Kwanini Saed Kubenea na Absalom Kibanda wanaweweseka baada ya taarifa ya kutimuliwa Lowassa CCM?

Kwanini Saed Kubenea na Absalom Kibanda wanaweweseka baada ya taarifa ya kutimuliwa Lowassa CCM?

Weston Songoro

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2014
Posts
2,793
Reaction score
1,085
Bandugu, natumai kuwa hamjambo na mko vema baada ya kuadhimisha Sherehe ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo kwa hakika ilifana sana.

Wakati wa mapumziko ya weekend na Sherehe ya Mapinduzi ya Zanzibar, zilisikika taarifa kuwa Kamati Kuu ya CCM ambayo inaketi leo Zanzibar katika kikao chake cha kawaida ina mpango wa kumfukuza uanachama kada maarufu wa chama hicho na ambaye anausaka urais kwa udi na uvumba huku akimwaga fedha nyingi, Edward Lowasa. Wengi tulifurahia kusikia taarifa hiyo kwa vile tunaamini kuwa LOWASA kupitia fedha anazomwaga kwa wajumbe wa Kamati Kuu na Mkutano mkuu wa CCM anaweza kusababisha chama kisimpendekeze mgombea mwenye sifa.

Huku wengi tukifurahia na tukikaa kitako kupokea kwa mikono miwili maamuzi hayo ya CCM ambapo inadaiwa kuwa Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana ameandaa mashtaka mapya dhidi ya Lowasa, kuna wadau wawili wa habari ambao kwa hakika wamepokea kwa uchungu wa shubiri taarifa za kufukuzwa Lowasa. Wadau hao ni Saed Kubenea ambaye kwa sasa anaandikia gazeti la Mawio baada ya gazeti lake la Mwanaha.lisi kufungiwa kutokana na kukiuka misingi ya utoaji habari. Mwingine anayeweweseka sana ni Absalom Kibanda. Hakika wadau hawa wanaonekana kuchanganyikiwa sana na wanakerwa pale Lowasa anaposemwa kwa ubaya. Mie sijui ila kama kuna wadau wanajua sababu za msingi za waandishi hawa nguli kuchanganyikiwa naomba mtujuze ili na sisi tusioelewa tupate mwanga. Ninachokijua tu juu ya watu hawa ni kwamba hawajawahi kumwandika vibaya Lowasa.

Nawasilisha
 
Kwa taarifa yako ni kwamba Saed Kubenea alipelekwa masomoni ng'ambo na gharama za masomo zote zimegharamiwa na Lowasa. Pia kanunuliwa gari na kujengewa nyumba. Aliahidiwa kuwa endapo Lowasa atakuwa Rais, atateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu.
 
Kwa taarifa yako ni kwamba Saed Kubenea alipelekwa masomoni ng'ambo na gharama za masomo zote zimegharamiwa na Lowasa. Pia kanunuliwa gari na kujengewa nyumba. Aliahidiwa kuwa endapo Lowasa atakuwa Rais, atateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu.


Acha uongo...haukusaidii
 
Hao ni paparazi wa UKAWA specific chadema, wanakifanya ni kwamba kila mgogoro unaotokea ndan ccm wao wana-u-pressurize(chochea) ili ccm kigawanyike na badae wakuu wao wachukue nchi haopo october 2015
 
Walau tupate signs za hao watu kuchanganyikiwa. Umewakuta uchi? Wanaogea peke yao? Wako hospital. Swali jingine...........wale waandishi wa Uhuru na Daily news kutomuandika vibaya JK nao wamechanganyikiwa?
 
CCM WAMFUKUZE lOWASA AU WAMWACHE BADO MACHUNGU NI YALE YALE. SASA HIVI CCM WAMEBANWA KWENYE CRITICAL ANGLE.

CCM HAITAFIKA MARCH MWAKA HUU
 
Walau tupate signs za hao watu kuchanganyikiwa. Umewakuta uchi? Wanaogea peke yao? Wako hospital. Swali jingine...........wale waandishi wa Uhuru na Daily news kutomuandika vibaya JK nao wamechanganyikiwa?
Dah! Mkuu, kuna tofauti kubwa baina ya kuweweseka na kuchanganyikiwa. Tulia na utafakari
 
sijawahi kuona kubenea aklimsifia lowasa.
 
Mleta mada umelewa! Nenda katafute kopi za magazeti ya -----------. Kubenea aliandika sana kukemea ufisadi wa Richmond huku akimtuhumu wazi kabisa Lowassa kuhusika pamoja na kuweka vielelezo vya kutosha.
Labda wewe ndo ueleze siri ya uongo huu ktk huu uzi wako usio na msingi wa hoja!
 
anaepaswa kutoa taarifa sahii za chama ni nan?kama wahusika hawajatamka ya nn kuyajadili maana hayana uthibitisho
 
Back
Top Bottom