wengi tunaichukia Rwanda na Kagame na hasa kutokana na mtafaruku na Raisi wetu lakini wenzetu wanafanya vizuri katika kupanga mipango yao na utawala wao unafuata sheria na hakuna ufujaji wa fedha za umma kama huku kwetu na hili linafanyika kutokana na Kagame kuwa mkali, tunatakiwa tujifunze mazuri kutoka huko ili nasi tuendelee.

Wizi wa dhahabu za DRCG
 
Unatokwa povu tu na uzushi wenu, lini uliona wanaiba madini, mtazusha wenzenu wanasonga mbele. Nyinyi c mmeridhika na biashara ya sembe
wewe lazima Utakuwa Mhamiaji Haramu huwezi ukamtetea kagame kiwango hiki!

Huu si Uzushi ni Ukweli na Dunia nzima wanajua Rwanda ni Mwizi number one wa Rasilimali za Congo akifuatiwa na ndugu yake Uganda na Mali ya Congo Ndio imemwinua kiuchumi Kagame na Serikari yake huku fedha nyingi ikitumika kuligharamia Jeshi lake kubwa na waasi wa m23 ambao Ndio wanalinda masilahi ya Rwanda Congo Ndio Maana Kagame sasa anamchukia Rais JK kisa amepeleka Jeshi Congo kuharibu vyanzo vyake vya mapato haramu hizi choko choko zote chanzo ni masilahi ya kagame Rwanda kuguswa kwani Kagame anahofia atafulia pindi akitolewa Congo na itamwia vigumu kuligharamia Jeshi lake Matokeo yake ni Uasi mkubwa kwani Njaa ikipiga hodi Jeshini lazima Majanga yajongee kwa kasi sana .hizi takwimu za kukua kwa Uchumi wa Rwanda zitakuwa aibu siku M23 waking'oka Congo kisha Hakuna njia ya kupora Mali huku wimbi la wahamiaji Haramu Kama wewe mkiendelea kurejeshwa Rwanda.
 
Wahamiaji Haramu wengi wapo Dsm huku wakiwa waumini wakubwa wa JF wakiwa na Lengo la kutumia nguvu kubwa kuutetea uporaji wa Mali za Congo na Nchi jirani kwa namna fulani Mfano harisi na Tanzania imeadhilika sana na Uhamiaji Haramu na Ukimbizi kwani uharibifu wa mazingira uliosababishwa na uhamiaji haramu hauna mfano Wizi ujambazi na uwingizaji wa siraha huko mipakani ni athali za Uhamiaji haramu Hivyo Uchumi wa Tz umemegwa na Hawa kwa staili ya ajabu kwani Tz imejikuta ipo busy kutatua matatizo yanayosababishwa na hao jirani kwa Gharama kubwa pasipo kujijua !ebu jiulize Leo Kama hz pesa zingelielekezwa kwenye maendeleo tungekuwa wapi?Nchi za Ulaya wao hawataki Uhamiaji Haramu na wanajua athali zake kiuchumi Hivyo Tz tujifunze mbinu za kisasa za kupambana na uhamiaji haramu unapora Mali na kuzinufaisha nchi zao kisha Takwimu za Uchumi kusifia Nchi eti zimekuwa kiuchumi wakati zinayumbisha Nchi zingine kiuchumi kwa faida yao .
 
Kupitia taarifa ya Habari
ITV saa 2, taarifa imesema katika utafiti uliofanyika na benki ya dunia
katika nchi 100 Rwanda imekuwa nchi ya 7 kati ya 100 ambayo uchumi wake
unakuwa kwa kasi kila mwaka na mfumuko wa bei umeshuka kwa kasi sana,
Najua wengi tunaichukia Rwanda na Kagame na hasa kutokana na mtafaruku
na Raisi wetu lakini wenzetu wanafanya vizuri katika kupanga mipango yao
na utawala wao unafuata sheria na hakuna ufujaji wa fedha za umma kama
huku kwetu na hili linafanyika kutokana na Kagame kuwa mkali, tunatakiwa
tujifunze mazuri kutoka huko ili nasi tuendelee.

subiri, kichapo wanachopata M23 kitaporomosha kabisa uchumi wa nchi hiyo. kwanza uchumi wa nchi nzima ya Rwanda haulingani hata chembe na uchumi wa Dar pekee
 
-------- mkubwa wewe swali gani hilo? Ukuaji wa uchumi wa rwanda si endelevu kwasababu hautegemei nguvukazi ya wanyarwanda bali mali asili zinazoporwa kutoka drc, vta ya kongo ikikoma hata panadol mtakuwa mnakopa .

hapa kung ukweli ...
 
Wahamiaji Haramu wengi wapo
Dsm huku wakiwa waumini wakubwa wa JF wakiwa na Lengo la kutumia nguvu
kubwa kuutetea uporaji wa Mali za Congo na Nchi jirani kwa namna fulani
Mfano harisi na Tanzania imeadhilika sana na Uhamiaji Haramu na Ukimbizi
kwani uharibifu wa mazingira uliosababishwa na uhamiaji haramu hauna
mfano Wizi ujambazi na uwingizaji wa siraha huko mipakani ni athali za
Uhamiaji haramu Hivyo Uchumi wa Tz umemegwa na Hawa kwa staili ya ajabu
kwani Tz imejikuta ipo busy kutatua matatizo yanayosababishwa na hao
jirani kwa Gharama kubwa pasipo kujijua !ebu jiulize Leo Kama hz pesa
zingelielekezwa kwenye maendeleo tungekuwa wapi?Nchi za Ulaya wao
hawataki Uhamiaji Haramu na wanajua athali zake kiuchumi Hivyo Tz
tujifunze mbinu za kisasa za kupambana na uhamiaji haramu unapora Mali
na kuzinufaisha nchi zao kisha Takwimu za Uchumi kusifia Nchi eti
zimekuwa kiuchumi wakati zinayumbisha Nchi zingine kiuchumi kwa faida
yao .

Mkuu, wahamiaji haramu wako wengi sana humu jf. kagame anatumia fedha nyingi kuimarisha kitengo cha propaganda nje ya nchi yake. inasadikika kuwa hata ndugu zetu wa CHADEMA ni miongoni mwa wanufaika wa ufadhili huo.
 
-------- mkubwa wewe swali gani hilo? Ukuaji wa uchumi wa rwanda si endelevu kwasababu hautegemei nguvukazi ya wanyarwanda bali mali asili zinazoporwa kutoka drc, vta ya kongo ikikoma hata panadol mtakuwa mnakopa .

Labda sisi tusiweke nia ya kwenda kupora rasilimali za nchi nyingine kama DRC, lakini mbona kila mkoa Tanzania una rasilimali nyingi na hazinufaishi Tanzania wala mkoa husika

Mfano, Shinyanga licha ya kuwa wanalima mpunga na pamba amapo pamba ni zao la biashara na mchele zao la chakula na biashara, pia kuna madini ya dhahabu na almasi

Shinyanga ina migodi 3 na tupo mbioni kuweka wa 4, maisha ya watanzania kule ni ya kusikitisha na wengi ni maskini na mafukara

Je? Kwa muktadha huo wa kwako sisi tunaibiwa na nani na kwa nini anatuibia na kwa nini hatuchukui hatua ili badala ya kwenda kuiba nchi jirani, tujinufaishe kwa urithi wetu tuliopewa na Muumba?
 
Kupitia taarifa ya Habari ITV saa 2, taarifa imesema katika utafiti uliofanyika na benki ya dunia katika nchi 100 Rwanda imekuwa nchi ya 7 kati ya 100 ambayo uchumi wake unakuwa kwa kasi kila mwaka na mfumuko wa bei umeshuka kwa kasi sana,
Najua wengi tunaichukia Rwanda na Kagame na hasa kutokana na mtafaruku na Raisi wetu lakini wenzetu wanafanya vizuri katika kupanga mipango yao na utawala wao unafuata sheria na hakuna ufujaji wa fedha za umma kama huku kwetu na hili linafanyika kutokana na Kagame kuwa mkali, tunatakiwa tujifunze mazuri kutoka huko ili nasi tuendelee.

watakuita mnyarwanda.....wana akili hao?wanachotaka ni kuona vita
 
subiri, kichapo wanachopata M23 kitaporomosha kabisa uchumi wa nchi hiyo. kwanza uchumi wa nchi nzima ya Rwanda haulingani hata chembe na uchumi wa Dar pekee

hahahahahaa...wabongo zile nyasi tulizoahidiwa na mramba ndo wakati wa kuzila ucha ushabiki wa vita kaka....
 
wewe lazima Utakuwa Mhamiaji Haramu huwezi ukamtetea kagame kiwango hiki!

Huu si Uzushi ni Ukweli na Dunia nzima wanajua Rwanda ni Mwizi number one wa Rasilimali za Congo akifuatiwa na ndugu yake Uganda na Mali ya Congo Ndio imemwinua kiuchumi Kagame na Serikari yake huku fedha nyingi ikitumika kuligharamia Jeshi lake kubwa na waasi wa m23 ambao Ndio wanalinda masilahi ya Rwanda Congo Ndio Maana Kagame sasa anamchukia Rais JK kisa amepeleka Jeshi Congo kuharibu vyanzo vyake vya mapato haramu hizi choko choko zote chanzo ni masilahi ya kagame Rwanda kuguswa kwani Kagame anahofia atafulia pindi akitolewa Congo na itamwia vigumu kuligharamia Jeshi lake Matokeo yake ni Uasi mkubwa kwani Njaa ikipiga hodi Jeshini lazima Majanga yajongee kwa kasi sana .hizi takwimu za kukua kwa Uchumi wa Rwanda zitakuwa aibu siku M23 waking'oka Congo kisha Hakuna njia ya kupora Mali huku wimbi la wahamiaji Haramu Kama wewe mkiendelea kurejeshwa Rwanda.
Mimi ni mtanzania halisi, tatizo lenu wauza unga hampendi kuambiwa ukweli, usifiche mshumaa chini ya uvungu wa kitanda ulete giza utaunguza kitanda na nyumba. Kagame anapiga kazi nchi yake inapiga hatua, nyinyi kupiga domo tu eti anaiba Kongo. Endeleeni kusafiri na mihadarati yetu muimarishe chama wenzenu wanafana mambo ya maendeleo.

Tuleteeni ushahidi acheni kuongozwa na mihemko na chuki zenu kwa Kagame
 
subiri, kichapo wanachopata M23 kitaporomosha kabisa uchumi wa nchi hiyo. kwanza uchumi wa nchi nzima ya Rwanda haulingani hata chembe na uchumi wa Dar pekee

Wazee wa propaganda m23, kwa sasa sioni post zao kwenye facebook.
 
Aisee una akili wewe! sijawahi ona, ni kweli rwanda pamoja na kujisifia na kupiga propaganda kwamba uchumi wao unakua lakini sio endelevu. Hawana rasilimali, hawana viwanda, hawana ardhi ya kutosha kulima na kuzalisha mazao ya chakula na biashara duh nisitaje mengi kifupi wana majanga mengi, watupigie magoti tu sisi baba zao TZ, ila tusiwapokee mpaka kagame atokeee!!

-------- mkubwa wewe swali gani hilo? Ukuaji wa uchumi wa rwanda si endelevu kwasababu hautegemei nguvukazi ya wanyarwanda bali mali asili zinazoporwa kutoka drc, vta ya kongo ikikoma hata panadol mtakuwa mnakopa .
 
-------- mkubwa wewe swali gani hilo? Ukuaji wa uchumi wa rwanda si endelevu kwasababu hautegemei nguvukazi ya wanyarwanda bali mali asili zinazoporwa kutoka drc, vta ya kongo ikikoma hata panadol mtakuwa mnakopa .

Muongo wewe, hakuna ubishi kuwa Kagame amedhibiti ufisadi Rwanda na matumizi mabaya ya rasilimali za umma, fuatilia hata magari wanayotumia viongozi wa Rwanda,
Kama uchumi wa Rwanda unakua kutokana na rasilimali zinazibwa DRC, je Tz yenye rasilimali nyingi na haina vita mbona imeshindwa kupata maendeleo endelevu?
Ukweli ni kwamba wenzetu wako serious na maendeleo ya taifa lao, sisi Tumeacha mafisadi wakituibia na kujificha kwenye kivuli cha chama dola.
 
Back
Top Bottom